Seif Tumekusikia; Sasa jiuzulu na iondoe CUF kwenye SUK!

Ah hawa hawawezi kutuachia, wanafaidika sana na sisi, lakini wanajifanya hawaoni, wananichekesha hawa, kisha wanajifanya wana confidence! Haya mnatupa ardhi uko bara, sisi tumewapa bahari mtumie mtakavyo, meli zinakuja dar bila ya wasiwasi! Sasa tukijitenga, bahari itakua mtihani kwenu, mana tunaweza kujenga articial islands karibu na katanganyika which will pose a threat! Afu mnapesa zetu nyingi sana nyinyi, kisha hamuna shukrani ata kidogo, bandari ya dar es salaam tumewajengea sisi, yani hamujiweziiiii, mnatuita mdebwedo lakini katika vita mnawaweka wazanzibari mbele, wakishinda mnajisifia nyinyi, ovyooo! Mnaboa kichizi

usiwe mjinga wewe bahari sasa inahusiana vipi na kutengana kwani kabla znz na tanganika azijaungana ina maana meli zilikuwa haziwezi kuja tanganika sababu ya znzbr??mpaka utarudi uleule wa kabla hatujaungana.kuhusu kujenga artificial islands hiyo ni rukhsa na itaendanana int'l law ukivuka kuingia eneo la watanganika tunawachapa au tunawashtaki int'l crt,hamwezi kujenga AI karibu na tznia bara sababu mpaka wenu unajulikana sijui uko chumbe pale sijui chumvini na hamwezi kujaza mchanga utakaoingia kwenye eneo letu sababu kufanya hivo ni kuvunja sheria za kimataifa na mtawekewa vikwazo vya kiuchumi sababu mtaonekana wachokozi.nyie ni kama wetu tu kabisa hamtuwezi.
 
daini mamlaka kamili ya nchi yenu,lakini ya kupoteza vilivyomo mikononi mwenu ambavyo ni haki yenu, halafu mtafute mikataba ya kupata vitu vile mlivyoviachia ni ukosefu wa busara. Muungano wa mkataba is the satanic idea. Unaweza dai mamlaka kamili bila kuvunja muungano wa sasa. Al mizan baba! Wekeni mizani mpime faida na hasara na tumieni vichwa vyenu vizuri kutafuta possible and harmless alternatives.

Tumekuja na wazo la Muungano wa Mkataba ya kuaona nyinyi Watanganyika munachukulia kama ni UHAINI kujaribu kuleta hoja ya kuuvunja Muungano! Rejea vitisho vya Nyerere, Mkapa "hatutomvumilia atakayejaribu kuyachezea Mapinduzi na Muungano", Gombani-Pemba na bila kusahau Hadidu rejea za Kikwete.
 
Kama Dr. Slaa anavyopigania haki na maisha mema kwa watanganyika ndivyo hivyo hivyo Maalim Seif Sharif anavyopigania haki na maslahi ya watu wa zanzibar.
sioni sababu ya kutokea mtu akaanza kumdhihaki maalim Seif wakati anachokipigania kina maslahi na watu anaowaogoza.

.
Mwalimu Nyerere - Videos inayo husiana na muungano
 
Bablii,

..muungano wa mkataba hukuTanganyika na Zanzibar zikiwa wanachama pekee utaendelea kutunyonya tu wa-Tanganyika.

..nyinyi lianzisheni tu kuvunja mkataba kuliko kuja na hoja ya kinafiki na kinyonyaji ya muungano wa mkataba.

..kuweni wawazi ktk vikao rasmi kama mnavyokuwa wawazi kwenye mikutano ya hadhara na mitandao.

..mbele ya tume ya katiba, Jussa alidai ana mifano 100+ ya miungano ya mkataba, huku kwenye mtandao anaandika kuwa EAST AFRICAN COMMUNITY ni muungano wa mkataba.

..kwanini Jussa hakuwa muwazi mbele ya Jaji Warioba na wajumbe wa tume, wakati aliulizwa specifically kuhusu ulinganifu wa muungano wa mkataba na EAST AFRICAN COMMUNITY??

upo sawa Walioba kamuuliza Jusa hakuwa na mfano hata mmoja zaidi ya maelezo. wakubali wasikubali labda nchi hii ichukuliwe na wapinzani kwa CCM watu wao wote wanaowategemea ni ccm wanakula na kuishi vizuri kupitia Muungano. Swala dogo tu amueni wote kwa sauti moja kuwa hamuutaki muungano wala swala la nani anafaidika haliwahusu Tanganyika hawatafaidika wala zanzibar yenu kila nchi itajipanga kivyake individuals wataathirika. Ila kuna mtu Zenji wa kumfunga kengere paka mtaishia maneno tu Muungano huu hamuwezi kuuvunja hapa JF
 
daini mamlaka kamili ya nchi yenu,lakini ya kupoteza vilivyomo mikononi mwenu ambavyo ni haki yenu, halafu mtafute mikataba ya kupata vitu vile mlivyoviachia ni ukosefu wa busara. Muungano wa mkataba is the satanic idea. Unaweza dai mamlaka kamili bila kuvunja muungano wa sasa. Al mizan baba! Wekeni mizani mpime faida na hasara na tumieni vichwa vyenu vizuri kutafuta possible and harmless alternatives.

Sijakuelewa uliposema kama tunaweza tukawa na mamlaka kamili na uku ukabakia kuwepo muungano uliopo.

Kwa uelewa wangu mimi, muungano uliopo umezalisha nchi 1 tu, nayo ni tanzania. Sasa vipi ndani ya nchi kuwepo nchi nyengine? Au muungano uliopo ndugu umeuelewa vipi?

Ni sawa na kusema kuwa tanzania na kenya wameumda nchi moja iitwayo TanKenia, kisha katika UN kuna kiti cha kenya, cha tz na cha Tk, jamaa hii inaingia akilini? Hebu nijibu ndugu yanguuu, ulosema mamlaka kamili inawezekana hata kama muungano uliopo utabaki..... Mhhh
 
usiwe mjinga wewe bahari sasa inahusiana vipi na kutengana kwani kabla znz na tanganika azijaungana ina maana meli zilikuwa haziwezi kuja tanganika sababu ya znzbr??mpaka utarudi uleule wa kabla hatujaungana.kuhusu kujenga artificial islands hiyo ni rukhsa na itaendanana int'l law ukivuka kuingia eneo la watanganika tunawachapa au tunawashtaki int'l crt,hamwezi kujenga AI karibu na tznia bara sababu mpaka wenu unajulikana sijui uko chumbe pale sijui chumvini na hamwezi kujaza mchanga utakaoingia kwenye eneo letu sababu kufanya hivo ni kuvunja sheria za kimataifa na mtawekewa vikwazo vya kiuchumi sababu mtaonekana wachokozi.nyie ni kama wetu tu kabisa hamtuwezi.

Sasa sijui nani mjinga, maana unashindwa kujua matumizi ya bahari, ndio zilikua zinapita meli kabla ya muungano, lakini ujue bahari ya zanzibar is not international waters kwamba utajipitia tu, lazima kuwe na masharti, wewe hujauona umuhimu wa kushare bahari ndo maana waropokwa tu!

Haya mpaka wa bahari wa zanzibar uko wapi? Naona unajifanya unaujua kisha unababaika ooh mara chumbe mara chumvini mara sukarini, vipi mbona unatapatapa? Sijakwambia kama artificial islands zitajengwa katika internal waters zenu, jitizame ulivokuwa mjinga sasa, mimi sijakwambia kama vitajengwa ktk maji yenu nduguuuuu......

Hatukuwezeni kwa kitu gani? Labda kwa kulewa na kudhulumu mali za watu, maana ndo mnavoongoza! Hebu nambie mna kitu gani cha kututisha sisi? Hamuna ata serikali mumo mumo tu duniani..... :-D
 
Sasa sijui nani mjinga, maana unashindwa kujua matumizi ya bahari, ndio zilikua zinapita meli kabla ya muungano, lakini ujue bahari ya zanzibar is not international waters kwamba utajipitia tu, lazima kuwe na masharti, wewe hujauona umuhimu wa kushare bahari ndo maana waropokwa tu!

Haya mpaka wa bahari wa zanzibar uko wapi? Naona unajifanya unaujua kisha unababaika ooh mara chumbe mara chumvini mara sukarini, vipi mbona unatapatapa? Sijakwambia kama artificial islands zitajengwa katika internal waters zenu, jitizame ulivokuwa mjinga sasa, mimi sijakwambia kama vitajengwa ktk maji yenu nduguuuuu......

Hatukuwezeni kwa kitu gani? Labda kwa kulewa na kudhulumu mali za watu, maana ndo mnavoongoza! Hebu nambie mna kitu gani cha kututisha sisi? Hamuna ata serikali mumo mumo tu duniani..... :-D

nafikiri wewe utakuwa na matatizo ya akili kidogo mimi nilishakwambia kabisa mpaka wa bahari kati a znzb na tanganika upo na hata sasa hivi wanajeshi wanaulinda upande wetu na kmkm wanaulinda kwao mpaka wa kimataifa ndi wa muungano tunashirikiana,sasa unasema kati ya unguja na bara hakuna mpaka wapi na wapi??uliza vizuri dogo labda ulikuwa mdogo sana kujua kama kulikuwa na mpaka,sisi wakongwe tunaujua na hata sasa hivi kila mtu anaulinda wake,kuhusu AI mtajenga kwa upande wenu unaoangalia int'l water na sio huu unaoangalia bara au sehemu yeyote ile inayotumika kama njia ya meli mana kisheria za kimataifa hamtaruhusiwa.Elewa hilo ewe mdebwedo mzee wa Ulojo.
 
Tumekuja na wazo la Muungano wa Mkataba ya kuaona nyinyi Watanganyika munachukulia kama ni UHAINI kujaribu kuleta hoja ya kuuvunja Muungano! Rejea vitisho vya Nyerere, Mkapa "hatutomvumilia atakayejaribu kuyachezea Mapinduzi na Muungano", Gombani-Pemba na bila kusahau Hadidu rejea za Kikwete.

lakini kwa nini uvunje muungano, tena baada ya kuwemo humo kwa zaidi ya nusu karne. Wazo la kuvunja muungano bila ya sababu ni la kishetani (the satanic idea). Mlaani huyo shetani, al-mizan baba. Weka mizan mbele pima faida za muungano na usumbufu wa muungano. Halafu tafuta njia za kuepuka usumbufu ambazo hazitokuzuwia kufurahia faida.
 
Sijakuelewa uliposema kama tunaweza tukawa na mamlaka kamili na uku ukabakia kuwepo muungano uliopo.

Kwa uelewa wangu mimi, muungano uliopo umezalisha nchi 1 tu, nayo ni tanzania. Sasa vipi ndani ya nchi kuwepo nchi nyengine? Au muungano uliopo ndugu umeuelewa vipi?

Ni sawa na kusema kuwa tanzania na kenya wameumda nchi moja iitwayo TanKenia, kisha katika UN kuna kiti cha kenya, cha tz na cha Tk, jamaa hii inaingia akilini? Hebu nijibu ndugu yanguuu, ulosema mamlaka kamili inawezekana hata kama muungano uliopo utabaki..... Mhhh
kwani sasa hivi si mnayo hayo mamlaka, kuanzia Raisi, baraza la wawakilishi, mahakama, wimbo wa taifa, kmkm, kikosi cha mafunzo, na bado mpo kwenye muungano.
Nyerere alishaelewa shida za kibinadamu , kwa hiyo aliziweka ili watu mpate kupumua, lakini shida hizo za kibinadamu si katika kumkomboa mwananchi wa ungaja au pemba, labda iwe wale ndugu zetu sultan
 
Sijakuelewa uliposema kama tunaweza tukawa na mamlaka kamili na uku ukabakia kuwepo muungano uliopo.

Kwa uelewa wangu mimi, muungano uliopo umezalisha nchi 1 tu, nayo ni tanzania. Sasa vipi ndani ya nchi kuwepo nchi nyengine? Au muungano uliopo ndugu umeuelewa vipi?

Ni sawa na kusema kuwa tanzania na kenya wameumda nchi moja iitwayo TanKenia, kisha katika UN kuna kiti cha kenya, cha tz na cha Tk, jamaa hii inaingia akilini? Hebu nijibu ndugu yanguuu, ulosema mamlaka kamili inawezekana hata kama muungano uliopo utabaki..... Mhhh

nitakujibu, lakini usinipandishie jazba. Mimi ni mtu mzima na sistahili wala sistahiki matusi ya mtandaoni. Unaipenda SUK enhe. Kiti si wanakalia wote,mamlaka wana share. Ndiyo maana yake wazanzibari tumeamua hivyo. Watanzania na tuamue kwa dhati. Kiti cha UN tuendelee kukalia sote. Nusu kiti paja la tanganyika na nusu nyengine paja la znz.
 
Tumekuja na wazo la Muungano wa Mkataba ya kuaona nyinyi Watanganyika munachukulia kama ni UHAINI kujaribu kuleta hoja ya kuuvunja Muungano! Rejea vitisho vya Nyerere, Mkapa "hatutomvumilia atakayejaribu kuyachezea Mapinduzi na Muungano", Gombani-Pemba na bila kusahau Hadidu rejea za Kikwete.

lakini kwa nini uvunje muungano, tena baada ya kuwemo humo kwa zaidi ya nusu karne. Wazo la kuvunja muungano bila ya sababu ni la kishetani (the satanic idea). Mlaani huyo shetani, al-mizan baba. Weka mizan mbele pima faida za muungano na usumbufu wa muungano. Halafu tafuta njia za kuepuka usumbufu ambazo hazitokuzuwia kufurahia faida.
 
lakini kwa nini uvunje muungano, tena baada ya kuwemo humo kwa zaidi ya nusu karne. Wazo la kuvunja muungano bila ya sababu ni la kishetani (the satanic idea). Mlaani huyo shetani, al-mizan baba. Weka mizan mbele pima faida za muungano na usumbufu wa muungano. Halafu tafuta njia za kuepuka usumbufu ambazo hazitokuzuwia kufurahia faida.

Kule Ulaya kuna nchi zimeungana zaidi ya miaka 200 nyuma na hivi sasa wanataka kuitisha kura ya maoni ya kukubali ama kukataa hivyo kwa nini Muungano huu ambao una miaka 48 usijadiliwe?
Wewe kama unasema kuwa na wazo la kuvunja Muungano ni Mawazo ya kishetani sisi Wazanzibari tunasema kuendelelea kubaki katika Muungano huu ni Ushetani na ni Dhambi hata mbele ya Mungu Muumba, na ndio maana katika ukusanyaji wa maoni hata watoto wa miaka 8 bila kusahau wazee wenye miaka zaidi 90 wanajitokeza kutaka Muungano wa Mkataba (Kwa vile mulijifanya Wakoloni tunaamini Mkataba utawashinda njiani) hivyo Muungano utavunjika tuu. Wewe endelea kubaki na akili zako za samaki sisi tunatia nyavu baharini!!
 
Binafsi nimezaliwa late 70s, nikakuta Nchi inaitwa Tanzania, nimesoma jina Tanganyika kwenye vitabu vya historia,..lakini kwa kutumia intellectual aweress naweza..... .... kukuta jina Tanzania kama TAIFA LETU.

Ila sijui umri wako wewe unae dai TANGANYIKA wakati unajua dhahiri tume ya marehemu Jaji Nyarari ilipita wakati kizazi komavu cha kujenga TAIFA sekta zote za uchumi, utamaduni kikiwa ni mababa zetu waliosoma baadhi elimu ya Tanganyika inapata uhuru,chukulia mimi Mama yangu kazaliwa nae Tanzania hivi ukiniambia TANGANYIKA brother Taso sikuelewi eti!!!!.Hivyo kwa wao kudi Tanganyika hiyo unayoizungumzia wewe ilikuwa sawa kwa kuwa hata jina wao walilolikuta ni Tanganyika.

Taso fanya utafiti mdogo Tanzania bara nenda katafute makundi ya vijana umri kuanzia +15 na kuendelea mpaka -41 kisha ongea nao habari za TAIFA hilo unalolizungumzia habari yake yani Tanganyika,...!

Ndugu DSN

Intellectual awareness yako inakufanya ufahamu kuwa baada ya kuzaliwa/kuundwa Muungano 1964 (Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar) na hata pale muungano huu ulipobadilishwa jina na kuitwa Muungano wa Tanzania (Jamhuri ya muungano wa Tanzania) awareness hiyo inakufanya pia uelewe kuwa ilizaliwa nchi/sehemu inayoitwa Tanzania bara?

Kama hii intellectual awareness inakushawishi ukubali ukiini macho, je Mafia ni Tanzania bara? Ukerewe je?
Tanzania visiwani itakuwa ni wapi?

Kaswali kadogo! Je Tanzania ni muungano wa nchi ngapi? Tafadhali zitaje.

Je katika dunia hii kuna muungano ambao ulifuta majina ya nchi wanachama wake?

Majibu yako yatasaidia kukurudisha katika intellectual awareness na kugundua kuwa kuna mazingaombwe/ukiini macho umefanyika.

Ukigundua kuwa umefanyika, jiulize kwa nini waliamua kufanya hayo mazingaombwe.

Pia pitia hii mada link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/334649-tundu-lissu-na-kiini-macho-cha-muungano-12.html
 
Bablii, Wnz wanaoingia Tanganyika ni kwasababu ya muungano. Ndio maana tunasema nje ya muungano hilo halitakuwepo nakitakachotambuliwa ni kitambulisho na kufuata tarataibu kama Mganda, Mkenya au Mchina. Period.
(2) Unazidi kutusadia hoja kuwa uchumi wa ZNZ unatgemea soko la Tanganyika. Nje ya muungano fursa ya bidhaa hizo itakuwa ya masharti kama ilivyo na nchi za jirani. Hakuna anayeweka vitisho, ni ukweli kuwa muda wa kubeba mabegi kwa hiari au lazima unakaribia. Muda huo uliokaribu sana utawakuta Waznz wengine wakivuka bahari kwa miguu.

(3)Kuingia katika muungano kumewasaidia sana wazanzibar. Wasomi wote na viongozi wote waliopo sasa akiwemo Maalim Seif na Jusa wamesoma Tanganyika bure. Znz haijawahi kuwa na bajeti ya elimu ya juu tangu mwaka 1964 kama ilivyo bajeti ya jeshi. Kwa mantiki hiyo muungano ni faraja vinginevyo Maalimu Seif angekuwa mvua samaki maarufu.

(4)Kwavile soko la ZNZ ni Tanganyika haiwezekani bidhaa ziteremkie ZNZ halafu ziingie Tanganyika bure. TRA watachukua kodi kama wanavyochukua Namanga, mbeya, au Kigoma. Kama wafanyabiashara wa ZNZ wanaona uonevu basi wauze bidhaa zao kwa soko la watu laki moja. Midhali wanataka soko la watu milioni 40 lazima walipe kodi kwa hiari au kwa lazima, kinyume cha hapo makontena yasivuke chumbe. Hapa pia unatusaidia kuainisha faida za muungano ZNZ.

(5)Mtaachwa mpumue mkiamua kumuunga mkono Maalim Seif mjitoe(sio mkataba), I mean mvunje muungano. Midhali bado mpo mgongoni mwa Tanganyika mtabanwa na mbeleko iwe kwa hiari au kwa lazima. Kwa mantiki hiyo tumewafungulia vitabu vyote vya kujitoa katika muungano, hamtaki! tuwasiaideje ili mpumue?

Pengine ulikuwa bado mdogo, OIC ikija Nyerere hakuwepo madarakani. Aliyekuwa kiongozi ni Mwinyi.
Wabunge wa ZNZ walikataa hoja ya serikali 3 hawakuuliza OIC. Maalim Seif alikuwa kiongozi ndani ya CCM na SMZ hakuuliza kwanini. Maalimu alikuwa bize kumchongea Mzee Jumbe ili apate Urais(mungu mkubwa hakupata na hatapata)

(6) Masimulizi ni kitu kibaya sana hasa kama huelewi unasimuliwa nini. Bablii, kulikuwa na PBZ. Aliyehamishia shughuli za PBZ kwenda BOT ni Ali Hassan Mwinyi. Halafu rejea katika historia ya UDSM kwanza kabla hajarudi hapa.

Kama madai yako ni kuwa kuvunjika kwa muungano itabidi kila kitu pasu hizo ni ndoto ima za mchana au hujui unachoandika.

Kumbuka kuwa katika fidia hiyo Maalimu Seifa na Jusa nao itabidi tuwadai ada za kusoma bure achilia SMZ yote iliyosomea Tanganyika bure.

Muhimu hapa ni kuwa itabidi tuangalie kila kitu. ZNZ haijawahi kuwa na bajeti ya elimu ya juu, ulinzi na mambo ya ndani.
ZNZ haina deni la nje wala la ndani,yote ni mzigo wa Tanganyika.

Muungano ukivunjika leo ni makosa kuidai ZNZ chochote kwasababu kufanya hivyo ni kumkamua ng'ombe tasa ukitegemea maziwa.

Nikukumbushe kuwa ZNZ haijaweza kulipa wafanyakazi wake mishahara tangu Salim Amour alipoingia madarakani hadi leo.
ZNZ haijaweza kulipa bili ya umeme tangu waya umefungwa hadi leo.

Hesabu za kukuonyesha jinsi gani uchumi wa ZNZ usivyo ruhusu kudaiwa hata senti tano.
BOT imetoa taarifa, makusanyao ya mwezi ya ZNZ katika kodi ni sh bilioni 10.
Kwa mwaka ni bilioni 120 kwa hesabu za makadirio.

Bajaeti ya ZNZ ni sh bilioni 630 kwa maan nyingine sh bilioni 520 ni ruzuku kutoka Tanganyika.
Sasa kwa uchumi kama huo ni tusi kumdai Mzanzibar. Tunachotaka waondoke na madeni yote ni ya Tanganyika.

Wakileta ujinga wa kugawana tutawapa bajeti ya jeshi tu ambayo yenyewe ni kubwa kuliko ya SMZ.
Hata kama ZNZ italipa 1/4 ZNZ itakuwa haina hata senti tano ya kumlipa mshahara Rais wao kwa miaka zaidi ya 10.

BOT inasema makusanyo ya kodi ya Tanganyika ni bilioni 790 kwa mwezi, yaani mwezi mmoja ni bajaeti ya SMZ kwahiyo neno pasu ni tusi na usilitumie tena. Pasu ya kitu gani?

Na mwisho usisahau kuwa mafao ya wastaafu akiwemo Maalim Seif, Nasoro Moyo, Mwinyi na Familia, Jumbe na Familia, Karume na Familia achilia wachovu wengine yanatoka Tanganyika.

Unaposema Tanzania una maana Tanganyika kwasababu bilioni 120 za mwaka mzima ZNZ haziwezi kuendesha idara ya akina mama na watoto. Ukipewa heshima ya kuwa mshirika, basi kuwa na adabu ati.

Ujumbe muhimu ni kuwa muda umekaribia, tutaachana kwa wema na tutawaaga bandarini mkiwa na mabegi na mifuko ya rambo tu. Hilo ni kwa hiari au lazima kwasababu utakapotimu wakati hamtakauwa na ujanja tutachukua nchi yetu Tanganyika na kila kilichomo. Trust me! it's on the way tunasubiri muda.

Huo ni ukweli na si vitisho, si mumeanza kuchoma Watanganyika moto, mbona. Waliofanya hivyo wapo huru sasa kipi cha jabu. Kama kuna mznz anayefikiri kuwekeza Tanganyika ni lazima afikiri mara 2 kwasababu tulipofika hakuna mwamana!

Tupo tayari kuwalipa kila manachodai na halali kwenu, tutachukua madeni yote na kuwaacha bila deni.
Lakini basi tutawataka muondoke mara moja ili mkachukue vibali vya kurudi Tanganyika. Muondoke na mabegi maana hamkuja na kitu kingine. Mtaondoka kwa lazima au hiari kwasababu mumeshatoa somo ns tumejifunza. Inakuja Bablii,soon sio vitisho ni ukweli.

Nimesoma hayo matapishi yako hapo juu sioni point hata moja...zaidi nnachokiona naona mtu wa kijiweni anaongea bila kujuwa anachoongea!

1. WaZanzibar wanakuja Tanganyika bila vibali sababu ya Muungano kama vile waTanganyika wanavyokuja Zanzibar! Sioni anae mbeba mwenzake! Muungano ukivunjika waZanzibar waliopo Tanganyika watafanya kazi na biashara huko Tanganyika kwa vibali, kama vile wale waTanganyika walipo Zanzibar watakavyofanya kazi kwa vibali maalum kutoka Zanzibar!

Kuhusu kusema eti Zanzibar inafaidikia kwa soko la Tanganyika kwa sababu wao ni laki 2....sio hoja ya kisomi! Mbona China wanafaidika na soko la Tanzania, kuanzia K.koo mpaka kibororoni bidhaa za mchina zimejaa, Jee wao wameUngana na Tanganyika? Hata muungano usingekuepo, nyinyi kwa wingi wenu (48+ million) mngehitaji bidhaa kutoka Zanzibar, wala tusingewafuata mngekuja wenyewewe! Bila muungano biashara bidhaa zingeingia Tanganyika, kama zinavyoingia za kenya, India, china n.k! Sioni itakachokosa ZANZIBAR!

Eti wasomi wa KiZanzibar wa hivi sasa wamesomeshwa na Tanganyika! Huu ni ufedhuli mkubwa! Hakuna chuo kikuu hata kimoja cha Tanganyika, vyuo vikuu vyote ni vya Tanzania (nchi mbili zilizo ungana, Tanganyika na Zanzibar), wasomi hao, akiwemo Seif wamesoma kwa kodi za WaZanzibar wenzao, waliochangi a katika kuvijenga na kuviendeleza vyuo vikuu hivyo! Utakapovunjika muungano tutagawana pasu pasu, tuliungana kama nchi mbili huru (regardless ukubwa wa maeneo), kila ncho nna haki sawa juu ya nchi nyengine.

Zanzibar ilibanwa isijenge vyuo vikuu vyake sababu, pesa yake yakujenga vyuo hivyo ilikuwa inakwenda kwenye kujenga na kuendeleza vyuo vikuu vya Tanzania vilivyoko kwenye ardhi ya Tanganyika (UDSM, UDOM,SUA, MZUMBE etec).

Wee inaonekana hujui chochote kuhusu siasa za Zanzibar na Tanzani, umeijuwa siasa 2010 kupitia CHADEMA! ishu ya OIC ilikuja wakati Dr.Salmin Amour akiwa rais wa ZANZIBAR (1992/93), Maalim Seif wakati huo hayupo tena kwenye uonogzi wa serkali wala CCM, wala si manachama wa CCM! Aliezuia hoja hii ni Nyerere, yeye alijiuzulu urais na uenyekiti wa CCM kwa nadharia tu, kivitendo ndie aliekuewa na maamuzi ya mwisho!

Kuhusu Bajeti ya jeshi au elimu ya juu, jibu unalo, hivyo vyote ni vya muungano, Zanzibar inaweka fedha zake kwenye JWTZ na Elimu ya juu kwa Tanzania. Haipati service hizo kutoka kwa Tanganyika, inagharamia service hizo kwa fedha zake. Hivyo wakati unalialia eti Zanzibar haina budget ya jeshi na elimu, ujuwe kwamba na TAANGANYIKA vile vile haina bajeti ya Jeshi, elimu, biashara, mambo ya nje, n.k!Au unieleze ni wapi bunge la Tanganyika linakutana kupanga bajeti za wizara hizo? Lini walipanga bajeti? Tunawabeba hapo hapo kwenye Bunge la MUUNGANO ndipo tunapowapangia bajeti ya viwizara vyenu visivyo vya muungano, lakini hapo hapo kwenyebunge la muungano ndio tunapopanga bajeti za wizara za muugano ikiwemo Jeshi! Muungano ukivunjika mtaanza mwanzo (starting from scratch)!

Mna hasara kubwa sana! Uchumi wenu utaanguka balaa, maana kila mnachokiona hivi sasa under the name Tanzania, mtapata nusu yake tu! Yet, wafanyabiashara wa kiZanzibar wengi watarudi ZANZIBAR, na kama mtajaribu uwafukuza (kama alivyofanya Iddi Amin kuwafukuza wahindi), basi zile zama za kula dona la njano itarudi! Mtabaki na ufisadi wenu unaowatafuna!

Eti hatulipi bili, sijui mishahara, ndio si sababu ya huu muungano...we ndo unaeongeza uzito hoja ya kudai ZANZIBAR huru, njia zote za Uchumi mmeziviza, kwa jina la muungano! Halafu unalalamika hatulipi umeme, ebo! Tuwachieni nchi yetu basi, kwanini ung'ang'anie nchi isiyokupa faida! Kwanini msiende kuungana na Uganda, Kenya, Rwanda au Burundi mkapata faida! Iweje wewe unaebeba ndo unang'ang'ania kubeba, lakini aliebebwa hataki tena kubebwa, anadai umshushe, hutaki!!! Halafu bado walalamika ebo! Ujuha huu!

Kama hali ni hivyo unasema, waTanganyika nendeeni kwenye tume ya maoni, mkaseme MUUNGANO UVUNJIKE wa ZANZIBAR wanaTunyonya! Muone waZANZIBAR watakavyo wafurahia na kuwa support! Ajabu nyinyi ndo hata kuzungumzia muuungano hamutaki, ndo kwanza wengine wanadai we serkali moja! So what? Ikiwa serkali moja ndo Wazanzibar wataweza kuwalipa bili za umeme, ndo wataacha kuwa nyonya? Hii nikuonesha kwamba kwenye muungano huu nyinyi mnanufaika zaidi, na sasa mnatamani muimeze Zanzibar yote..lakini yaguju!
 
Hata kwenye mpira tumeanza kuwatenga na kuwafunga bila ya huluma.
 
Hayo niliyokujibu, yanachipukia kwenye hiyo quote hapo juu. Tatizo unapost bila hata kujua wapi umesema nini na lini! Mimi sio mwana mipashe, matusi nakuachia wewe uwanja uendelee kudhalilisha wazazi wako jamvini kuwa hawakukufundisha maadili ya kuishi na watu kistaarabu.

Unaumwa wewe. tena una wazimu sana. Ulipaswa kuanzia mwanzo wa mjada na sio kukurupuka kama magugu ya kiangazi. Hebu angalia kwanza nimemjibu huyo kwa lipi aliloliongea. Au ni wewe una ID mbili sasa unajichanganya?
 
Na kama hawataki Muungano,waje wamchukue na Bilal wamrudishe Zenj...
Na inasadikika Maalim anaishi Dar,kama vp nae afungashe virago aondoke

Hawa wachuma karafuu wana matatizo sana. Tanganyika wanaipenda kweli kweli hata Makamu wa Kwanza wa Mkuu wa Mkoa (Seif Sharif Hamad) wao anakaa huku. Wanatumika na anayewatuma hawamjui, full kuhangaika
 
Back
Top Bottom