jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,990
- 22,523
Shukran kwa taarifa mkuu,sasa ni Dorothea ama ni Dorcas?Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa Mwanza Injinia Everest Ndikillo amesema kuwa Kamanda Barlow alikuwa anatoka katika kikao cha harusi na ndugu yake aitwaye Sembeli Maleto kilichokuwa kinafanyika katika Hotel ya Florida na kisha kumpeleka mwanamke aitwaye Dorcas Moses Mwalimu wa Shule ya Msingi ya Nyamagana maeneo ya barabara ya Kona ya Bwiru kwenda Kitangiri.
"Walipofika getini kwa Mama Dorcas mara waliwaona watu wawili wakiwa wamevaa makoti ya Polisi-Jamii, Mama Dorcas alimuuliza Kamanda Barlow kama anawafahamu Kamanda akasema kuwa hawa na watu wa ulinzi wa Jamii wako doria." Alieleza Mkuu wa Mkoa.
Aliongeza kusema: "Mara wale watu waliongezeka na kuwa sita wakaanza kama kuzozana wao kwa wao na ndipo Kamanda alipowauuliza kuna nini, Mmoja wao akajibu hakuna kitu na ikapelekea Kamanda kutaka kutoka nje ila wale watu watatu wakaizingira gari ya Kamanda Barlow aina ya Rav 4. Kamanda Barlow alipoona kama hali hewa inabadilika alichukua redio call ili aweze kuwa taarifu askari na ndipo wale jamaa walipompiga risasi kichwani nakupelekea kifo chake."
Taratibu za mazishi ya Kijeshi bado zinaendelea na nyumbani kwa marehemu ambapo watu mbalimbali wako katika hali ya majonzi sana. Mke wa Kamanda Barlow yuko Dar es Salaam na anatarajia kufika Mwanza.
Mpaka sasa Polisi wanamshikilia mtu mmoja aitwaye Dorcas kwa ajili ya Mahojiano huku uchunguzi mkali ukiendelea kuhusiana na kifo cha kamanda Liberetus Barlow.
Na huyo "mtu mmoja" anayeshikiliwa na polisi anayeitwa Dorcas ndiye huyo huyo aliyekuwa naye wakati wa tukio?
Kwasababu mara wamu address kama "mwalimu Dorcas",halafu tena "mama Dorcas", na mwishowe tena "mtu anayeitwa Dorcas".Yani hakuna flow inayoonyesha kwamba wana nia ya kuulewesha umma ukweli.
Sijui kwanini hawa watu huwa hawawezi kutoa taarifa zisizokuwa na mizengwe na utata.
Halafu kila mtu anaongea lake,thread kama hii ilitakiwa ifungwe hadi kuwe updates za kueleweka,maana kuna wanaodai mara hana mke,mara ana mke,mara mke yuko anaishi Dar!Mara mke wake alifariki!duh!