Serikali pigeni marufuku upimaji na ugawaji wa ardhi kutumia futi. Haiakisi mipango miji

Tafakari yetu

JF-Expert Member
Apr 19, 2021
1,502
4,408
Kuna dhuluma kubwa na utapeli mwingi unatendeka kwenye kipimo cha futi kinachotumiwa katika upimaji na ugawaji kwa wasiojua. Kipimo cha futi ni cha kufikirika tu na zaidi kinatumika kipimo hicho kuficha ukweli halisi wa udogo wa viwanja vinavyotolewa.

Kwa mfano, unakuta kiwanja unaambiwa kina ukubwa futi 50 kwa 40 ambacho ni sawa kusema futi za mraba 2000 ambazo ni sawa na mita za mraba 186. Kipimo cha futi kimetumika kuficha ukweli halisi wa mita za mraba 186 ambacho ni kidogo mno.

Pia, kipimo cha futi ni hatari katika upangaji wa miji kisasa. Kinachochea ujenzi holela kwa sababu ya ufinyu wa kiwanja mtu alichonacho.

Ombi kwa serikali kabla hatujawa na miji mingine kama Manzese, Gongolamboto na mingine, upimaji na ugawaji wa viwanja wa namna hii upigwe marufuku.
 
Hata ukubwa wa viwanja kwa mita. Ni aibu kubwa kwa Serikali kutoa vibali vya viwanja vya mita 20x20 tu. Mji wowote lazima uwe na high, medium na low density. Haiwezekani mji au eneo lote liwa na viwanja vidogo vinavyolingana kama walivyoharibu dodoma na kama wanavyoendelea kuharibu Kibaha na Kigamboni.
 
Very correct and agreed your concern is very genuine. But hiyo sq m 186 si mtu anazunguka kakiwanja hako na kuona kuwa kanatosha shimo la choo, anakubalije upuuzi huo? Sema wanatumia miguu/hatua ambazo hazina uhalisia wa metric units!

Ulichoongea uko sawa kabisa, huo unakuwa ni uchafu katika mipango miji
 
Futi hazitumiki saivi, viwanja vinapimwa kwa mita za mraba, hao wanatumia futi ukute kakiwanja chako chenyewe ni kidogo, hasa huku uswazi unakuta mtu ana eneo kumi kwa kumi 😅 Si hatari hiyo.
 
Screenshot_20230310-105321.jpg
 
Kuna dhuluma kubwa na utapeli mwingi unatendeka kwenye kipimo Cha futi kinachotumiwa katika upimaji na ugawaji kwa wasiojua. Kipimo Cha futi ni Cha kufikirika tu na zaidi kinatumika kipimo hicho kuficha ukweli halisi wa udogo wa viwanja vinavyotolewa. Kwa mfano, unakuta kiwanja unaambiwa kina ukubwa futi 50 kwa 40 ambacho ni sawa kusema futi za mraba 2000 ambazo ni sawa na mita za mraba 186. Kipimo Cha futi kimetumika kuficha ukweli halisi wa mita za mraba 186 ambacho ni kidogo mno.

Pia , kipimo Cha futi ni hatari katika upangaji wa miji kisasa. Kinachochea ujenzi holela kwa sababu ya ufinyu wa kiwanja mtu alichonacho.

Ombi, kwa serikali kabla hatujawa na miji mingine kama manzese ,gongolamboto na mingine upimaji na ugawaji wa viwanja wa namna hii upigwe marufuku.
Futi au mita?
 
Wewe mtoa mada sikuelewi kabisa, ujinga wa mtu usiwe sababu ya kutapeliwa, vipimo vya ft, inch, cm, km, m, ni standard ya kidunia, na huwezi kumtapeli mtu anayejua, ni jukumu lako kujua conversation ya vipimo tofauti. Ungesema labda tufute vipimo vya hatua za miguu watu wanatapeliwa ningekuelewa Kwa sababu Kila mtu ana hatua zake na kipimo hiki hakijawa standardized, ila ft haina shida hata kidogo, wewe ni kilaza wa hesabu na umeshatapeliwa.

Mimi hata ukiniuzia Kiwanja Kwa inch, hectometer, nakubali hakuna tatizo, hatua za miguu ndo sitaki. Pole samaki
 
Back
Top Bottom