Matokeo ya Arumeru mashariki yamenipa raha sana,nawapa salamu zangu za dhati viongozi wa dini niliowataja hapo juu na wengine wanaofanana nao ya kwamba wananchi tukiamua kufanya kitu hawawezi kutuzuia. Wamekuwa msitari wa mbele kumsafisha Lowasa na maufisadi yake na kudhani wananchi wote wanapumbazika kumbe kumekucha,wananchi wanajitambua vilivyo. Na infact wanatakiwa kujua heshima waliyonayo ni sisi wananchi tunawapa ila kwa mwendo huu wa kuambatana na mafisadi tutawapuuza na hawataweza kutuzuia. Kila siku mtu mmoja anasimika maaskofu,mara harambee mara kuchangia shule,mara kwenye maulidi usiku asbh yake kusimika askofu!!!!how?why???viongozi wa dini mnatumika siyo bure...harambee kigoma mara shinyanga mara moro mara dar..kwa nini mtu huyo huyo? Tena mwenye kashfa?? Kwa matokeo ya arumeru mjifunze,tumewashinda wote mafisadi na matawi yao na wote wanaowasafisha...ccm inasemekana ziko kadhaa na hatukuchagua tumepiga kichwani wote ili waamke itachukua muda.hizi ni salamu zangu kwenu viongozi wa dini na wote mnaodhani mna mbeleko ya kubeba mafisadi.