Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,172
- 20,641
Salma Kikwete ambaye ni Mwalimu Mstaafu wa Oystrbay Primary, Mbunge huko Mtwara na pia Mmiliki. wa WAMA -NGO ya Kitajiri:
Ikumbukwe huyu Salma Kikwete alikuwa Mwalimu shule ya Msingi{elimu yake nadhani mnaijua} , kakatishwa kazi , mshahara wa Certificate ya ualimu ni 420,000/kwa mwezi mwaka 2004}- LAKI NNE NA NUSU , sasa basi kwa kumkatisha kazi maisha yake yakawa magumu na ndio maana kaomba yeye na wenzake waliokatishwa kazi walipwe:
Ikumbukwe huyu Salma Kikwete alikuwa Mwalimu shule ya Msingi{elimu yake nadhani mnaijua} , kakatishwa kazi , mshahara wa Certificate ya ualimu ni 420,000/kwa mwezi mwaka 2004}- LAKI NNE NA NUSU , sasa basi kwa kumkatisha kazi maisha yake yakawa magumu na ndio maana kaomba yeye na wenzake waliokatishwa kazi walipwe:
Wenza ni :
1. Maria Nyerere.
2. Siti Mwinyi.
3 Anna Mkapa.
4. Salma Kikwete
5. Janeth Magufuli
Bunge lijalo 2024 , kama atatokea kiongozi mwengine mwenye IQ kubwa kama ya Salma basi ipendekezwe na watoto wa wastaafu wapewe mafao, baba zao na mama zao wametumikia nchi, wametumia muda mwingi kufikiria taidfa na kuliongoza taifa.
Kifungu kipya cha 13 ambapo makamu wa rais anapofariki akiwa madarakani, au baada ya kustaafu (kabla hajalipwa mafao yake), wategemezi wake (dependants) watalipwa kiasi cha fedha sawa na mshahara wote wa makamu wa rais alioupokea wakati akiwa madarakani. Mfano, kama makamu wa rais alikaa madarakani kwa miaka 10, akalipwa TZS 2B kama mshahara, basi wategemezi wake watalipwa kiasi hiko cha TZS 2B kama pension. Ifahamike, kwa mujibu wa sheria hii, neno "dependants" limefafanuliwa kwenye kifungu cha 4, na maana yake ni mke au wake, mume, watoto (ambao walikuwa ni tegemezi kwa marehemu), pamoja na wazazi wa marehemu (wategemezi).
Badiliko la JEDWALI la sheria hii linalotaja nyongeza ya mafao ya viongozi.
1. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka magari 2, sasa atapata magari 3 yasiyopungua uzito wa tani 3 (yaani hawezi pewa Corola, bali ni gari kubwa kama V8 ,vxr nk, ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.
2. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 2 na sasa atapewa 3.
3. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.
4. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.
5. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.
6. Makamu wa Rais atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.
7. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Makamu wa Rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama Makamu wa Rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.
8. Makamu wa Rais atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.
9. Waziri Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.
10. Warizi Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.
11. Waziri Mkuu mstaafu atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.
12. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Waziri Mkuu mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake atakapofariki.
13. Waziri Mkuu atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.
14. Mjane wa Rais mstaafu, kwa sheria ya sasa anapata 40% ya mshahara wa rais aliye madarakani kila mwezi kama "maintenance allowance", asilimia hii imepanda sasa atalipwa 60%.
15. Sheria ya sasa inatoa gharama za matibabu kwa mjane wa Rais mstaafu kwenye hospitali za ndani ya nchi tu, lakini badiliko la sheria mpya, atalipiwa na Serikali matibabu ya hospitali za nje ya nchi pia.
16. Mjane wa Rais mstaafu ameongezewa huduma za gari toka gari moja mpaka magari mawili, na dereva 2 kufanya shughuli zake za kila siku. Serikali inalipia gharama za mafuta pia. Magari haya yatakuwa yanabadilishwa kila baada ya miaka 5. Pia, ameongezewa mpishi, mfua nguo na mtunza bustani. Atapata ulinzi wa TISS.
17. Mjane wa Makamu wa Rais, anapata stahiki kama za mjane wa rais isipokuwa tofauti yake ni moja, yeye atapata gari moja la Serikali na dereva mmoja.
18. Mjane wa Waziri Mkuu mstaafu anapata stahiki za ziada kama mjane wa Makamu wa Rais, isipokuwa gari analotumia la Serikali litakuwa linabadilishwa kila baada ya miaka 7.
19. Hili ni badiliko linalohusu Waziri, Naibu Waziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wastaafu ambapo watapata ziada ya mafao yao: wind-up allowance, Diplomatic passport kwao na wenza wao, gari moja ambalo atapewa jipya kila baada ya miaka 5, Ulinzi wa TISS, Msaidizi mmoja, Bima ya Afya bure yeye na mwenza wake, Matumizi ya VIP lounge.
20. Hii ni nyongeza kwa Spika wa Bunge kwenye mafao yake: gari moja, Bima ya Afya yake binafsi, matumizi ya VIP lounge, pia anapata stahiki nyingine kama LITA 70 za mafuta kwa wiki.
Kifungu kipya cha 13 ambapo makamu wa rais anapofariki akiwa madarakani, au baada ya kustaafu (kabla hajalipwa mafao yake), wategemezi wake (dependants) watalipwa kiasi cha fedha sawa na mshahara wote wa makamu wa rais alioupokea wakati akiwa madarakani. Mfano, kama makamu wa rais alikaa madarakani kwa miaka 10, akalipwa TZS 2B kama mshahara, basi wategemezi wake watalipwa kiasi hiko cha TZS 2B kama pension. Ifahamike, kwa mujibu wa sheria hii, neno "dependants" limefafanuliwa kwenye kifungu cha 4, na maana yake ni mke au wake, mume, watoto (ambao walikuwa ni tegemezi kwa marehemu), pamoja na wazazi wa marehemu (wategemezi).
Badiliko la JEDWALI la sheria hii linalotaja nyongeza ya mafao ya viongozi.
1. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka magari 2, sasa atapata magari 3 yasiyopungua uzito wa tani 3 (yaani hawezi pewa Corola, bali ni gari kubwa kama V8 ,vxr nk, ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.
2. Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 2 na sasa atapewa 3.
3. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.
4. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.
5. Makamu wa Rais mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.
6. Makamu wa Rais atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.
7. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Makamu wa Rais mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake. Yaani kama Makamu wa Rais mstaafu atafiwa na mke/mume wake, basi Serikali itagharamia mazishi hayo.
8. Makamu wa Rais atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.
9. Waziri Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya magari kutoka gari 1, sasa atapata magari 2 yasiyopungua uzito wa tani 3 ambapo atapewa magari mapya kila baada ya miaka 5.
10. Warizi Mkuu mstaafu ameongezewa idadi ya madereva toka 1 na sasa atapewa madereva 2.
11. Waziri Mkuu mstaafu atajengewa nyumba ya kifahari. Ikumbukwe, kwa sheria ya sasa, ni Rais mstaafu pekee ndiye anajengewa nyumba.
12. Sheria ya sasa inataja gharama za mazishi kwa Waziri Mkuu mstaafu tu, nyongeza iliyowekwa ni gharama ya mazishi kwa mwenza wake atakapofariki.
13. Waziri Mkuu atapewa ulinzi yeye binafsi,na wana familia wake kama mke/mume na watoto. Ulinzi huu utatolewa na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kutokana na mabadiliko ya sheria ya TISS ya hivi karibuni.
14. Mjane wa Rais mstaafu, kwa sheria ya sasa anapata 40% ya mshahara wa rais aliye madarakani kila mwezi kama "maintenance allowance", asilimia hii imepanda sasa atalipwa 60%.
15. Sheria ya sasa inatoa gharama za matibabu kwa mjane wa Rais mstaafu kwenye hospitali za ndani ya nchi tu, lakini badiliko la sheria mpya, atalipiwa na Serikali matibabu ya hospitali za nje ya nchi pia.
16. Mjane wa Rais mstaafu ameongezewa huduma za gari toka gari moja mpaka magari mawili, na dereva 2 kufanya shughuli zake za kila siku. Serikali inalipia gharama za mafuta pia. Magari haya yatakuwa yanabadilishwa kila baada ya miaka 5. Pia, ameongezewa mpishi, mfua nguo na mtunza bustani. Atapata ulinzi wa TISS.
17. Mjane wa Makamu wa Rais, anapata stahiki kama za mjane wa rais isipokuwa tofauti yake ni moja, yeye atapata gari moja la Serikali na dereva mmoja.
18. Mjane wa Waziri Mkuu mstaafu anapata stahiki za ziada kama mjane wa Makamu wa Rais, isipokuwa gari analotumia la Serikali litakuwa linabadilishwa kila baada ya miaka 7.
19. Hili ni badiliko linalohusu Waziri, Naibu Waziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wastaafu ambapo watapata ziada ya mafao yao: wind-up allowance, Diplomatic passport kwao na wenza wao, gari moja ambalo atapewa jipya kila baada ya miaka 5, Ulinzi wa TISS, Msaidizi mmoja, Bima ya Afya bure yeye na mwenza wake, Matumizi ya VIP lounge.
20. Hii ni nyongeza kwa Spika wa Bunge kwenye mafao yake: gari moja, Bima ya Afya yake binafsi, matumizi ya VIP lounge, pia anapata stahiki nyingine kama LITA 70 za mafuta kwa wiki.
NOTE: Pongezi kwa Wenza, walikuwa wanaishi kimaskini Sana !
View: https://www.youtube.com/watch?v=fYGKoLzTWRg