Samuel Sitta aunda Kamati ya maridhiano ya kuwasikiliza waliopiga kura za HAPANA

only83

JF-Expert Member
Oct 15, 2010
5,343
2,525
Katika hali ya kuonekana kuanza kukwama kwa katiba, M/kiti wa bunge la Katiba nduguSamuel Sitta ameunda kamati ya maridhiano kwa ajili ya kujadiliana na wale waliosema HAPANA. Hii ni njia ya kutafuta 2/3 ya kura.

Wadau, amani iwe kwenu.

Muda mfupi uliopita, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Sammuel Sitta ameunda kamati ya Mashauriano yenye Wajumbe 9 kuwasikiliza Wabunge wa BMK waliopiga kura ya HAPANA kwa Ibara zote siku ya Jana na leo. Anasema kuwa hiyo ni kwa mujibu wa Kanuni ya 36. Anasema kuwa kati ya wajumbe waliopiga kura za Hapana, Wajumbe wawili wameomba kusikilizwa. Kutokana na hali hiyo analazimika kuunda kamati hiyo ambayo amesema kuwa itaongozwa na Makamu Mwenyekiti Samia Suluhu Hassan. Wajumbe wengine ni;

  1. Rashid Mtuta
  2. Omar Yusuph Mzee
  3. Shamsi Vuai Nahodha
  4. Abood Mohamed
  5. Andrew Chenge
  6. Dr. Asha Rose Migiro
  7. Dr Francis Michael na
  8. Hassan Ngwilizi
Anawataka wajumbe kukutana mara moja ili wawasikilize wabunge walioomba kusikilizwa. Tuvute subira na kila kitu kitakuwa wazi kupitia mtandao huu wa Jamiiforums
 
Kaunda kamati ya mashauriano kutokana na kura za hapana,ni wazi amesoma ishara akajua zikiwekwa mezani biashara imekwisha,kaunda kamati kuwashauri,tuwaombee wagome ushauri mpaka kieleweke .
 
Wakishajadiliana wanaweza kubadili kura walizopiga before ?? Nasikia kuna waliopiga Hapana wazi jana leo wamepiga kura ya siri.
 
...Katika hali ya kuonekana kuanza kukwama kwa katiba, m/kiti wa bunge la katiba ndugu Sitta ameunda kamati ya maridhiano kwa ajili ya kujadiliana na wale waliosema HAPANA. Hii ni njia ya kutafuta 2/3 ya kura.

Hata akifanya hivyo sisi wenye akili zetu tumeishapiga mahesabu na sidhani kama katika sheria za upigaji kura kuna kurudia hivyo hayo maridhiano anayoyatafuta sielewi lengo lake.
 
Hivi kanuni zinasemaje? Kwamba mtu baada ya kupiga kura kesho yake anabadili uamuzi akipenda? Kumbe waliosema Dodoma unaofanyika ni utapeli mtupu hawakukosea.

kama ulipata shinikizo kufanya hivyo, ukihakikishiwa usalama kwa nini usibadili uamuzi.
 
Salaleeeeeeeeeeeee..............Mie nilidhani counseling ni kwa TAMBWE na OKWI ili wafunge mabao zaidi kumbe hata huku vipo lohhh.........................!!!!!!!
 
Uhuni mtupu. Kwani kura zinapigwa mara ngapi?? Ccm acheni mambo ya aibu. Nijuavyo mimi kura haina negotiations baada ya kupigwa. Ndio maana kiunakuiwa na kampeni kabla ya zoezi la kipiha kura. Sitta ni janga la Watanzania.
 
waliopiga kura za hapana kwa sura zote ndiyo wameomba wasikilizwe sababu ni nni?

Sababu sii ni kuwa mtu hajaridhika na katiba ilivyo! Kwa hiyo hapo serikali ikitangaza dau la milioni kumi kumi kubadili uamuzi kuwa ni ndiyo basi 2/3 itapatikana kirahisi.
 
Demokrasia ya aina hii iko Tanzania pekee.

Halafu Hilo zee linataka kuwa raisi wa Tanzania!!!! Samwel Sitta Ni janga la kidunia
 
Kufuatia baadhi ya wajumbe kupiga kura ya hapana apo jana kwa sura ya kwanza hadi ya kumi "Eti kuna wajumbe wawili kati ya wale waliosema hapana wameomba kamati iundwe ili waeleze kwann walisema hapana ili wasije wakaeleweka vibaya".
Hivyo mwenyekiti ameunda tume hiyo na baadhi ya wajumbe wake ni Asha Migiro, Hassan Ngwilizi, Chenge, Shamc Vuai Nahodha kwa uchache.
Pia 6 amewaalika na wale wengine waliosema hapana kwa sura hzo 10 wakitaka nao kusikilizwa waende mbele ya tume hiyo.
 
Watoto wa Bavicha, Acheni kupotosha umma!!! Kuna Wabunge wameomba kusikilizwa kama special case. Sitta ameunda
kamati ili wapate haki yao.
 
Ngoja na Mimi niunde tume kujadiliana na waliompa dhaifu Kikwete kura za ndio 2010, Nina uhakika wote watabatilisha NDIYO zao kuwa HAPANA
 
Back
Top Bottom