Kuna vyuo mbalimbali vilivyokumbwa na kashfa mbalimbali nchini, suala hili lisipochuliwa hatua litaidhalilisha elimu ya Tanzania. Mfano Chuo cha Ustawi wa Jamii Kijitonyama ilishakubwa na kashfa na Serikali ikachukua hatua na inaendelea kuchukua hatua. Hivyo ni vema ikachukuliwa hatua pia kwa vyuo vingine ili kulinda heshima ya elimu yetu kwa manufaa ya Taifa letu. WanaJF tusaidiane kutaja vyuo vyote vyenye kashfa mbalimbali katika elimu. Mojawapo ya Vyuo hivyo ni CBE ilishawahi kukumbwa na kashfa ya kuhonga Fedha ili mwanafunzi afaulu. Chuo Kingine ni UDOM kukumbwa na Kashfa ya kutoa maksi kwa masomo yasiyofundishwa kwa kutokuwepo wahadhiri. Chuo kingine ni MNMA kimetolewa na Gzeti la DIRA kukumbwa na kashfa ya ngono (aibu tupu) na mambo mengi kadhaa utadhani haina uongozi. Serikali ichukue hatua haraka kwani kuyalea haya ni hatari sana kwa mustakabali wa taifa letu. Wanajamvi toeni maoni yenu na mtaje vyuo vingine.