Samweli Sitta aanza kazi kwa kukiuka kanuni za bunge la katiba

Nevioti kama wewe ni msomi wa sheria tafadhali jibu swali kwa kufuta kanuni za kisheria. Nadhani mie ambaye sijasoma kabisa sheria na wala sijui sheria ninadhani ungepaswa kwanza kunukuu hiyo kanuni ya 85 uonyeshe inampa mwenyekiti mamlaka kiasi gani. Pili unukuu kanuni ya saba na vipengele vyake ndipo uonyeshe jinsi kanuni ya 85 ilivyotumika kutengeua kanuni ya 7 na vipengele vyake. Baada ya hapo ndipo uonyeshe jinsi hoja ya Samwel Sita iliyoenea au kutokuenea kwa hoja husika. Lakini unapojibu hoja kama muuzaji wa nyanya na kudai kuwa unayo CV nzito ya shahada ya uzamili hapo unanipa kutilia wasiwasi elimu yako hiyo.

Duu aise mkuu umemchanachana jamaa na ka mastaz kake kiungwana kabisa. Safi sana
 
Hapo kwenye bold ---Hatuko hapa kubishana nani anajua sheria zaidi kati yako na mimi kwakua hata wewe hujui mimi ni nani na cv yangu na hakuna haja ya kujua hayo maana hayatakusaidia lolote. Aidha, sihitaji kujua una elimu gani ya sheria ila ninachoangalia ni hoja yako. Nikuambie tu kwa ufupi kwamba mimi nina shahada ya uzamivu katika sheria kutoka chuo kikuu cha HUMBOLDT kilichopo Berlin Ujerumani. Katika andiko lako hapakua na hoja ya msingi na kama umesoma kanuni za bunge maalum kwa ufasaha basi ungeelewa kwamba SITTA hajakiuka KANUNI YOYOTE. Nakusihi tu kwamba si afya kupotosha watu hapa hasa katika kipindi hichi muhimu ambacho taifa letu liko katika mchakato wa mabadiliko ya katiba. Tanzania Kwanza, Tanzania Milele!!!!!!!!!!!!

Hujajibu kama mwanasheria ila kama mwanamipasho kwenye jukwaa la maigizo
 
Unaposema haipo mezani una maana gani hasa? kwamba wajumbe wa bunge maalumu la katiba hawana rasimu? acha kukariri wewe, hizo ni protocol tu maana hata rais asipozindua, hakuna athari hata moja.
Kabisa kabisa ingekuwa ni wehu wa hali ya juu rais anazindua bunge hata rasimu haipo mezani sijui ingekuwa kitu gani.
 
Sina imani nae huyu. Huwa anafanya kazi kwa sifa.na ni mbaguzi. Wabunge alokua hapatani nao alikua hawapi nafasi au akiwakatisha.
Time will tell
 
NEVIOT, kama ni kweli umesoma sheria kama unavyodai hungeandika point ya kipuuzi kama ulivyoandika katika jibu lako la awali, eti;

My God, are you serious? Unaelewa jukumu la bunge la Katiba? Hizo ratiba zingine anazoweza kuwa nazo Raisi zikawa na umuhimu kupita kuzindua Bunge la Katiba ni zipi? Kwa mtu anayedai eti kasomea sheria, this logic is more than ridiculous...it is stupid. Je ilitokea ghafla tu akatakiwa kuzindua hilo Bunge au ni jambo limepangwa kwa muda mrefu, hii hasa ndio thinking ya usanii/uswahili uliotufikisha Watanzania hapa tulipo, it is pitiful...na nakuapia kitu kama hiki kinaweza kutokea tu katika nchi yenye watu kama NEVIOT, anayesemekana kusomea sheria chuo kikuu cha HUMBOLDT Ujerumani. Samahani mods kwa lugha kali lakini ni vigumu kwangu kuuita ujinga werevu.

I am sorry, I don't have time for you!!
 
Back
Top Bottom