Shocking Truth Kutoka Loliondo

karibu magugu na ngano vinakuwa dhahiri.

sijui wanaotutukana hapa kila siku watajificha kwenye ID gani. ila msihofu tutawasamehe tu wapendwa kwa maana tunajua hamjui msemalo

asante Yesu
 
Howdy!! Mimi sio opponent wa babu kabisa... Actually miss Judith why should u thank God for people's deaths?
This concortion is certified, so are million other drugs, survival and death r happening daily @ hospitals so I wouldn't expect any less or different at this 'public traditional hospital'

Personnaly I rate it as panadol..not 'blessed panadol'
 
karibu magugu na ngano vinakuwa dhahiri.

sijui wanaotutukana hapa kila siku watajificha kwenye ID gani. ila msihofu tutawasamehe tu wapendwa kwa maana tunajua hamjui msemalo

asante Yesu
usijali kutukanwa wala kunyanyaswa, tutatukanwa sana kwa sababu hatuko hapa kumpendeza mtu bali kuusimamia UKWELI....
tatizo la WATANZANIA... WANADANGANYIKA KIRAHISI SANA....
NDIO MAANA WANASIASA WANAWATUMIA KWA FAIDA YAO,
WAANDISHI WA HABARI PIA WANANUFAIKA, BILA KUJALI WANAOWAHADAA NI NDUGU ZAOILI WAUZE HABARI ZAO
 
Wasiopona ndio mnawaambia hawana imani, yaani mna excuse kwenye kila kitu...

Na kama wale vigogo waliokwenda kupata kikombe hawatapona basi Babu itabidi aongeze hili katika masharti yake ya kupona: "Kwamba dawa yake haitawasaidia mafisadi na jamaa zao."

RA alisema jamaa zake walikwenda kupata kikombe kwa Babu na hawakupona.
 
Watanzania inabidi tumulilie mungu hatufunulie yale tusiyo yajua lasi hivyo tuna hali mbaya
 
Howdy!! Mimi sio opponent wa babu kabisa... Actually miss Judith why should u thank God for people's deaths?
This concortion is certified, so are million other drugs, survival and death r happening daily @ hospitals so I wouldn't expect any less or different at this 'public traditional hospital'

Personnaly I rate it as panadol..not 'blessed panadol'

mpendwa, sijawahi kumshukuru Mungu specifically kwa sababu mtu fulani kafa au watu fulani wamekufa, ninaposema asante Yesu kuna mambo kadhaa

1. tunapaswa kumshukuru Mungu kwa kila jambo kwani yote yatokeayo hapa duniani, mzuri kwa mabaya, matamu kwa machungu, ya hekima na ya kipumbavu nk ni mapenzi yake

2. kwa tukio specific kama la babu na huduma yake ya tiba, namshukuru Mungu kwani ukweli unaanza kuonekana.

mimi toka mwanzo niliweka wazi kuwa sikubaliani kuwa hii dawa imetoka kwa Mungu mwenye kuianzisha na kuitimiza imani yetu wakristo. nilitahadharisha watu wasikimbilie kuamini kuwa ni kipawa cha huyu Mungu wetu kwa vile tu anayeendesha huduma hiyo anasema kuwa imetoka kwa Mungu na hata kama ni mchungaji mstaafu, wasikubali.

pamoja na wapendwa wengine wengi tu tuliopewa neema ya kuona mashaka juu ya ukweli wa tiba hii toka mwanzo tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu, si kwa sababu watu wanaokufa wanaongezeka, bali kwa sababu karibu ngano na magugu vinakuwa dhahiri na hivyo karibu vifo vitokanavyo na imani potofu juu ya kikombe na ukosefu wa maarifa, vitaanza kupungua.

kwa kweli tumshukuru Mungu sana kwamba karibu ukweli juu ya hii mitishamba na namna iliyopumbaza watu wa Mungu, utakuwa wazi kwa kila mtu

jina la Bwana libarikiwe
 
karibu magugu na ngano vinakuwa dhahiri.

sijui wanaotutukana hapa kila siku watajificha kwenye ID gani. ila msihofu tutawasamehe tu wapendwa kwa maana tunajua hamjui msemalo

asante Yesu

.
Kwa mtizamo wa kujionea huruma kama wako hata watu kama kina paulo na mitume wengi waliouawa kwa aibu ungechukulia kwamba Mungu amewafariji wapinzani wao. Inaonekana ukristo ulio nao unawafuata wazazi wako tu kwa vile wamesema wale waliouawa walikuwa ni watu wazuri na sii vinginevyo.
Dua la kuku siku zote halimpati mwewe, hivyo acha dhana ya kufikiri kuna kitu kipya chini ya mbingu.
.
 
Ah ah ah, ile ilikuwa story ya Abdul au Abunuwas (soma Hekaya za Abunuwasi) kama sikosei, inasemekana jamaa alikuwa amechacha yaani hana hela sasa akaamuwa kuwadanganya wanachi kuwa kuna malaika ndani ya kibanda, na mtu ambaye hana dhambi ndiye atakaye weza kumuona...! Hapo hata mfalme aliingizwa mkenge...! Kwa kuveshwa nguo isiyo onekana...!

Kama siyo wewe umebadili jina, basi UMEIGA.......

Hiyo habari imeandikwa jana na iko hapa chini:
https://www.jamiiforums.com/jamii-photos/123865-the-invisible-man.html

Ndiyo maana nikasema Mmezidi na hizi Abunuwasi zenu. Kama hutaki si uache kwenda?

Mie sina mpango wa kwenda ila siwakatizi watu tamaa wanaotaka kwenda.

Wandugu, kama huna DAWA, heri ukafie kwa BABU kuliko kufia Muhimbili.

Kwanza Muhimbili, ugonjwa wa Kichwa, wanaweza kukukata MGUU..........


Babu alichokifanya ni kama kilichowahi simuliwa na Abunuasi:…
"Jamaa(Abunuwasi) aliwaambia watu kuwa kwake kuna malaika waje kumuona kwa hela ila aliye na dhambi hatamuona …watu wakamiminika kwa wingi sana ikawa kila anayetoka ndani anasema nimemuona nimemuona nimemuona ili asionekane ana dhambi…"
Sasa hadith hii babu aliisoma na akaielewa akanza kuwafanyia watanzania na ndio maana kila aliyekuwa anakunywa alijifanya kutoa ushuhuda kuwa amepona amepona amepona, na kwa sababu hiyo walilazimika kuacha dawa zao kumbe ile danganya toto matokeo yake ni hayo na bado tutasikia mengi, ipo siku tutaambiwa wote waliokunywa watakufa in a short period, hapo ndio babu atakamatwa.
 
Sababu ya akina Rostam na kundi lake kutumia vyombo vya habari kumkuza mzee wa Loliondo na dawa zake ni ili wafanye dili la kuandika muswada wa sheria ya marekebisho ya katiba yenye kutufunga na kuipitisha bungeni.

Mungu anatupenda UDASA wakastuka wakaitisha kongamano la maudhui ya katiba ukweli ukawekwa wazi.

Sasa kazi yetu ni moja tu, kufuatilia hili mpaka tuone mwisho wake, Loliondo ishachuja tena.
 
Next time try your level best to be objective and rational! After all who told you that babu anatoa dawa ya kuzui kifo.

My apology. Sikujua kwamba kumbe anayeponya ni babu na si Mungu. Get your point. Mungu pekee ndiye aletaye uzima kamili. Ukiponywa na Mungu fahamu kwamba umepona. Ukitibiwa na mitishamba ya babu fahamu kuwa ugonjwa huo huo uliodhani umeponywa ndio utakuondoa. Know why? Kwa sababu Mungu hajahusika na wewe. Ndio maana wote wanaopoteza maisha ni kwa cases zile zile zilizowapeleka Samunge. I can't be more objective than that!
 
Hawa wanao mtetea babu (a.k.a Kinjeketile Ngwale) wa Rolly, wana sera kama za serikali ya Marekani...! Walipotaka kuivamia Iraq, walidai kuwa Sadam alishiriki kuanguza Twin Tower, hii sababu haikukubalika, mara wakadai kuwa Sadam Hussein ana siraha za maangamizi, walipozikosa wakaja na msemo mwingine kuwa wanamuondoa dikteta, walipoona kuwa bado jamaa anaungwa mkono wakaja na msemo mwingine kuwa wanapeleka demokrasia ya kweli kwa Wairaq...! Matokeo yake wao ndio wameiangamiza nchi ya watu...!

Sawa na hao wanao mtetea huyu babu, kila kukicha wana kuja sera na mpya...!

Watu sasa wanaonekana wakifa wengi tunasikia jinsi wanavyo mtetea...! Oooh babu hazuii kifo, ndio tunajuwa kuwa hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzuiya vifo... ndio hata hao mitume tunao waamini kwenye dini zetu, ziwe za jadi au hizi ambazo tuna ziita za kimapokeo, hawakuwa na uwezo wa kuzuiya watu wasife... Lakini kama vifo vinatokana na uzembe na ujinga wa makusudi kwa kuacha kula dawa zenye kukuongezea uhai, mnataka tuwaeleweje?

Sasa tunasikia tena kuwa watu wasiache kula dawa zao, japokuwa wamepata kunywa dawa za Kinjeketile Ngwale wa karne hii ya ishirini na mbili... Kulikoni tena?

Hao waliokwisha kunywa dawa mpaka leo hatusikii wakisema kuwa wamekwenda kupima... Wanaogopa kitu gani...!? Utawasikia wakijisifia kuwa wamepona kwa kujiangalia kwenye kioo...! Na hali maradhi yanawatafuna ndani kwa ndani...!

Mwisho hao watetezi watakuja na utetezi mpya kuwa wale wote ambao hawakupona hawana imani ndio maana dawa ya babu Kinjeketile haikufanyakazi...!

Hivi hao waathirika waliozidiwa baada ya kuto endelea na dawa zao za mahospitalini, watajisikiaje watakapo simangwa kwa kushutumiwa kuwa hawakupona kwa kuwa hawana imani...! Je hamuoni ni kuwadhidishia maradhi zaidi?

Hivi anayetakiwa kuwa na imani hapa ni nani mgonjwa au babu kinje...! Yeye si ndiye aliye dai kuwa kaoteshwa na mungu na dawa yake inaponyesha maradhi yote...!? Hivi Mwenyezi Mungu anapoleta Neema huwa anachaguwa wa kumpa? Au huwa anawapa hata wale wasio muamini?

Hivi ni kweli uwezi kupona mpaka huwe na imani ...!? Inaingia akilini kweli?

Mbona tunasoma kwenye maandiko ya biblia kuwa kuna watu waliponywa na wala hawakuwa na hiyo imani...! Na wengine walifufuliwa...! Je wale walioponywa na kufufuliwa na Nabii Elisha...! Walikuwa na imani? tena wengine walifufuka kwa kugusa mifupa ya manabii tu.

Jamani tuwache kushabikia vitu ambavyo haviwezekani kwenye karne hii... karne ambayo mwenyezi Mungu ametujaalia utaalam wa kutengeneza madawa ya kutibu maradhi mbali mbali...! Kinacho wafanya watu wasitumie hiyo miujiza ya kunywa dawa mahospitalini ni kitu gani kama si ulimbukeni na kutafuta njia za mkato ni nini...!? Kwani hizo dawa za mahospitalini hazina baraka za Mwenyezi Mungu!?

Hivi tunamwambia nini Mwenyezi Mungu siku ya hukumu... Na hali ametupa akili na tunashindwa kuitumia... Hivi ni neema gani zaidi ya kutumia akili zako na kutambua kuwa hapo Lolly hakuna uponyaji zaidi ya kuwapumbaza watu kwa kivuli cha imani!?

Mara nyingi ni vigumu sana kushindana na wajinga, watakushinda tu...!

Watakusumbua na hoja zao za kijinga na kukushusha mpaka ufikie level yao...!

Kisha watajiona kuwa wao ni mahodari na kuanza kujisifia na hali wanaona kuwa ujinga wao umepelekea maangamizi ya ndugu, marafiki na jamaa zao wenyewe...! Ukiwauliza haya mambo yamekuwaje... Hawakosi hoja hata siku moja...! Utawasikia wakisema "Aaah wale, wale wamekosa imani ndio maana hawakupona, unatakiwa umkili bwana kwanza..." Jamani hivi hakuna viongozi wa dini ambao wamefariki kwa maradhi ya kutibika, lakini wakafariki? Je hawakuwa na imani!?

Msije sema kuwa hatukuwaonya na kuwatahadharisha na hatari iliyoko mbele yenu...! Sisi tunawapenda zaidi ya hao ambao wanao wapeleka kwenye mdomo wa mauti, uko mnakoenda hakuna uponyaji, bali kuna mauwaji...!
 
niliwahi kumsikia babu akisema wasiache kutumia dawa za hospitali!

Nakumbuka niliposoma mara ya kwanza kuhusu tiba ya babu watu wengi walikua wanachangia na mtu akijaribu kusema think criticaly anaonekana hana imani etc. Mwanzo walisema hata waislam na wafwasi wa dini zingine waende, watapona instantly. inamaana kuamini kua Yesu ni Bwana haikua condition na katika ukarimu wake Yesu aliponya hata wale wasio mchagua kama Bwana wao.
Sasa nashangaa kusikia kwamba imani ndio inaponya. kwa mtazamo wangu mimi Babu sio tofauti na pasta wowote maana hata jijini Dar naweza pata pasta atakae kuombea na akwambie ukiwa na imani utapona, kama huna huwezi pona.
Sasa kama Babu anasema watu wasiache dawa za hosii, anatibu nini? maana dawa tunakunywa kutibu magonjwa. Ikiwa kikombe chake kinatibu, niendelee na dawa kwa kutibu nini hapo?
 
Leo redio WAPO imeripoti kuwa idadi kubwa ya watu wamepoteza maisha siku chache baada ya kunywa kikombe cha babu. Hii ni kwa mujibu wa riporter kutoka Arusha. Wanaoongoza kwa kukumbwa na madhila hayo ni wagonjwa wa kisukari ambao walidhani wamepona na hivyo kuacha kutumia dawa za hospitali. Nawasilisha.

1Yoh 3:8 Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi

A smooth sea never made a skilled mariner.
-English proverb

Wee acha ubwege,tusime Tanzania redio ipo moja,kwann redio zingine zistangaze? Au kwanini usikie wewe mwenyewe? Watu wengine bhana! Acha kupotosha jamii..
 
Nasikia waliokufa wengi ni waislamu ambao hata baada ya kuombewa na babu bado huendelea kuwa na mioyo yao migumu kwa kusema eti yesu sio mungu wakati anawaponya................
 
Naam! Shetani ameanza kujidhihirisha!
Wale waliokuwa wanashadidia " Mungu Wetu Anaponya" sasa itabidi mtuombe radhi na huyo 'mungu' wenu tumkate kichwa kama BAALI
 
Hawa wanao mtetea babu (a.k.a Kinjeketile Ngwale) wa Rolly, wana sera kama za serikali ya Marekani...! Walipotaka kuivamia Iraq, walidai kuwa Sadam alishiriki kuanguza Twin Tower, hii sababu haikukubalika, mara wakadai kuwa Sadam Hussein ana siraha za maangamizi, walipozikosa wakaja na msemo mwingine kuwa wanamuondoa dikteta, walipoona kuwa bado jamaa anaungwa mkono wakaja na msemo mwingine kuwa wanapeleka demokrasia ya kweli kwa Wairaq...! Matokeo yake wao ndio wameiangamiza nchi ya watu...! Sawa na hao wanao mtetea huyu babu, kila kukicha wana kuja sera na mpya...!

Watu sasa wanaonekana wakifa wengi tunasikia jinsi wanavyo mtetea...! Oooh babu hazuii kifo, ndio tunajuwa kuwa hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzuiya vifo... ndio hata hao mitume tunao waamini kwenye dini zetu, ziwe za jadi au hizi ambazo tuna ziita za kimapokeo, hawakuwa na uwezo wa kuzuiya watu wasife... Lakini kama vifo vinatokana na uzembe na ujinga wa makusudi kwa kuacha kula dawa zenye kukuongezea uhai, mnataka tuwaeleweje? Sasa tunasikia tena kuwa watu wasiache kula dawa zao, japokuwa wamepata kunywa dawa za Kinjeketile Ngwale wa karne hii ya ishirini na mbili... Kulikoni tena?

Hao waliokwisha kunywa dawa mpaka leo hatusikii wakisema kuwa wamekwenda kupima... Wanaogopa kitu gani...!? Utawasikia wakijisifia kuwa wamepona kwa kujiangalia kwenye kioo...! Na hali maradhi yanawatafuna ndani kwa ndani...! Mwisho hao watetezi watakuja na utetezi mpya kuwa wale wote ambao hawakupona hawana imani ndio maana dawa ya babu Kinjeketile haikufanyakazi...! Hivi hao waathirika waliozidiwa baada ya kuto endelea na dawa zao za mahospitalini, watajisikiaje watakapo simangwa kwa kushutumiwa kuwa hawakupona kwa kuwa hawana imani...! Je hamuoni ni kuwadhidishia maradhi zaidi?

Hivi anayetakiwa kuwa na imani hapa ni nani mgonjwa au babu kinje...! Yeye si ndiye aliye dai kuwa kaoteshwa na mungu na dawa yake inaponyesha maradhi yote...!? Hivi Mwenyezi Mungu anapoleta Neema huwa anachaguwa wa kumpa? Au huwa anawapa hata wale wasio muamini?

Hivi ni kweli uwezi kupona mpaka huwe na imani ...!? Inaingia akilini kweli? Mbona tunasoma kwenye maandiko ya biblia kuwa kuna watu waliponywa na wala hawakuwa na hiyo imani...! Na wengine walifufuliwa...! Je wale walioponywa na kufufuliwa na Nabii Elisha...! Walikuwa na imani? tena wengine walifufuka kwa kugusa mifupa ya manabii tu.

Jamani tuwache kushabikia vitu ambavyo haviwezekani kwenye karne hii... karne ambayo mwenyezi Mungu ametujaalia utaalam wa kutengeneza madawa ya kutibu maradhi mbali mbali...! Kinacho wafanya watu wasitumie hiyo miujiza ya kunywa dawa mahospitalini ni kitu gani kama si ulimbukeni na kutafuta njia za mkato ni nini...!? Kwani hizo dawa za mahospitalini hazina baraka za Mwenyezi Mungu!? Hivi tunamwambia nini Mwenyezi Mungu siku ya hukumu... Na hali ametupa akili na tunashindwa kuitumia... Hivi ni neema gani zaidi ya kutumia akili zako na kutambua kuwa hapo Lolly hakuna uponyaji zaidi ya kuwapumbaza watu kwa kivuli cha imani!?

Mara nyingi ni vigumu sana kushindana na wajinga, watakushinda tu...! Watakusumbua na hoja zao za kijinga na kukushusha mpaka ufikie level yao...!

Kisha watajiona kuwa wao ni mahodari na kuanza kujisifia na hali wanaona kuwa ujinga wao umepelekea maangamizi ya ndugu, marafiki na jamaa zao wenyewe...! Ukiwauliza haya mambo yamekuwaje... Hawakosi hoja hata siku moja...! Utawasikia wakisema "Aaah wale, wale wamekosa imani ndio maana hawakupona, unatakiwa umkili bwana kwanza..." Jamani hivi hakuna viongozi wa dini ambao wamefariki kwa maradhi ya kutibika, lakini wakafariki? Je hawakuwa na imani!? Msije sema kuwa hatukuwaonya na kuwatahadharisha na hatari iliyoko mbele yenu...! Sisi tunawapenda zaidi ya hao ambao wanao wapeleka kwenye mdomo wa mauti, uko mnakoenda hakuna uponyaji, bali kuna mauwaji...!

X-Paster, this is so well written mpaka naona nikiongeza neno nitaharibu. I work in one of the biggest HIV clinics in the country na wagonjwa wetu wengi sana walienda Loliondo ila hakuna hata mmoja amepona mpaka leo hii, including children. Sasa nabaki nashangaa sijui ni imani gani hiyo wanayoizungumzia. Umenigusa sana uliposema ambao wamekunywa hiyo dawa na hawajapona wanajisikiaje wanapoambiwa kuwa hawajapona kwa sababu hawakuwa na imani? Its not fair at all. Ila kama ulivyomalizia, ukishindana na mjinga utajikuta amekushusha mpaka umefikia level yake na bado ataendelea kujigamba kuwa kakushinda wakati what he did, was strongly believing in his illusion. Thats what these people are doing, wanatetea illusions zao. Can you imagine believing in your illusion?
 
Mwanzoni ilianza kwa mbwembwe nyingi kwamba "yeyote atakaye fika kwa babu hatakufa." Remember?
Then ikaja "Wagonjwa mahututi wapewe priority." Picha nyingi tu zikaonyesha watu kwenye machela wakivushwa kwenye foleni
Kisha "Waliozidiwa wasiletwe Samunge." Baada ya vifo kuripotiwa
Mwishowe "Wagonjwa waje na dozi zao na wasiache kutumia hata baada ya kunywa kkombe." Why? Uhakika wa kutibu mashakani hapa. Taarifa wa watu kufariki hata baada ya kunywa kikombe.

Shuhuda za immediate healing ambazo zilichangia kwa kiasi kikubwa debe la babu zikafifia ghafla. Nguvu ya dawa ikapungua. Sasa watu wanatakiwa waendelee na dozi za hospitali walizozipuuza. Wale waliojigamba kuanza kula nyama hapohapo samunge baada ya kupona allergy, wale walio anza kushindilia dozi za soda na bia baada ya kuponywa kisukari , hawa wote hatuwasikii tena. Do you learn something here. Think critically, ushabiki kando.

Fool me once, shame on you. Fool me twice, shame on me ! Wise Quotes

Jesus is Lord

Hata waumini wengi sana wa Kakobe, Mwingira na wengineo tunawaona wakitoa ushuhuda kwamaba alikuwa na uvimbe au ugonjwa fulani baada ya maombezi amepona kabisa. Lakini kesho yake unamuona mtu yule yule tena anakwenda huko huko kuombewa ugonjwa ule ule. Kwa hiyo tiba ya BABU ni kiimani zaidi, ukinywa kwa imani unapona kama ilivyo Ukiombewa na ukawa na imani unapona, Lakini kama huna imani hata wakuombee namana gani huponi ng'ooo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom