Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Akizungumza katika hafla hiyo Naibu Waziri, Sagini ameihakikishia Jumuiya ya Maridhiano na Amani JMAT kuwa salamu zao walizomtuma kufikiasha kwa Waziri Mkuu zimefika bila wasiwasi na wategemee ushirikiano mkubwa.
"Mimi kama Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi nimepokea salamu zenu niwahakikishie kuwa yote mliyoeleza katika hotuba yenu pia kuhusu Wizara yangu yatafanyiwa kazi," amesema.
Aidha, Sagini amewapongeza JMAT kwa kuwa na Idara nyingi zenye wasomi na kutaka wasomi hao kutenda kazi kwa taaluma zao ili kuleta matokeo chanya katika Jumuiya na kwamba Idara mbalimbali zinazoenda kuanzishwa ndani ya Jumuiya hiyo zitaleta tija na watakamilisha majukumu yao kikamilifu.
Amewataka watu wa Idara ya uchumi kuhakikisha watatumia mbinu mbalimbali ili kujikwamua kwenye changamoto ya kibajeti pindi wanapokuwa wanatekeleza shughuli mbalimbali ikiwemo uandaaji wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya hiyo.