Serikali kuwatumbua wadaiwa bodi ya mikopo

Ni muhimu taarifa zote za mikopo kwa wanafunzi ziwekwe wazi ili wanufaika waweze ku access taarifa hizo kupitia index number zao kwenye website ya bodi ama taarifa zitumwe kwenye email zao.
Hivi sasa kuna student wanapata allocation ya mkopo but sio pesa zote zinaingizwa kwenye account zao. Kuna loan officers wanachezea pesa za watu. Dr. Ndalichako tunaamini utalimaliza hili, maana kama utaratibu wa utoaji hauko makini basi hata utaratibu wa ulipaji tusitegemee uwe makini.
 
BODI ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) imetoa onyo kwa wadaiwa sugu ambao hawajajitokeza kuanza kulipa madeni yao, kwamba hatua mbalimbali dhidi yao zinatafuata kokote waliko.

Miongoni mwa hatua hizo, bodi hiyo imetaja kuwa ni kuwatoza wadaiwa hao sugu riba ya asilimia kumi katika deni lao na kutumia taarifa zao kuwazuia kufanya safari za nje ya nchi.

Imeeleza kuwa wadaiwa hao wa tangu mwaka wa masomo wa 1994/95, wataanza kusakwa kupitia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambaye anawajibika kukagua mali zote za Serikali.

Mbali na CAG, ambaye ana mkono mrefu wa kuwasaka katika ofisi zote za Serikali Kuu, mashirika ya Umma, Serikali za Mitaa na katika miradi ambayo Serikali ina ubia na sekta binafsi, pia kampuni binafsi za ukaguzi wa hesabu, zenye mkono mrefu katika sekta binafsi, zitatumika kuwasaka katika kampuni binafsi na asasi za kiraia.

“Jukumu la CAG na kampuni zingine binafsi za ukaguzi wa mahesabu, ni kulazimisha waajiri kuwasilisha taarifa za wafanyakazi wao ambao ni wahitimu wa elimu ya juu na makato ya mkopo waliopewa,” imeeleza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imefanya marejeo ya Sheria ya Bodi namba 9 ya 2004 na marekebisho yake, inayomtaka kila mwajiri kutoa maelezo kwa maandishi kwa bodi, kuhusu mwajiriwa ambaye ni mnufaika wa mkopo huo, ndani ya siku 28 tangu mdaiwa alipoajiriwa.

Hatua kali
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mdaiwa yeyote wa bodi hiyo atakayeshindwa kulipa deni lake bila sababu za msingi, kwanza atakuwa akikabiliwa na kesi ya madai chini ya kifungu cha 6 C na H cha Sheria ya Bodi ya Mikopo namba 9 ya mwaka 2004.

Mbali na kukabiliwa na kesi hiyo, pia mkopo wake kwa namna unavyochelewa kuanza kulipwa, utakuwa ukijilimbikizia riba ya asilimia 10. Taarifa hiyo ya bodi imeeleza kuwa mdaiwa huyo taarifa zake zitapelekwa katika taasisi za kumbukumbu ya mikopo zilizo chini ya Benki Kuu (BoT), ambazo zitazuia wadaiwa hao kupata mikopo katika mabenki na asasi zote za fedha.

Mdaiwa huyo pia atazuiwa kupata udhamini wa Serikali katika muendelezo wa masomo yake, lakini pia atazuiwa kujiunga na chuo chochote cha elimu ya juu ndani na nje ya nchi. Aidha kwa mujibu wa taarifa hiyo, taarifa zao pia zitawasilishwa katika Idara ya Uhamiaji iliyo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na katika ofisi zote za kibalozi, ili wakose kibali cha kusafiri nje ya nchi.

Hasara nyingine watakayokabiliwa nayo wadaiwa hao, ni Tozo ya Kulinda Thamani ya Mkopo (VRF) ya asilimia sita kila mwaka, itakayotozwa kwa kila mkopo, ili wadaiwa watakapoanza kulipa mkopo waliochukua, walipe kwa thamani ya sasa.

Tozo hiyo imelenga kuepuka athari ya mfumuko wa bei tangu mdaiwa aliponufaika, lakini pia kuwezesha urejeshwaji wa deni, uwe na thamani ya kumhudumia mwanafunzi mwingine mwenye mahitaji kwa sasa na baadaye.

Ambao hawajaajiriwa
Taarifa hiyo pia imeonya wadaiwa wanaodhani kuwa kutokuajiriwa ni sababu ya kutolipa mkopo huo, kwamba mkopo huo unatakiwa kulipwa baada ya kumalizika kwa mwaka mmoja tangu mdaiwa alipofanikiwa kuhitimu masomo yake, au mwaka mmoja tangu mhusika alipokatisha masomo yake kwa sababu yoyote.

Aidha, taarifa hiyo imeelekeza watakaojitokeza, kama wameajiriwa, asilimia nane ya mshahara wao wa kila mwezi, itatakiwa kukatwa na kuwasilishwa kwenye Bodi ili kulipa deni husika. Lakini pia Bodi hiyo imetengeneza utaratibu kwa ambao hawajaajiriwa, kwamba wanaweza kulipa kiasi cha chini cha Sh laki moja kila mwezi katika akaunti za Bodi zilizopo Benki ya Posta yenye namba CCA0240000032; Benki ya NMB namba 2011100205 na Benki ya CRDB namba 01J1028467503.

Deni lenyewe
Kwa mujibu wa Ripoti ya CAG, hadi Juni 2014, bodi hiyo ilikuwa imewakopesha wanafunzi Sh trilioni 1.8 kuanzia mwaka wa masomo 1994/95 na kati ya fedha hizo, Sh bilioni 51 zilitolewa na iliyokuwa Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia.

Taarifa hiyo ya HESLB imetolewa siku chache kabla ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, ya kusitisha ajira ya Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, George Nyatega kwa tuhuma za udhaifu katika fedha za mikopo zaidi ya Sh bilioni 3.2. Miongoni mwa waliosimamishwa pamoja na Nyatega ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Yusufu Kisare, Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo, Juma Chagonja na Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo, Onesmo Laizer.
karibia nusu ya wafanyakazi wote tz hawata ruhusiwa kusafiri.
 
Hapa kuna tatizo. Wale waliopewa mkopo kutoka Zanzibar hawadaiwi kwasababu ni wazanzibar, wanapewa bure!!

Walipewa mikopo hiyo kwasababu ya uzanzibar na sasa anayebeba mzigo ni Mtanganyika

Hata wakiambiwa walipe, CAG hana mkono, na wala wizara ya elimu haihusiki huko znz

Hakuna anayeweza kufuatilia nani kaajiriwa wapi huko znz.

Wanafunzi wa znz wanatakiwa kurudisha ZHSLB tu, haya mengine hayawahusu Watanganyika si ndio JMT?
 
kusema mtu ambaye hana kazi maalumu ya kumpa kipato alipe mkopo ni kubwabwaja....wanufaika wengi wa mikopo hii ni watoto wa maskini hawana nyumba hawana shamba hawana kiwanja sasa hizo fedha atazirejesha vipi wakati hana ajira.
Mara ya kwanza mlisema wanufaika wa mkopo ni watoto wa matajiri!
 
BODI ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) imetoa onyo kwa wadaiwa sugu ambao hawajajitokeza kuanza kulipa madeni yao, kwamba hatua mbalimbali dhidi yao zinatafuata kokote waliko.

Miongoni mwa hatua hizo, bodi hiyo imetaja kuwa ni kuwatoza wadaiwa hao sugu riba ya asilimia kumi katika deni lao na kutumia taarifa zao kuwazuia kufanya safari za nje ya nchi.

Imeeleza kuwa wadaiwa hao wa tangu mwaka wa masomo wa 1994/95, wataanza kusakwa kupitia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambaye anawajibika kukagua mali zote za Serikali.

Mbali na CAG, ambaye ana mkono mrefu wa kuwasaka katika ofisi zote za Serikali Kuu, mashirika ya Umma, Serikali za Mitaa na katika miradi ambayo Serikali ina ubia na sekta binafsi, pia kampuni binafsi za ukaguzi wa hesabu, zenye mkono mrefu katika sekta binafsi, zitatumika kuwasaka katika kampuni binafsi na asasi za kiraia.

“Jukumu la CAG na kampuni zingine binafsi za ukaguzi wa mahesabu, ni kulazimisha waajiri kuwasilisha taarifa za wafanyakazi wao ambao ni wahitimu wa elimu ya juu na makato ya mkopo waliopewa,” imeeleza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imefanya marejeo ya Sheria ya Bodi namba 9 ya 2004 na marekebisho yake, inayomtaka kila mwajiri kutoa maelezo kwa maandishi kwa bodi, kuhusu mwajiriwa ambaye ni mnufaika wa mkopo huo, ndani ya siku 28 tangu mdaiwa alipoajiriwa.

Hatua kali
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mdaiwa yeyote wa bodi hiyo atakayeshindwa kulipa deni lake bila sababu za msingi, kwanza atakuwa akikabiliwa na kesi ya madai chini ya kifungu cha 6 C na H cha Sheria ya Bodi ya Mikopo namba 9 ya mwaka 2004.

Mbali na kukabiliwa na kesi hiyo, pia mkopo wake kwa namna unavyochelewa kuanza kulipwa, utakuwa ukijilimbikizia riba ya asilimia 10. Taarifa hiyo ya bodi imeeleza kuwa mdaiwa huyo taarifa zake zitapelekwa katika taasisi za kumbukumbu ya mikopo zilizo chini ya Benki Kuu (BoT), ambazo zitazuia wadaiwa hao kupata mikopo katika mabenki na asasi zote za fedha.

Mdaiwa huyo pia atazuiwa kupata udhamini wa Serikali katika muendelezo wa masomo yake, lakini pia atazuiwa kujiunga na chuo chochote cha elimu ya juu ndani na nje ya nchi. Aidha kwa mujibu wa taarifa hiyo, taarifa zao pia zitawasilishwa katika Idara ya Uhamiaji iliyo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na katika ofisi zote za kibalozi, ili wakose kibali cha kusafiri nje ya nchi.

Hasara nyingine watakayokabiliwa nayo wadaiwa hao, ni Tozo ya Kulinda Thamani ya Mkopo (VRF) ya asilimia sita kila mwaka, itakayotozwa kwa kila mkopo, ili wadaiwa watakapoanza kulipa mkopo waliochukua, walipe kwa thamani ya sasa.

Tozo hiyo imelenga kuepuka athari ya mfumuko wa bei tangu mdaiwa aliponufaika, lakini pia kuwezesha urejeshwaji wa deni, uwe na thamani ya kumhudumia mwanafunzi mwingine mwenye mahitaji kwa sasa na baadaye.

Ambao hawajaajiriwa
Taarifa hiyo pia imeonya wadaiwa wanaodhani kuwa kutokuajiriwa ni sababu ya kutolipa mkopo huo, kwamba mkopo huo unatakiwa kulipwa baada ya kumalizika kwa mwaka mmoja tangu mdaiwa alipofanikiwa kuhitimu masomo yake, au mwaka mmoja tangu mhusika alipokatisha masomo yake kwa sababu yoyote.

Aidha, taarifa hiyo imeelekeza watakaojitokeza, kama wameajiriwa, asilimia nane ya mshahara wao wa kila mwezi, itatakiwa kukatwa na kuwasilishwa kwenye Bodi ili kulipa deni husika. Lakini pia Bodi hiyo imetengeneza utaratibu kwa ambao hawajaajiriwa, kwamba wanaweza kulipa kiasi cha chini cha Sh laki moja kila mwezi katika akaunti za Bodi zilizopo Benki ya Posta yenye namba CCA0240000032; Benki ya NMB namba 2011100205 na Benki ya CRDB namba 01J1028467503.

Deni lenyewe
Kwa mujibu wa Ripoti ya CAG, hadi Juni 2014, bodi hiyo ilikuwa imewakopesha wanafunzi Sh trilioni 1.8 kuanzia mwaka wa masomo 1994/95 na kati ya fedha hizo, Sh bilioni 51 zilitolewa na iliyokuwa Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia.

Taarifa hiyo ya HESLB imetolewa siku chache kabla ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, ya kusitisha ajira ya Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, George Nyatega kwa tuhuma za udhaifu katika fedha za mikopo zaidi ya Sh bilioni 3.2. Miongoni mwa waliosimamishwa pamoja na Nyatega ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Yusufu Kisare, Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo, Juma Chagonja na Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo, Onesmo Laizer.


SAFI SANA MAGUFULI. HII KITU NIMEKATWA SANA NA MWAJIRI NIKAWA NAHUZUNIKA KWA KUCHEKWA SASA NA MIMI NITACHEKA KIDOGO.

DAWA YA DENI NI KULIPA.
 
Zikirejeshwa fedha zote tulizoobiwa na mafisadi nami nitawapa hilo deni vinginevyo nami ni mgawo wangu wa keki ya taifa kufidia maumivu niliyosababishiwa na mafisadi
 
Hivi kesi za madai wanaona ni kama Maji ya kunywa sio. Haya ngoja tuone. Huruma kwa MAHAKAMA kuendelea kurundikiwa mizigo hisiyostahili.
 
Hapa kuna tatizo. Wale waliopewa mkopo kutoka Zanzibar hawadaiwi kwasababu ni wazanzibar, wanapewa bure!!

Walipewa mikopo hiyo kwasababu ya uzanzibar na sasa anayebeba mzigo ni Mtanganyika

Hata wakiambiwa walipe, CAG hana mkono, na wala wizara ya elimu haihusiki huko znz

Hakuna anayeweza kufuatilia nani kaajiriwa wapi huko znz.

Wanafunzi wa znz wanatakiwa kurudisha ZHSLB tu, haya mengine hayawahusu Watanganyika si ndio JMT?
Mzizi wa tatizo ni set up ya Muungano!

Hili tatizo la mikopo kuhusu Wanafunzi wanaotoka Zanzibar ni tawi tu la mzizi wa tatizo.

Huu Muungano wetu kwa karibu unafanana na Muungano wa UK.

Kama ilivyo kwa Watanganyika na Wazanzibar, wanafunzi wa vyuo kutoka Scotland hawana mikopo bali wanapewa education grant lakini wale wa England walidaiwa mikopo ya elimu kwa sababu wanapewa education loan.

Dawa ya muungano wa aina hii siyo serikali mbili, tatu au nne. Dawa yake ni kuuvunja tu ili kila nchi ibebe mzigo wake.
 
Mzizi wa tatizo ni set up ya Muungano!

Hili tatizo la mikopo kuhusu Wanafunzi wanaotoka Zanzibar ni tawi tu la mzizi wa tatizo.

Huu Muungano wetu kwa karibu unafanana na Muungano wa UK.

Kama ilivyo kwa Watanganyika na Wazanzibar, wanafunzi wa vyuo kutoka Scotland hawana mikopo bali wanapewa education grant lakini wale wa England walidaiwa mikopo ya elimu kwa sababu wanapewa education loan.

Dawa ya muungano wa aina hii siyo serikali mbili, tatu au nne. Dawa yake ni kuuvunja tu ili kila nchi ibebe mzigo wake.
Kitu kisichoeleweka ni hiki, wanafunzi wa ZNZ kupitia ZHSLB ni wachache kuliko wanaopewa grant ya HESLB.

SMZ inawakalia kidete warudishe ZHESLB, wakiambiwa warudishe HESLB kama wenzao wa Tanganyika inakuwa nongwa.

SMZ inawakingia kifua hawana uwezo, wakati wana uwezo wa kurudisha ZHESLB.

Kwa maneno mengine wao wana uhalali wa kusoma kupitia migongo ya Watanganyika ambao hawawezi kupata ZHESL hata kwa bahati mbaya kwasababu tu si Wazanzibar

Kupata HESLB lazima uwe mtanzania,wznz wapo, ili upate ZHESB lazima uwe mzanzibar.

Gharama za wananfunzi wa znz,wengi kuliko SMZ inavyodhamini inalipwa na Tanganyika.

Tunasikia wakatwe 8% ya mishahara ili baadaye itoe grant kwa wznz siku za baadaye

Halafu utawasikia wazanzibar wakipiga makelele ya kuonewa na muungano.
Haya hawazungumzi kabisa kwasababu kupata ni haki yao.

Nadhani serikali 3 zinaweza kutoa jibu, kila mmoja ajitahidi kwa upande wake. Panapohitajika nguvu ya pamoja wote wawe washiriki.

Kwanini kusiwe na grant kwa wananchi wa Singida ambao kieleimu wanahitaji msaada!

Yaani grant zetu zinatoka kwa uzanzibar na si kwa kigezo cha uwezo! hili halipo sawa

Nimemsikia waziri makamba akisema wanashughulikia suala ajira na mgao wa benki kuu

Kwasababu za kisiasa watawatwisha Watanganyika mzigo usio na sababu

Ukitoa ajira kwasababu ya muungano, una maana wznz wapate ajira maalumu hata maeneo yasiyo ya muungano.

Hao watakaopata ni wale waliochukua mkopo HESLB bure kwa uzanzibar, upendeleo unaendelea katika ajira. Wanaolipa 8% hawana upendeleo bara na wala visiwani

Akina Makamba wana entertain haya bila kujali ili tu wadumu kisiasa

Kuhusu bank kuu, sioni kwanini wasipewe shea yao.

Huko nako kuna tatizo tusiloliona. ZNZ wanpewa 4% ya pato la Taifa.

Yaani pato la Tanganyika hata kama hawachangii, linasemwa ni shea yao benki kuu.

Piga hesabu za pato la Taifa halafu uangalie ni kiasi gani wanapata ukilinganisha na uchumi wao unavyotoa. Haya hatuyaoni
 
Back
Top Bottom