waislamu inabidi tuwe waangalifu, kuwa endapo waisraeli nao watatoa msaada fedha katika serikali ya tanzania na hela hiyo hiyo ikatumika ktk ujenzi wa mahakama ya kadhi je waislau tutaitenganishaje na kodi nyingine?
Wito kwa ndugu zangu waislamu tuanzishe mahakama yetu kama ibada nyingine bila kutegemea serikali.mbona tuaenda kuhiji makka na hatuombi ruksa wala msaada kutoka serikalini,mbona tunafanya ibada nyingi bila kuhusisha serikali.
Hivi ndivyo wenzetu wanatuona hatuwezi kufanya lolote bila kusimamiwa na serikali, tunajiaibisha ndugu zangu
Mkuu tatizo labda huelewi mahakama ya kadhi ni kwamba inagusa moja ya mihimili ya dola nayo ni jurisdiction sasa utasema vp iwe kama msikiti. Wewe katika shughuli zako za kila siku si unaulizwa marital status au religion yako sasa kwani wasiulize wewe unasali wapi au wasiache kabisa kuuliza?