Shukrani ya malezi . . . . . !!

Eiyer

JF-Expert Member
Apr 17, 2011
28,258
20,712
Najua jambo hili linaweza kuwa gumu kwa wengi,hii ni kutokana na mazoea.Hebu tutoke kwenye mazoea. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Ni jambo la kawaida kusikia kauli kama "hivi we mtoto nikikuambia unilipe kwa jinsi nilivyokulea utaweza" au "we mtoto huna shukrani,nimekulea vyema hivi" au "sijui nikulipe nini kwa malezi yako kwangu" n.k,kauli hizi mara nyingi hutolewa na wazazi au jamii inayotuzunguka au na watoto,kwanini uwaze kulipa mtu fadhila kwa kufanya kazi aliyojitakia mwenyewe tena kwa raha zake bila kukushirikisha?Ooo sijui nikulipe nini mama/baba kwa kunilea ili iweje?. . . . . . . . , . . . . . . , . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Hivi kulea mtoto ni sadaka?Au ni hisani?Wakati unamtafuta mtoto unajua kabisa atakachohitaji na yeye wakati huo hayupo na hachangii kwenye mjadala wenu,kwa kifupi hausiki na mipango ya kumleta duniani,iweje leo kumpa yaliyo HAKI yake ifananishwe na msaada?Mnawanyanyasa watoto kisa malez,kwa nini? . . . . . . . . , . . . . . . . . , . . Kumlea mtoto ni LAZIMA na mtoto asihusishwe na ujinga wa kumtisha kuhusu malezi.Najua hii ni ngumu kwa wengi,kwani ndivyo tumekaririshwa kutokujaji haya eti tutapata laana,ujinga tu.Usiogope malezi ni haki ya mtoto yoyote na hatakiwi kutishiwa nayo.Tuache kufikiri kimazoea ala!!!!
 
Mhh Eiyer yamekukuta nini
Ni kweli ni wajibu wao kuwalea wale waliowaleta duniani na mtu anayesema hayo hajui kuwa ni wajibu wake kumpa mtoto wake aliyemleta duniani malezi na elimu na kila hitaji lake mpaka atakapoweza kujitegemea au kufika ule umri ambao anaweza kujitegemea mwenyewe
Ila wengi hawajui hilo wanaona malezi kama hisani ambayo inatakiwa kuja kulipiwa baadae
 
Last edited by a moderator:
Mr Rocky hayajanikuta,ila nimeona watoto wengi sana wakinyanyaswa kwa kivuli cha malezi.Mtoto anatishiwa,eti"nikikuambia unilipe kwa jinsi nilivyokulea utaweza?" kauli hizi ni za kijinga sana!
 
Last edited by a moderator:
kweli mkuu umenena vyema yatupasa kufurahia kuwalea watoto wetu kama tulivyo furahi kuwaleta duniani.a
 
Cha ajabu wazazi wanaosemaga hizo kauli ni wale ambao hata malezi yao sio bora kiasi cha kuyapigia debe hivyo! Wazazi wanao walea watoto wao vyema kabisa hua hawana muda wa kauli kama hizo, wanajua fika kua ni wajibu na sio msaada..
 
Baby braza, acha kum-mind mzazi bwana. Mrushie airtel money, wewe ndo pensheni yake mwenzio.
 
most of time nnapozinguana na mshua, utasikia ivi wewe tungekuacha ulivyougua ulivokuwa mtoto ufe, au utasikia wewe unajua gharama tulizotumia kukusomesha? nguo tulizokununulia....nk. sasa uwa kila siku najiuliza ivi kweli iyo haikuwa haki yangu? maana ya kupata mtoto ni nini? nnachoamini ni kuwa mtoto uliyemzaa tena kwa raha zako ni wajibu wako kumpa mahitaji yote mpaka atakapofikia umri ambao ataweza kujimudu na ajitegemee
 
most of time nnapozinguana na mshua, utasikia ivi wewe tungekuacha ulivyougua ulivokuwa mtoto ufe, au utasikia wewe unajua gharama tulizotumia kukusomesha? nguo tulizokununulia....nk. sasa uwa kila siku najiuliza ivi kweli iyo haikuwa haki yangu? maana ya kupata mtoto ni nini? nnachoamini ni kuwa mtoto uliyemzaa tena kwa raha zako ni wajibu wako kumpa mahitaji yote mpaka atakapofikia umri ambao ataweza kujimudu na ajitegemee

Yaani wanakera sana hawa watu!
 
Najua jambo hili linaweza kuwa gumu kwa wengi,hii ni kutokana na mazoea.Hebu tutoke kwenye mazoea. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Ni jambo la kawaida kusikia kauli kama "hivi we mtoto nikikuambia unilipe kwa jinsi nilivyokulea utaweza" au "we mtoto huna shukrani,nimekulea vyema hivi" au "sijui nikulipe nini kwa malezi yako kwangu" n.k,kauli hizi mara nyingi hutolewa na wazazi au jamii inayotuzunguka au na watoto,kwanini uwaze kulipa mtu fadhila kwa kufanya kazi aliyojitakia mwenyewe tena kwa raha zake bila kukushirikisha?Ooo sijui nikulipe nini mama/baba kwa kunilea ili iweje?. . . . . . . . , . . . . . . , . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Hivi kulea mtoto ni sadaka?Au ni hisani?Wakati unamtafuta mtoto unajua kabisa atakachohitaji na yeye wakati huo hayupo na hachangii kwenye mjadala wenu,kwa kifupi hausiki na mipango ya kumleta duniani,iweje leo kumpa yaliyo HAKI yake ifananishwe na msaada?Mnawanyanyasa watoto kisa malez,kwa nini? . . . . . . . . , . . . . . . . . , . . Kumlea mtoto ni LAZIMA na mtoto asihusishwe na ujinga wa kumtisha kuhusu malezi.Najua hii ni ngumu kwa wengi,kwani ndivyo tumekaririshwa kutokujaji haya eti tutapata laana,ujinga tu.Usiogope malezi ni haki ya mtoto yoyote na hatakiwi kutishiwa nayo.Tuache kufikiri kimazoea ala!!!!


Hili ni tatizo la baadhi ya wazazi kutokufahamu wajibu wao kama wazazi! Ni wazazi wasiojijuwa kama ni wazazi na hivyo kufikiria kuwa kumlea, kumtunza na kumsomesha mtoto ni kama msaada tu wanatoa! Kazi kweli kweli!
 
Kwa upande mmoja ni sawa Mtoto kutonyanyaswa kwa sababu ya Malezi ya wazazi wake kwake..
But lazima pia tufikirie kuwa hakuna HAKI bila Wajibu..Unao wajibu as mtoto unaotakiwa kuufanya kwa mzazi wako..
Haijalishi ni malezi gani unapata lakini ni lazima ufikirie na wewe mtoto unao wajibu gani kwa mzazi wako?
Mfano unakuta watoto wengine hawana adabu kabisa,wana dharau na pengine wanaanza kujifunza tabia mbaya kama wizi..
Katika mazingira kama haya ni nadra kukuta mzazi anakuwa na mapenzi na mwanae na ndio hapo unaposikia..'ningekuwa najua hata mimba yako ningeitoa'..
 
ni kweli malezi ni wajibu wa mzazi lakini a small appreciation is nice, kumbuka mtoto anapaswa kumthamini/kuheshimu mzazi wake (4th commandment).
 
Hili ni tatizo la baadhi ya wazazi kutokufahamu wajibu wao kama wazazi! Ni wazazi wasiojijuwa kama ni wazazi na hivyo kufikiria kuwa kumlea, kumtunza na kumsomesha mtoto ni kama msaada tu wanatoa! Kazi kweli kweli!

Tena kazi kubwa sana . . . . .
 
Kwa upande mmoja ni sawa Mtoto kutonyanyaswa kwa sababu ya Malezi ya wazazi wake kwake..
But lazima pia tufikirie kuwa hakuna HAKI bila Wajibu..Unao wajibu as mtoto unaotakiwa kuufanya kwa mzazi wako..
Haijalishi ni malezi gani unapata lakini ni lazima ufikirie na wewe mtoto unao wajibu gani kwa mzazi wako?
Mfano unakuta watoto wengine hawana adabu kabisa,wana dharau na pengine wanaanza kujifunza tabia mbaya kama wizi..
Katika mazingira kama haya ni nadra kukuta mzazi anakuwa na mapenzi na mwanae na ndio hapo unaposikia..'ningekuwa najua hata mimba yako ningeitoa'..

Nakubaliana na wewe SnowBall kuwa Mtoto ana wajibu kwa mzazi wake na pia anapaswa kuonyesha appreciation kwa upendo aliopata toka kwa wazazi. Lakini anachozungumzia mtoa mada siyo tatizo la mto kukosa kuwajibika au kuwa na tabia mbaya, nafikiri anamaanisha ile hali ya mzazi kutumia nafasi yake vibaya kumnyanyasa mwanae! Mathalani, baba yako mzazi kakupiga mzinga kuwa ana hali mbaya anaomba kiasi fulani cha fedha, kwa wakati huo na wewe huna hivyo unajitahidi na kumtumia nusu - Majibu anayokupa ndo kama hayo, wewe mtoto unanifanyia mambo kama vile sikukuzaa wala kukutunza, pesa gani unayonipa? Sasa wazazi wa staili hizi ndo tunaowazungumzia, wanatumia nafasi ya uzazi vibaya.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom