Samson Mwigamba: Zitto ajiandae kupambana na Seif, hana hadhi ya Magufuli

Shigganza

Senior Member
May 24, 2018
160
412
KALAMU YA Samson Mwigamba

Zitto ajiandae kupambana na Maalim Seif, hana hadhi ya kupambana na JPM

QURAN Tukufu inasema alama za mnafiki ni tatu. Kwanza, akisema hasemi ukweli. Pili, akiaminiwa haaminiki. Na tatu, akiweka ahadi hatekelezi!

Nimekaa na kufanya kazi na wanasiasa wengi tokea niingie rasmi kwenye siasa. Katika wanasiasa wote niliofanya nao kazi mpaka leo, sijawahi kuona mwanasiasa mnafiki kama Zitto Zuberi Kabwe!

Hakuna mwanasiasa aliyewahi kumwamini Zitto Kabwe akaaminika. Kuanzia kwa Freeman Mbowe mpaka CCM ya Kikwete.

Aliaminiwa na Chacha Zakayo Wangwe hakuaminika. Siku anashirikiana na Mbowe kumshughulikia Chacha Wangwe pale Dodoma, Wangwe alimwambia Zitto Kabwe kwamba mkuki aliokuwa. anautumia kumchoma ndio huo huo utakaomchoma Zitto Kabwe mwenyewe.

Wakati anashikishwa adabu na akina Mbowe wale wale, Msafiri Mtemelwa alimkumbusha Zitto maneno ya Wangwe, akalia machozi.

Mwaka 2009 alipochukua fomu kwa mara ya kwanza ya kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA, ilikuwa ni wiki moja tu tokea apange namna ya kugawana nafasi za juu za chama na wakurugenzi wa makao makuu ya CHADEMA.

Zitto Kabwe alikaa na akina Benson Kigaila na wakurugenzi wengine makao makuu ya CHADEMA wakapanga kwamba kwa kuwa Dkt. Willibrod Slaa alikuwa ametangaza kustaafu ukatibu mkuu, basi yeye Zitto awe Katibu Mkuu, mwenyekiti taifa aendelee kuwa Freeman Mbowe. Anthony Komu awe Naibu Katibu Mkuu, nk.

Wiki moja tu, akina Kigaila wakasikia Zitto amechukua fomu ya kugombea uenyekiti wa taifa. Wengi wao wakamgeuka na kukataa huo mradi wake mpya alioshauriwa na akina Msafiri Mtemelwa. Akaanza kupanga safu nyingine tena.

Makamu mwenyekiti bara awe Mzee Philemon Ndesamburo, Katibu Mkuu awe Mzee Sylivester Masinde, Naibu Katibu Mkuu Bara awe Anthony Komu. Lakini tena wiki chache baadaye Zitto akajitoa kwenye kinyang’anyiro hicho na kumwachia Mbowe!

Kuanzisha ACT na kuondoka CHADEMA nako kulikuwa na rangi nyingi sana za Zitto Kabwe. Mwanzo kabisa aliweka msimamo kwamba CHADEMA wakimfukuza uanachama hawezi kuwa mbunge wa mahakama. Atakubali kufukuzwa waende kwenye uchaguzi mdogo.

Agombee kupitia chama kipya halafu yeye aiombe CCM (ya wakati huo) imsaidie kwa kuweka mgombea dhaifu na kuacha kumsaidia ili Zitto ashinde. Akadai kwamba akiwashinda wagombea wa CHADEMA na CCM, atakuwa amerejesha nguvu yake (renewing mandate).

Tuliposikia kikao cha kutujadili na kutufukuza uanachama kimekaribia, Zitto akasema sisi wawili tukubali kufutwa ila yeye anakwenda mahakamani kupinga kufukuzwa ili kulinda ubunge wake. Akageuka!

Alifanya hivyo kwenye kuhamia rasmi ACT, aligeuka mara tatu. Alifanya hivyo kwenye chama kusimamisha mgombea 2015. Mwanzo alitaka tuwe na mgombea, lakini tusishirikiane na Lowassa kwa namna yoyote ile. Baadaye akasema tukimpata Lowassa kuwa mgombea wetu itakuwa safi sana.

Tulipokaribia kabisa uchaguzi baada ya Dkt. Magufuli kupitishwa kuwa mgombea wa CCM akasema tusimamishe mgombea atakayeshindana na Lowassa halafu Magufuli ashinde. Na akawa anatushawishi tumteue Kitila Mkumbo awe mgombea wetu.

Alipoitwa na upande wa Lowassa akaahidiwa uwaziri mkuu, akageuka tena. Kwenye kikao cha kamati kuu akaungana na maswahiba wake kukataa mgombea wa ACT.

Baada ya Kitila kukataa kugombea, rafiki yake waliyepanga naye mwanzo kwamba wamshawishi Kitila agombee, akamfuata.
Baada ya kushawishiwa na huyo tena, akageuka kwa mara nyingine.

Akataka Kitila akubali kugombea, Kitila akakataa. Ni Zitto aliyetoa shilingi milioni 5 zilizokusanya watu mitaani Mbagala wasio wanachama wa ACT wakaja Makao Makuu ya ACT na kujifanya wana ACT wanaotaka Kitila agombee urais kupitia ACT.

Baadhi yao walipoulizwa mnayetaka agombee urais kupitia ACT anaitwa nani, walisema “Tunataka Prof. Mtikila agombee urais”. Walikuwa hawajui hata jina la Kitila.

Baada ya mpango huo kushindikana, akarudi tena kwenye mpango wa Lowassa. Alitumia nguvu kubwa sana kukishawishi chama kutosimamisha mgombea urais. Lakini Kamati Kuu na Halmashauri Kuu zikamgomea na baada ya kampeni zake dhidi yangu, hatimaye akapitishwa Mama Anna Mghwira kugombea.

Nikamwambia shida yangu ilikuwa chama kiwe na mgombea urais na siyo mimi kugombea. Niliombwa baada ya kukosekana mgombea, kwa kuwa Mama Mghwira amekubali, safi!Tuliotaka mgombea urais tukafurahi, yeye akanuna.

Akafanya mpango wa kuhujumu fomu za wadhamini wa mgombea urais mkoa wa Dar es salaam, pia akashindwa. Mwisho akaamua kususia kabisa kampeni za mgombea urais. Zitto Kabwe huyo!

Lakini ni Zitto Kabwe huyu huyu aliyegombana na akina Mbowe na Lissu walipokuwa wanampinga Magufuli baada ya kuchaguliwa. Alibaki bungeni akina mbowe waliposusia kikao cha Bunge cha Rais Magufuli kulizindua bunge, akamsifia sana Magufuli kwamba hotuba yake imetoka kwenye ilani ya ACT kwa asilimia 60.

Hata mara kadhaa alionekana kumsifia sana Magufuli wakati mwingine akimponda, na pale aliposhindwa kabisa kupata kile alichokitaka kwa Magufuli, ndipo akaamua kujiunga tena na akina Mbowe na Lissu kumpinga Magufuli hadi leo.

Huyo ni Zitto Kabwe aliyekuwa upande wa Lipumba wakati mgogoro wa ndani ya CUF umeanza. Alimsaidia Lipumba kwa kumpa vijana wa kufanya fitna. Lakini pia alimpa Lipumba wanasheria wa kumtetea kwenye kesi aliyofunguliwa na upande wa Maalim Seif.

Kabla kesi haijaisha akahamia upande wa Maalim Seif na leo Maalim Seif ni mwanachama namba moja wa ACT.

Sasa ameamua kuongeza dozi ya kumpinga Rais Magufuli. Na kwa vile sasa yuko na hasimu wa Dkt. Shein, ameanza kuwachanganya Rais Magufuli na Dkt. Shein. Ili awapendeze wagombea wake wote.

Anampinga Magufuli kwa ajili ya kumfurahisha yule mwana CCM aliyemwahidi pesa za kujengea chama anayefadhili harakati zake zote za hivi sasa na ambaye ameahidi kugombea urais wa Muungano kupitia ACT uchaguzi ujao. Wakati huo anampinga Rais Shein ili kumfurahisha Maalim Seif aliyejipanga kugombea urais wa Zanzibar kupitia ACT 2020.

Hiyo ndiyo mantiki ya mazungumzo yake na vyombo vya habari Jumanne ya wiki iliyopita. Aliponda serikali ya muungano na ile ya Zanzibar kwa pamoja. Alisema uchumi wa nchi yetu unaporomoka na akasema anatumia takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BOT) hususan tathmini za uchumi za kila mwezi.

Leo nataka niwaonyeshe uongo wake. Nimechukua ‘Tathmini ya uchumi ya kila mwezi kwa mwezi Aprili 2019’. Hebu tuipitie tuone anachokizungumza anayejiita mchumi Zitto Kabwe na kilichoelezwa na Benki Kuu ya Tanzania.

Tuanze na Wastani wa Pato la Taifa kwa mtu mmoja (GDP per capita). Wakati Rais Magufuli anaingia madarakani mwaka 2015, GDP per Capita ilikuwa dola za kimarekani 991.7. Mwaka 2016 ikapanda kuwa dola 1,006.5 na mwaka 2017 ikafikia dola 1,045.1.

Amezungumzia urari wa biashara (trade balance) katika nchi yetu. Kwa kawaida urari wa biashara unapatikana kwa kuchukua mauzo yetu ya nje na kutoa manunuzi yetu ya nje. Ili taifa lionekane linafanya vizuri kiuchumi, inatakiwa mauzo ya nje yawe makubwa kuliko manunuzi kutoka nje.

Manunuzi kutoka nje yakiwa madogo kuliko mauzo yetu nje, urari wa biashara unakuwa chanya (positive) na kadri hiyo tarakimu chanya inavyokuwa kubwa, ndivyo uchumi unavyozidi kuwa mzuri.

Mauzo ya nje yakiwa madogo kuliko manunuzi yetu toka nje, urari unakuwa hasi (negative) na kadri tarakimu hasi inavyozidi kuongezeka, ndivyo uchumi wetu unavyozidi kuonekana taaban. Twende kwenye takwimu sasa.

Tathmini ya uchumi ya Benki Kuu kwa mwezi Aprili mwaka huu inaonyesha kwamba urari wa biashara ulikuwa kama ifuatavyo: Mwaka 2013 dola -5,771.1; mwaka 2014 dola -5,723.7; mwaka 2015 dola 4,526.3; mwaka 2016 dola -3,513.9 na mwaka 2017 dola -3,027.8.

Nilijaribu pia kuangalia uwiano wa matumizi ya miradi ya maendeleo ikilinganishwa na pato la taifa (Development Expenditure to GDP ratio). Nao ulikuwa kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 5.0%; mwaka 2014/15 – 4.2%; mwaka 2015/16 – 4.3%; mwaka 2016/17 – 6.4%; na mwaka 2017/18 – 6.1%. Uwiano wa matumizi ya kawaida dhidi ya pato la taifa ni kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 12.9%; mwaka 2014/15 – 12.3%; mwaka 2015/16 – 13.2%; mwaka 2016/17 – 10.2%; na mwaka 2017/18 – 10.4%. Tumeongeza matumizi ya maendeleo wakati matumizi ya kawaida yanapungua.

Hiki kilikuwa kilio cha wapinzani enzi hizo. Tulitaka taifa litumie fedha nyingi kwenye matumizi ya maendeleo. Tulitaka hata taifa linapokopa litumie mikopo kwa matumizi ya maendeleo na si matumizi ya kawaida. Hili ndilo linalofanyika hivi sasa.

Takwimu hizi zote Zitto anadai uchumi unaporomoka. Hivi ni uchumi wa Tanzania ndio unaporomoka au ni uchumi wa Zitto ndio unaporomoka?

Mimi namfahamu Zitto kuliko watanzania wengi sana. Akiniambia uchumi wake umeporomoka, nitakubaliana naye mara moja. Sihitaji kujiuliza hata mara moja. Najua pesa alizokuwa anaziingiza kwenye ACT wakati huo achilia mbali za kwake binafsi.

Zitto Kabwe ni mbunge pekee aliyekuwa na watumishi binafsi 12. Jijini Dar es salaam alikuwa na madereva wawili, mhasibu (wa fedha zake binafsi) mmoja, mshauri wa uchumi mmoja, msaidizi maalum mmoja na katibu wake kama kiongozi wa chama mmoja.

Mjini Kigoma alikuwa na Katibu wa Mbunge mmoja, Afisa wa utawala ofisi ya Mbunge mmoja, afisa maendeleo ya jamii ofisi ya mbunge mmoja, dereva mmoja na wasaidizi maalum wa mbunge wawili. Kwa sasa kinachoendelea, Mungu ndiye anajua.

Wako waliompeleka idara ya kazi kudai mishahara yao, wapo walioamua kuacha kimya kimya bila kumwaibisha kiongozi wao, wapo wanaotaka kuondoka ila anawaahidi kila kukicha na wapo wanaovumilia.

Sasa anaponda hata hatua ya Rais kuwaita wafanyabiashara ili apate kutoka kwenye mizizi taarifa za uhakika za nini kinachoendelea kwa upande wao. Amekutana na wadau wa madini, amekuwa akikutana na wajumbe wa Baraza la Biashara Taifa, lakini wakati huu akasema akutane na wafanyabiashara wa kutoka kwenye kila wilaya ili apate taarifa muhimu.

Mkutano ule umempa picha pana na amechukua hatua muhimu za kinidhamu dhidi ya wasaidizi wake. Lakini hatua za kubadili kanuni au hata sheria zitafuata ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji kodi na kukuza biashara. Hilo nalo anaponda!

Hizi nguvu anazotumia kupambana na ‘jabali’ JPM anazipoteza bure na atazijutia. Magufuli anazidi kuchanja mbuga. Treni yake ya kuelekea uchumi wa kati imeshika kasi na kama Zitto anadhani anaweza kuizuia kwa tamaa yake ya madaraka, asimame relini kujaribu kuizuia ‘treni’ hii aone itakavyompasua vipande vipande!

Nguvu anazotumia kupambana na Magufuli, azitunze aje azitumie kupambana na Maalim Seif. Kwenye kila chama anachokuwemo Maalim Seif, kila mpemba aliyemo kwenye chama hicho anakuwa kiongozi na thamani zaidi ya kiongozi yeyote wa bara. Mpemba huyo anaweza kuelekeza jambo lolote.

Msimamo na malengo ya chama ni lazima yajikite Zanzibar kibajeti. Lazima kutakuwa na kikao cha wazanzibari walioko kwenye uongozi wa chama hicho nje ya vikao vya chama vya kikatiba kabla na baada ya vikao hivyo. Kila mtanganyika ni adui wa Zanzibar hata kama ni mwanachama wa chama alichomo Maalim Seif.

Maalim Seif ni Sultani wa pili wa Zanzibar baada ya yule wa kwanza kuondolewa kwa mapanga kwenye mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964. Sultani wa pili anawekwa mbali na ikulu kwa sanduku la kura!

Sultani huyu ana wapambe wake akina Ismail Jussa Ladhu, Salim Bimani, Nassor Mazrui na Issah Kheri. Kwenye chama chochote alichomo Maalim Seif, yeye na hawa wapambe wake ndio watakuwa na maamuzi. Hivi tunavyozungumza karibu wote hawa na wengine wengi wa upande wa Maalim Seif wameshaingizwa kwenye kamati kuu.

Baada ya uchaguzi wa ndani ya chama, watazidi kuingia wengine. Tayari mikakati ya ‘kuwapiga chini’ baadhi ya viongozi wa zamani ndani ya ACT imeshaanza.

Hata uchaguzi uliosimamiwa na viongozi wa zamani kwenye majimbo na mikoa nusura ufutwe na kamati kuu ili uanze upya. Baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 ACT itakapokuwa na wabunge wote kutoka Pemba, ndipo tutakaposhuhudia mtanange wa maana kati ya Zitto na Maalim Seif. Mmoja mnafiki, mmoja Sultani.

Badala atunze nguvu zake za kupambana aje apambane na Maalim Seif, yeye anazimalizia kupambana na ngome asizokuwa na uwezo hata robo ya robo wa kupambana nazo!
 
KALAMU YA Samson Mwigamba

Zitto ajiandae kupambana na Maalim Seif, hana hadhi ya kupambana na JPM

QURAN Tukufu inasema alama za mnafiki ni tatu. Kwanza, akisema hasemi ukweli. Pili, akiaminiwa haaminiki. Na tatu, akiweka ahadi hatekelezi!

Nimekaa na kufanya kazi na wanasiasa wengi tokea niingie rasmi kwenye siasa. Katika wanasiasa wote niliofanya nao kazi mpaka leo, sijawahi kuona mwanasiasa mnafiki kama Zitto Zuberi Kabwe!

Hakuna mwanasiasa aliyewahi kumwamini Zitto Kabwe akaaminika. Kuanzia kwa Freeman Mbowe mpaka CCM ya Kikwete.

Aliaminiwa na Chacha Zakayo Wangwe hakuaminika. Siku anashirikiana na Mbowe kumshughulikia Chacha Wangwe pale Dodoma, Wangwe alimwambia Zitto Kabwe kwamba mkuki aliokuwa. anautumia kumchoma ndio huo huo utakaomchoma Zitto Kabwe mwenyewe.

Wakati anashikishwa adabu na akina Mbowe wale wale, Msafiri Mtemelwa alimkumbusha Zitto maneno ya Wangwe, akalia machozi.

Mwaka 2009 alipochukua fomu kwa mara ya kwanza ya kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA, ilikuwa ni wiki moja tu tokea apange namna ya kugawana nafasi za juu za chama na wakurugenzi wa makao makuu ya CHADEMA.

Zitto Kabwe alikaa na akina Benson Kigaila na wakurugenzi wengine makao makuu ya CHADEMA wakapanga kwamba kwa kuwa Dkt. Willibrod Slaa alikuwa ametangaza kustaafu ukatibu mkuu, basi yeye Zitto awe Katibu Mkuu, mwenyekiti taifa aendelee kuwa Freeman Mbowe. Anthony Komu awe Naibu Katibu Mkuu, nk.

Wiki moja tu, akina Kigaila wakasikia Zitto amechukua fomu ya kugombea uenyekiti wa taifa. Wengi wao wakamgeuka na kukataa huo mradi wake mpya alioshauriwa na akina Msafiri Mtemelwa. Akaanza kupanga safu nyingine tena.

Makamu mwenyekiti bara awe Mzee Philemon Ndesamburo, Katibu Mkuu awe Mzee Sylivester Masinde, Naibu Katibu Mkuu Bara awe Anthony Komu. Lakini tena wiki chache baadaye Zitto akajitoa kwenye kinyang’anyiro hicho na kumwachia Mbowe!

Kuanzisha ACT na kuondoka CHADEMA nako kulikuwa na rangi nyingi sana za Zitto Kabwe. Mwanzo kabisa aliweka msimamo kwamba CHADEMA wakimfukuza uanachama hawezi kuwa mbunge wa mahakama. Atakubali kufukuzwa waende kwenye uchaguzi mdogo.

Agombee kupitia chama kipya halafu yeye aiombe CCM (ya wakati huo) imsaidie kwa kuweka mgombea dhaifu na kuacha kumsaidia ili Zitto ashinde. Akadai kwamba akiwashinda wagombea wa CHADEMA na CCM, atakuwa amerejesha nguvu yake (renewing mandate).

Tuliposikia kikao cha kutujadili na kutufukuza uanachama kimekaribia, Zitto akasema sisi wawili tukubali kufutwa ila yeye anakwenda mahakamani kupinga kufukuzwa ili kulinda ubunge wake. Akageuka!

Alifanya hivyo kwenye kuhamia rasmi ACT, aligeuka mara tatu. Alifanya hivyo kwenye chama kusimamisha mgombea 2015. Mwanzo alitaka tuwe na mgombea, lakini tusishirikiane na Lowassa kwa namna yoyote ile. Baadaye akasema tukimpata Lowassa kuwa mgombea wetu itakuwa safi sana.

Tulipokaribia kabisa uchaguzi baada ya Dkt. Magufuli kupitishwa kuwa mgombea wa CCM akasema tusimamishe mgombea atakayeshindana na Lowassa halafu Magufuli ashinde. Na akawa anatushawishi tumteue Kitila Mkumbo awe mgombea wetu.

Alipoitwa na upande wa Lowassa akaahidiwa uwaziri mkuu, akageuka tena. Kwenye kikao cha kamati kuu akaungana na maswahiba wake kukataa mgombea wa ACT.

Baada ya Kitila kukataa kugombea, rafiki yake waliyepanga naye mwanzo kwamba wamshawishi Kitila agombee, akamfuata.
Baada ya kushawishiwa na huyo tena, akageuka kwa mara nyingine.

Akataka Kitila akubali kugombea, Kitila akakataa. Ni Zitto aliyetoa shilingi milioni 5 zilizokusanya watu mitaani Mbagala wasio wanachama wa ACT wakaja Makao Makuu ya ACT na kujifanya wana ACT wanaotaka Kitila agombee urais kupitia ACT.

Baadhi yao walipoulizwa mnayetaka agombee urais kupitia ACT anaitwa nani, walisema “Tunataka Prof. Mtikila agombee urais”. Walikuwa hawajui hata jina la Kitila.

Baada ya mpango huo kushindikana, akarudi tena kwenye mpango wa Lowassa. Alitumia nguvu kubwa sana kukishawishi chama kutosimamisha mgombea urais. Lakini Kamati Kuu na Halmashauri Kuu zikamgomea na baada ya kampeni zake dhidi yangu, hatimaye akapitishwa Mama Anna Mghwira kugombea.

Nikamwambia shida yangu ilikuwa chama kiwe na mgombea urais na siyo mimi kugombea. Niliombwa baada ya kukosekana mgombea, kwa kuwa Mama Mghwira amekubali, safi!Tuliotaka mgombea urais tukafurahi, yeye akanuna.

Akafanya mpango wa kuhujumu fomu za wadhamini wa mgombea urais mkoa wa Dar es salaam, pia akashindwa. Mwisho akaamua kususia kabisa kampeni za mgombea urais. Zitto Kabwe huyo!

Lakini ni Zitto Kabwe huyu huyu aliyegombana na akina Mbowe na Lissu walipokuwa wanampinga Magufuli baada ya kuchaguliwa. Alibaki bungeni akina mbowe waliposusia kikao cha Bunge cha Rais Magufuli kulizindua bunge, akamsifia sana Magufuli kwamba hotuba yake imetoka kwenye ilani ya ACT kwa asilimia 60.

Hata mara kadhaa alionekana kumsifia sana Magufuli wakati mwingine akimponda, na pale aliposhindwa kabisa kupata kile alichokitaka kwa Magufuli, ndipo akaamua kujiunga tena na akina Mbowe na Lissu kumpinga Magufuli hadi leo.

Huyo ni Zitto Kabwe aliyekuwa upande wa Lipumba wakati mgogoro wa ndani ya CUF umeanza. Alimsaidia Lipumba kwa kumpa vijana wa kufanya fitna. Lakini pia alimpa Lipumba wanasheria wa kumtetea kwenye kesi aliyofunguliwa na upande wa Maalim Seif.

Kabla kesi haijaisha akahamia upande wa Maalim Seif na leo Maalim Seif ni mwanachama namba moja wa ACT.

Sasa ameamua kuongeza dozi ya kumpinga Rais Magufuli. Na kwa vile sasa yuko na hasimu wa Dkt. Shein, ameanza kuwachanganya Rais Magufuli na Dkt. Shein. Ili awapendeze wagombea wake wote.

Anampinga Magufuli kwa ajili ya kumfurahisha yule mwana CCM aliyemwahidi pesa za kujengea chama anayefadhili harakati zake zote za hivi sasa na ambaye ameahidi kugombea urais wa Muungano kupitia ACT uchaguzi ujao. Wakati huo anampinga Rais Shein ili kumfurahisha Maalim Seif aliyejipanga kugombea urais wa Zanzibar kupitia ACT 2020.

Hiyo ndiyo mantiki ya mazungumzo yake na vyombo vya habari Jumanne ya wiki iliyopita. Aliponda serikali ya muungano na ile ya Zanzibar kwa pamoja. Alisema uchumi wa nchi yetu unaporomoka na akasema anatumia takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BOT) hususan tathmini za uchumi za kila mwezi.

Leo nataka niwaonyeshe uongo wake. Nimechukua ‘Tathmini ya uchumi ya kila mwezi kwa mwezi Aprili 2019’. Hebu tuipitie tuone anachokizungumza anayejiita mchumi Zitto Kabwe na kilichoelezwa na Benki Kuu ya Tanzania.

Tuanze na Wastani wa Pato la Taifa kwa mtu mmoja (GDP per capita). Wakati Rais Magufuli anaingia madarakani mwaka 2015, GDP per Capita ilikuwa dola za kimarekani 991.7. Mwaka 2016 ikapanda kuwa dola 1,006.5 na mwaka 2017 ikafikia dola 1,045.1.

Amezungumzia urari wa biashara (trade balance) katika nchi yetu. Kwa kawaida urari wa biashara unapatikana kwa kuchukua mauzo yetu ya nje na kutoa manunuzi yetu ya nje. Ili taifa lionekane linafanya vizuri kiuchumi, inatakiwa mauzo ya nje yawe makubwa kuliko manunuzi kutoka nje.

Manunuzi kutoka nje yakiwa madogo kuliko mauzo yetu nje, urari wa biashara unakuwa chanya (positive) na kadri hiyo tarakimu chanya inavyokuwa kubwa, ndivyo uchumi unavyozidi kuwa mzuri.

Mauzo ya nje yakiwa madogo kuliko manunuzi yetu toka nje, urari unakuwa hasi (negative) na kadri tarakimu hasi inavyozidi kuongezeka, ndivyo uchumi wetu unavyozidi kuonekana taaban. Twende kwenye takwimu sasa.

Tathmini ya uchumi ya Benki Kuu kwa mwezi Aprili mwaka huu inaonyesha kwamba urari wa biashara ulikuwa kama ifuatavyo: Mwaka 2013 dola -5,771.1; mwaka 2014 dola -5,723.7; mwaka 2015 dola 4,526.3; mwaka 2016 dola -3,513.9 na mwaka 2017 dola -3,027.8.

Nilijaribu pia kuangalia uwiano wa matumizi ya miradi ya maendeleo ikilinganishwa na pato la taifa (Development Expenditure to GDP ratio). Nao ulikuwa kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 5.0%; mwaka 2014/15 – 4.2%; mwaka 2015/16 – 4.3%; mwaka 2016/17 – 6.4%; na mwaka 2017/18 – 6.1%. Uwiano wa matumizi ya kawaida dhidi ya pato la taifa ni kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 12.9%; mwaka 2014/15 – 12.3%; mwaka 2015/16 – 13.2%; mwaka 2016/17 – 10.2%; na mwaka 2017/18 – 10.4%. Tumeongeza matumizi ya maendeleo wakati matumizi ya kawaida yanapungua.

Hiki kilikuwa kilio cha wapinzani enzi hizo. Tulitaka taifa litumie fedha nyingi kwenye matumizi ya maendeleo. Tulitaka hata taifa linapokopa litumie mikopo kwa matumizi ya maendeleo na si matumizi ya kawaida. Hili ndilo linalofanyika hivi sasa.

Takwimu hizi zote Zitto anadai uchumi unaporomoka. Hivi ni uchumi wa Tanzania ndio unaporomoka au ni uchumi wa Zitto ndio unaporomoka?

Mimi namfahamu Zitto kuliko watanzania wengi sana. Akiniambia uchumi wake umeporomoka, nitakubaliana naye mara moja. Sihitaji kujiuliza hata mara moja. Najua pesa alizokuwa anaziingiza kwenye ACT wakati huo achilia mbali za kwake binafsi.

Zitto Kabwe ni mbunge pekee aliyekuwa na watumishi binafsi 12. Jijini Dar es salaam alikuwa na madereva wawili, mhasibu (wa fedha zake binafsi) mmoja, mshauri wa uchumi mmoja, msaidizi maalum mmoja na katibu wake kama kiongozi wa chama mmoja.

Mjini Kigoma alikuwa na Katibu wa Mbunge mmoja, Afisa wa utawala ofisi ya Mbunge mmoja, afisa maendeleo ya jamii ofisi ya mbunge mmoja, dereva mmoja na wasaidizi maalum wa mbunge wawili. Kwa sasa kinachoendelea, Mungu ndiye anajua.

Wako waliompeleka idara ya kazi kudai mishahara yao, wapo walioamua kuacha kimya kimya bila kumwaibisha kiongozi wao, wapo wanaotaka kuondoka ila anawaahidi kila kukicha na wapo wanaovumilia.

Sasa anaponda hata hatua ya Rais kuwaita wafanyabiashara ili apate kutoka kwenye mizizi taarifa za uhakika za nini kinachoendelea kwa upande wao. Amekutana na wadau wa madini, amekuwa akikutana na wajumbe wa Baraza la Biashara Taifa, lakini wakati huu akasema akutane na wafanyabiashara wa kutoka kwenye kila wilaya ili apate taarifa muhimu.

Mkutano ule umempa picha pana na amechukua hatua muhimu za kinidhamu dhidi ya wasaidizi wake. Lakini hatua za kubadili kanuni au hata sheria zitafuata ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji kodi na kukuza biashara. Hilo nalo anaponda!

Hizi nguvu anazotumia kupambana na ‘jabali’ JPM anazipoteza bure na atazijutia. Magufuli anazidi kuchanja mbuga. Treni yake ya kuelekea uchumi wa kati imeshika kasi na kama Zitto anadhani anaweza kuizuia kwa tamaa yake ya madaraka, asimame relini kujaribu kuizuia ‘treni’ hii aone itakavyompasua vipande vipande!

Nguvu anazotumia kupambana na Magufuli, azitunze aje azitumie kupambana na Maalim Seif. Kwenye kila chama anachokuwemo Maalim Seif, kila mpemba aliyemo kwenye chama hicho anakuwa kiongozi na thamani zaidi ya kiongozi yeyote wa bara. Mpemba huyo anaweza kuelekeza jambo lolote.

Msimamo na malengo ya chama ni lazima yajikite Zanzibar kibajeti. Lazima kutakuwa na kikao cha wazanzibari walioko kwenye uongozi wa chama hicho nje ya vikao vya chama vya kikatiba kabla na baada ya vikao hivyo. Kila mtanganyika ni adui wa Zanzibar hata kama ni mwanachama wa chama alichomo Maalim Seif.

Maalim Seif ni Sultani wa pili wa Zanzibar baada ya yule wa kwanza kuondolewa kwa mapanga kwenye mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964. Sultani wa pili anawekwa mbali na ikulu kwa sanduku la kura!

Sultani huyu ana wapambe wake akina Ismail Jussa Ladhu, Salim Bimani, Nassor Mazrui na Issah Kheri. Kwenye chama chochote alichomo Maalim Seif, yeye na hawa wapambe wake ndio watakuwa na maamuzi. Hivi tunavyozungumza karibu wote hawa na wengine wengi wa upande wa Maalim Seif wameshaingizwa kwenye kamati kuu.

Baada ya uchaguzi wa ndani ya chama, watazidi kuingia wengine. Tayari mikakati ya ‘kuwapiga chini’ baadhi ya viongozi wa zamani ndani ya ACT imeshaanza.

Hata uchaguzi uliosimamiwa na viongozi wa zamani kwenye majimbo na mikoa nusura ufutwe na kamati kuu ili uanze upya. Baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 ACT itakapokuwa na wabunge wote kutoka Pemba, ndipo tutakaposhuhudia mtanange wa maana kati ya Zitto na Maalim Seif. Mmoja mnafiki, mmoja Sultani.

Badala atunze nguvu zake za kupambana aje apambane na Maalim Seif, yeye anazimalizia kupambana na ngome asizokuwa na uwezo hata robo ya robo wa kupambana nazo!
Chuki binafsi kazini!

Wewe siyo mwanasiasa bali ulikuwa unatembelea Nyota ya Zitto na Prof Kitila Mkumbo!
 
Mimi mwenyewe zitto zijawahi kumwamini hata dakika moja

Mimi akili za kufuata mkumbo huwa sina

Namsikiliza MTU kisha namfanyia analysis

Zitto kwa upinzani ni kirusi kikuu,upinzani hauwezi kupiga hatua yeyote kwa kushirikiana na huyo bwana mdogo kiburi,mnafki na sifa kama hizo

Ni kijana ambaye ana maarifa ila sio muungwana hata kidogo
 
Ni mawazo yako, lakini edit kule juu, alama za mnafiki ni tatu, ni hadith ya mtume swalallahu alaihi wasalam na wala sio Quran.
 
KALAMU YA Samson Mwigamba

Zitto ajiandae kupambana na Maalim Seif, hana hadhi ya kupambana na JPM

QURAN Tukufu inasema alama za mnafiki ni tatu. Kwanza, akisema hasemi ukweli. Pili, akiaminiwa haaminiki. Na tatu, akiweka ahadi hatekelezi!

Nimekaa na kufanya kazi na wanasiasa wengi tokea niingie rasmi kwenye siasa. Katika wanasiasa wote niliofanya nao kazi mpaka leo, sijawahi kuona mwanasiasa mnafiki kama Zitto Zuberi Kabwe!

Hakuna mwanasiasa aliyewahi kumwamini Zitto Kabwe akaaminika. Kuanzia kwa Freeman Mbowe mpaka CCM ya Kikwete.

Aliaminiwa na Chacha Zakayo Wangwe hakuaminika. Siku anashirikiana na Mbowe kumshughulikia Chacha Wangwe pale Dodoma, Wangwe alimwambia Zitto Kabwe kwamba mkuki aliokuwa. anautumia kumchoma ndio huo huo utakaomchoma Zitto Kabwe mwenyewe.

Wakati anashikishwa adabu na akina Mbowe wale wale, Msafiri Mtemelwa alimkumbusha Zitto maneno ya Wangwe, akalia machozi.

Mwaka 2009 alipochukua fomu kwa mara ya kwanza ya kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA, ilikuwa ni wiki moja tu tokea apange namna ya kugawana nafasi za juu za chama na wakurugenzi wa makao makuu ya CHADEMA.

Zitto Kabwe alikaa na akina Benson Kigaila na wakurugenzi wengine makao makuu ya CHADEMA wakapanga kwamba kwa kuwa Dkt. Willibrod Slaa alikuwa ametangaza kustaafu ukatibu mkuu, basi yeye Zitto awe Katibu Mkuu, mwenyekiti taifa aendelee kuwa Freeman Mbowe. Anthony Komu awe Naibu Katibu Mkuu, nk.

Wiki moja tu, akina Kigaila wakasikia Zitto amechukua fomu ya kugombea uenyekiti wa taifa. Wengi wao wakamgeuka na kukataa huo mradi wake mpya alioshauriwa na akina Msafiri Mtemelwa. Akaanza kupanga safu nyingine tena.

Makamu mwenyekiti bara awe Mzee Philemon Ndesamburo, Katibu Mkuu awe Mzee Sylivester Masinde, Naibu Katibu Mkuu Bara awe Anthony Komu. Lakini tena wiki chache baadaye Zitto akajitoa kwenye kinyang’anyiro hicho na kumwachia Mbowe!

Kuanzisha ACT na kuondoka CHADEMA nako kulikuwa na rangi nyingi sana za Zitto Kabwe. Mwanzo kabisa aliweka msimamo kwamba CHADEMA wakimfukuza uanachama hawezi kuwa mbunge wa mahakama. Atakubali kufukuzwa waende kwenye uchaguzi mdogo.

Agombee kupitia chama kipya halafu yeye aiombe CCM (ya wakati huo) imsaidie kwa kuweka mgombea dhaifu na kuacha kumsaidia ili Zitto ashinde. Akadai kwamba akiwashinda wagombea wa CHADEMA na CCM, atakuwa amerejesha nguvu yake (renewing mandate).

Tuliposikia kikao cha kutujadili na kutufukuza uanachama kimekaribia, Zitto akasema sisi wawili tukubali kufutwa ila yeye anakwenda mahakamani kupinga kufukuzwa ili kulinda ubunge wake. Akageuka!

Alifanya hivyo kwenye kuhamia rasmi ACT, aligeuka mara tatu. Alifanya hivyo kwenye chama kusimamisha mgombea 2015. Mwanzo alitaka tuwe na mgombea, lakini tusishirikiane na Lowassa kwa namna yoyote ile. Baadaye akasema tukimpata Lowassa kuwa mgombea wetu itakuwa safi sana.

Tulipokaribia kabisa uchaguzi baada ya Dkt. Magufuli kupitishwa kuwa mgombea wa CCM akasema tusimamishe mgombea atakayeshindana na Lowassa halafu Magufuli ashinde. Na akawa anatushawishi tumteue Kitila Mkumbo awe mgombea wetu.

Alipoitwa na upande wa Lowassa akaahidiwa uwaziri mkuu, akageuka tena. Kwenye kikao cha kamati kuu akaungana na maswahiba wake kukataa mgombea wa ACT.

Baada ya Kitila kukataa kugombea, rafiki yake waliyepanga naye mwanzo kwamba wamshawishi Kitila agombee, akamfuata.
Baada ya kushawishiwa na huyo tena, akageuka kwa mara nyingine.

Akataka Kitila akubali kugombea, Kitila akakataa. Ni Zitto aliyetoa shilingi milioni 5 zilizokusanya watu mitaani Mbagala wasio wanachama wa ACT wakaja Makao Makuu ya ACT na kujifanya wana ACT wanaotaka Kitila agombee urais kupitia ACT.

Baadhi yao walipoulizwa mnayetaka agombee urais kupitia ACT anaitwa nani, walisema “Tunataka Prof. Mtikila agombee urais”. Walikuwa hawajui hata jina la Kitila.

Baada ya mpango huo kushindikana, akarudi tena kwenye mpango wa Lowassa. Alitumia nguvu kubwa sana kukishawishi chama kutosimamisha mgombea urais. Lakini Kamati Kuu na Halmashauri Kuu zikamgomea na baada ya kampeni zake dhidi yangu, hatimaye akapitishwa Mama Anna Mghwira kugombea.

Nikamwambia shida yangu ilikuwa chama kiwe na mgombea urais na siyo mimi kugombea. Niliombwa baada ya kukosekana mgombea, kwa kuwa Mama Mghwira amekubali, safi!Tuliotaka mgombea urais tukafurahi, yeye akanuna.

Akafanya mpango wa kuhujumu fomu za wadhamini wa mgombea urais mkoa wa Dar es salaam, pia akashindwa. Mwisho akaamua kususia kabisa kampeni za mgombea urais. Zitto Kabwe huyo!

Lakini ni Zitto Kabwe huyu huyu aliyegombana na akina Mbowe na Lissu walipokuwa wanampinga Magufuli baada ya kuchaguliwa. Alibaki bungeni akina mbowe waliposusia kikao cha Bunge cha Rais Magufuli kulizindua bunge, akamsifia sana Magufuli kwamba hotuba yake imetoka kwenye ilani ya ACT kwa asilimia 60.

Hata mara kadhaa alionekana kumsifia sana Magufuli wakati mwingine akimponda, na pale aliposhindwa kabisa kupata kile alichokitaka kwa Magufuli, ndipo akaamua kujiunga tena na akina Mbowe na Lissu kumpinga Magufuli hadi leo.

Huyo ni Zitto Kabwe aliyekuwa upande wa Lipumba wakati mgogoro wa ndani ya CUF umeanza. Alimsaidia Lipumba kwa kumpa vijana wa kufanya fitna. Lakini pia alimpa Lipumba wanasheria wa kumtetea kwenye kesi aliyofunguliwa na upande wa Maalim Seif.

Kabla kesi haijaisha akahamia upande wa Maalim Seif na leo Maalim Seif ni mwanachama namba moja wa ACT.

Sasa ameamua kuongeza dozi ya kumpinga Rais Magufuli. Na kwa vile sasa yuko na hasimu wa Dkt. Shein, ameanza kuwachanganya Rais Magufuli na Dkt. Shein. Ili awapendeze wagombea wake wote.

Anampinga Magufuli kwa ajili ya kumfurahisha yule mwana CCM aliyemwahidi pesa za kujengea chama anayefadhili harakati zake zote za hivi sasa na ambaye ameahidi kugombea urais wa Muungano kupitia ACT uchaguzi ujao. Wakati huo anampinga Rais Shein ili kumfurahisha Maalim Seif aliyejipanga kugombea urais wa Zanzibar kupitia ACT 2020.

Hiyo ndiyo mantiki ya mazungumzo yake na vyombo vya habari Jumanne ya wiki iliyopita. Aliponda serikali ya muungano na ile ya Zanzibar kwa pamoja. Alisema uchumi wa nchi yetu unaporomoka na akasema anatumia takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BOT) hususan tathmini za uchumi za kila mwezi.

Leo nataka niwaonyeshe uongo wake. Nimechukua ‘Tathmini ya uchumi ya kila mwezi kwa mwezi Aprili 2019’. Hebu tuipitie tuone anachokizungumza anayejiita mchumi Zitto Kabwe na kilichoelezwa na Benki Kuu ya Tanzania.

Tuanze na Wastani wa Pato la Taifa kwa mtu mmoja (GDP per capita). Wakati Rais Magufuli anaingia madarakani mwaka 2015, GDP per Capita ilikuwa dola za kimarekani 991.7. Mwaka 2016 ikapanda kuwa dola 1,006.5 na mwaka 2017 ikafikia dola 1,045.1.

Amezungumzia urari wa biashara (trade balance) katika nchi yetu. Kwa kawaida urari wa biashara unapatikana kwa kuchukua mauzo yetu ya nje na kutoa manunuzi yetu ya nje. Ili taifa lionekane linafanya vizuri kiuchumi, inatakiwa mauzo ya nje yawe makubwa kuliko manunuzi kutoka nje.

Manunuzi kutoka nje yakiwa madogo kuliko mauzo yetu nje, urari wa biashara unakuwa chanya (positive) na kadri hiyo tarakimu chanya inavyokuwa kubwa, ndivyo uchumi unavyozidi kuwa mzuri.

Mauzo ya nje yakiwa madogo kuliko manunuzi yetu toka nje, urari unakuwa hasi (negative) na kadri tarakimu hasi inavyozidi kuongezeka, ndivyo uchumi wetu unavyozidi kuonekana taaban. Twende kwenye takwimu sasa.

Tathmini ya uchumi ya Benki Kuu kwa mwezi Aprili mwaka huu inaonyesha kwamba urari wa biashara ulikuwa kama ifuatavyo: Mwaka 2013 dola -5,771.1; mwaka 2014 dola -5,723.7; mwaka 2015 dola 4,526.3; mwaka 2016 dola -3,513.9 na mwaka 2017 dola -3,027.8.

Nilijaribu pia kuangalia uwiano wa matumizi ya miradi ya maendeleo ikilinganishwa na pato la taifa (Development Expenditure to GDP ratio). Nao ulikuwa kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 5.0%; mwaka 2014/15 – 4.2%; mwaka 2015/16 – 4.3%; mwaka 2016/17 – 6.4%; na mwaka 2017/18 – 6.1%. Uwiano wa matumizi ya kawaida dhidi ya pato la taifa ni kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 12.9%; mwaka 2014/15 – 12.3%; mwaka 2015/16 – 13.2%; mwaka 2016/17 – 10.2%; na mwaka 2017/18 – 10.4%. Tumeongeza matumizi ya maendeleo wakati matumizi ya kawaida yanapungua.

Hiki kilikuwa kilio cha wapinzani enzi hizo. Tulitaka taifa litumie fedha nyingi kwenye matumizi ya maendeleo. Tulitaka hata taifa linapokopa litumie mikopo kwa matumizi ya maendeleo na si matumizi ya kawaida. Hili ndilo linalofanyika hivi sasa.

Takwimu hizi zote Zitto anadai uchumi unaporomoka. Hivi ni uchumi wa Tanzania ndio unaporomoka au ni uchumi wa Zitto ndio unaporomoka?

Mimi namfahamu Zitto kuliko watanzania wengi sana. Akiniambia uchumi wake umeporomoka, nitakubaliana naye mara moja. Sihitaji kujiuliza hata mara moja. Najua pesa alizokuwa anaziingiza kwenye ACT wakati huo achilia mbali za kwake binafsi.

Zitto Kabwe ni mbunge pekee aliyekuwa na watumishi binafsi 12. Jijini Dar es salaam alikuwa na madereva wawili, mhasibu (wa fedha zake binafsi) mmoja, mshauri wa uchumi mmoja, msaidizi maalum mmoja na katibu wake kama kiongozi wa chama mmoja.

Mjini Kigoma alikuwa na Katibu wa Mbunge mmoja, Afisa wa utawala ofisi ya Mbunge mmoja, afisa maendeleo ya jamii ofisi ya mbunge mmoja, dereva mmoja na wasaidizi maalum wa mbunge wawili. Kwa sasa kinachoendelea, Mungu ndiye anajua.

Wako waliompeleka idara ya kazi kudai mishahara yao, wapo walioamua kuacha kimya kimya bila kumwaibisha kiongozi wao, wapo wanaotaka kuondoka ila anawaahidi kila kukicha na wapo wanaovumilia.

Sasa anaponda hata hatua ya Rais kuwaita wafanyabiashara ili apate kutoka kwenye mizizi taarifa za uhakika za nini kinachoendelea kwa upande wao. Amekutana na wadau wa madini, amekuwa akikutana na wajumbe wa Baraza la Biashara Taifa, lakini wakati huu akasema akutane na wafanyabiashara wa kutoka kwenye kila wilaya ili apate taarifa muhimu.

Mkutano ule umempa picha pana na amechukua hatua muhimu za kinidhamu dhidi ya wasaidizi wake. Lakini hatua za kubadili kanuni au hata sheria zitafuata ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji kodi na kukuza biashara. Hilo nalo anaponda!

Hizi nguvu anazotumia kupambana na ‘jabali’ JPM anazipoteza bure na atazijutia. Magufuli anazidi kuchanja mbuga. Treni yake ya kuelekea uchumi wa kati imeshika kasi na kama Zitto anadhani anaweza kuizuia kwa tamaa yake ya madaraka, asimame relini kujaribu kuizuia ‘treni’ hii aone itakavyompasua vipande vipande!

Nguvu anazotumia kupambana na Magufuli, azitunze aje azitumie kupambana na Maalim Seif. Kwenye kila chama anachokuwemo Maalim Seif, kila mpemba aliyemo kwenye chama hicho anakuwa kiongozi na thamani zaidi ya kiongozi yeyote wa bara. Mpemba huyo anaweza kuelekeza jambo lolote.

Msimamo na malengo ya chama ni lazima yajikite Zanzibar kibajeti. Lazima kutakuwa na kikao cha wazanzibari walioko kwenye uongozi wa chama hicho nje ya vikao vya chama vya kikatiba kabla na baada ya vikao hivyo. Kila mtanganyika ni adui wa Zanzibar hata kama ni mwanachama wa chama alichomo Maalim Seif.

Maalim Seif ni Sultani wa pili wa Zanzibar baada ya yule wa kwanza kuondolewa kwa mapanga kwenye mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964. Sultani wa pili anawekwa mbali na ikulu kwa sanduku la kura!

Sultani huyu ana wapambe wake akina Ismail Jussa Ladhu, Salim Bimani, Nassor Mazrui na Issah Kheri. Kwenye chama chochote alichomo Maalim Seif, yeye na hawa wapambe wake ndio watakuwa na maamuzi. Hivi tunavyozungumza karibu wote hawa na wengine wengi wa upande wa Maalim Seif wameshaingizwa kwenye kamati kuu.

Baada ya uchaguzi wa ndani ya chama, watazidi kuingia wengine. Tayari mikakati ya ‘kuwapiga chini’ baadhi ya viongozi wa zamani ndani ya ACT imeshaanza.

Hata uchaguzi uliosimamiwa na viongozi wa zamani kwenye majimbo na mikoa nusura ufutwe na kamati kuu ili uanze upya. Baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 ACT itakapokuwa na wabunge wote kutoka Pemba, ndipo tutakaposhuhudia mtanange wa maana kati ya Zitto na Maalim Seif. Mmoja mnafiki, mmoja Sultani.

Badala atunze nguvu zake za kupambana aje apambane na Maalim Seif, yeye anazimalizia kupambana na ngome asizokuwa na uwezo hata robo ya robo wa kupambana nazo!
Intelejensia ya chadema ni kiboko angalia wasaliti wanavyodundana wenyewe. Mwigamba alikamatwa na wapenda chama chao Arusha akanynganywa laptop mambo yakatoka adharani. Zitto, Mkumbo, Mwigamba wote wakatemwa. Akaachwa mmoja ambaye kanunuliwa juzi kwa kupewa ubunge wa Ukonga
 
Intelejensia ya chadema ni kiboko angalia wasaliti wanavyodundana wenyewe. Mwigamba alikamatwa na wapenda chama chao Arusha akanynganywa laptop mambo yakatoka adharani. Zitto, Mkumbo, Mwigamba wote wakatemwa. Akaachwa mmoja ambaye kanunuliwa juzi kwa kupewa ubunge wa Ukonga
Du!,Mimi sijui hilo
 
KALAMU YA Samson Mwigamba

Zitto ajiandae kupambana na Maalim Seif, hana hadhi ya kupambana na JPM

QURAN Tukufu inasema alama za mnafiki ni tatu. Kwanza, akisema hasemi ukweli. Pili, akiaminiwa haaminiki. Na tatu, akiweka ahadi hatekelezi!

Nimekaa na kufanya kazi na wanasiasa wengi tokea niingie rasmi kwenye siasa. Katika wanasiasa wote niliofanya nao kazi mpaka leo, sijawahi kuona mwanasiasa mnafiki kama Zitto Zuberi Kabwe!

Hakuna mwanasiasa aliyewahi kumwamini Zitto Kabwe akaaminika. Kuanzia kwa Freeman Mbowe mpaka CCM ya Kikwete.

Aliaminiwa na Chacha Zakayo Wangwe hakuaminika. Siku anashirikiana na Mbowe kumshughulikia Chacha Wangwe pale Dodoma, Wangwe alimwambia Zitto Kabwe kwamba mkuki aliokuwa. anautumia kumchoma ndio huo huo utakaomchoma Zitto Kabwe mwenyewe.

Wakati anashikishwa adabu na akina Mbowe wale wale, Msafiri Mtemelwa alimkumbusha Zitto maneno ya Wangwe, akalia machozi.

Mwaka 2009 alipochukua fomu kwa mara ya kwanza ya kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA, ilikuwa ni wiki moja tu tokea apange namna ya kugawana nafasi za juu za chama na wakurugenzi wa makao makuu ya CHADEMA.

Zitto Kabwe alikaa na akina Benson Kigaila na wakurugenzi wengine makao makuu ya CHADEMA wakapanga kwamba kwa kuwa Dkt. Willibrod Slaa alikuwa ametangaza kustaafu ukatibu mkuu, basi yeye Zitto awe Katibu Mkuu, mwenyekiti taifa aendelee kuwa Freeman Mbowe. Anthony Komu awe Naibu Katibu Mkuu, nk.

Wiki moja tu, akina Kigaila wakasikia Zitto amechukua fomu ya kugombea uenyekiti wa taifa. Wengi wao wakamgeuka na kukataa huo mradi wake mpya alioshauriwa na akina Msafiri Mtemelwa. Akaanza kupanga safu nyingine tena.

Makamu mwenyekiti bara awe Mzee Philemon Ndesamburo, Katibu Mkuu awe Mzee Sylivester Masinde, Naibu Katibu Mkuu Bara awe Anthony Komu. Lakini tena wiki chache baadaye Zitto akajitoa kwenye kinyang’anyiro hicho na kumwachia Mbowe!

Kuanzisha ACT na kuondoka CHADEMA nako kulikuwa na rangi nyingi sana za Zitto Kabwe. Mwanzo kabisa aliweka msimamo kwamba CHADEMA wakimfukuza uanachama hawezi kuwa mbunge wa mahakama. Atakubali kufukuzwa waende kwenye uchaguzi mdogo.

Agombee kupitia chama kipya halafu yeye aiombe CCM (ya wakati huo) imsaidie kwa kuweka mgombea dhaifu na kuacha kumsaidia ili Zitto ashinde. Akadai kwamba akiwashinda wagombea wa CHADEMA na CCM, atakuwa amerejesha nguvu yake (renewing mandate).

Tuliposikia kikao cha kutujadili na kutufukuza uanachama kimekaribia, Zitto akasema sisi wawili tukubali kufutwa ila yeye anakwenda mahakamani kupinga kufukuzwa ili kulinda ubunge wake. Akageuka!

Alifanya hivyo kwenye kuhamia rasmi ACT, aligeuka mara tatu. Alifanya hivyo kwenye chama kusimamisha mgombea 2015. Mwanzo alitaka tuwe na mgombea, lakini tusishirikiane na Lowassa kwa namna yoyote ile. Baadaye akasema tukimpata Lowassa kuwa mgombea wetu itakuwa safi sana.

Tulipokaribia kabisa uchaguzi baada ya Dkt. Magufuli kupitishwa kuwa mgombea wa CCM akasema tusimamishe mgombea atakayeshindana na Lowassa halafu Magufuli ashinde. Na akawa anatushawishi tumteue Kitila Mkumbo awe mgombea wetu.

Alipoitwa na upande wa Lowassa akaahidiwa uwaziri mkuu, akageuka tena. Kwenye kikao cha kamati kuu akaungana na maswahiba wake kukataa mgombea wa ACT.

Baada ya Kitila kukataa kugombea, rafiki yake waliyepanga naye mwanzo kwamba wamshawishi Kitila agombee, akamfuata.
Baada ya kushawishiwa na huyo tena, akageuka kwa mara nyingine.

Akataka Kitila akubali kugombea, Kitila akakataa. Ni Zitto aliyetoa shilingi milioni 5 zilizokusanya watu mitaani Mbagala wasio wanachama wa ACT wakaja Makao Makuu ya ACT na kujifanya wana ACT wanaotaka Kitila agombee urais kupitia ACT.

Baadhi yao walipoulizwa mnayetaka agombee urais kupitia ACT anaitwa nani, walisema “Tunataka Prof. Mtikila agombee urais”. Walikuwa hawajui hata jina la Kitila.

Baada ya mpango huo kushindikana, akarudi tena kwenye mpango wa Lowassa. Alitumia nguvu kubwa sana kukishawishi chama kutosimamisha mgombea urais. Lakini Kamati Kuu na Halmashauri Kuu zikamgomea na baada ya kampeni zake dhidi yangu, hatimaye akapitishwa Mama Anna Mghwira kugombea.

Nikamwambia shida yangu ilikuwa chama kiwe na mgombea urais na siyo mimi kugombea. Niliombwa baada ya kukosekana mgombea, kwa kuwa Mama Mghwira amekubali, safi!Tuliotaka mgombea urais tukafurahi, yeye akanuna.

Akafanya mpango wa kuhujumu fomu za wadhamini wa mgombea urais mkoa wa Dar es salaam, pia akashindwa. Mwisho akaamua kususia kabisa kampeni za mgombea urais. Zitto Kabwe huyo!

Lakini ni Zitto Kabwe huyu huyu aliyegombana na akina Mbowe na Lissu walipokuwa wanampinga Magufuli baada ya kuchaguliwa. Alibaki bungeni akina mbowe waliposusia kikao cha Bunge cha Rais Magufuli kulizindua bunge, akamsifia sana Magufuli kwamba hotuba yake imetoka kwenye ilani ya ACT kwa asilimia 60.

Hata mara kadhaa alionekana kumsifia sana Magufuli wakati mwingine akimponda, na pale aliposhindwa kabisa kupata kile alichokitaka kwa Magufuli, ndipo akaamua kujiunga tena na akina Mbowe na Lissu kumpinga Magufuli hadi leo.

Huyo ni Zitto Kabwe aliyekuwa upande wa Lipumba wakati mgogoro wa ndani ya CUF umeanza. Alimsaidia Lipumba kwa kumpa vijana wa kufanya fitna. Lakini pia alimpa Lipumba wanasheria wa kumtetea kwenye kesi aliyofunguliwa na upande wa Maalim Seif.

Kabla kesi haijaisha akahamia upande wa Maalim Seif na leo Maalim Seif ni mwanachama namba moja wa ACT.

Sasa ameamua kuongeza dozi ya kumpinga Rais Magufuli. Na kwa vile sasa yuko na hasimu wa Dkt. Shein, ameanza kuwachanganya Rais Magufuli na Dkt. Shein. Ili awapendeze wagombea wake wote.

Anampinga Magufuli kwa ajili ya kumfurahisha yule mwana CCM aliyemwahidi pesa za kujengea chama anayefadhili harakati zake zote za hivi sasa na ambaye ameahidi kugombea urais wa Muungano kupitia ACT uchaguzi ujao. Wakati huo anampinga Rais Shein ili kumfurahisha Maalim Seif aliyejipanga kugombea urais wa Zanzibar kupitia ACT 2020.

Hiyo ndiyo mantiki ya mazungumzo yake na vyombo vya habari Jumanne ya wiki iliyopita. Aliponda serikali ya muungano na ile ya Zanzibar kwa pamoja. Alisema uchumi wa nchi yetu unaporomoka na akasema anatumia takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BOT) hususan tathmini za uchumi za kila mwezi.

Leo nataka niwaonyeshe uongo wake. Nimechukua ‘Tathmini ya uchumi ya kila mwezi kwa mwezi Aprili 2019’. Hebu tuipitie tuone anachokizungumza anayejiita mchumi Zitto Kabwe na kilichoelezwa na Benki Kuu ya Tanzania.

Tuanze na Wastani wa Pato la Taifa kwa mtu mmoja (GDP per capita). Wakati Rais Magufuli anaingia madarakani mwaka 2015, GDP per Capita ilikuwa dola za kimarekani 991.7. Mwaka 2016 ikapanda kuwa dola 1,006.5 na mwaka 2017 ikafikia dola 1,045.1.

Amezungumzia urari wa biashara (trade balance) katika nchi yetu. Kwa kawaida urari wa biashara unapatikana kwa kuchukua mauzo yetu ya nje na kutoa manunuzi yetu ya nje. Ili taifa lionekane linafanya vizuri kiuchumi, inatakiwa mauzo ya nje yawe makubwa kuliko manunuzi kutoka nje.

Manunuzi kutoka nje yakiwa madogo kuliko mauzo yetu nje, urari wa biashara unakuwa chanya (positive) na kadri hiyo tarakimu chanya inavyokuwa kubwa, ndivyo uchumi unavyozidi kuwa mzuri.

Mauzo ya nje yakiwa madogo kuliko manunuzi yetu toka nje, urari unakuwa hasi (negative) na kadri tarakimu hasi inavyozidi kuongezeka, ndivyo uchumi wetu unavyozidi kuonekana taaban. Twende kwenye takwimu sasa.

Tathmini ya uchumi ya Benki Kuu kwa mwezi Aprili mwaka huu inaonyesha kwamba urari wa biashara ulikuwa kama ifuatavyo: Mwaka 2013 dola -5,771.1; mwaka 2014 dola -5,723.7; mwaka 2015 dola 4,526.3; mwaka 2016 dola -3,513.9 na mwaka 2017 dola -3,027.8.

Nilijaribu pia kuangalia uwiano wa matumizi ya miradi ya maendeleo ikilinganishwa na pato la taifa (Development Expenditure to GDP ratio). Nao ulikuwa kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 5.0%; mwaka 2014/15 – 4.2%; mwaka 2015/16 – 4.3%; mwaka 2016/17 – 6.4%; na mwaka 2017/18 – 6.1%. Uwiano wa matumizi ya kawaida dhidi ya pato la taifa ni kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 12.9%; mwaka 2014/15 – 12.3%; mwaka 2015/16 – 13.2%; mwaka 2016/17 – 10.2%; na mwaka 2017/18 – 10.4%. Tumeongeza matumizi ya maendeleo wakati matumizi ya kawaida yanapungua.

Hiki kilikuwa kilio cha wapinzani enzi hizo. Tulitaka taifa litumie fedha nyingi kwenye matumizi ya maendeleo. Tulitaka hata taifa linapokopa litumie mikopo kwa matumizi ya maendeleo na si matumizi ya kawaida. Hili ndilo linalofanyika hivi sasa.

Takwimu hizi zote Zitto anadai uchumi unaporomoka. Hivi ni uchumi wa Tanzania ndio unaporomoka au ni uchumi wa Zitto ndio unaporomoka?

Mimi namfahamu Zitto kuliko watanzania wengi sana. Akiniambia uchumi wake umeporomoka, nitakubaliana naye mara moja. Sihitaji kujiuliza hata mara moja. Najua pesa alizokuwa anaziingiza kwenye ACT wakati huo achilia mbali za kwake binafsi.

Zitto Kabwe ni mbunge pekee aliyekuwa na watumishi binafsi 12. Jijini Dar es salaam alikuwa na madereva wawili, mhasibu (wa fedha zake binafsi) mmoja, mshauri wa uchumi mmoja, msaidizi maalum mmoja na katibu wake kama kiongozi wa chama mmoja.

Mjini Kigoma alikuwa na Katibu wa Mbunge mmoja, Afisa wa utawala ofisi ya Mbunge mmoja, afisa maendeleo ya jamii ofisi ya mbunge mmoja, dereva mmoja na wasaidizi maalum wa mbunge wawili. Kwa sasa kinachoendelea, Mungu ndiye anajua.

Wako waliompeleka idara ya kazi kudai mishahara yao, wapo walioamua kuacha kimya kimya bila kumwaibisha kiongozi wao, wapo wanaotaka kuondoka ila anawaahidi kila kukicha na wapo wanaovumilia.

Sasa anaponda hata hatua ya Rais kuwaita wafanyabiashara ili apate kutoka kwenye mizizi taarifa za uhakika za nini kinachoendelea kwa upande wao. Amekutana na wadau wa madini, amekuwa akikutana na wajumbe wa Baraza la Biashara Taifa, lakini wakati huu akasema akutane na wafanyabiashara wa kutoka kwenye kila wilaya ili apate taarifa muhimu.

Mkutano ule umempa picha pana na amechukua hatua muhimu za kinidhamu dhidi ya wasaidizi wake. Lakini hatua za kubadili kanuni au hata sheria zitafuata ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji kodi na kukuza biashara. Hilo nalo anaponda!

Hizi nguvu anazotumia kupambana na ‘jabali’ JPM anazipoteza bure na atazijutia. Magufuli anazidi kuchanja mbuga. Treni yake ya kuelekea uchumi wa kati imeshika kasi na kama Zitto anadhani anaweza kuizuia kwa tamaa yake ya madaraka, asimame relini kujaribu kuizuia ‘treni’ hii aone itakavyompasua vipande vipande!

Nguvu anazotumia kupambana na Magufuli, azitunze aje azitumie kupambana na Maalim Seif. Kwenye kila chama anachokuwemo Maalim Seif, kila mpemba aliyemo kwenye chama hicho anakuwa kiongozi na thamani zaidi ya kiongozi yeyote wa bara. Mpemba huyo anaweza kuelekeza jambo lolote.

Msimamo na malengo ya chama ni lazima yajikite Zanzibar kibajeti. Lazima kutakuwa na kikao cha wazanzibari walioko kwenye uongozi wa chama hicho nje ya vikao vya chama vya kikatiba kabla na baada ya vikao hivyo. Kila mtanganyika ni adui wa Zanzibar hata kama ni mwanachama wa chama alichomo Maalim Seif.

Maalim Seif ni Sultani wa pili wa Zanzibar baada ya yule wa kwanza kuondolewa kwa mapanga kwenye mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964. Sultani wa pili anawekwa mbali na ikulu kwa sanduku la kura!

Sultani huyu ana wapambe wake akina Ismail Jussa Ladhu, Salim Bimani, Nassor Mazrui na Issah Kheri. Kwenye chama chochote alichomo Maalim Seif, yeye na hawa wapambe wake ndio watakuwa na maamuzi. Hivi tunavyozungumza karibu wote hawa na wengine wengi wa upande wa Maalim Seif wameshaingizwa kwenye kamati kuu.

Baada ya uchaguzi wa ndani ya chama, watazidi kuingia wengine. Tayari mikakati ya ‘kuwapiga chini’ baadhi ya viongozi wa zamani ndani ya ACT imeshaanza.

Hata uchaguzi uliosimamiwa na viongozi wa zamani kwenye majimbo na mikoa nusura ufutwe na kamati kuu ili uanze upya. Baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 ACT itakapokuwa na wabunge wote kutoka Pemba, ndipo tutakaposhuhudia mtanange wa maana kati ya Zitto na Maalim Seif. Mmoja mnafiki, mmoja Sultani.

Badala atunze nguvu zake za kupambana aje apambane na Maalim Seif, yeye anazimalizia kupambana na ngome asizokuwa na uwezo hata robo ya robo wa kupambana nazo!
Huu uzi kilometers ngapi?
 
KALAMU YA Samson Mwigamba

Zitto ajiandae kupambana na Maalim Seif, hana hadhi ya kupambana na JPM

QURAN Tukufu inasema alama za mnafiki ni tatu. Kwanza, akisema hasemi ukweli. Pili, akiaminiwa haaminiki. Na tatu, akiweka ahadi hatekelezi!

Nimekaa na kufanya kazi na wanasiasa wengi tokea niingie rasmi kwenye siasa. Katika wanasiasa wote niliofanya nao kazi mpaka leo, sijawahi kuona mwanasiasa mnafiki kama Zitto Zuberi Kabwe!

Hakuna mwanasiasa aliyewahi kumwamini Zitto Kabwe akaaminika. Kuanzia kwa Freeman Mbowe mpaka CCM ya Kikwete.

Aliaminiwa na Chacha Zakayo Wangwe hakuaminika. Siku anashirikiana na Mbowe kumshughulikia Chacha Wangwe pale Dodoma, Wangwe alimwambia Zitto Kabwe kwamba mkuki aliokuwa. anautumia kumchoma ndio huo huo utakaomchoma Zitto Kabwe mwenyewe.

Wakati anashikishwa adabu na akina Mbowe wale wale, Msafiri Mtemelwa alimkumbusha Zitto maneno ya Wangwe, akalia machozi.

Mwaka 2009 alipochukua fomu kwa mara ya kwanza ya kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA, ilikuwa ni wiki moja tu tokea apange namna ya kugawana nafasi za juu za chama na wakurugenzi wa makao makuu ya CHADEMA.

Zitto Kabwe alikaa na akina Benson Kigaila na wakurugenzi wengine makao makuu ya CHADEMA wakapanga kwamba kwa kuwa Dkt. Willibrod Slaa alikuwa ametangaza kustaafu ukatibu mkuu, basi yeye Zitto awe Katibu Mkuu, mwenyekiti taifa aendelee kuwa Freeman Mbowe. Anthony Komu awe Naibu Katibu Mkuu, nk.

Wiki moja tu, akina Kigaila wakasikia Zitto amechukua fomu ya kugombea uenyekiti wa taifa. Wengi wao wakamgeuka na kukataa huo mradi wake mpya alioshauriwa na akina Msafiri Mtemelwa. Akaanza kupanga safu nyingine tena.

Makamu mwenyekiti bara awe Mzee Philemon Ndesamburo, Katibu Mkuu awe Mzee Sylivester Masinde, Naibu Katibu Mkuu Bara awe Anthony Komu. Lakini tena wiki chache baadaye Zitto akajitoa kwenye kinyang’anyiro hicho na kumwachia Mbowe!

Kuanzisha ACT na kuondoka CHADEMA nako kulikuwa na rangi nyingi sana za Zitto Kabwe. Mwanzo kabisa aliweka msimamo kwamba CHADEMA wakimfukuza uanachama hawezi kuwa mbunge wa mahakama. Atakubali kufukuzwa waende kwenye uchaguzi mdogo.

Agombee kupitia chama kipya halafu yeye aiombe CCM (ya wakati huo) imsaidie kwa kuweka mgombea dhaifu na kuacha kumsaidia ili Zitto ashinde. Akadai kwamba akiwashinda wagombea wa CHADEMA na CCM, atakuwa amerejesha nguvu yake (renewing mandate).

Tuliposikia kikao cha kutujadili na kutufukuza uanachama kimekaribia, Zitto akasema sisi wawili tukubali kufutwa ila yeye anakwenda mahakamani kupinga kufukuzwa ili kulinda ubunge wake. Akageuka!

Alifanya hivyo kwenye kuhamia rasmi ACT, aligeuka mara tatu. Alifanya hivyo kwenye chama kusimamisha mgombea 2015. Mwanzo alitaka tuwe na mgombea, lakini tusishirikiane na Lowassa kwa namna yoyote ile. Baadaye akasema tukimpata Lowassa kuwa mgombea wetu itakuwa safi sana.

Tulipokaribia kabisa uchaguzi baada ya Dkt. Magufuli kupitishwa kuwa mgombea wa CCM akasema tusimamishe mgombea atakayeshindana na Lowassa halafu Magufuli ashinde. Na akawa anatushawishi tumteue Kitila Mkumbo awe mgombea wetu.

Alipoitwa na upande wa Lowassa akaahidiwa uwaziri mkuu, akageuka tena. Kwenye kikao cha kamati kuu akaungana na maswahiba wake kukataa mgombea wa ACT.

Baada ya Kitila kukataa kugombea, rafiki yake waliyepanga naye mwanzo kwamba wamshawishi Kitila agombee, akamfuata.
Baada ya kushawishiwa na huyo tena, akageuka kwa mara nyingine.

Akataka Kitila akubali kugombea, Kitila akakataa. Ni Zitto aliyetoa shilingi milioni 5 zilizokusanya watu mitaani Mbagala wasio wanachama wa ACT wakaja Makao Makuu ya ACT na kujifanya wana ACT wanaotaka Kitila agombee urais kupitia ACT.

Baadhi yao walipoulizwa mnayetaka agombee urais kupitia ACT anaitwa nani, walisema “Tunataka Prof. Mtikila agombee urais”. Walikuwa hawajui hata jina la Kitila.

Baada ya mpango huo kushindikana, akarudi tena kwenye mpango wa Lowassa. Alitumia nguvu kubwa sana kukishawishi chama kutosimamisha mgombea urais. Lakini Kamati Kuu na Halmashauri Kuu zikamgomea na baada ya kampeni zake dhidi yangu, hatimaye akapitishwa Mama Anna Mghwira kugombea.

Nikamwambia shida yangu ilikuwa chama kiwe na mgombea urais na siyo mimi kugombea. Niliombwa baada ya kukosekana mgombea, kwa kuwa Mama Mghwira amekubali, safi!Tuliotaka mgombea urais tukafurahi, yeye akanuna.

Akafanya mpango wa kuhujumu fomu za wadhamini wa mgombea urais mkoa wa Dar es salaam, pia akashindwa. Mwisho akaamua kususia kabisa kampeni za mgombea urais. Zitto Kabwe huyo!

Lakini ni Zitto Kabwe huyu huyu aliyegombana na akina Mbowe na Lissu walipokuwa wanampinga Magufuli baada ya kuchaguliwa. Alibaki bungeni akina mbowe waliposusia kikao cha Bunge cha Rais Magufuli kulizindua bunge, akamsifia sana Magufuli kwamba hotuba yake imetoka kwenye ilani ya ACT kwa asilimia 60.

Hata mara kadhaa alionekana kumsifia sana Magufuli wakati mwingine akimponda, na pale aliposhindwa kabisa kupata kile alichokitaka kwa Magufuli, ndipo akaamua kujiunga tena na akina Mbowe na Lissu kumpinga Magufuli hadi leo.

Huyo ni Zitto Kabwe aliyekuwa upande wa Lipumba wakati mgogoro wa ndani ya CUF umeanza. Alimsaidia Lipumba kwa kumpa vijana wa kufanya fitna. Lakini pia alimpa Lipumba wanasheria wa kumtetea kwenye kesi aliyofunguliwa na upande wa Maalim Seif.

Kabla kesi haijaisha akahamia upande wa Maalim Seif na leo Maalim Seif ni mwanachama namba moja wa ACT.

Sasa ameamua kuongeza dozi ya kumpinga Rais Magufuli. Na kwa vile sasa yuko na hasimu wa Dkt. Shein, ameanza kuwachanganya Rais Magufuli na Dkt. Shein. Ili awapendeze wagombea wake wote.

Anampinga Magufuli kwa ajili ya kumfurahisha yule mwana CCM aliyemwahidi pesa za kujengea chama anayefadhili harakati zake zote za hivi sasa na ambaye ameahidi kugombea urais wa Muungano kupitia ACT uchaguzi ujao. Wakati huo anampinga Rais Shein ili kumfurahisha Maalim Seif aliyejipanga kugombea urais wa Zanzibar kupitia ACT 2020.

Hiyo ndiyo mantiki ya mazungumzo yake na vyombo vya habari Jumanne ya wiki iliyopita. Aliponda serikali ya muungano na ile ya Zanzibar kwa pamoja. Alisema uchumi wa nchi yetu unaporomoka na akasema anatumia takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BOT) hususan tathmini za uchumi za kila mwezi.

Leo nataka niwaonyeshe uongo wake. Nimechukua ‘Tathmini ya uchumi ya kila mwezi kwa mwezi Aprili 2019’. Hebu tuipitie tuone anachokizungumza anayejiita mchumi Zitto Kabwe na kilichoelezwa na Benki Kuu ya Tanzania.

Tuanze na Wastani wa Pato la Taifa kwa mtu mmoja (GDP per capita). Wakati Rais Magufuli anaingia madarakani mwaka 2015, GDP per Capita ilikuwa dola za kimarekani 991.7. Mwaka 2016 ikapanda kuwa dola 1,006.5 na mwaka 2017 ikafikia dola 1,045.1.

Amezungumzia urari wa biashara (trade balance) katika nchi yetu. Kwa kawaida urari wa biashara unapatikana kwa kuchukua mauzo yetu ya nje na kutoa manunuzi yetu ya nje. Ili taifa lionekane linafanya vizuri kiuchumi, inatakiwa mauzo ya nje yawe makubwa kuliko manunuzi kutoka nje.

Manunuzi kutoka nje yakiwa madogo kuliko mauzo yetu nje, urari wa biashara unakuwa chanya (positive) na kadri hiyo tarakimu chanya inavyokuwa kubwa, ndivyo uchumi unavyozidi kuwa mzuri.

Mauzo ya nje yakiwa madogo kuliko manunuzi yetu toka nje, urari unakuwa hasi (negative) na kadri tarakimu hasi inavyozidi kuongezeka, ndivyo uchumi wetu unavyozidi kuonekana taaban. Twende kwenye takwimu sasa.

Tathmini ya uchumi ya Benki Kuu kwa mwezi Aprili mwaka huu inaonyesha kwamba urari wa biashara ulikuwa kama ifuatavyo: Mwaka 2013 dola -5,771.1; mwaka 2014 dola -5,723.7; mwaka 2015 dola 4,526.3; mwaka 2016 dola -3,513.9 na mwaka 2017 dola -3,027.8.

Nilijaribu pia kuangalia uwiano wa matumizi ya miradi ya maendeleo ikilinganishwa na pato la taifa (Development Expenditure to GDP ratio). Nao ulikuwa kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 5.0%; mwaka 2014/15 – 4.2%; mwaka 2015/16 – 4.3%; mwaka 2016/17 – 6.4%; na mwaka 2017/18 – 6.1%. Uwiano wa matumizi ya kawaida dhidi ya pato la taifa ni kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 12.9%; mwaka 2014/15 – 12.3%; mwaka 2015/16 – 13.2%; mwaka 2016/17 – 10.2%; na mwaka 2017/18 – 10.4%. Tumeongeza matumizi ya maendeleo wakati matumizi ya kawaida yanapungua.

Hiki kilikuwa kilio cha wapinzani enzi hizo. Tulitaka taifa litumie fedha nyingi kwenye matumizi ya maendeleo. Tulitaka hata taifa linapokopa litumie mikopo kwa matumizi ya maendeleo na si matumizi ya kawaida. Hili ndilo linalofanyika hivi sasa.

Takwimu hizi zote Zitto anadai uchumi unaporomoka. Hivi ni uchumi wa Tanzania ndio unaporomoka au ni uchumi wa Zitto ndio unaporomoka?

Mimi namfahamu Zitto kuliko watanzania wengi sana. Akiniambia uchumi wake umeporomoka, nitakubaliana naye mara moja. Sihitaji kujiuliza hata mara moja. Najua pesa alizokuwa anaziingiza kwenye ACT wakati huo achilia mbali za kwake binafsi.

Zitto Kabwe ni mbunge pekee aliyekuwa na watumishi binafsi 12. Jijini Dar es salaam alikuwa na madereva wawili, mhasibu (wa fedha zake binafsi) mmoja, mshauri wa uchumi mmoja, msaidizi maalum mmoja na katibu wake kama kiongozi wa chama mmoja.

Mjini Kigoma alikuwa na Katibu wa Mbunge mmoja, Afisa wa utawala ofisi ya Mbunge mmoja, afisa maendeleo ya jamii ofisi ya mbunge mmoja, dereva mmoja na wasaidizi maalum wa mbunge wawili. Kwa sasa kinachoendelea, Mungu ndiye anajua.

Wako waliompeleka idara ya kazi kudai mishahara yao, wapo walioamua kuacha kimya kimya bila kumwaibisha kiongozi wao, wapo wanaotaka kuondoka ila anawaahidi kila kukicha na wapo wanaovumilia.

Sasa anaponda hata hatua ya Rais kuwaita wafanyabiashara ili apate kutoka kwenye mizizi taarifa za uhakika za nini kinachoendelea kwa upande wao. Amekutana na wadau wa madini, amekuwa akikutana na wajumbe wa Baraza la Biashara Taifa, lakini wakati huu akasema akutane na wafanyabiashara wa kutoka kwenye kila wilaya ili apate taarifa muhimu.

Mkutano ule umempa picha pana na amechukua hatua muhimu za kinidhamu dhidi ya wasaidizi wake. Lakini hatua za kubadili kanuni au hata sheria zitafuata ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji kodi na kukuza biashara. Hilo nalo anaponda!

Hizi nguvu anazotumia kupambana na ‘jabali’ JPM anazipoteza bure na atazijutia. Magufuli anazidi kuchanja mbuga. Treni yake ya kuelekea uchumi wa kati imeshika kasi na kama Zitto anadhani anaweza kuizuia kwa tamaa yake ya madaraka, asimame relini kujaribu kuizuia ‘treni’ hii aone itakavyompasua vipande vipande!

Nguvu anazotumia kupambana na Magufuli, azitunze aje azitumie kupambana na Maalim Seif. Kwenye kila chama anachokuwemo Maalim Seif, kila mpemba aliyemo kwenye chama hicho anakuwa kiongozi na thamani zaidi ya kiongozi yeyote wa bara. Mpemba huyo anaweza kuelekeza jambo lolote.

Msimamo na malengo ya chama ni lazima yajikite Zanzibar kibajeti. Lazima kutakuwa na kikao cha wazanzibari walioko kwenye uongozi wa chama hicho nje ya vikao vya chama vya kikatiba kabla na baada ya vikao hivyo. Kila mtanganyika ni adui wa Zanzibar hata kama ni mwanachama wa chama alichomo Maalim Seif.

Maalim Seif ni Sultani wa pili wa Zanzibar baada ya yule wa kwanza kuondolewa kwa mapanga kwenye mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964. Sultani wa pili anawekwa mbali na ikulu kwa sanduku la kura!

Sultani huyu ana wapambe wake akina Ismail Jussa Ladhu, Salim Bimani, Nassor Mazrui na Issah Kheri. Kwenye chama chochote alichomo Maalim Seif, yeye na hawa wapambe wake ndio watakuwa na maamuzi. Hivi tunavyozungumza karibu wote hawa na wengine wengi wa upande wa Maalim Seif wameshaingizwa kwenye kamati kuu.

Baada ya uchaguzi wa ndani ya chama, watazidi kuingia wengine. Tayari mikakati ya ‘kuwapiga chini’ baadhi ya viongozi wa zamani ndani ya ACT imeshaanza.

Hata uchaguzi uliosimamiwa na viongozi wa zamani kwenye majimbo na mikoa nusura ufutwe na kamati kuu ili uanze upya. Baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 ACT itakapokuwa na wabunge wote kutoka Pemba, ndipo tutakaposhuhudia mtanange wa maana kati ya Zitto na Maalim Seif. Mmoja mnafiki, mmoja Sultani.

Badala atunze nguvu zake za kupambana aje apambane na Maalim Seif, yeye anazimalizia kupambana na ngome asizokuwa na uwezo hata robo ya robo wa kupambana nazo!
Kunauwezekano Zitto ni CCM Project
 
KALAMU YA Samson Mwigamba

Zitto ajiandae kupambana na Maalim Seif, hana hadhi ya kupambana na JPM

QURAN Tukufu inasema alama za mnafiki ni tatu. Kwanza, akisema hasemi ukweli. Pili, akiaminiwa haaminiki. Na tatu, akiweka ahadi hatekelezi!

Nimekaa na kufanya kazi na wanasiasa wengi tokea niingie rasmi kwenye siasa. Katika wanasiasa wote niliofanya nao kazi mpaka leo, sijawahi kuona mwanasiasa mnafiki kama Zitto Zuberi Kabwe!

Hakuna mwanasiasa aliyewahi kumwamini Zitto Kabwe akaaminika. Kuanzia kwa Freeman Mbowe mpaka CCM ya Kikwete.

Aliaminiwa na Chacha Zakayo Wangwe hakuaminika. Siku anashirikiana na Mbowe kumshughulikia Chacha Wangwe pale Dodoma, Wangwe alimwambia Zitto Kabwe kwamba mkuki aliokuwa. anautumia kumchoma ndio huo huo utakaomchoma Zitto Kabwe mwenyewe.

Wakati anashikishwa adabu na akina Mbowe wale wale, Msafiri Mtemelwa alimkumbusha Zitto maneno ya Wangwe, akalia machozi.

Mwaka 2009 alipochukua fomu kwa mara ya kwanza ya kugombea uenyekiti wa taifa wa CHADEMA, ilikuwa ni wiki moja tu tokea apange namna ya kugawana nafasi za juu za chama na wakurugenzi wa makao makuu ya CHADEMA.

Zitto Kabwe alikaa na akina Benson Kigaila na wakurugenzi wengine makao makuu ya CHADEMA wakapanga kwamba kwa kuwa Dkt. Willibrod Slaa alikuwa ametangaza kustaafu ukatibu mkuu, basi yeye Zitto awe Katibu Mkuu, mwenyekiti taifa aendelee kuwa Freeman Mbowe. Anthony Komu awe Naibu Katibu Mkuu, nk.

Wiki moja tu, akina Kigaila wakasikia Zitto amechukua fomu ya kugombea uenyekiti wa taifa. Wengi wao wakamgeuka na kukataa huo mradi wake mpya alioshauriwa na akina Msafiri Mtemelwa. Akaanza kupanga safu nyingine tena.

Makamu mwenyekiti bara awe Mzee Philemon Ndesamburo, Katibu Mkuu awe Mzee Sylivester Masinde, Naibu Katibu Mkuu Bara awe Anthony Komu. Lakini tena wiki chache baadaye Zitto akajitoa kwenye kinyang’anyiro hicho na kumwachia Mbowe!

Kuanzisha ACT na kuondoka CHADEMA nako kulikuwa na rangi nyingi sana za Zitto Kabwe. Mwanzo kabisa aliweka msimamo kwamba CHADEMA wakimfukuza uanachama hawezi kuwa mbunge wa mahakama. Atakubali kufukuzwa waende kwenye uchaguzi mdogo.

Agombee kupitia chama kipya halafu yeye aiombe CCM (ya wakati huo) imsaidie kwa kuweka mgombea dhaifu na kuacha kumsaidia ili Zitto ashinde. Akadai kwamba akiwashinda wagombea wa CHADEMA na CCM, atakuwa amerejesha nguvu yake (renewing mandate).

Tuliposikia kikao cha kutujadili na kutufukuza uanachama kimekaribia, Zitto akasema sisi wawili tukubali kufutwa ila yeye anakwenda mahakamani kupinga kufukuzwa ili kulinda ubunge wake. Akageuka!

Alifanya hivyo kwenye kuhamia rasmi ACT, aligeuka mara tatu. Alifanya hivyo kwenye chama kusimamisha mgombea 2015. Mwanzo alitaka tuwe na mgombea, lakini tusishirikiane na Lowassa kwa namna yoyote ile. Baadaye akasema tukimpata Lowassa kuwa mgombea wetu itakuwa safi sana.

Tulipokaribia kabisa uchaguzi baada ya Dkt. Magufuli kupitishwa kuwa mgombea wa CCM akasema tusimamishe mgombea atakayeshindana na Lowassa halafu Magufuli ashinde. Na akawa anatushawishi tumteue Kitila Mkumbo awe mgombea wetu.

Alipoitwa na upande wa Lowassa akaahidiwa uwaziri mkuu, akageuka tena. Kwenye kikao cha kamati kuu akaungana na maswahiba wake kukataa mgombea wa ACT.

Baada ya Kitila kukataa kugombea, rafiki yake waliyepanga naye mwanzo kwamba wamshawishi Kitila agombee, akamfuata.
Baada ya kushawishiwa na huyo tena, akageuka kwa mara nyingine.

Akataka Kitila akubali kugombea, Kitila akakataa. Ni Zitto aliyetoa shilingi milioni 5 zilizokusanya watu mitaani Mbagala wasio wanachama wa ACT wakaja Makao Makuu ya ACT na kujifanya wana ACT wanaotaka Kitila agombee urais kupitia ACT.

Baadhi yao walipoulizwa mnayetaka agombee urais kupitia ACT anaitwa nani, walisema “Tunataka Prof. Mtikila agombee urais”. Walikuwa hawajui hata jina la Kitila.

Baada ya mpango huo kushindikana, akarudi tena kwenye mpango wa Lowassa. Alitumia nguvu kubwa sana kukishawishi chama kutosimamisha mgombea urais. Lakini Kamati Kuu na Halmashauri Kuu zikamgomea na baada ya kampeni zake dhidi yangu, hatimaye akapitishwa Mama Anna Mghwira kugombea.

Nikamwambia shida yangu ilikuwa chama kiwe na mgombea urais na siyo mimi kugombea. Niliombwa baada ya kukosekana mgombea, kwa kuwa Mama Mghwira amekubali, safi!Tuliotaka mgombea urais tukafurahi, yeye akanuna.

Akafanya mpango wa kuhujumu fomu za wadhamini wa mgombea urais mkoa wa Dar es salaam, pia akashindwa. Mwisho akaamua kususia kabisa kampeni za mgombea urais. Zitto Kabwe huyo!

Lakini ni Zitto Kabwe huyu huyu aliyegombana na akina Mbowe na Lissu walipokuwa wanampinga Magufuli baada ya kuchaguliwa. Alibaki bungeni akina mbowe waliposusia kikao cha Bunge cha Rais Magufuli kulizindua bunge, akamsifia sana Magufuli kwamba hotuba yake imetoka kwenye ilani ya ACT kwa asilimia 60.

Hata mara kadhaa alionekana kumsifia sana Magufuli wakati mwingine akimponda, na pale aliposhindwa kabisa kupata kile alichokitaka kwa Magufuli, ndipo akaamua kujiunga tena na akina Mbowe na Lissu kumpinga Magufuli hadi leo.

Huyo ni Zitto Kabwe aliyekuwa upande wa Lipumba wakati mgogoro wa ndani ya CUF umeanza. Alimsaidia Lipumba kwa kumpa vijana wa kufanya fitna. Lakini pia alimpa Lipumba wanasheria wa kumtetea kwenye kesi aliyofunguliwa na upande wa Maalim Seif.

Kabla kesi haijaisha akahamia upande wa Maalim Seif na leo Maalim Seif ni mwanachama namba moja wa ACT.

Sasa ameamua kuongeza dozi ya kumpinga Rais Magufuli. Na kwa vile sasa yuko na hasimu wa Dkt. Shein, ameanza kuwachanganya Rais Magufuli na Dkt. Shein. Ili awapendeze wagombea wake wote.

Anampinga Magufuli kwa ajili ya kumfurahisha yule mwana CCM aliyemwahidi pesa za kujengea chama anayefadhili harakati zake zote za hivi sasa na ambaye ameahidi kugombea urais wa Muungano kupitia ACT uchaguzi ujao. Wakati huo anampinga Rais Shein ili kumfurahisha Maalim Seif aliyejipanga kugombea urais wa Zanzibar kupitia ACT 2020.

Hiyo ndiyo mantiki ya mazungumzo yake na vyombo vya habari Jumanne ya wiki iliyopita. Aliponda serikali ya muungano na ile ya Zanzibar kwa pamoja. Alisema uchumi wa nchi yetu unaporomoka na akasema anatumia takwimu za Benki Kuu ya Tanzania (BOT) hususan tathmini za uchumi za kila mwezi.

Leo nataka niwaonyeshe uongo wake. Nimechukua ‘Tathmini ya uchumi ya kila mwezi kwa mwezi Aprili 2019’. Hebu tuipitie tuone anachokizungumza anayejiita mchumi Zitto Kabwe na kilichoelezwa na Benki Kuu ya Tanzania.

Tuanze na Wastani wa Pato la Taifa kwa mtu mmoja (GDP per capita). Wakati Rais Magufuli anaingia madarakani mwaka 2015, GDP per Capita ilikuwa dola za kimarekani 991.7. Mwaka 2016 ikapanda kuwa dola 1,006.5 na mwaka 2017 ikafikia dola 1,045.1.

Amezungumzia urari wa biashara (trade balance) katika nchi yetu. Kwa kawaida urari wa biashara unapatikana kwa kuchukua mauzo yetu ya nje na kutoa manunuzi yetu ya nje. Ili taifa lionekane linafanya vizuri kiuchumi, inatakiwa mauzo ya nje yawe makubwa kuliko manunuzi kutoka nje.

Manunuzi kutoka nje yakiwa madogo kuliko mauzo yetu nje, urari wa biashara unakuwa chanya (positive) na kadri hiyo tarakimu chanya inavyokuwa kubwa, ndivyo uchumi unavyozidi kuwa mzuri.

Mauzo ya nje yakiwa madogo kuliko manunuzi yetu toka nje, urari unakuwa hasi (negative) na kadri tarakimu hasi inavyozidi kuongezeka, ndivyo uchumi wetu unavyozidi kuonekana taaban. Twende kwenye takwimu sasa.

Tathmini ya uchumi ya Benki Kuu kwa mwezi Aprili mwaka huu inaonyesha kwamba urari wa biashara ulikuwa kama ifuatavyo: Mwaka 2013 dola -5,771.1; mwaka 2014 dola -5,723.7; mwaka 2015 dola 4,526.3; mwaka 2016 dola -3,513.9 na mwaka 2017 dola -3,027.8.

Nilijaribu pia kuangalia uwiano wa matumizi ya miradi ya maendeleo ikilinganishwa na pato la taifa (Development Expenditure to GDP ratio). Nao ulikuwa kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 5.0%; mwaka 2014/15 – 4.2%; mwaka 2015/16 – 4.3%; mwaka 2016/17 – 6.4%; na mwaka 2017/18 – 6.1%. Uwiano wa matumizi ya kawaida dhidi ya pato la taifa ni kama ifuatavyo:

Mwaka wa fedha 2013/14 – 12.9%; mwaka 2014/15 – 12.3%; mwaka 2015/16 – 13.2%; mwaka 2016/17 – 10.2%; na mwaka 2017/18 – 10.4%. Tumeongeza matumizi ya maendeleo wakati matumizi ya kawaida yanapungua.

Hiki kilikuwa kilio cha wapinzani enzi hizo. Tulitaka taifa litumie fedha nyingi kwenye matumizi ya maendeleo. Tulitaka hata taifa linapokopa litumie mikopo kwa matumizi ya maendeleo na si matumizi ya kawaida. Hili ndilo linalofanyika hivi sasa.

Takwimu hizi zote Zitto anadai uchumi unaporomoka. Hivi ni uchumi wa Tanzania ndio unaporomoka au ni uchumi wa Zitto ndio unaporomoka?

Mimi namfahamu Zitto kuliko watanzania wengi sana. Akiniambia uchumi wake umeporomoka, nitakubaliana naye mara moja. Sihitaji kujiuliza hata mara moja. Najua pesa alizokuwa anaziingiza kwenye ACT wakati huo achilia mbali za kwake binafsi.

Zitto Kabwe ni mbunge pekee aliyekuwa na watumishi binafsi 12. Jijini Dar es salaam alikuwa na madereva wawili, mhasibu (wa fedha zake binafsi) mmoja, mshauri wa uchumi mmoja, msaidizi maalum mmoja na katibu wake kama kiongozi wa chama mmoja.

Mjini Kigoma alikuwa na Katibu wa Mbunge mmoja, Afisa wa utawala ofisi ya Mbunge mmoja, afisa maendeleo ya jamii ofisi ya mbunge mmoja, dereva mmoja na wasaidizi maalum wa mbunge wawili. Kwa sasa kinachoendelea, Mungu ndiye anajua.

Wako waliompeleka idara ya kazi kudai mishahara yao, wapo walioamua kuacha kimya kimya bila kumwaibisha kiongozi wao, wapo wanaotaka kuondoka ila anawaahidi kila kukicha na wapo wanaovumilia.

Sasa anaponda hata hatua ya Rais kuwaita wafanyabiashara ili apate kutoka kwenye mizizi taarifa za uhakika za nini kinachoendelea kwa upande wao. Amekutana na wadau wa madini, amekuwa akikutana na wajumbe wa Baraza la Biashara Taifa, lakini wakati huu akasema akutane na wafanyabiashara wa kutoka kwenye kila wilaya ili apate taarifa muhimu.

Mkutano ule umempa picha pana na amechukua hatua muhimu za kinidhamu dhidi ya wasaidizi wake. Lakini hatua za kubadili kanuni au hata sheria zitafuata ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji kodi na kukuza biashara. Hilo nalo anaponda!

Hizi nguvu anazotumia kupambana na ‘jabali’ JPM anazipoteza bure na atazijutia. Magufuli anazidi kuchanja mbuga. Treni yake ya kuelekea uchumi wa kati imeshika kasi na kama Zitto anadhani anaweza kuizuia kwa tamaa yake ya madaraka, asimame relini kujaribu kuizuia ‘treni’ hii aone itakavyompasua vipande vipande!

Nguvu anazotumia kupambana na Magufuli, azitunze aje azitumie kupambana na Maalim Seif. Kwenye kila chama anachokuwemo Maalim Seif, kila mpemba aliyemo kwenye chama hicho anakuwa kiongozi na thamani zaidi ya kiongozi yeyote wa bara. Mpemba huyo anaweza kuelekeza jambo lolote.

Msimamo na malengo ya chama ni lazima yajikite Zanzibar kibajeti. Lazima kutakuwa na kikao cha wazanzibari walioko kwenye uongozi wa chama hicho nje ya vikao vya chama vya kikatiba kabla na baada ya vikao hivyo. Kila mtanganyika ni adui wa Zanzibar hata kama ni mwanachama wa chama alichomo Maalim Seif.

Maalim Seif ni Sultani wa pili wa Zanzibar baada ya yule wa kwanza kuondolewa kwa mapanga kwenye mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964. Sultani wa pili anawekwa mbali na ikulu kwa sanduku la kura!

Sultani huyu ana wapambe wake akina Ismail Jussa Ladhu, Salim Bimani, Nassor Mazrui na Issah Kheri. Kwenye chama chochote alichomo Maalim Seif, yeye na hawa wapambe wake ndio watakuwa na maamuzi. Hivi tunavyozungumza karibu wote hawa na wengine wengi wa upande wa Maalim Seif wameshaingizwa kwenye kamati kuu.

Baada ya uchaguzi wa ndani ya chama, watazidi kuingia wengine. Tayari mikakati ya ‘kuwapiga chini’ baadhi ya viongozi wa zamani ndani ya ACT imeshaanza.

Hata uchaguzi uliosimamiwa na viongozi wa zamani kwenye majimbo na mikoa nusura ufutwe na kamati kuu ili uanze upya. Baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 ACT itakapokuwa na wabunge wote kutoka Pemba, ndipo tutakaposhuhudia mtanange wa maana kati ya Zitto na Maalim Seif. Mmoja mnafiki, mmoja Sultani.

Badala atunze nguvu zake za kupambana aje apambane na Maalim Seif, yeye anazimalizia kupambana na ngome asizokuwa na uwezo hata robo ya robo wa kupambana nazo!
Umeandika Ukweli mtupu Vijana tuwe makini sna na Zitto Nape Bashe ni zaidi ya Wanafiki nimewai kuleta Uzi humu khs watu hao...
 
Back
Top Bottom