Sagini ashiriki mazishi ya Mjukuu wa Baba wa Taifa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
26e0ba14-9f8f-4310-8a6a-a2294707c29d.jpeg

8c8f9616-b312-40c2-9790-3b42baa4f1c4.jpeg

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Jimbo la Butiama, Jumanne Sagini na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Deogratius Ndejembi wakiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Daudi Charle's Nyerere mtoto wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Charle's Makongoro Nyerere wakati wa mazishi yaliyofanyika nyumbani kwao Mtaa wa Haile - Sillas Jijini Arusha Novemba 02, 2023.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi (Mb), Jumanne Sagini ameshiriki mazishi ya Marehemu Daudi Charle’s Nyerere mtoto wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Charle's Makongoro Nyerere na Mjukuu wa Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere, yaliyofanyika Novemba 02, 2023 nyumbani kwao Mtaa wa Haile - Sillas Jijini Arusha.

Akizungumza katika mazishi hayo, Naibu Waziri Sagini ametoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kuwaomba wazidi kumuombea aendelee kupumzika kwa amani.

fb50c130-536a-446b-b743-89c079aa1d37.jpeg

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Jimbo la Butiama, Jumanne Sagini akiwafariji wazazi wa marehemu Daudi Charle's Nyerere Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Makongoro Nyerere na Mkewe Jaji Mstaafu, Aisha Nyerere wakati wa ibada maalum ya mazishi iliyofanyika Novemba 02, 2023 nyumbani kwao Mtaa wa Haile - Sillas Jijini Arusha.

Mazishi hayo pia yalihudhuriwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Deogratius Ndejembi, Wakuu wa Mikoa na Wilaya, Majaji pamoja na Viongozi wengine wa Serikali, Vyama vya Kisiasa na Kidini.

Marehemu Daudi, alifariki siku ya Jumapili Oktoba 29, 2023 kwa ajali ya gari iliyotokea katika barabara ya By-pass Jijini Arusha.
 
Duh! Ni bahati mbaya sana. Pole sana Makongoro kwa kuondokewa na mwanao. Mungu awajalieni mioyo ya pekee kuweza kuyahimili mambo makubwa haya yenye kuumiza moyo na fikra.
 
Nilidhani title ingekuwa Mjukuu wa Baba wa Taifa azikwa ndani yake Sagini atajwe kama moja ya waombolezaji
 
Kuna eneo maalum la makaburi/kuzika hapo Arusha. Hiyo mitaa ninaifahamu, sidhani kama ni halali kuzika.
Ila kwa vile kuna watu na viatu...basi sawa.

R.I.P mjukuu.
Labda wameamua kuzika sehemu tarajiwa atakayopumzika Makongoro na mkewe kama ilivyo kule Butiama
 
Duh! Ni bahati mbaya sana. Pole sana Makongoro kwa kuondokewa na mwanao. Mungu awajalieni mioyo ya pekee kuweza kuyahimili mambo makubwa haya yenye kuumiza moyo na fikra.
Nafikiri mjukuu wa baba wa Taifa ingefaa hata Majaliwa ahudhurie...
 
Back
Top Bottom