n00b
JF-Expert Member
- Apr 10, 2008
- 1,006
- 2,667
Wakuu,
Habari nilizozipata punde ni kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA tawi la Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga (jina sijalipata vema) amechomwa mkuki usiku wa kuamkia leo mpaka utumbo ukatoka nje. Amekimbizwa hospitali muda si mrefu ili kuyanusuru maisha yake.
Mwandishi aliyechukua tukio hilo ameanza kusumbuliwa sana na watu wanaohisiwa kuwa viongozi wa CCM ili kuiharibu kamera yake.
Chanzo: Mashuhuda walio eneo la tukio
===========
UPDATE
===========
Habari nilizozipata punde ni kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA tawi la Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga (jina sijalipata vema) amechomwa mkuki usiku wa kuamkia leo mpaka utumbo ukatoka nje. Amekimbizwa hospitali muda si mrefu ili kuyanusuru maisha yake.
Mwandishi aliyechukua tukio hilo ameanza kusumbuliwa sana na watu wanaohisiwa kuwa viongozi wa CCM ili kuiharibu kamera yake.
Chanzo: Mashuhuda walio eneo la tukio
===========
UPDATE
===========
Sasa ametolewa theatre kupelekwa ICU. Vitu viwili mpaka sasa vinashangaza.
1. Pamoja na Polisi kupewa taarifa tangu saa 8 usiku hawajafika eneo la tukio, wala hakuna dalili za wao kufanya hivyo kwa ajili ya hatua zaidi.
2. Kuwepo kwa viongozi wawili senior wa CCM eneo la hospitali wakilazimisha kuingia chumbani kwa daktari aliyefanya operesheni. That was a bit unusual kwa hiyo ikaibua curiosity ya habari, waliposhtuka kuwa wamepigwa au wanapigwa picha, wakaanza kumsakama mwandishi aliyekuwepo eneo la tukio wakitaka kumnyang'anya kamera kwa nguvu.
Nitaendelea kuwajuza. Asante mod kwa kuweka breaking news kadri...
Nimepigiwa simu saa 11 alfajiri, nikajaribu Kimpigia simu mkuu wa kituo cha polisi, lkn kwa maelezo yake alikuwa Hana taarifa kuhusu tukio Hilo.
Polisi hawajafanyia kazi taarifa tulizowapa mapema, kwani viongozi wa CCM wamedhamiria kuhakikisha wanatumia vijana wao kwenye kata hiyo ili wafanye mauaji na ndio wameanza kazi.
MUNGU amsaidie kamanda wangu apone haraka na kata tuichukue saa 4 asubuhi.