Serikali 'sikivu' Inaposikia nusu nusu

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
28,180
36,174
Amesikika mheshimiwa SSH jana akiongelea tozo za miamala na bei za mbolea. Akijinasibu kuwa huko ndiko kusikia kwa serikali yake sikivu.

Ikumbukwe kuwa za moto zaidi kwenye ajenda zimekuwa:

1. Ongezeko la kodi na tozo mbalimbali.
2. Vita dhidi ya Corona ikiwamo chanjo na tahadhari husika.
3. Mahitajio ya katiba mpya.

(a) Kodi na Tozo:
Ongezeko la tozo za miamala na bei za mbolea yalikuwa ni sehemu ndogo sana ya hoja hii. Kodi kwenye mafuta ya magari imepelekea gharama zaidi katika nyanja zote (ikiwamo mbolea).

Tozo za miamala ni msumari wa ziada tu kwenye maswahiba ya kadhia hizi dhidi ya maisha ya mtanzania huyu.

Kwa uchumi wa mwananchi yupi kustahili maongezeko ya kodi au tozo zozote ndani ya janga hili la Corona? Vipi gharama za matibabu ya ugonjwa huu kuwa kwetu? Vipi vigogo kutolipa kodi? Vipi wizi kwa mujibu wa ripoti za CAG? Nk.

Kwa aliyoyaongelea SSH, hoja hii hadi sasa itakuwa imesikika kiwango kidogo sana.

(b) Vita dhidi ya Corona:
Hili lilikuwa la dharura na kipaumbele sana. Mengine yote yanakuwa na maana iwapo tu tuko hai. Pamoja na mapungufu yote, la msingi zaidi hapa ni kuwa, hatimaye chanjo inaanza kutolewa leo.

Kwa vile tokea pale mtu atakapokuwa ameipokea, Corona itakuwa imegeuka kuwa historia kwake, basi hili litakuwa liko pazuri.

Inatia moyo kuwa hoja hii imesikika.

(c) Katiba mpya:
SSH hakugusia lolote kuhusu katiba mpya, kadhia ya Mwanza wala lolote kuhusiana na maridhiano.

Mama hajasikia na hafahamu lolote lililotokea Mwanza wala mwendelezo wake.

Mama hatambui kuwa tuna tatizo lolote katika umoja wetu linalomhitaji yeye kwa dharura kama kiongozi wa taifa.

Hoja hii haijasikika kabisa.

Sauti itakuwa haitoshi.

Asilaumiwe msikilizaji kwa usikivu kwake kuwa mdogo.

Sauti haitoshi!

Ninawasilisha.
 
Hili la mwisho wala halitajwi.

La mwisho hakulitaja bila shaka kwa sababu atakuwa hajalisikia tu, kwani kasema mwenyewe, yeye ni msikivu.

#1. Kasikia kidogo mno - wapi kodi ya mafuta, vipi vigogo kutolipa kodi, vipi gharama za tiba corona?

#2. Hili kalisikia lote. Kimsingi nikishapata Johnson Johnson, nadhani hata kuandika kuhusu Corona itakuwa basi tena 😁😁😁.

#3. Hilo hajalisikia kabisa.

Shime makamanda. Biashara asubuhi. Msikivu asiposikia sauti tafadhali.

Tuongeze sauti ikibidi hata lugha kubadili, atasikia tu. Mbona hata mawe husikia?
 
Watanzania bado hawajafahamu nguvu waliyonayo juu ya watawala. Ufaransa kabla ya mapinduzi waliokua na uwezo wa kupanga sera za nchi ni viongozi wa dini na ukoo wa kifalme. Wananchi wa kawaida walionekana kama third class citizens.

Pressure ya maisha ilisababisha third class citizens ku retaliate ndiyo chimbuko la mapinduzi. Hatimae waliunda bunge la ki demokrasia linaloongoza nchi mpaka leo.
 
Watanzania bado hawajafahamu nguvu wakiyonayo juu ya watawala. Ufaransa kabla ya mapinduzi waliokua na uwezo wa kupanga sera za nchi ni viongozi wa dini na ukoo wa kifalme. Wananchi wa kawaida walionekana kama third class citizens.

Pressure ya maisha ilisababisha third class citizens ku retaliate ndiyo chimbuko la mapinduzi. Hatimae waliunda bunge la ki demokrasia linaloongoza nchi mpaka leo.

Unajua chakula kuwiva ni shuruti kwanza kutokota vilivyo. Tutafika tu.

Kudai haki hakuwezi kuwa bila gharama

1. Watu (including the learned) hawajui kuwa rais au serikali hawawezi kuwa na vipaumbele vyao bali vipaumbele ni vyetu sisi.

2. Watu (including the learned) hawajui kuwa vipaumbele vyao haviwezi kuzingatiwa kwa hisani au huruma ya rais au serikali.

3. Watu (including the learned) ni waoga wa kumkosoa rais au serikali kwa hofu au ubinafsi uliopitiliza ukiwamo wenye harufu ya kusaka zaidi teuzi na maslahi binafsi hata ya kijinga au kipumbavu tu.

4. Watu (including the learned) hawako tayari kuhatarisha sura zao kwa watawala kwa maslahi binafsi.

Matokeo yake ni kuwa watu kama hao hawawezi kutokea katika jitihada yoyote ya kudai haki (in person au hata kwa fake ID) ila kujificha nyuma ya migongo ya kina Mbowe na kina Mdude huku wakiwakosoa kuwa wamekosea hapa au pale.

Pole pole lakini. Tutafika tu. Tulikotoka na Corona tunakujua. Tulipo tunashangilia pamoja na kuwa it's not over yet.
 
Unajua chakula kuwiva ni shuruti kwanza kutokota vilivyo. Tutafika tu.


1. Watu (including the learned) hawajui kuwa rais au serikali hawawezi kuwa na vipaumbele vyao bali vipaumbele ni vyetu sisi.

2. Watu (including the learned) hawajui kuwa vipaumbele vyao haviwezi kuzingatiwa kwa hisani au huruma ya rais au serikali.

3. Watu (including the learned) ni waoga wa kumkosoa rais au serikali kwa hofu au ubinafsi uliopitiliza ukiwamo wenye harufu ya kusaka zaidi teuzi na maslahi binafsi hata ya kijinga au kipumbavu tu.

4. Watu (including the learned) hawako tayari kuhatarisha sura zao kwa watawala kwa maslahi binafsi.

Matokeo yake ni kuwa watu kama hao hawawezi kutokea katika jitihada yoyote ya kudai haki (in person au hata kwa fake ID) ila kujificha nyuma ya migongo ya kina Mbowe na kina Mdude huku wakiwakosoa kuwa wamekosea hapa au pale.

Pole pole lakini. Tutafika tu. Tulikotoka na Corona tunakujua. Tulipo tunashangilia pamoja na kuwa it's not over yet.
1627454887436.png
 
Kwasasa hatuna kiongozi tuna dikteta hatari

Mkuu, hata madikteta huwa kuna lugha wanayoisikia:

IMG_20210707_084839_278.jpg


Wako wapi wakoloni au wako wapi makaburu?

Wako wapi kina Iddi Amini, Bashir, Charles Taylor, Saddam, Mobotu nk?

Udikteta wao ni tatizo lao. Watajiju, hilo haliwezi kuwa letu. Tukiuridhia udikteta huo wa kulaumiwa watakuwa si wao bali itakuwa sisi.

Dikteta atakuwa dikteta kwa kuridhiwa na sisi wenyewe na si vinginevyo.
 
Ameacha kuupiga mwingi siku hizi,

Hapana, ni suala la sauti tu.

Katika kutoridhishwa na utendaji wake kwenye:

1. Ongezeko la kodi na tozo
2. Corona na yatokanayo ikiwamo chanjo.
3. Umuhimu wa katiba mpya na maridhiano.

Amesikia suala la Corona vyema na vipengele vya tozo za miamala na bei za mbolea ambazo ongezeko la kodi za mafuta haliwezi kupuuzwa.

Msikilizaji kutokusikia lawama si kwake bali watoa sauti.

Sauti zaidi wakuu, nyama ziko chini!
 
Mkuu, hata madikteta huwa kuna lugha wanayoisikia:

View attachment 1871275

Wako wapi wakoloni au wako wapi makaburu?

Wako wapi kina Iddi Amini, Bashir, Charles Taylor, Saddam, Mobotu nk?

Udikteta wao ni tatizo lao. Watajiju, hilo haliwezi kuwa letu. Tukiuridhia udikteta huo wa kulaumiwa watakuwa si wao bali itakuwa sisi.

Dikteta atakuwa dikteta kwa kuridhiwa na sisi wenyewe na si vinginevyo.
Tutawapinga vipi wana kila aina ya silaha
 
Hapana, ni suala la sauti tu.

Katika kutoridhishwa na utendaji wake kwenye:

1. Ongezeko la kodi na tozo
2. Corona na yatokanayo ikiwamo chanjo.
3. Umuhimu wa katiba mpya na maridhiano.

Amesikia suala la Corona vyema na vipengele vya tozo za miamala na bei za mbolea ambazo ongezeko la kodi za mafuta haliwezi kupuuzwa.

Msikilizaji kutokusikia lawama si kwake bali watoa sauti.

Sauti zaidi wakuu, nyama ziko chini!
Huyu ni katili sn
 
Amesikika mheshimiwa SSH jana akiongelea tozo za miamala na bei za mbolea. Akijinasibu kuwa huko ni kusikia kwa serikali yake sikivu.

Ikumbukwe kuwa za moto zaidi kwenye ajenda zimekuwa:

1. Ongezeko la kodi na tozo mbalimbali.
2. Vita dhidi ya Corona ikiwamo chanjo na tahadhari husika.
3. Mahitajio ya katiba mpya.

(a) Kodi na Tozo:
Ongezeko la tozo za miamala na bei za mbolea yalikuwa ni sehemu ndogo sana ya hoja hii. Kodi kwenye mafuta ya magari imepelekea gharama zaidi katika nyanja zote (ikiwamo mbolea).

Tozo za miamala ni msumari wa ziada tu kwenye maswahiba ya kadhia hizi dhidi ya maisha ya mtanzania huyu.

Kwa uchumi wa mwananchi yupi kustahili maongezeko ya kodi au tozo zozote ndani ya janga hili la Corona? Vipi gharama za matibabu ya ugonjwa huu kuwa kwetu? Vipi vigogo kutolipa kodi? Vipi wizi kwa mujibu wa ripoti za CAG? Nk.

Kwa aliyoyaongelea SSH, hoja hii hadi sasa itakuwa amesikika kiwango kidogo sana.

(b) Vita dhidi ya Corona:
Hili lilikuwa la dharura na kipaumbele sana. Mengine yote yanakuwa na maana iwapo tu tuko hai. Pamoja na mapungufu yote, la msingi zaidi hapa ni kuwa, hatimaye chanjo inaanza kutolewa leo.

Kwa vile tokea pale mtu atakapokuwa ameipokea, Corona itakuwa imegeuka kuwa historia kwake, basi hili litakuwa liko pazuri.

Inatia moyo kuwa hoja hii imesikika.

(c) Katiba mpya:
SSH hakugusia lolote kuhusu katiba mpya, kadhia ya Mwanza wala lolote kuhusiana na maridhiano.

Mama hajasikia na hafahamu lolote lililotokea Mwanza wala mwendelezo wake.

Mama hatambui kuwa tuna tatizo lolote katika umoja wetu linalomhitaji yeye kwa dharura kama kiongozi wa taifa.

Hoja hii haijasikika kabisa.

Sauti itakuwa haitoshi.

Asilaumiwe msikilizaji kwa usikivu kwake kuwa mdogo.

Sauti haitoshi!

Ninawasilisha.
Watu wanayomba kwa kisukuma kuwa mama anaupiga mwingi
 
Namna ya kuwapinga hata kama angekuwa nuclear weapons ni hii hapa:


Mbona wanapigika vizuri tu?
Tumewashindwa
 
Tumewashindwa
Hahaahaaa. Nyerere akicheka kama mazuri kuwa Kaburu SA atakomaa na hakuna litakolompata.

Labda kama umewashindwa utakuwa wewe tu mkuu. Lakini makamanda wengi akiwamo Mbowe na wengine wanaoweza kuhesabika wanajua mapambano yanaendelea na kuna gharama kubwa tu za kulipa.

IMG_20210728_114925_905.jpg


Hii ndiyo maana yake kwa nini safari hii tedhamiria hasa.

Kwenye vita hivi kama unataka kuishi tu, unataka mafanikio tu, hutaki kusumbuliwa, huku si kwako.

Hawaoni kina Pascal Mayalla waliko au kina mzee Mdee au kina Silinde? Huko ni kwa wasiotaka mikwaruzo.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Back
Top Bottom