mbwigule
JF-Expert Member
- Jan 21, 2012
- 235
- 103
Majuzi serikali imewalipa wastaafu waliokuwa wakilipwa kila baada ya miezi sita pensheni ya miezi mitatu badala ya sita waliyoisubiria kwa kipindi hicho. Mara ya mwisho wazee hawa walilipwa mwezi Julai mwaka jana yaani miezi sita iliyopita. Hakuna anayepinga mpango wa serikali kubadili ulipwaji huo kufanyika miezi mitatu mitatu badala ya sita ya awali, lakini swali ni kwa nini mabadiliko hayo yaanze kwa wazee hao kudhulumiwa malipo yao ya miezi mitatu? Wengi walifikiri serikali ingelipa kwanza malipo yao ya kawaida ya miezi sita yaani Julai hadi Januari kisha kuendelea na utaratibu wao mpya wa miezi mitatu mitatu.
Izingatiwe wengi wa wazee hawa wanalipwa kiwango kidogo cha pensheni na pengine cha kudhalilisha, sasa kuwadhulumu kama ilivyofanyika si kujitakia laana ya bure? Hivi kwa nini serikali hii ya awamu ya nne inahaha kujitafutia migogoro kila kukicha hata kutoka kwa watu walioonekana kuuvumilia udhaifu wao?
Izingatiwe wengi wa wazee hawa wanalipwa kiwango kidogo cha pensheni na pengine cha kudhalilisha, sasa kuwadhulumu kama ilivyofanyika si kujitakia laana ya bure? Hivi kwa nini serikali hii ya awamu ya nne inahaha kujitafutia migogoro kila kukicha hata kutoka kwa watu walioonekana kuuvumilia udhaifu wao?