Netanyahu
Senior Member
- Oct 2, 2008
- 147
- 22
Nilibahatika kuwemo katika msafara wa wapiganaji wa misituni wasiokuwa na kombati wala vyeo wala pasipoti kutembelea nchi zinazoongozwa na maraisi waliokuwa wapiganaji wa misituni za Rwanda,Sudan Kusini na Eritria ili kujifunza kama viongozi hao wapiganaji wa zamani kama wana uwezo wa kukisimamia kile walichokuwa wakipigania au walikuwa wakipigania tu wapate utawala ili wafisadi nchi na kujaza matumbo yao tu.
Katika nchi hizo kwa ujumla kila nchi ilituvutia kivyake.Niseme wazi maraisi wa nchi hizo tatu wanakijua wanachosimamia.
Katika nchi ya Eriteria nililojifunza ni jinsi nchi ile kwanza inavyojua kutumia jeshi lake.Tenda za ujenzi kama wa barabara muhimu za nchi hiyo hufanywa na jeshi.Serikali hutoa tenda hizo kwa jeshi na ukiziona barabara zilizojengwa na jeshi hazina tofauti na za kampuni ya kijapani ya Konoike au Kajima zilizojengwa Tanzania.Labour costs huwa ziko chini kwani wanajeshi wale hujenga bila malipo ya ziada zaidi ya mishahara yao ya mwezi walipwayo.Serikali ya Eritria imejiwekea utaratibu wa kuhakikisha wanajeshi wanatumika productively wakati hakuna vita kufanya miradi mikubwa ya kusaidia nchi badala ya kulala kwenye makambi na kufyeka majani na makwanja kuzunguka kambi wakisubiri tarehe za mshahara zifike wachukue wakalewe pombe za bei nafuu zisizolipiwa kodi.
Kitu kingine nimejifunza kule ni jinsi serikali ya Eriteria isivyopenda mikopo iwe toka benki ya Dunia IMF au kutoka ndani.Raisi wao ana msemo usemao USE YOUR SWEAT NOT DEBTS akihamasisha kila mahali watu wapende kutumia nguvu zao zaidi kujikwamua kibinafsi na kiinchi kuliko kutegemea mikopo.Ni muumini mkubwa wa ule msemo usemao MTAJI WA MASKINI NI NGUVU ZAKE.Kila mahali apitapo raisi yule huhamasisha watu kutumia nguvu zao zaidi kujikwamua kuliko kutegemea mikopo.Anaita mikopo kuwa ni utumwa wa hiari mambo leo ambao mtu au nchi huishia kuwa kibarua wa mkopeshaji milele asipokuwa makini.
Japo Tanzania haina uhusiano mzuri sana na Eritria kwa sababu ambazo Tanzania inajua yenyewe lakini kuna mambo ya kujifunza kule.
I salute you president of Eritria.keep it up.
Katika nchi hizo kwa ujumla kila nchi ilituvutia kivyake.Niseme wazi maraisi wa nchi hizo tatu wanakijua wanachosimamia.
Katika nchi ya Eriteria nililojifunza ni jinsi nchi ile kwanza inavyojua kutumia jeshi lake.Tenda za ujenzi kama wa barabara muhimu za nchi hiyo hufanywa na jeshi.Serikali hutoa tenda hizo kwa jeshi na ukiziona barabara zilizojengwa na jeshi hazina tofauti na za kampuni ya kijapani ya Konoike au Kajima zilizojengwa Tanzania.Labour costs huwa ziko chini kwani wanajeshi wale hujenga bila malipo ya ziada zaidi ya mishahara yao ya mwezi walipwayo.Serikali ya Eritria imejiwekea utaratibu wa kuhakikisha wanajeshi wanatumika productively wakati hakuna vita kufanya miradi mikubwa ya kusaidia nchi badala ya kulala kwenye makambi na kufyeka majani na makwanja kuzunguka kambi wakisubiri tarehe za mshahara zifike wachukue wakalewe pombe za bei nafuu zisizolipiwa kodi.
Kitu kingine nimejifunza kule ni jinsi serikali ya Eriteria isivyopenda mikopo iwe toka benki ya Dunia IMF au kutoka ndani.Raisi wao ana msemo usemao USE YOUR SWEAT NOT DEBTS akihamasisha kila mahali watu wapende kutumia nguvu zao zaidi kujikwamua kibinafsi na kiinchi kuliko kutegemea mikopo.Ni muumini mkubwa wa ule msemo usemao MTAJI WA MASKINI NI NGUVU ZAKE.Kila mahali apitapo raisi yule huhamasisha watu kutumia nguvu zao zaidi kujikwamua kuliko kutegemea mikopo.Anaita mikopo kuwa ni utumwa wa hiari mambo leo ambao mtu au nchi huishia kuwa kibarua wa mkopeshaji milele asipokuwa makini.
Japo Tanzania haina uhusiano mzuri sana na Eritria kwa sababu ambazo Tanzania inajua yenyewe lakini kuna mambo ya kujifunza kule.
I salute you president of Eritria.keep it up.