Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
Kuna mhuni kaja hapa atakuwa ni magamba huyu na kusambaza eti baba yake Selasini katutoka ..Selasin mwenyewe kajibu hivi.
ndio kaiponda JF inawezekana hajui maana ya forums ....[h=6]Pamoja na Shukrani zangu kwa Waheshimiwa Wabunge,Mawaziri,na Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana nami leo katika msiba ya marehemu Mama yangu... Nimeshitishwa sana na Uzushi uliosambazwa kwenye mtandao wa Jamii Forums kuwa Mke wangu na Baba yangu Mzazi nao wamefariki!... Kiukweli huu mtandao si tu unapoteza maana ya THE GREAT THINKERS bali unakuwa wa kihuni!..... Ni mtandao gani huu ambao hauwezi kuth
ibitisha taarifa kabla ya kuziandika public?...
Mtandao unaoandika uzushi wa kuzulia wengine vifo visivyokuwepo ni Mtandao wa ajabu!... Binafsi naomba kuwapa pole waliopata taarifa hizi (Wengine wameniandikia Inbox).. Naomba kuwajulisha kuwa Mke wangu na Baba yangu bado wanaendelea na Matibabu... Tuendelee kuwaombea wapone warejee kwenye majukumu yao kama kawaida!...
Nawatakia Usiku Mwema Ndugu zangu, Mungu awabariki.
Joseph Selasini
Mb. Rombo
Chadema.[/h]