Serikali yaingia makubaliano kufuta deni la bilion 170 la Mbeya Cement

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Serikali imeingia makubaliano na wawekezaji wa kiwanda cha Mbeya Cement ya kuboresha na kuongeza ufanisi wa uzalishaji wa kiwanda hicho ikiwa ni Pamoja na kufutwa kwa Deni la Shilingi Billion 170 ili kukiwezesha kiwanda hicho kutengeneza Faida.

Serikali inamiliki asilimia 35 ya hisa katika kiwanda hicho huku asilimia 65 ikimilikiwa na wawekezaji wengine wawili, Lafarge na Pan African Cement kutoka nchini Mauritius.

Kiwanda hicho cha Mbeya Cement kilikua hakizalisha faida kwa ipindi kirefu kutokana na kuelemewa na madeni ambapo akizungumzia makubaliano hayo msajili wa Hazina, Neemia Mchechu amesema hatua zilizochukuliwa ni kufanya Mabadiliko ya Muundo wa Uongozi Pamoja na kufuta Deni hilo la Billion 170 lililokua likidaiwa na mmoja wa wanahisa.

Pia Neemia amesema hatua iliyofanyika kufufua kiwanda hicho itafanyika pia kwa kampuni zingine ambazo serikali ina hisa chache ili kuziwezesha kufanya vizuri na kutoa gawio kwa Serikali.

Kiwanda hicho kilikua kikihudumia Mikoa 7 jirani ambapo Meneja wa kanda ya Afrika KMashariki na Kusini wa HOLCIM Group Rajesh Surana amesema kuwa makubaliano hayo yatawezesha kampuni kusonga mbele na kuwanufaisha wateja na wana hisa.
 
Sikuelewa vizuri. Mwenye asilimia ndogo ndiye analipa deni. Hesabu hii imenichanganya. Mwenye uelewa naomba anifafanulie. Natanguliza shukrani.
 
Sikuelewa vizuri. Mwenye asilimia ndogo ndiye analipa deni. Hesabu hii imenichanganya. Mwenye uelewa naomba anifafanulie. Natanguliza shukrani.
Yaani serikali ina asilimia ndogo ya umiliki, lakini ndio mdhamini wa hao wenye asilimia kubwa.

Yaani kwenye faida serikali inagawiwa kwa asilimia, ila kwenye hasara serikali inabeba kwa asilimia zote.
 
Serikali imeingia makubaliano na wawekezaji wa kiwanda cha Mbeya Cement ya kuboresha na kuongeza ufanisi wa uzalishaji wa kiwanda hicho ikiwa ni Pamoja na kufutwa kwa Deni la Shilingi Billion 170 ili kukiwezesha kiwanda hicho kutengeneza Faida.

Serikali inamiliki asilimia 35 ya hisa katika kiwanda hicho huku asilimia 65 ikimilikiwa na wawekezaji wengine wawili, Lafarge na Pan African Cement kutoka nchini Mauritius.

Kiwanda hicho cha Mbeya Cement kilikua hakizalisha faida kwa ipindi kirefu kutokana na kuelemewa na madeni ambapo akizungumzia makubaliano hayo msajili wa Hazina, Neemia Mchechu amesema hatua zilizochukuliwa ni kufanya Mabadiliko ya Muundo wa Uongozi Pamoja na kufuta Deni hilo la Billion 170 lililokua likidaiwa na mmoja wa wanahisa.

Pia Neemia amesema hatua iliyofanyika kufufua kiwanda hicho itafanyika pia kwa kampuni zingine ambazo serikali ina hisa chache ili kuziwezesha kufanya vizuri na kutoa gawio kwa Serikali.

Kiwanda hicho kilikua kikihudumia Mikoa 7 jirani ambapo Meneja wa kanda ya Afrika KMashariki na Kusini wa HOLCIM Group Rajesh Surana amesema kuwa makubaliano hayo yatawezesha kampuni kusonga mbele na kuwanufaisha wateja na wana hisa.
Huyu Mchechu ni tapeli tu,si ndiyo alikuwa mjumbe wa Bodi ya TANESCO na akina Maharage.

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Sikuelewa vizuri. Mwenye asilimia ndogo ndiye analipa deni. Hesabu hii imenichanganya. Mwenye uelewa naomba anifafanulie. Natanguliza shukrani.

..Mramba na Yona walisamehe bilioni 10 za kodi wakafungwa.

..hawa wa sasa hivi walisamehe bilioni 170 na wanadunda mtaani.

..hicho kiwanda kwanini kisiuzwe kama zinavyouza mali za wengine wenye madeni?

..hapo kuna harufu mbaya ya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.
 
Back
Top Bottom