Sauti ya wengi sio sauti ya Mungu. Huu msemo ni kuchanganya dini na siasa

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,586
15,370
kuna msemo wa kirumi Vox Populi Vox dei ( Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu).

Huu msemo ni sahihi kisiasa sio kidini au kiimani. Wanasiasa walitumia huu msemo kujihalalishia mambo yao hata kinyume cha Mungu na wengine ilikula kwao. Sasa ni aibu kwa kauli hii kusikika kwa watu wa dini. Ibaki kutumika katika mimbari ya kisiasa sio dinini.

Ushahidi
Nebukadneza Sauti ya wengi ilimjaza na akajiona mungu. Mungu alimpa adhabu ya kuishi porini na wanyama miaka saba hadi kiburi kiliposhuka.

Sauti ya wengi ndio ilimkataa Samweli aloyetumwa na Mungu, na kutaka waisrael watawaliwe kama mataifa mengine kisiasa.

Sauti ya Wengi ingekuwa ya Mungu, basi Nuhu na familia yake ndio wangekufa kwa mafuriko huku wengi wakiokolewa na safina.

Sauti ya wengi ya kumsifu Herode ilimsabajishia apigwe na chango akafia kwenye mimbari za kisiasa huku waliomsifu wamemkimbia.

Wengi waliwahi kusema afunguliwe jambazi Baraba na asurubiwe Yesu Yusuph aliyewafufulia watoto wao na kuwatoa mapepo yaliyowatesa.

Sauti ya wengi ni sauti ya hao wengi sio lazima iwe sauti ya Mungu. Linaweza kuwa kundi la wengi waliopotoshwa au wenye maslahi jifichi kwa kumpakazia Mungu kuwa sauti zao ni sauti yake.

Ni hayo tu waungwana.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki afrika kusini mwa jangwa la sahara.
 
kuna msemo wa kirumi Vox Populi Vox dei ( Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu).

Huu msemo ni sahihi kisiasa sio kidini au kiimani. Wanasiasa walitumia huu msemo kujihalalishia mambo yao hata kinyume cha Mungu na wengine ilikula kwao...
Kwa mifano yako inaonyesha dhahiri namna Mungu anavyosikiliza na kuheshimu sauti ya wengi maana katika mifano yako yote sauti ya wengi ilishinda......sasa Kama Mungu anasikiliza sauti ya wengi nyie ni kina nani
 
Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu … watu wakisema usulubiwe , utasulubiwa tu hata kama huna hatia…
 
kuna msemo wa kirumi Vox Populi Vox dei ( Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu).

Huu msemo ni sahihi kisiasa sio kidini au kiimani. Wanasiasa walitumia huu msemo kujihalalishia mambo yao hata kinyume cha Mungu na wengine ilikula kwao. Sasa ni aibu kwa kauli hii kusikika kwa watu wa dini. Ibaki kutumika katika mimbari ya kisiasa sio dinini.

Ushahidi
Nebukadneza Sauti ya wengi ilimjaza na akajiona mungu. Mungu alimpa adhabu ya kuishi porini na wanyama miaka saba hadi kiburi kiliposhuka.

Sauti ya wengi ndio ilimkataa Samweli aloyetumwa na Mungu, na kutaka waisrael watawaliwe kama mataifa mengine kisiasa.

Sauti ya Wengi ingekuwa ya Mungu, basi Nuhu na familia yake ndio wangekufa kwa mafuriko huku wengi wakiokolewa na safina.

Sauti ya wengi ya kumsifu Herode ilimsabajishia apigwe na chango akafia kwenye mimbari za kisiasa huku waliomsifu wamemkimbia.

Wengi waliwahi kusema afunguliwe jambazi Baraba na asurubiwe Yesu Yusuph aliyewafufulia watoto wao na kuwatoa mapepo yaliyowatesa.

Sauti ya wengi ni sauti ya hao wengi sio lazima iwe sauti ya Mungu. Linaweza kuwa kundi la wengi waliopotoshwa au wenye maslahi jifichi kwa kumpakazia Mungu kuwa sauti zao ni sauti yake.

Ni hayo tu waungwana.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki afrika kusini mwa jangwa la sahara.
Faida za kisiasa zimekufanya uwe muasi.
 
kuna msemo wa kirumi Vox Populi Vox dei ( Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu).

Huu msemo ni sahihi kisiasa sio kidini au kiimani. Wanasiasa walitumia huu msemo kujihalalishia mambo yao hata kinyume cha Mungu na wengine ilikula kwao. Sasa ni aibu kwa kauli hii kusikika kwa watu wa dini. Ibaki kutumika katika mimbari ya kisiasa sio dinini.

Ushahidi
Nebukadneza Sauti ya wengi ilimjaza na akajiona mungu. Mungu alimpa adhabu ya kuishi porini na wanyama miaka saba hadi kiburi kiliposhuka.

Sauti ya wengi ndio ilimkataa Samweli aloyetumwa na Mungu, na kutaka waisrael watawaliwe kama mataifa mengine kisiasa.

Sauti ya Wengi ingekuwa ya Mungu, basi Nuhu na familia yake ndio wangekufa kwa mafuriko huku wengi wakiokolewa na safina.

Sauti ya wengi ya kumsifu Herode ilimsabajishia apigwe na chango akafia kwenye mimbari za kisiasa huku waliomsifu wamemkimbia.

Wengi waliwahi kusema afunguliwe jambazi Baraba na asurubiwe Yesu Yusuph aliyewafufulia watoto wao na kuwatoa mapepo yaliyowatesa.

Sauti ya wengi ni sauti ya hao wengi sio lazima iwe sauti ya Mungu. Linaweza kuwa kundi la wengi waliopotoshwa au wenye maslahi jifichi kwa kumpakazia Mungu kuwa sauti zao ni sauti yake.

Ni hayo tu waungwana.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki afrika kusini mwa jangwa la sahara.
Kama hayo yote yalitimia kutokana na sauti ya wengi, likiwamo la Yesu kusulubiwa, basi ni sauti ya Mungu kwa kuwa huo ulikuwa ni utaratibu wake wa kutimiza unabii. Bila hivyo unabii ungetimiaje?
 
Habari wanajamvi,

Bila shaka sote tumesikia kinachojiri kuhusu watu ama vikundi vya watu kuamaua kupotosha hoja za msingi kwa makusudi yao. Hivi karibuni kumekuwa na hoja ya Baraza la maaskofu wa katoliki (TEC) wakidai kuwa mkataba wa bandari na DP World ufutwe kwa kile wanachosema watuwengi wanapinga. Na isitoshe wametumia msemo wao maarufu wa "sauti ya wengi ni sauti ya Mungu".

Ukizingatia kwa makini kama wewe ni muumini wa maandiko Matakatifu, hususani Biblia, utagundua kasoro kubwa kwenye hoja hiyo. Hii hoja inapingwa na kisa cha wana Israel wawili ( Yoshua na Kalebu) waliosimama imara kuwahamasisha wenzao wavuke hadi nchi ya ahadi (kanani) kwa kuwa Mungu atawapigania. Wengi walikataa wakisema ile nchi ina majitu na wakataka kuwapiga mawe Yoshua na Kalebu. Nini kilitokea? Mungu alisimama na hawa wawili na kuwaadhibu wengi. hivyo si lazima sauti ya wengi kuwa sauti ya Mungu.

Vile vile Bwana Yesu alipokamatwa na kuteswa, ni wachache tu walimuunga mkono, wengi walipaza sauti "Asulubiweeee" na kweli alikusulubiwa. lakini siku ya tatu alifufuka na wengi walishikwa na butwaa kwani hawakuamini.Je wale wengi waliosema asulubiwe ni sauti ya Mungu? la hasha.

Kwa hoja hizi, waraka wa dhehebu la katoliki ni mufilisi unapswa kutupiliwa mbali na kupuuzwa.

karibuni tujadili kwa hoja.
 
Sawa hata ikiwa sauti ya shetani, sisi tunachotaka ni maboresho kwenye mkataba.

Kwani kwenye biblia ni wapi wameandika nendeni mkaingie mikataba mibovu ya kuligharimu taifa?
 
Mule TEC wanazungumzia Mkataba na DP world, wewe unazungumiza walaka wa TEC. Hauoni kama mnazungumzia vitu viwili tofauti.
Anashangaza mno. Watu waliobobea kwenye Biblia Takatifu zaidi ya 30 wamekubaliana kuweka kauli mbiu hiyo, huyu ni nani mpaka awakosoe?
 
hili sakata mpaka sasa limefanya niamini bado kuna kundi kubwa la watanzania bado ni manduza sana.

elimu ya sekondari ya juu ifanywe elimu ya msingi pia.
 
Anashangaza mno. Watu waliobobea kwenye Biblia Takatifu zaidi ya 30 wamekubaliana kuweka kauli mbiu hiyo, huyu ni nani mpaka awakosoe?
Ubobezi kwenye Biblia ni pale unapotumia hiyo Biblia kujenga hoja na sio kuleta siasa kama hao maaskofu walichofanya. kimsingi Roma wameonyesha wao sio dhehebu la kikristo bali ni kikundi kinachohitaji kushika dola.
 
Back
Top Bottom