Sakata la nauli za vivuko: Magufuli asema asiye na nauli Sh. 200 apige mbizi

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,896
Magufuli achafua hali ya hewa Dar

WAZIRI wa Ujenzi, Dk John Magufuli amechafua hali ya hewa na kuingia kwenye mgogoro na wakazi wa Kigamboni, Dar es Salaam baada ya kuwaeleza kuwa ni lazima walipe nauli mpya za vivuko vya Mv Kigamboni na Alina na kama watashindwa, wapige mbizi baharini kuvuka. Kauli hiyo ya Dk Magufuli imekuja siku mbili baada ya wizara hiyo kutangaza viwango vipya vya nauli mnamo Desemba 29, mwaka jana ambavyo vimepanda kwa asilimia 100 na vilianza kutumika jana Januari Mosi nchi nzima.


Baada ya kutangazwa kwa viwango hivyo vipya vya nauli, wakazi wengi wa Kigamboni walipinga kutokana na kile wanachosema hawakushirikishwa na ndipo jana asubuhi, Dk Magufuli alipoamua kufanya ziara ya ghafla katika vivuko hivyo na kusisitiza kwamba viwango hivyo lazima vilipwe. Katika ziara hiyo, vyanzo vya kuaminika vilisema Dk Magufuli alipofika eneo hilo la Kivukoni, alitoa msimamo huo na ndipo wananchi waliokuwa wakimsikiliza walipoanza kumzomea na kukatisha hotuba yake mara kwa mara.

Vyanzo hivyo viliongeza kwamba, kitendo hicho cha zomeazomea, kilimkera Dk Magufuli ambaye pamoja na mambo mengine, alisisitiza nauli hizo lazima zilipwe na mtu asiyetaka ni vyema akapiga mbizi kwa kuogelea kutoka Kigamboni hadi ng'ambo ya pili au apite Kongowe kuingia katika katikati ya jiji.

Msemaji: Waziri amechukizwa
Akizungumzia tukio hilo, Msemaji Mkuu wa wizara hiyo, Martin Ntemo alisema Waziri Magufuli hakufurahishwa na kitendo cha baadhi ya watu kumzomea wakati alipokuwa akizungumza... "Amechukizwa na baadhi ya watu kuzomea wakati alipokuwa akizungumza. Alichokuwa akisisitiza ni kwamba nauli mpya lazima ilipwe lakini wapo waliokuwa hawataki kuelewa wakawa wanapinga." Alisema kuna watu walikuwa wamepangwa kufanya mgomo kupinga nauli mpya kitendo ambacho pia kilimkera waziri alipokuwa kwenye ziara hiyo.


Magufuli na waandishi
Baada ya kuzomewa Kigamboni, Dk Magufuli alifanya mkutano na waandishi wa habari na kusisitiza kwamba, "Kuanzia Januari, Mosi, mwaka huu Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), imeongeza viwango vya nauli katika vivuko vyote vya Serikali nchini." Alisema kwa muda wa miaka 14 iliyopita Kivuko cha Kigamboni kimekuwa kikitoza nauli ya Sh100 kwa mtu mmoja, wakati vivuko vingine vyote nchini, vimepandisha nauli zaidi ya mara mbili tangu mwaka 1997 kuendana na gharama za uendeshaji. "'Kwa mfano, Kivuko cha Pangani ambako umbali wa uvushaji hauzidi ule wa Magogoni kilikuwa kinatoza Sh 200 na hali ya uchumi kwa wananchi ni ya chini kuliko Dar es Salaam. Kivuko cha Kilombero kilikuwa kikitoza Sh200 ikilinganishwa na Sh100 zilizokuwa zikitozwa hapa Magogoni."


Dk Magufuli alitaja sababu zilizochangia kupandisha nauli hizo kwamba ni pamoja na ongezeko la mishahara ya watumishi serikalini kwa zaidi ya asilimia 100, ongezeko alilosema la zaidi ya asilimia 400 la bei ya mafuta ya dizeli na mafuta ya kulainishia mitambo ambayo hutumika kuendeshea vivuko hivyo. Alitaja sababu nyingine kwamba ni pamoja na: "Ongezeko la bei za vipuri na kodi zake linalowiana na kushuka kwa thamani ya shilingi na ongezeko la bei kwa jumla."

Alisema upandishaji wa nauli hizo ulifanywa kwa kuzingatia taratibu za kisheria na hatimaye kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali toleo Na. 367 la Novemba 4, mwaka jana kwa mujibu wa sheria za uendeshaji wa vivuko vya Serikali. "Sura 173 Kifungu cha 11(b), mwenye mamlaka ya kupanga nauli za vivuko vya Serikali ni Waziri mwenye dhamana na vivuko vya Serikali. Hata hivyo, kabla ya kufikia uamuzi huu, kumekuwa na jitihada za aina mbalimbali katika kuimarisha mapato ya vivuko. Machi, 2009, Wakala wa Ufundi na Umeme wakishirikiana na Jeshi la Polisi pamoja na Askari kutoka Kikosi cha Wanamaji waliendesha zoezi la kudhibiti mapato ya Kivuko."

Alisema hilo liliwahi kufanywa na na Kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart mnamo Aprili 17 hadi 20, mwaka jana kwa makubaliano na Temesa. "Zoezi hilo liliendeshwa tena Septemba 16 hadi 20, 2010 na Wizara kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi." Alisema Julai, 2011, Temesa iliamua kubadili wakata tiketi na kuajiri wengine akisisitiza kuwa Serikali imechukua hatua mbalimbali kupambana na matukio ya watumishi wasio waaminifu. Hatua nyingine ni ile ya Temesa kuondoa askari wa kuajiriwa na badala yake kuingia mikataba na kampuni za ulinzi. "Kwa sasa katika Kivuko cha Magogoni, Kampuni ya ulinzi ya Suma JKT ndiyo inayotumika kufanya kazi hiyo," alisema.

Alisema juhudi hizo zimesaidia kuongeza mapato kwa siku kutoka Sh5.5 milioni mwaka 2009 hadi Sh9 milioni kwa sasa katika Kivuko cha Magogoni na kusisitiza kwamba wizara itaendeleza hatua hizi kwa lengo la kubana uvujaji wa mapato na matumizi yasiyo ya lazima kwa vivuko vyote. Magufuli alisema kwa utaratibu, watumiaji wote wa huduma za vivuko wanatakiwa walipie huduma hiyo na kuongeza: "Tunaomba utaratibu huu uzingatiwe isipokuwa kwa wanafunzi waliovaa sare za shule. Tunasisitiza watumiaji wa vivuko waheshimu sheria na taratibu zote za vivuko kwa ajili ya usalama wao na ufanisi wa huduma."



Mbunge achukizwa

Kwa upande wake Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile alikiri kusikia maneno ya Magufuli ambayo hayakuwafurahisha wapiga kura wake na kuahidi kuendelea kufuatilia kujua undani hasa wa kauli hizo. Dk Ndugulile alifafanua kwamba baada ya tangazo hilo la ongezeko la nauli, aliwasiliana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki na taarifa alizonazo ni kwamba nauli hizo zimesitishwa.Alifafanua kwamba baada ya kuwasiliana na waziri mkuu, jibu alilopata jana saa 1: 00 usiku ni kwamba mpango huo wa kupandisha nauli umesitishwa hadi hapo itakapoamuliwa vinginevyo.


Dk Ndugulile alisema sababu zilizomfanya yeye na wananchi kupinga nyongeza hiyo ya nauli ni Serikali kushindwa kueleza wazi vigezo vilivyotumika na kushindwa kuwashirikisha wananchi wa maeneo husika. Alitoa mfano wa Bajaji ambao alisema ni usafiri wa wanyonge uliokuwa ukitozwa Sh300 lakini kwa viwango hivyo vipya, itavushwa kwa Sh1,300 huku baiskeli ya miguu mitatu inayotumiwa na wanyonge pia kuchukulia bidhaa kutoka Kariakoo ikiongezewa nauli kutoka Sh200 hadi Sh1,800 na gari ndogo sasa zinatakiwa kulipa Sh1,500 badala ya Sh800.

"Sasa angalia hivyo vigezo, utaona mwananchi wa kawaida amezidi kuumizwa. Leo hii tayari bei za bidhaa zinazoletwa Kigamboni kutoka sokoni kama Kariakoo kwa kutumia maguta zimepanda. Mtu mwenye gari anapadishiwa bei chini ya mwenye guta, vigezo gani hivi? Baada ya kuona hivyo, niliwasiliana na Waziri Mkuu Ijumaa (Desemba 30, mwaka jana) na jana Mkuu wa Mkoa akanipa jibu kwamba Waziri Mkuu kasema nauli hizo zisipandishwe kwanza. Kwa hiyo mimi na wananchi wangu tunajua hivyo," alisema na kuongeza: "Hili ni jambo la ajabu sana. Yaani Waziri Mkuu anasema hivi halafu waziri wake anafanya vingine! Uko wapi sasa utendaji kazi wa pamoja wa Serikali?"

Baadhi ya wananchi wamelaani kauli hiyo za Dk Magufuli wakisema haikupaswa kutolewa na waziri ambaye ana dhamana ya kuhakikisha matatizo ya wananchi yanatatuliwa. Mmoja wa wakazi wa Kigamboni aliyejitambulisha kwa jina la Hamis Bwamkuu alisema: "Waziri anatoa kauli za kejeli namna hii! Ametusikitisha sana na kwa kweli tunamuomba Rais Jakaya Kikwete amchukulie hatua za kinidhamu." Pia wananchi hao wamemshutumu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Dk Hurbet Mrango na Temesa kwa kushindwa kuwashirikisha na pia kumshauri vibaya waziri katika jambo hilo. "Katibu Mkuu ndiye mtendaji na Temesa wao ndiyo wakala lakini hawakumwambia kwamba wananchi hawakujua na hata mbunge wetu. Kwa hiyo hawa ni sehemu ya tatizo na hii si mara ya kwanza."

Mwananchi
 
magufuli.JPG


Waziri wa Ujenzi Dakt. John Pombe Magufuli (kushoto) akisisitiza jambo wakati akiongea
na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Jan, 1,2012 kuhusu ongezeko la viwango vya nauli katika vivuko vyote vya serikali nchini, ambapo kuanzia Jan, 1 ,2012, Wizara yake kupitia[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif] [/FONT]Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) imeongeza viwango vya nauli kutokana na maeneo mbalimbali ya vivuko,
amezitaja nauli hizo kwa mfano MV. Magogoni na Mv. Kigamboni kwa Mkoa wa DSM ni kati ya

  • shilingi 200 kwa watu wazima ,
  • watoto chini ya miaka 14, shilingi 50, na
  • wanafunzi waliovaa sare za shule na vitambul;isho ni bure,


Pia akatoa mfano wa Kivuko cha
MV. Chato kitatoza nauli ya watu
  • wazima shilingi 3,000/
  • watoto chini ya miaka 14 ni Tsh 50 ,na
  • wanafunzi wenye sare za shule ni bure.
Bei hizi zimepanda kutokana na gharama kupanda za uendesaji. (kulia) ni Mwenyekiti wa Bodi ya TEMESA Prof, Idrissa Mshoro. (kushoto) ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Balozi Herbert Mrango.
 
Alitoa mfano wa Bajaji ambao alisema ni usafiri wa wanyonge uliokuwa ukitozwa Sh300 lakini kwa viwango hivyo vipya, itavushwa kwa Sh1,300 huku baiskeli ya miguu mitatu inayotumiwa na wanyonge pia kuchukulia bidhaa kutoka Kariakoo ikiongezewa nauli kutoka Sh200 hadi Sh1,800 na gari ndogo sasa zinatakiwa kulipa Sh1,500 badala ya Sh800.

Huo uwiano wa kupandisha unatumia fomula gani?...gari na guta ni chombo gani kinatakiwa kulipa zaidi?
 
Kwa upande wake Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile alikiri kusikia maneno ya Magufuli ambayo hayakuwafurahisha wapiga kura wake na kuahidi kuendelea kufuatilia kujua undani hasa wa kauli hizo. Dk Ndugulile alifafanua kwamba baada ya tangazo hilo la ongezeko la nauli, aliwasiliana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki na taarifa alizonazo ni kwamba nauli hizo zimesitishwa. Alifafanua kwamba baada ya kuwasiliana na waziri mkuu, jibu alilopata jana saa 1: 00 usiku ni kwamba mpango huo wa kupandisha nauli umesitishwa hadi hapo itakapoamuliwa vinginevyo.

Hii nchi inavyoendeshwa hata haileweki. Huyu anasema hivi, yule anasema vingine.
 
Waacheni wafanye mambo ya ajabu wananchi waamke, hata huko Misri mambo yalianza polepole, mara serikali imepandisha bei ya mkate October 2009 etc etc. Siku moja watu watasema tumechoka.

Kwa nini unasubiri miaka yote hupandishi nauli ya kivuko, na siku unapopandisha unapandisha 100% ?
 
Hii nchi inavyoendeshwa hata haileweki. Huyu anasema hivi, yule anasema vingine.

Mkuu EMT, ndio nchi inayoendeshwa kama gari bovu maamuzi siku zote yanafanyika kiholela holela tu bila kutathmini athari za maamuzi hayo. Kweli hii ni Serikali taahira.

 
Tunapoelekea Tanzania itakuwa nchi ya kambale kila Mtu Ana ndevu hutofautishi mkubwa na mdogo Sasa tumuelewe nani? Magufuli au Pindar?
 
Hivi kauli hii ya John Magufuli kwamba wananchi wa Kigamboni kama hawataki kulipa nauli mpya basi wapige mbizi ina tofauti gani na ile kauli ya Basil Pesambili Mramba kwamba Ndege ya Rais lazima inunuliwe ikiwezekana hata tule nyasi?
 
Waacheni wafanye mambo ya ajabu wananchi waamke, hata huko Misri mambo yalianza polepole, mara serikali imepandisha bei ya mkate October 2009 etc etc. Siku moja watu watasema tumechoka.

Kwa nini unasubiri miaka yote hupandishi nauli ya kivuko, na siku unapopandisha unapandisha 100% ?

ndio maana nasema huyu Mrema type hafai kabisa kufikiriwa kuwa Rais wa nchi hii
 
Alitoa mfano wa Bajaji ambao alisema ni usafiri wa wanyonge uliokuwa ukitozwa Sh300 lakini kwa viwango hivyo vipya, itavushwa kwa Sh1,300 huku baiskeli ya miguu mitatu inayotumiwa na wanyonge pia kuchukulia bidhaa kutoka Kariakoo ikiongezewa nauli kutoka Sh200 hadi Sh1,800 na gari ndogo sasa zinatakiwa kulipa Sh1,500 badala ya Sh800.

Huo uwiano wa kupandisha unatumia fomula gani?...gari na guta ni chombo gani kinatakiwa kulipa zaidi?
samahani mkuu hizi tarakimu umeandika vizuri ?
yaani baiskeli ya miguu 3 - ya
walemavu sh. 1800 na gari sh 1500 au ....
 
Huyu si ndiye mnasema awe Rais wa nchi hii hajui hata wa kuwashirisha ktk maamuzi

ila hapa panachanganya ina maana SUMATRA hawahusiki na nauli za vivuko kweli Hawa jamaa ni mzigo tutakoma tu nauli zinapandda kwa zaidi ya asilimia 500 kweli hii ni CCM asante
 
Kulingana na kupanda kwa bei ya mafuta na gharama nyingine za uendeshaji ni sawa kabisa kupandisha nauri ya kivuko!
 
magufuli-top-mikono.gif

Waziri wa ujenzi Dk John Magufuli
Magufuli achafua hali ya hewa Dar

Mbunge achukizwa
Kwa upande wake Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile alikiri kusikia maneno ya Magufuli ambayo hayakuwafurahisha wapiga kura wake na kuahidi kuendelea kufuatilia kujua undani hasa wa kauli hizo. Dk Ndugulile alifafanua kwamba baada ya tangazo hilo la ongezeko la nauli, aliwasiliana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki na taarifa alizonazo ni kwamba nauli hizo zimesitishwa.Alifafanua kwamba baada ya kuwasiliana na waziri mkuu, jibu alilopata jana saa 1: 00 usiku ni kwamba mpango huo wa kupandisha nauli umesitishwa hadi hapo itakapoamuliwa vinginevyo.

Dk Ndugulile alisema sababu zilizomfanya yeye na wananchi kupinga nyongeza hiyo ya nauli ni Serikali kushindwa kueleza wazi vigezo vilivyotumika na kushindwa kuwashirikisha wananchi wa maeneo husika. Alitoa mfano wa Bajaji ambao alisema ni usafiri wa wanyonge uliokuwa ukitozwa Sh300 lakini kwa viwango hivyo vipya, itavushwa kwa Sh1,300 huku baiskeli ya miguu mitatu inayotumiwa na wanyonge pia kuchukulia bidhaa kutoka Kariakoo ikiongezewa nauli kutoka Sh200 hadi Sh1,800 na gari ndogo sasa zinatakiwa kulipa Sh1,500 badala ya Sh800.

"Sasa angalia hivyo vigezo, utaona mwananchi wa kawaida amezidi kuumizwa. Leo hii tayari bei za bidhaa zinazoletwa Kigamboni kutoka sokoni kama Kariakoo kwa kutumia maguta zimepanda. Mtu mwenye gari anapadishiwa bei chini ya mwenye guta, vigezo gani hivi? Baada ya kuona hivyo, niliwasiliana na Waziri Mkuu Ijumaa (Desemba 30, mwaka jana) na jana Mkuu wa Mkoa akanipa jibu kwamba Waziri Mkuu kasema nauli hizo zisipandishwe kwanza. Kwa hiyo mimi na wananchi wangu tunajua hivyo," alisema na kuongeza: "Hili ni jambo la ajabu sana. Yaani Waziri Mkuu anasema hivi halafu waziri wake anafanya vingine! Uko wapi sasa utendaji kazi wa pamoja wa Serikali?"

Baadhi ya wananchi wamelaani kauli hiyo za Dk Magufuli wakisema haikupaswa kutolewa na waziri ambaye ana dhamana ya kuhakikisha matatizo ya wananchi yanatatuliwa. Mmoja wa wakazi wa Kigamboni aliyejitambulisha kwa jina la Hamis Bwamkuu alisema: "Waziri anatoa kauli za kejeli namna hii! Ametusikitisha sana na kwa kweli tunamuomba Rais Jakaya Kikwete amchukulie hatua za kinidhamu." Pia wananchi hao wamemshutumu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Dk Hurbet Mrango na Temesa kwa kushindwa kuwashirikisha na pia kumshauri vibaya waziri katika jambo hilo. "Katibu Mkuu ndiye mtendaji na Temesa wao ndiyo wakala lakini hawakumwambia kwamba wananchi hawakujua na hata mbunge wetu. Kwa hiyo hawa ni sehemu ya tatizo na hii si mara ya kwanza."

Mwananchi


Yale yale ya hifadhi ya barabara au?
 
Tatizo lililopo hapa ni ukosefu wa mawasiliano baina ya wizara na wananchi yaani hapakuwa na ushirikishwa wa wananchi katika kupanga hizo nauli mpya, pia kutukuwepo kwa mawasiliano serikalini Pinda anasema lake na Magufuli anasema lake. Lakini ni safi sana maana kujichanganya kwa ccm na serikali yake ndo mwanzo wa ukombozi kwa wananchi dhidi ya serikali legelege ya pale Magogoni
 
WanaJF

Hivi ni sawa kwa kiongozi kama Mhe. Waziri wa Ujenzi Dr. Magufuli kutoa kauli yenye Jeuri, kibuli, majigambo na ubabe dhidi ya Wananchi wanyonge kuwa kwa asiye na uweza "APIGE MBIZI kutoka Kigamboni hadi Magogoni"? Hivi ni sawa, Bajaj kulipia Sh 1,800 na Gari ndogo (mfano taxi, benz, BMW, Mark X etc) kulipia sh. 1,500?

Huyu ni Mhe. Dr. Magufuli alitaka kuvunja jengo la TANESCO, pia alitaka kuvunja Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, bahati Mhe. Rais na Waziri Mkuu wakaingilia kati. Ni Mhe. Magufuli huyu huyu ambaye anaendelea kuwachefua wananchi na kauli zake za ubabe na jaziba...Kauli, Jeuri, Ubabe na Majigambo ni sifa kwa kiongozi kama Dr. Magufuli?

Ndugu zangu wanaJF, naomba mnisaidie kujua zaidi hivi....JEURI, KIBULI, UBABE na MAJIGAMBO ya Mhe. Dr. Magufuli yanatokana na nini? Kaona anasifiwa sana? Ama kweli, Mgema akisifiwa sana.........

Matusi kwa Wananchi wa Kigamboni ni Matusi kwa Watanzania "
An Injury to ONE is an Injury to ALL"
 
Wakuu vyombo mbalimbali vya habari vimemnukuu Waziri wa Ujenzi Magufuli akisistiza msimamo wa serikali wa kuongeza nauli ya abiria katika vivuko vyote vya serikali nchini. Alifanya ziara ya ghafla kutembelea kivuko cha Kigamboni ambako nauli iliyopandishwa kutoka sh. 100 hadi 200, ilizua mzozo, wananchi wakionekana kuipinga. Anaweza (kama waziri) au serikali ikawa sahihi au si sahihi katika kupandisha nauli hiyo, lakini tatizo ni lugha aliyotumia katika kuwasilisha msimamo wake.

Amenukuliwa akiwaambia wananchi kuwa kama hawawezi kulipa nauli mpya, WAPIGE MBIZI KUVUKA BAHARI, WAHAMIE VIJIJINI AU WAPITIE MBAGARA. Ingawa pia naona Mbunge amepingana naye, hivyo ni kama hawakubaliani katika hii kitu na imeandikwa wazi katika magazeti.

Magufuli anaonekana kuchukua njia ya akina Mramba (ikibdi mtakula hata nyasi ndege ya Rais inunuliwe), Malecela (They can go to hell), mwingine simkumbuki aliwahi kuwaambia wanafunzi waliomlalamikia ukosefu wa maji shuleni kwao, akwaambia wakojoe maji yapatikane! Katika nchi za kidemokrasia na serikali iliyo makini kwa ajili ya watu, kauli mbaya ya kiongozi wa umma kwa wananchi ni kitu kinachoweza kumgharimu nafasi yake, kuitia serikali matatani au kulazimika yeye/serikali kuomba radhi.

Kwani lazima utumie lugha ya kuuzi na kuonekana kama unadharau wananchi katika kusukuma kazi za serikali?
 
Back
Top Bottom