Keylogger

Member
Oct 13, 2016
13
14
The big brain theory kipindi kimoja kizuri sana kipo Discovery science wale jamaa wamechukua magenius af wanawapa challenge mbalimbali za kisayansi daaah.. wanavyo solve sasa kwa teamwork hadi raha kuna jamaa anaitwa erick ana IQ 142 kumbe keyboard yangu nzima ngoja nianze andika sasa..

seriously hivi sisi watanzania tuna tatizo gani unajua kuna vitu vinaboa sana hivi kuna kipindi gani cha television ambacho kipo tofauti na kizuri ambacho mtu unaweza ukaangalia ukainjoy? kiwe cha ubunifu wa hali ya juu kwenye nyanja mbili yaani idea ya kipindi in general pia kiwe na highy quality ya production.. ukweli ni hakuna, ndio hakuna kipindi ambacho mtu unaweza angalia mwanzo mwisho ukafurahi kuwa umeangalia kipindi television zote za Tanzania sio hiyo azam wala hao cloudstv eeeh..hata huko DSTV hakuna!!!! mi nakupa mfano wa hiki kipindi cha The big brain theory najua wachache wameiona ile tv show ya The big bang theory sasa sio hiyo yaani hiyo The big brain theory jamaa wanaidea sio kubwa sana ila budget ndo kubwa jamaa wamewachukua watu wenye akili, hivi ni akili au akiri? aaah.. ndo hivyo hivyo basi kifupi mwenye IQ ndogo ni 120 hao wanakua ni wa field tofauti kun robotics engeneers, mechanical engineers etc..

Then wanakua wanawapa scientific challenges mbali mbali basi ukianza angalia kile kipindi mtu huwezi acha mbaka kiishe na unafurahi kweri sio hicho tu,
Kuna channel inaitwa investigation discovery(ID) yaani hapa utachoka hii channel ina vipindi ukianza angalia kimoja tu unaweza usiondoke siku nzima yaani hadi natamani nistaaf mapema ili niwe naangalia vipindi vya hii channel siku nzima yaani hawa jamaa wana vipindi vya upelelezi mbali mbali yaani ni zaidi ya movie
Sasa ukija hapa bongo kwenye vipindi vyetu mungu wangu yaani ni majanga kuanzia idea hadi production, jamani siri ya hivi vitu kama mtu una idea miyeyusho haina shida ila production ndo kila kitu, idea mbovu itazibwa na ubora wa kipindi ukiwa na idea nzuri ila production mbovu pia ni tatizo tena kubwa tu.

Tanzania kuna media house moja inaitwa clouds wanachannel yao inaitwa Cloudstv those guys they claim kuwa wao ndo no 1 in Tanzania sina tatizo nao wala sihitaji jua if it's true ila what i know hawana hata kipindi kimoja kizuri ambacho unaweza mwambia mtu tuangalie..ndio hamna wewe unaetaka ubishe unataka useme kipi shilawadu? clouds e? eti clouds360, hiki ambacho hata sauti huwa hakuna for almost 30min za kipindi? jamani ukweri huwa ni mchungu kuna vipindi vinaangaliwa sababu hakuna option yaani sio kwamba watu wanakipenda kipindi cha SHILAWADU ila hakuna option nyingine unakuta kipindi sijui hata sound engineer hawana ni kelele tu wanatumia camera sijui za namna gan..ooh for God sake..

TBC msitake kuniaminisha kuwa hii ndo ya taifa hakuna hata kipindi kimoja yaani hata maonesho ya moja kwa moja huwezi angalia ukamaliza it's a shame!
azamtv, azamtv wanajitahidi kwa baadhi ya sehemu ambazo ni interior design ya studios na kuonesha live, lakin kiukweri hata mpira bado, ndio bado hivi yule mtangazaji wa azamtv mrembo hivi watu washaweka ndani nini mbona haonekani?
 
Back
Top Bottom