Shirika la ICAP halijalipa mishahara wafanyakazi wake walio chini ya Halmashauri Mwanza na Geita kwa miezi mitatu sasa

Kiroboto10

Member
Nov 30, 2023
71
296
Ndugu Waziri wa Afya Ummy Mwalimu,

International Center for AIDS Care and Treatment Program - ICAP, Mkoa wa Mwanza, shirika halijalipa mishahara ya watumishi wake kwa miezi 3 sasa. Hakuna taarifa kwanini hawajalipa mishahara kwa miezi 3. DAS na RACC (wasimamizi wa kazi na mikataba) hawatoi majibu kwa wafanyakazi.Pia, wakati wa kuajiri watumishi wa ICAP katika mkoa wa Mwanza, hawakutoa pesa za kujikimu kwa watumishi. Watumishi walisafiri kwa gharama zao.

Haijalishi mtumishi anatokea eneo na umbali gani, watumishi waliofaulu usaili walitakiwa kufika katika vituo vyao vya kazi kwa muda waliopangiwa. Mwaka umemalizika, pesa za kujikimu watumishi wa ICAP - Mwanza hawajarejeshewa na hakuna maelezo ya ziada au ufafanuzi wanapewa kutoka kwa waajiri.

Mkataba wa ICAP na mtumishi unasainiwa chini ya Mkurugenzi wa Halmashauri lakini mwajiri halisi na anayelipa mishahara ya watumishi ni ICAP - MSPH. Wilaya zote saba za Mkoa wa Mwanza, anayeendesha mradi wa UKIMWI na KIFUA KIKUU ni ICAP - MSPH. Zote hajalipa watumishi mishahara kwa miezi mitatu.

ICAP wanashirikiana na Tanzania tangu 2004 kupunguza maambukizi ya VVU wakati wa kujifungua na kuongeza kasi ya matunzo na matibabu ya VVU. International Center for AIDS Care and Treatment Program - ICAP inafanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na Wizara ya Afya (Wizara ya Afya Tanzania )

ICAP wanafanya kazi na Wizara ya Afya kutoa msaada kujenga uwezo na usaidizi wa kiufundi (TA) kwa ajili ya programu za kitaifa za VVU na kifua kikuu (TB). ICAP imejikita katika msaada wa kiufundi kuimarisha na kupanua kinga, matunzo na matibabu ya VVU, tohara ya hiari ya matibabu kwa wanaume (VMMC), Pia, huduma ya utambuzi wa TB kwa watoto na huduma ya TB/VVU, na watoto wanaoanzishwa na mtoa huduma. upimaji wa VVU na ushauri nasaha. Mchezo huu ni utapeli, kuaminisha watu ICAP wanaweza kutibu Kifua Kikuu (TB) na UKIMWI wakati hata uwezo mishahara ya watumishi hawawezi.

Wizara ya Afya imetulia kama ujinwa mgonjwa kwa kuwa imeingia mkataba na ICAP, ikiamini huduma ipo na inaendelea vizuri ikifanywa na ICAP - MSPH. Mnahatarisha maisha ya wagonjwa wa Kifua Kikuu (TB) na UKIMWI, na pesa mfadhili anatoa. Tuelezeni, pesa zipo wapi? Wizara mnajua fedha zilipo? Au, Wizara ya Afya tuelezeni haraka, mnaingia, mkataba na matapeli, au Wizara inashirikiana na coordinators wa Mwanza kutafuna fedha za mfadhili.

Source: Twitter page ya, MMM, Martin Maranja Masese

View: https://x.com/IAMartin_/status/1730625620856438883?t=E6Q8hbd5gAU8ak2UMDtEvw&s=09
 
Ndugu Waziri wa Afya Ummy Mwalimu,

International Center for AIDS Care and Treatment Program - ICAP, Mkoa wa Mwanza, shirika halijalipa mishahara ya watumishi wake kwa miezi 3 sasa. Hakuna taarifa kwanini hawajalipa mishahara kwa miezi 3. DAS na RACC (wasimamizi wa kazi na mikataba) hawatoi majibu kwa wafanyakazi.Pia, wakati wa kuajiri watumishi wa ICAP katika mkoa wa Mwanza, hawakutoa pesa za kujikimu kwa watumishi. Watumishi walisafiri kwa gharama zao.

Haijalishi mtumishi anatokea eneo na umbali gani, watumishi waliofaulu usaili walitakiwa kufika katika vituo vyao vya kazi kwa muda waliopangiwa. Mwaka umemalizika, pesa za kujikimu watumishi wa ICAP - Mwanza hawajarejeshewa na hakuna maelezo ya ziada au ufafanuzi wanapewa kutoka kwa waajiri.

Mkataba wa ICAP na mtumishi unasainiwa chini ya Mkurugenzi wa Halmashauri lakini mwajiri halisi na anayelipa mishahara ya watumishi ni ICAP - MSPH. Wilaya zote saba za Mkoa wa Mwanza, anayeendesha mradi wa UKIMWI na KIFUA KIKUU ni ICAP - MSPH. Zote hajalipa watumishi mishahara kwa miezi mitatu.

ICAP wanashirikiana na Tanzania tangu 2004 kupunguza maambukizi ya VVU wakati wa kujifungua na kuongeza kasi ya matunzo na matibabu ya VVU. International Center for AIDS Care and Treatment Program - ICAP inafanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na Wizara ya Afya (@wizara_afyatz)

ICAP wanafanya kazi na Wizara ya Afya kutoa msaada kujenga uwezo na usaidizi wa kiufundi (TA) kwa ajili ya programu za kitaifa za VVU na kifua kikuu (TB). ICAP imejikita katika msaada wa kiufundi kuimarisha na kupanua kinga, matunzo na matibabu ya VVU, tohara ya hiari ya matibabu kwa wanaume (VMMC), Pia, huduma ya utambuzi wa TB kwa watoto na huduma ya TB/VVU, na watoto wanaoanzishwa na mtoa huduma. upimaji wa VVU na ushauri nasaha. Mchezo huu ni utapeli, kuaminisha watu ICAP wanaweza kutibu Kifua Kikuu (TB) na UKIMWI wakati hata uwezo mishahara ya watumishi hawawezi.

Wizara ya Afya imetulia kama ujinwa mgonjwa kwa kuwa imeingia mkataba na ICAP, ikiamini huduma ipo na inaendelea vizuri ikifanywa na ICAP - MSPH. Mnahatarisha maisha ya wagonjwa wa Kifua Kikuu (TB) na UKIMWI, na pesa mfadhili anatoa. Tuelezeni, pesa zipo wapi? Wizara mnajua fedha zilipo? Au, Wizara ya Afya tuelezeni haraka, mnaingia, mkataba na matapeli, au Wizara inashirikiana na coordinators wa Mwanza kutafuna fedha za mfadhili.

Source: Twitter page ya, MMM, Martin Maranja Masese

View: https://x.com/IAMartin_/status/1730625620856438883?t=E6Q8hbd5gAU8ak2UMDtEvw&s=09

Africa kuna matatizo sana.....wakati wa kula.mbususu na kula.mipalange mnajiona wajanja sana.

Ukimwi ukiwapata mnataka Nchi zingine ndio ziwasaidie madawa na matibabu hadi mishahara.
 
Moja ya passions zangu ni kuingia kwenye hizo international NGO's hususani zile ambazo zipo affilliated na UN.

ICAP ilikuwa mojawapo, sasa kama mishahara hawalipwi miezi mitatu na kwa ninavyojua wapo fresh. Mbona hii habari inakuwa na ukakasi
 
Moja ya passions zangu ni kuingia kwenye hizo international NGO's hususani zile ambazo zipo affilliated na UN.

ICAP ilikuwa mojawapo, sasa kama mishahara hawalipwi miezi mitatu na kwa ninavyojua wapo fresh. Mbona hii habari inakuwa na ukakasi
Mkuu hicho kitu hakipo kwa ICAP Head Office.
Anayelalamika ni kibarua anayehusika huko chiiiiini kabisa ngazi ya Vituo vya afya kutoa huduma ya Kaya kwa kaya kufuatilia wagonjwa majumbani, wengine wanakaa kwenye vituo vya afya kuingiza taarifa/Data entry kwenye mifumo ya ICAP ili wapate taarifa za mwenendo wa mradi.
kwa kifupi mlalamikaji sio mwajiriwa ICAP. Kwasababu ICAP inaingia mkataba na Halmashauri then ili halmashauri itekeleze mradi wa ICAP inatakiwa iajiri wafanyakazi wa mkataba ili kutekeleza majukumu hayo. Hata malipo inapewa Halmashauri halafu ndio hawa Vibarua wanapewa chao so usikate tamaa wale jamaa mpunga upo. Hapo DAC yaani msimamizi wa Mradi ngazi ya Halmashauri na RAC msimamizi wa Mradi ngazi ya Mkoa ndio Vimeo.
 
Moja ya passions zangu ni kuingia kwenye hizo international NGO's hususani zile ambazo zipo affilliated na UN.

ICAP ilikuwa mojawapo, sasa kama mishahara hawalipwi miezi mitatu na kwa ninavyojua wapo fresh. Mbona hii habari inakuwa na ukakasi
Endelea na passion yako, usikate tamaa.
Hawa wanaolalamika ni watumishi ambao wanakua chini ya Halmashauri, ila pesa inalipwa na shirika kwenye halmashauri, halafu halmashauri ndo inalipa sasa kwenye akaunti za watu.
Hapa ndo huwa kunakua na michakato na siasa nyingi. Unaweza kuta pesa imeshaingia kwa akaunti za halmashauri, ila sasa halmashauri hazijalipa bado (sababu labda kuna issues-hakuna vifungu vya kulipia, au michakato ya kiserikali, au hata pesa imetumika kwa mengine). Target yako wewe hakikisha unaingia kama mwajiriwa direct wa shirika husika mfano hao ICAP, usiwe chini ya Halmashauri sijui. Ukiwa direct unalipwa na Icap wenyewe huwezi sikia hayo malalamiko.
 
Mkuu hicho kitu hakipo kwa ICAP Head Office.
Anayelalamika ni kibarua anayehusika huko chiiiiini kabisa ngazi ya Vituo vya afya kutoa huduma ya Kaya kwa kaya kufuatilia wagonjwa majumbani, wengine wanakaa kwenye vituo vya afya kuingiza taarifa/Data entry kwenye mifumo ya ICAP ili wapate taarifa za mwenendo wa mradi.
kwa kifupi mlalamikaji sio mwajiriwa ICAP. Kwasababu ICAP inaingia mkataba na Halmashauri then ili halmashauri itekeleze mradi wa ICAP inatakiwa iajiri wafanyakazi wa mkataba ili kutekeleza majukumu hayo. Hata malipo inapewa Halmashauri halafu ndio hawa Vibarua wanapewa chao so usikate tamaa wale jamaa mpunga upo. Hapo DAC yaani msimamizi wa Mradi ngazi ya Halmashauri na RAC msimamizi wa Mradi ngazi ya Mkoa ndio Vimeo.
Ahaa kwa hiyo ni kama ambavyo huwa wanafanya kwa kuzipa hizi NGO's ndogo ndogo miradi labda ya kufanya awareness campaigns au kukusanya data halafu unakuta wahusika wanapigwa na hao viongozi wa hizo NGO's..

Hapo nimekuelewa,
 
Endelea na passion yako, usikate tamaa.
Hawa wanaolalamika ni watumishi ambao wanakua chini ya Halmashauri, ila pesa inalipwa na shirika kwenye halmashauri, halafu halmashauri ndo inalipa sasa kwenye akaunti za watu.
Hapa ndo huwa kunakua na michakato na siasa nyingi. Unaweza kuta pesa imeshaingia kwa akaunti za halmashauri, ila sasa halmashauri hazijalipa bado (sababu labda kuna issues-hakuna vifungu vya kulipia, au michakato ya kiserikali, au hata pesa imetumika kwa mengine). Target yako wewe hakikisha unaingia kama mwajiriwa direct wa shirika husika mfano hao ICAP, usiwe chini ya Halmashauri sijui. Ukiwa direct unalipwa na Icap wenyewe huwezi sikia hayo malalamiko.

Nishawahi apply mara mbili tu, Plan na WWF na hapo ni baada ya kuona job description imefit vizuri CV yangu ila hata kuwa shortlisted haikutokea 😁😁😁

Ikabidi niingie chimbo ndio nikajua sometimes kuna lobbying huwa zinaendelea nyuma ya pazia hasa kwa hizi NGO's community za vijana ukiitoa UN agencies.

Kwa hiyo sijakata tamaa maana mimi sio mtu wa kukata tamaa. Nikitaka kitu flani hata kama kitachukua miaka mitano ila nitapambana hadi nikipate so, hata hili naamini ni matter of time tu mkuu na pia shukrani kwa clarification 🙏🏽🙏🏽
 
Mkuu hicho kitu hakipo kwa ICAP Head Office.
Anayelalamika ni kibarua anayehusika huko chiiiiini kabisa ngazi ya Vituo vya afya kutoa huduma ya Kaya kwa kaya kufuatilia wagonjwa majumbani, wengine wanakaa kwenye vituo vya afya kuingiza taarifa/Data entry kwenye mifumo ya ICAP ili wapate taarifa za mwenendo wa mradi.
kwa kifupi mlalamikaji sio mwajiriwa ICAP. Kwasababu ICAP inaingia mkataba na Halmashauri then ili halmashauri itekeleze mradi wa ICAP inatakiwa iajiri wafanyakazi wa mkataba ili kutekeleza majukumu hayo. Hata malipo inapewa Halmashauri halafu ndio hawa Vibarua wanapewa chao so usikate tamaa wale jamaa mpunga upo. Hapo DAC yaani msimamizi wa Mradi ngazi ya Halmashauri na RAC msimamizi wa Mradi ngazi ya Mkoa ndio Vimeo.
Mkuu mmteule usituite vibarua tafadhali. Sisi ni watumishi ambao tuna mikataba kabisa na Mkurugenzi wa Halmashauri. Na usipotoshe kwamba ni vibarua wa kutoa huduma kwenye kaya, wakati tupo kada tofauti, na wengine sisi ni madaktari na manesi kabisa ambao tuko kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya zenye kliniki za HIV kuanzia hospitali kubwa ya kanda ya Bugando, Hospitali ya mkoa ya Sekou Toure, hospitali za wilaya, na vituo vikubwa vya afya. Unatukosea heshima sana na kupotosha kutuita vibarua.
Pili, hili shirika la ICAP ni wababaishaji tu inaonekana, kwa sababu tangu mwezi wa kumi wamepewa kufanya kazi mkoa wa Geita, ambako alikua anafanya MDH, na wao wana shida hii hii kuanzia mwezi wa kumi hadi sasa watumishi walio chini ya halmashauri hawajalipwa mishahara yao, wakati alipokwepo MDH hajawahi kuchelewesha mshahara hata mwezi mmoja. Kwa nini kila mkoa wanakofanya kazi wao ndo kunakua na hizi matatizo? Kuna shida kubwa kwa hili shirika, wizra ya Afya ifanye uchunguzi.
 
Ukweli ndio huo.
Unaweza kuta mzigo upo Halmashauri kitaaaaaambo lkn unaambiwa hakuna vifungu vya kulipia. Yaani watumishi wa Halmashauri kila mmoja ni kambare.
Sio kweli. Hawa ICAP wana shida, kwa sababu hata Geita pia ambako wameanza kufanya kazi mwezi Oktoba naambiwa na wao hawajlipwa tangu waanze kazi huo mwezi wa 10, wakati kabla yake alikwepo shirika linaitwa MDH, hawajawahi kuchelewesha malipo hata mwezi mmoja. Kwa nini kila mkoa anaofanya kazi ICAP kuna shida?
 
Ahaa kwa hiyo ni kama ambavyo huwa wanafanya kwa kuzipa hizi NGO's ndogo ndogo miradi labda ya kufanya awareness campaigns au kukusanya data halafu unakuta wahusika wanapigwa na hai viongozi wa hizo NGO's..

Hapo nimekuelewa,
Hapana. Wanaolalamika ni watumishi ambao wameajiriwa na ICAP kupitia halmashauri husika. Kwa vile ICAP hawaruhusiwi kuajiri na kuwalipa watoa huduma za afya kwenye vituo vya serikali moja kwa moja, hivyo ICAP huingia mkataba na halamshauri, halafu halmashauri ndo inaajiri sasa, kwa hiyo hela inalipwa na ICAP kwenda halmashauri, halafu halmashauri ndo zinawalipa sasa hawa watumishi. Na hawa watumishi ni madaktari, manesi, wataalamu wa maabara, wataalamu wa data. ICAP hili shirika lina shida kubwa, kila wanapofanya kazi kuna haya malalamiko. Geita wameanza kufanya kazi mwezi wa 10, tangu waanze kufanya kazi hawajalipa mishahara pia, malalamiko ni yale yale. Mikoa mingine ambapo wapo wadau wengine kama MDH, AMREF hawana malalamiko ya aina hii. Kwa hiyo kuna shida ndani ya ICAP, na sio ishu ya urasimu wa halmashauri.
 
Hapa shida iko halmashauri amini usiamini.....subiri watatoka handaki kama Hamasi kwa hasiraa
Mikoa mingine yote inafanya kazi na haya mashirika kwa utaratibu huu huu, mbona wao hawana hizo changamoto (mfano: Kagera yupo MDH, Pwani THPS, na kadhalika). Pia, ICAP wamepewa Geita kuanzia Oktoba wafanye shughuli hii hii, na Geita pia watumishi wanalalamika haya haya, hawajalipwa kuanzia Oktoba. Kabla ya hapo, Geita lilikwepo shirika la MDH, ila hakujawahi kuwepo malalamiko haya. Kwa nini kila wanakofanya kazi wao ndo kuwe na matatizo?
 
Mkuu mmteule usituite vibarua tafadhali. Sisi ni watumishi ambao tuna mikataba kabisa na Mkurugenzi wa Halmashauri. Na usipotoshe kwamba ni vibarua wa kutoa huduma kwenye kaya, wakati tupo kada tofauti, na wengine sisi ni madaktari na manesi kabisa ambao tuko kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya zenye kliniki za HIV kuanzia hospitali kubwa ya kanda ya Bugando, Hospitali ya mkoa ya Sekou Toure, hospitali za wilaya, na vituo vikubwa vya afya. Unatukosea heshima sana na kupotosha kutuita vibarua.
Pili, hili shirika la ICAP ni wababaishaji tu inaonekana, kwa sababu tangu mwezi wa kumi wamepewa kufanya kazi mkoa wa Geita, ambako alikua anafanya MDH, na wao wana shida hii hii kuanzia mwezi wa kumi hadi sasa watumishi walio chini ya halmashauri hawajalipwa mishahara yao, wakati alipokwepo MDH hajawahi kuchelewesha mshahara hata mwezi mmoja. Kwa nini kila mkoa wanakofanya kazi wao ndo kunakua na hizi matatizo? Kuna shida kubwa kwa hili shirika, wizra ya Afya ifanye uchunguzi.
Nimefuta kauli mkuu.
Am deeply sorry for that.
 
Back
Top Bottom