Nobunaga
JF-Expert Member
- Mar 22, 2019
- 1,169
- 4,986
Utapeli wa mtandaoni ndiyo habari ya mjini kwa sasa. Kuna aina nyingi sana huu utapeli wa huko mitandaoni. Ukiachana na wale wazee wa "Hiyo pesa tuma kwenye namba hii", kuna huu utapeli mpya ulioingia wa kuwakusanya vijana kisha kuwaaminisha kuna kampuni fulani inatoa commission unapofanya mambo flani flani huko online, ila kujiunga lazima uwe na kianzio kiasi kadhaa.
Hivi majuzi tuliona habari iliyorushwa na ITV kupitia kipindi chao cha "Ripoti Maalumu" ambapo walionesha makundi kwa makundi ya vijana waliosombwa huko vijijini na kupelekwa Dar wakiaminishwa kuna biashara mtandao wanayoenda kufanya ambayo itawapatia utajiri ndani ya muda mfupi.
Baada ya hiyo kampuni hewa ya utapeli kuumbuliwa sasa kuna kampuni nyingine ya utapeli wa aina hiyo inayoibukia kwa kasi kwenye miji mbalimbali hapa nchini, huku waathirika wakubwa wakiwa na vijana.
Hizi kampuni zipo nyingi sana, lakini hii ndiyo ambayo naona imeshika kasi maana nimekutana na watu kadhaa walionishawishi nijiunge, huku wakiwa hawajui tayari wameshatapeliwa.
Hivyo kama una ndugu au rafiki ambaye yupo kwenye huu msururu wa Kalynda Investment basi muambie wanaenda kupigwa za uso mchana kweupee, hakuna biashara ya namna hii, wote wataishia kutapeliwa pesa zao tuu.
------------------
FEEDBAKS ZA WADAU
Hivi majuzi tuliona habari iliyorushwa na ITV kupitia kipindi chao cha "Ripoti Maalumu" ambapo walionesha makundi kwa makundi ya vijana waliosombwa huko vijijini na kupelekwa Dar wakiaminishwa kuna biashara mtandao wanayoenda kufanya ambayo itawapatia utajiri ndani ya muda mfupi.
Baada ya hiyo kampuni hewa ya utapeli kuumbuliwa sasa kuna kampuni nyingine ya utapeli wa aina hiyo inayoibukia kwa kasi kwenye miji mbalimbali hapa nchini, huku waathirika wakubwa wakiwa na vijana.
Hizi kampuni zipo nyingi sana, lakini hii ndiyo ambayo naona imeshika kasi maana nimekutana na watu kadhaa walionishawishi nijiunge, huku wakiwa hawajui tayari wameshatapeliwa.
Hivyo kama una ndugu au rafiki ambaye yupo kwenye huu msururu wa Kalynda Investment basi muambie wanaenda kupigwa za uso mchana kweupee, hakuna biashara ya namna hii, wote wataishia kutapeliwa pesa zao tuu.
------------------
FEEDBAKS ZA WADAU