Serikali ijiandae kupata hasara na kupata takwimu zisizo sahihi katika sensa!

tatanyengo

JF-Expert Member
Mar 30, 2011
1,134
280
Wakati siku za sensa ya watu na makazi zikikaribia, wanachi wenye imani ya dini ya Kiislamu, wamezidi kusisitiza kuwa kama kipengele cha dini hakitawekwa hawatahesabiwa ng'o. Maamuzi hayo yalifikiwa siku ya jumamosi tarehe 7/7/2012 katika mkutano wao uliofanyika mjini Arusha.

Walisema siku ya sensa Waislamu wataandika mabango yanayosomeka SIHESABIWI na kuyaweka kwenye milango ya nyumba zao. Mkutano huo ulihudhuriwa na Pro. Lipumba aliyekuwa mgeni rasmi. Pia katika mkutano alikuwepo Mh. Tundu Lissu.

My take: Serikali isipochukua hatua stahiki itatumia fedha nyingi katika zoezi la sensa ambalo halitakuwa na matokeo tarajiwa.
 
mimi ustadhi maalim Daruwesh wa hapa buguruni kwa mnyamani nasema sigomi na nitahesabiwa mimi pa1 na wake zangu na watoto wangu..
 
NI ujinga huu wa kugomea maendeleo yako kwa upuuzi na mapokeo ya Waarabu na Wazungu.lakini leo naomba nitoe siri moja ya kuonesha kuwa hapa Dar karibu waislamu wote wamesha hesabiwa kama unabisha ni PM nitakujulisha ni kwa jinsi gani sensa imefanyika Dar
 
Wala mimi sisimamii kwenye msimamo wa kidini,ila sitaki kuhesabiwa kwa vile sioni sensa zilizopita zimesaidiaje mwananchi wa kawaida wa Tanzania.Kigezo wapuuzi hawa wanachotumia kuwaingiza wananchi wa kawaida mkenge ni kwamba inasaidia kupanga mipango ya maendeleo.Hii ni kweli kwa serikali makini. Lakini kwa serikali hii ya kihuni,si kweli.Sensa frankly speaking ni kwa faida ya wakubwa wa dunia.Wanataka kujua sera zao hasa za depopulation using all posible means,including wars,hunger,AIDS, etc.etc. zimefanikiwa vipi.No,I wouldn't seriously like to be part of that nonsense.
Wakati siku za sensa ya watu na makazi zikikaribia, wanachi wenye imani ya dini ya Kiislamu, wamezidi kusisitiza kuwa kama kipengele cha dini hakitawekwa hawatahesabiwa ng'o. Maamuzi hayo yalifikiwa siku ya jumamosi tarehe 7/7/2012 katika mkutano wao uliofanyika mjini Arusha.

Walisema siku ya sensa Waislamu wataandika mabango yanayosomeka SIHESABIWI na kuyaweka kwenye milango ya nyumba zao. Mkutano huo ulihudhuriwa na Pro. Lipumba aliyekuwa mgeni rasmi. Pia katika mkutano alikuwepo Mh. Tundu Lissu.

My take: Serikali isipochukua hatua stahiki itatumia fedha nyingi katika zoezi la sensa ambalo halitakuwa na matokeo tarajiwa.
 
NI ujinga huu wa kugomea maendeleo yako kwa upuuzi na mapokeo ya Waarabu na Wazungu.lakini leo naomba nitoe siri moja ya kuonesha kuwa hapa Dar karibu waislamu wote wamesha hesabiwa kama unabisha ni PM nitakujulisha ni kwa jinsi gani sensa imefanyika Dar


Kuna maendeleo gani ktk nchi hii hadi nipoteze mda wangu wa kazi kusubiri magamba na mafisadi wapite kuniuliza maswali ya kitoto................./ mimi mapema asubuhi naenda DA-R-SA msikitini kwetu.
 
Sasa usipohesabiwa utakuwa unamkomoa nani? Kumbuka gharama za sensa zinatokana na kodi uliyolipa.
 
Liwalo naliwe lazima sheikh lipumba atakuwa ikulu siku ya sensa yeye na sheikh ponda wakipata kahawa na wali maharage.

Nadhani watahesabiwa wakiwa ikulu.
 
Wakati siku za sensa ya watu na makazi zikikaribia, wanachi wenye imani ya dini ya Kiislamu, wamezidi kusisitiza kuwa kama kipengele cha dini hakitawekwa hawatahesabiwa ng'o. Maamuzi hayo yalifikiwa siku ya jumamosi tarehe 7/7/2012 katika mkutano wao uliofanyika mjini Arusha.

Walisema siku ya sensa Waislamu wataandika mabango yanayosomeka SIHESABIWI na kuyaweka kwenye milango ya nyumba zao. Mkutano huo ulihudhuriwa na Pro. Lipumba aliyekuwa mgeni rasmi. Pia katika mkutano alikuwepo Mh. Tundu Lissu.

My take: Serikali isipochukua hatua stahiki itatumia fedha nyingi katika zoezi la sensa ambalo halitakuwa na matokeo tarajiwa.

Kaka uko sahihi kabisa. wao wanaona kama wanataniwa sasa wasubiri moto wake, maana siku hiyo ya sensa Maandamano itakuwa nchi nzima.
Kama hawaamini hilo ebu wawaulize watu wa vitambulisho vya taifa waliotangaza kuwa watapita majumbani kuchukua takwimu nini walichokutana nacho. Zoezi lao walilitangaza sana na lilikuwa linaanzia tar 22 -june mpaka 9-july, lakini mpaka sasa wameamua kujifariji kwa kuongeza muda na hawatofanikiwa kama ilivyotarajiwa kwani waislam wanahasira na isue ya sensa na wanaona hiyo ni staili ya kuwahesabu kijanja, walikuwa wanakimbizwa kama wezi kwa kupopolewa kwa mawe, wakaamua kuzirejesha ofisini kwa mtendaji na matokeo yake hakuna wanaokwenda kujiandikisha.

Ivi serikali ikiweka hicho kipengere itapungukiwa nini? hizo dhana zao wanazotaka kuzifanya kuwa zitatokea wakikiweka hazitotokea ila wasipokiweka ndio nahisi zinaweza tokea. Humu Jf unaweza andika vile ujisikiavyo kuhusu waislam lakini waislam huko mittani wanamsimamo wao.

Sensa bila kuwasikiliza wananchi wanataka nini katika zoezi zima la sensa ni batili. wananchi hawapendezwi na suala linaloendelea la kila kikundi kujitolea takwimu za watu kwa mujibu wa dini zao nawakati serikali ikiegemea upande unaotoa takwimu hewa. Hatukubali na hili zoezi serikali inatengeneza mazingira ya kujiingiza kwenye hasara ya sensa mara mbili mbili.
 
Back
Top Bottom