Said Mwamba Kizota has comeback to life as Kibu Dennis and Mohamed Mwameja has comeback to the pitch as Djigui Diarra.

LIKUD

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
15,120
27,126
Said Mwamba Kizota ni nani? Said Mwamba Kizota ni mchezaji bora kabisa wa wakati wote, wa mpira wa miguu kutoka Tanzania.


Nikiambiwa nimtaje mchezaji mmoja alie wapi kucheza mpira wa Tanzania ambae ndio bora kabisa kuliko wachezaji wote basi kwa haraka sana nitamtaja Said Mwamba Nassoro Kizota. Hayo si maneno yangu. Ni maneno ya Mahamoud Zubeir ( Bin Zubeir) wa Azam Tv. Kwangu huyu ni expert number moja wa mpira wa Tanzania.


Maneno ya Bin Zubeir yanaungwa mkono na Haji Manara a.k.a Shareef El Buggati a.k.a Shareef Matrophy. Maneno haya aliyataja wakati huo akiwa msemaji wa Simba.

Asilimia kubwa ya Wapenzi wa mpira wa Tanzania wanaofuatilia mpira wa Tanzania kuanzia miaka ya sabini watathibitisha kauli hii kuhusu Said Mwamba.

Said Mwamba aliyajibu kwa ufasaha maswali yote ambayo mpira wa miguu ulimuuliza. Ndio maana aliitwa Kizota.


Mwameja Mohamed Mwameja ni nani? Ni moja kati ya makipa bora kabisa kuwahi kutokea katika historia ya mpira wa miguu wa Tanzania. Kwa kizazi chake na kizazi kilicho fuatia baada yake hakujawahi kutokea kipa mwenye kufanana nae.

Mwamba huyu ambae anatajwa kuwa na mapenzi makubwa sana na klabu ya Yanga tangu utoto wake ( ingawa hakuwahi kuichezea/mwaka 93 alisaini Yanga ukatokea mgogoro hadi Rais Mwingi akaingilia kati) aliyezaliwq pale Mwakidila Tanga kutoka Mzee Mohamed Mwameja ( Mnazi wa Yanga) alikuwa hafungiki.

Ili kumfunga Mwameja ( anasema mdau mmoja wa Soka la bongo) ilibidi Abbas Gulamali atoe bahasha ndio kina Lunyamila watikise nyavu za Simba.


1. I see a lot of Said Mwamba in Kibu Dennis. It is as if Said Mwamba has come back to life as Kibu Dennis.


2. I look at Jiji Ziara ( Djugui Diarra) and see how Mwameja used to be on pitch.
 
Back
Top Bottom