Riwaya: Jina langu ni Pheady

GITWA

JF-Expert Member
Apr 1, 2012
1,495
1,690
MTUNZI : SELOPHEADY H. MAGEMBE
HAKI ZOTE ZIMEHIFADHIWA
Huruhusiwi kunakili au kutumia sehemu ya hadithi hii bila ruhusa ya mwandishi.


Nilikua nimehitimu masomo ya shule ya upili na kuchaguliwa kwenda kusomea ualimu katika chuo cha ualimu.Hii ilikuwa ni miaka ya 1990 hivi, ualimu ni kazi ambayo haikuniingia akilini kuifanya hivyo niliamua kutoenda chuo cha ualimu na kufuata mfumo wa maisha ambao ni UBATILI.

1
Ilikuwa yapata saa mbili asubuhi wakati nilipopokea telegram iliyonihitaji kwenda Tabora, nilikumbuka miaka mitano iliyopita,wakati nilipoacha masomo na kujiunga katika kikundi cha wizi kinachoitwa “COOL BLOOD”.Hiki ni kikundi chenye matawi mengi mikoani pamoja na matawi yake ya kitapeli,hii telegram ilitoka katika mojawapo ya ofisi hizo mkoani Tabora. Nilijaribu kubashiri ni kazi gani naitiwa lakini sikupata jibu la moja kwa moja kwani kulikuwa na aina nyingi za kazi nilizowahi kuzifanya chini ya kikundi hiki. Nilikumbuka jinsi nilivyotumwa kwa mara ya mwisho na ofisi iliyoko Musoma, kwenda Nairobi kutoa roho za watu watatu ambao hawakutakiwa kufika mahakamani kutoa ushaidi. Ilikuwa ni pata shika nguo chanika kwani watu wenyewe walikua maarufu na wana ulinzi wa nguvu.

Ghafl a nilirudisha mawazo yangu kwenye ujumbe niliopokea nilirudia kusoma ile telegram na kuona kuwa niliitajika kuripoti Tabora kabla ya kupita siku tatu kuanzia siku ya leo.Kutokana na usafiri ulivyo kutoka hapa Ukerewe kwenda Tabora ni safari isiyochukua zaidi ya siku mbili. Hivyo niliamua kuanza safari yangu hapo kesho jumapili.

Niliangalia saa yangu ya ukutani iliyokuwa ikipiga kelele majira haya ya alfajiri, ilionyesha kuwa ilitimia saa kumi na mbili kamili. Nilitoka kitandani na kuwasha jiko linalotumia mafuta ya taa tayari kwa kuchemsha maji ya kahawa.Baada ya hapo niliingia katika chumba changu cha mazoezi na kuanza kuupasha mwili kwa mazoezi ya viungo,kubeba chuma kidogo kwa ajili ya kuupa mwili nguvu pamoja na mazoezi mengine kama kuvuta na kutanua spring na kujinyoosha kwa kutumia kitairi kidogo. Ilipotimia saa mbili na nusu nilikuwa nimemaliza kufungua kinywa,kuoga pamoja na kupanga mizigo yangu katika begi maalumu la safari.

Nilianza safari yangu kwa kuelekea forodhani kukata tiketi huku begi langu nimeliacha nyumbani, kwani nilijua saa ya kuondoka meli hapa kwetu kisiwani Ukerewe ni saa saba mchana, hivyo niliamua kuacha mzigo nyumbani kwani kwangu na forodhani sio mbali ni mwendo wa dakika kumi kwa mguu. Nilipofika forodhani niliingia moja kwa moja katika chumba cha kukatia tiketi. Sikuwa na haja ya kujipanga katika foleni ya kukata tiketi kwani mkatisha tiketi tulielewana sana.

“Habari za asubuhi ndugu James” Nilimsalimu baada ya kukuta akigonga mihuli na tarehe katika tiketi.“nzuri” Alijibu na kuuliza “ Vipi mshirika wangu unasafiri leo nininini”“Ndio ndugu yangu unajua, unajua miangaiko ya tumbo ndio mingi” nilijibu na kuendelea “Naomba unupatie tiketi ya Tabora” Nilisema.

“Samahani Mr Pheady, tiketi za moja kwa moja kwenda Tabora zimekwisha zipo za Dodoma na kuendelea” Alisema.
“Haidhuru nipe ya Dodoma, ni shillingi ngapi?”

“Shilingi elfu moja na mia mbili” alijibu huku akiongezea na utani “Naona safari hii unaenda kutengeneza pesa sio za utani”

“Ha! Wapi ndugu yangu ni shida tu ndizo zinazotusumbua”“Shida wapi? Wakati mwenzangu unapendeza “ Alisema huku ananipatia tiketi.

“Nashukuru” Nilimwambia wakati nampatia pesa na kumtakia kazi njema naye alinitakia safari njema.

Nilishika barabara ya boma na kuanza kutembea, nilipofika Fora Hotel niliamua nipumzike kidogo na kupata soda baridi. Nilirudisha mawazo yangu katika kazi niliyoitiwa nilihisi sio kazi ya kawaida kutokana na hisia zilizopita kichwani mangu. Lakini la ajabu kama ninavyoelewa ofisi ya Tabora hushughurika hasa na mipango ya “kibeshi” yaani utendaji wake wa kazi ni mzuri hauna sekeseke yoyote, hutumii nguvu ni uongo mwingi unapata pesa bila haja ya kukunjiana ngumi.

Hivyo hizi hisia zilizokuwa zinakuja zilikuwa kama kitendawili mawazoni mwangu.

Nilpoangalia saa yangu ilinionyesha saa tano na dakika ishirini na nane,nililipia soda niliyokunywa na kuanza kuondoka kuelekea nyumbani ambako ni barabara ya Msoma.Nilichukua mzigo wangu na kuanza kuondoka, nilipofika mlangoni nilikumbuka saa moja pamoja na ringi ya mkononi ambayo nilipewa na jasusi mmoja aliyenifindisha kutumia silaha pamoja na michezo ya kareti na judo. Nilirudi na kufungua kabati ninayotunza vitu maalumu na kuchukua vitu hivyo na vingine nilivyoona ni muhimu.

Zilikuwa zimesalia dakika kumi meli iondoke wakati nilipochukua nafasi inayonifaa na kukaa,ilikuwwa ni baada ya kutoka nyumbani na kupita nyumba mbili tatu na kuaga ndugu zangu huku nikikabidhi uangalizi wa nyumba yangu kwa mmoja wao. Niliposhuka forodha ya Mwanza niliongoza moja kwa moja hadi stesheni kwani kulikuwa na treni jioni hiyo.

Niliwekewa namba ya behewa na ya kiti katika tiketi yangu na kuondoka maana mda wa kuondoka ulionyesha nina saa mbili za kusubiri.Nilipita madukani na kufanya window shopping kama wasemavyo waingereza,sikuwa na lolote muhumu hapa Mwana.Ilipotimu saa moja kasorobo nilikuwa tayari ndani ya treni nikisubiri kuondoka tayari kwa kazi ninayoitiwa.
…………………………………………………………………………………………….
Ilikuwa majira ya alfajiri wakati treni ilipofika Tabora, niliondoka stesheni na kuelekea Tabora Hotel kwani ipo karibu tu na ni hotel inayonifaa kwa kua ina hadhi ya kitalii. Nilimkuta mtu wa mapokezi akiawa anaelekea kulemewa na usingizi.

“Habari za saa hizi dada?” Nilimsalimia.

“nzuri kaka, karibu, nikusaidie nini?” Aliongea huku akipanusa uso wake kwa leso.
Nilikuwa sijamwangalia vizuri sasa ndio nilibaini kuwa ni mzuri wa sura,sikujua umbile lake kwani alikua amekaa.

“Nahitaji chumba” hatimaye nilijibu.

“vyumba vimebaki viwili vyote double”
Kutokana na jinsi ambavyo sikupenda Hotel za uswahilini niliamua kuchukua kimojawapo nitabadiri endapo kuna mtu atatoka katika chumba single.

“Nipatie kimoja ambacho utaona kinanifaa”

“Kipo kinachoangalia shule ya upili nadhani kitakufaa” Alisema.

“Ok, kanionyeshe”

Nililipa malopo ya chumba na kuondoka kuelekea chumbani, tuliongozana na huyu msichana mimi mbele yeye nyuma yangu huku akiwa amebeba mzigo wangu.Tulipofika njia panda ya korido nilifuata njia isiyo sahihi, nikamsikia akisema,”kaka umekosea,sio huko”

“Du! Unajua kitu ambacho hukijui ni sawa na usiku wa giza” Niliongea huku nikimfuata nyuma yake.

Nilipokuwa nyuma yake ndio niliweza kuona uzuri wa umbile lake,ukilinganisha na uzuri wa sura yake niliyoiona wakati naingia ni dhahiri kuwa nilikua naongozana na kiumbe mzuri kiasi kuwa ndugu msomaji kama wewe ni we kiume na rijali ungependa kuwa na uhusiano naye zaidi ya ule wa kawaida, ila kwa kuwa nilikuja kikazi sikutilia maanani mawazo hayo zaidi ya kumsifu Mwenyezi Mungu kwa uumbaji iliotukuka.

Hatimaye tulifika kwenye chumba na kukifungua huku akisema”Chumba ndio hiki natumaini utakifurahia”
“sitaweza kukifurahia iwapo nitaendelea kukaa peke yangu bila mtu wa kuniliwaza” nilimtania.

“Kwa jinsi unavyoonekana sidhani kama mabinti wa Tabora watakuruhusu ulale peke yako” Alisema
“Labda! Nilisema na kuendelea, vilevile sitajisikia raha iwapo hatakuwa mtu aliyeushitua moyo wangu” Nilisema huku nikikaa kwenye sofa iliyokuwa pembeni ya kitanda. “Samahani dada pamoja na kunihudumia ningependa kujua jina lako yamkini nikapata shida itakayohitaji msaada wako”

“Naitwa Saumu” Alijibu huku akiwa amesimama mlangoni.

“Jina zuri sana,unatoka kazini saa ngapi?” Niliendeleza maongezi.

“natoka saa nne asubuhi hii” Alisema.

“Ok, kazi njema” Nilimwambia

“kwa heri” Alisema akiwa nje ya mlango.

Sikumjibu kwa kuwa sikupendelea kuongea na mtu nisiyemuona.
Nlilipoangalia saa yangu ilinionyesha saa kumi na mbili kasoro dakika tano.Niliamua nipumzike mpaka saa mbili kwani nilikua na uchovu wa safari. Nilishituka usingizini saa mbili na robo,mawazo na akili yangu viliamia kwenye kazi niliyoitiwa. Niliondoka kitandani na kuliendea dirisha, niliona wanafunzi kwa wanafunzi mbali,nilitoka dirishani na kuelekea bafuni kuoga na ilipotimu saa tatu kamili nilikua tayari kuelekea ofisini. Nilichukua sigara na kuasha wakati huo lilinijia wazo hivyo nilichukua simu iliyokuwa mezani na kuzungusha namba za ofisi yetu ya hapa Tabora. Simu ilinyanuliwa upande wa pili.

“Halo nani mwenzangu?” Nilisikia sauti nzito

“Pheady” Nilijibu.

“Unaongea toka wapi” Sauti iliendelea.

“Mwanza” Nilidanganya.

“Hujapata ujumbe wowote wa kukuitaji toka kwa Chata”
Kwa jinsi ninavyoelewa Chata ndiye mkuu wa ofisi hii ya Tabora.

“Sikiliza ndugu, kabla hatujaongea zaidi ningependa kujua ninae ongea naye” Nilisema.

“Unaongea na Mr Kikakika” Alijibu.

“Ok. Vp mwenzangu una fununu zozote kuhusiana na huo ujumbe” Niliuliza.

“Sijui lolote hata mimi nimeitwa kama wewe na nilifika hapa jana sikuambiwa lolote zaidi ya kuambiwa wewe”

“Sawa, mimi nitafika hapo ofisini mida ya saa tano”

“ Sawa” Alijibu bila kufikiri.

“Kwa heri” Niliaga na kukata simu.
Mara nilianza kumfikilia Kikakika,nilikumbuka ujasiri wake kwani niliwahi kufanya naye kazi Kampala Uganda.
Niliondoka chumbani baada ya kuhakikisha kuwa vitu vyangu vyote nilivipanga katika mpangilio wa tahadhali.Nilipofika kaunta nilimkuta Saumu akijiandaa kutoka.

“Vipi Saumu? Uliniambia unaondoka saa nne, inakuwaje haraka yote hii saa tatu tu?” Nilimshitua baada ya kuona anaweka mfuko begani.

“Ohoo!!” Alishituka kwani alikuwa hajaniona, “Naona imekuwa bahati kwani mwenzangu amekuja kunipokea” Alisema.

“ Je? Tunaweza kuongozana.” Niliuliza.

“Kama hutaona usumbufu, kuna sehemu napitia kwanza kabla ya kufika mjini” Alisema.

“Unafikiri utatumia mda gani kabla ya kufika mjini?”

“Kama saa moja na nusu hivi.”

“Hakuna tabu tunaweza kuongozana” Nilieleza.

“Rose!!” Alimuita mwenzie aliyekuwa kwenye chumba cha wahudumu.

“Unasemaje? Rose aliitikia kwa njia ya swali”

“Mimi naondoka tutaonana kesho”

“Sawa shoga yangu” Alijibu huku akiwa chumbani.

Tuliondoka kaunta tukiongozana mpaka tulipofika maegesho ya gari nikachukua taxi.
Ilikuwa ni saa tano kasoro dakika kumi na mbili nilipofika ofisini, nilimkuta Chata akiwa amekaa na Kikakika pamoja na kijana mwingine wa kishombeshombe.

“Habari zenu, niliwasalimu kwa pamoja”

“Shikamoo” Nilimsalimu mzee Chata huku nikivuta kiti tayari kwa kukaa.

“Marahaba kijana, habari za safari? Alijibu na kuuliza.

“Sio mbaya maadamu Mungu anasaidia” nilijibu.

“Nimesikia taarifa ako kutoka kwa Kikakika kuwa utafika sasa hivi, hivyo inabidi mnisikilize kwa nyote makini” Alisema mzee Chata na kuendelea.

Kutokana na taarifa zilizopo hapa kutoka Head office mnatakiwa wote mkafanye kazi mjini Mwanza, alinyamaza na kutoa sigara akawasha.Wakati huo mawazo yaliniruka kwani sikupenda kufanya Mwanza hasa ukizingatia kuwa ni mkoa wa nyumbani hivyo nilifahamika kwa watu wengi. Nilitoka kwanye mawazo yangu baada ya kusikia mzee Chata akiendelea kuongea.

Kuna tajiri mmoja aitwae Sule Catto mwenye kiwanda cha kuunganisha radio ambaye hufanya biashara ya madini ya dhahabu kwa siri na kupeleka Japani na ndio kiini cha utajiri wake hata serikali haijashituka. Kutokana na habari tuluzozipokea, anategemea kuondoka juma mosi ya wiki hii kupeleka dhahabu yenye yenye thamani ya bilioni mia tano. Mnachotakiwa ni kuchukua hizo dhahabu, alinyamaza na kutuangalia usoni mmoja baada ya mwingine kama mtu ayesoma mawazo yetu.

Namna ya kuzipata mtajua wenyewe ila jinsi zinavyosafilrishwa ni kama ifuatavyo; Wananuliwa samaki na kuondolewa minofu badala yake hujazwa dhahabu kulingana na uzito alafu zinashonwa na kukaangwa tayari kwa kusafirishwa.Sasa ni juu yenu kuangalia ni wakati gani unaofaa kuzichukua. Mr Catto mwenyewe anaishi Isamilo nyumba namba 72 imezungushiwa uzio wa michongoma na seng’enge ambazo hutegeshwa nyaya za umeme. Vilevile ndani kuna ulinzi wa mbwa wanne. Je mpaka hapo kuna mtu mwenye swali? Alimaliza kwa kuuliza.

“Umesema anaishi Isamilo, Je hana familia hapo nyumbani? Aliuliza Kikakika.

“Tofauti na walinzi watatu kuna vijana wawili ambao ndio huandaa samaki na kupakia dhahabu tayari kwa safari. Mke na watoto wake wanaishi Nyakato. Nafikiri nyumba ya Isamilo ni maalumu kwa shughuli zake nyeti.” Alisema Kikakika.

“Ina maana hao vijana wanaoshughurika na samaki wanaelewa siri yake au?” Nilisahili.

“Haswaa, wanaelewa lakini sio rahisi kumsaliti maana wanalipwa donge nono, vilevile inasemekana ni ndugu zake.

“Sawa mpaka hapo tumekuelewa” Tulisema kwa pamoja.
Mzee Chata alivuta saraka ya meza na kutoa bunda la pesa ambazo alizigawanya laki tano tano kwa kila mtu. Kwa miaka hii ya Tisini zilikuwa ni pesa nyingi sana.Baada ya hapo alitoa bastola tatu zenye viwambo vya kuzuia sauti pamoja na magazine tatu tatu kwa kwa kila mtu. Baada ya kupokea kila kitu na kuweka sehemu salama, alitueleza turudi saa nane kuchukua tiketi zetu za safari ya Mwanza.

Palepale lilinijia wazo nikaamua nifanye kama akili yangu inavyojua. “Lakini mzee mimi ningependelea nichukue pikipiki ndio niondoke nayo ili iweze kuturahishia kazi hapo baadae.” Nilieleza.

“Sawa kabisa” Aliongea yule Chotara.

“Sawa nitashughurikia utaikuta tayari” Alisema mzee Chata na kuendelea kueleza kuwa “ Ndugu Pheady utakuwa mkuu wa msafara vilevile itabidi niwape gari badala ya kutumia usafiri wa public. Nadhani itakuwa njia nzuri kutekeleza majukumu yenu kwa urahisi. Sonno na Kikakika njooni baada ya masaa mawili mtakuta gari tayari.”
Tuliagana na mzee Chata, sisi tuliongozana kutoka nje na tulipofika nje tuliagana na wezangu kila mtu akaendela na shuguli zake huku tukiwa tumeahidiana tukutane juma tano Vijana Social Hall Kirumba Mwanza tayari kwa maandalzi ya kazi.

2
Ilkuwa saa tatu kasoro robo wakati nilipopaki pikipiki nje ya ukumbia wa Vijana Social Hall, nilisikia kelele za mziki wa disko pamoja na watu wakishangilia. Nilikata tiketi ya kuingia ukumbi wa disko na kuingia ndani, nilitafuta kona nzuri itakayoniwezesha eneo lote kwa urahisi. Niliagiza chupa ya konyagi baada ya muhudumu kuniletea nilianza kunywa huku nikiangalia wanaocheza disko.
Nilikuwa nimekaa zaidi ya nusu saa huku nikiangalia uwezekano wa kuwaona akina Kikakika, mara ghafla nilisikia naguswa begani kwa nyuma. Niligeuka na kukutanisha uso na Sonno.
“Ohoo!! Mr Sonno habari za siku?” Nilisaili
“Salama tu, sijui mwenzangu vipi?
“Kwangu poa, nimefika salama” Nilijibu.
“Sasa inabidi tutafute sehemu inayotufaa tujadili mambo yetu “ Nilieleza na kuendelea kuuliza “Kikakika yuko wapi?
“Yupo katika chumba cha faragha huko pembeni” Alijibu.
“Basi twende tukaongelee huko.” Nilieleza huku nikinyanyua chupa yangu ya konyagi tayari kwa kuondoka.
“Hapana, inabidi nimwaendee Kikakika tukaongelee sehemu nyingine, kwani kule kuna wasichana hivyo hapatufai.”
“Sawa kamuite, alafu wambie hao wasichana wenu wawasubiri kwani hatutachukua mda mrefu.” Sonno aliondoka akiniacha nikimimina konyagi kwenye bilauri, nilimimina pombe yote iliyokuwa imebaki kwenye chupa na kuinywa kwa mkupuo. Baada ya hapo niliwasha sigara na kuanza kuvuta taratibu.
Sonno na Kikakika walinipitia tukaongozana mpaka kwenye gari lao,niliamua kuacha pale pikipiki kwani nilijua tutawahi kurudi. Sonno alishika usukani nikamwambia aongoze moja kwa moja mpaka Msufini Restaurant iliyoko Nyamanolo kwani ndio nilitegemea kuchukua chumba.
“Vipi mmechukua vyumba wapi? Niliuliza.
“mimi nipo Mwanza Guest namba kumi na mbili na Sonno yupo Nsimbo namba thelathini na tatu.” Alisema Kikakika.
“mmefanya vizuri kuchukua guest tofauti,mimi nataka nikachukue chumba hapo msufini. Tulikuwa tumekata kona kushika barabara iendayo AIR PORT hivyo nilionelea huu ni wakati wa kutoa mikakati ya kazi. Sasa inabidi tufanye kazi iliyotuleta, nafikiri mnaelewa ninachoongelea” Nilieleza.
“Ndiyo” Walijibu kwa pamoja huku Sonno akipunguza mwendo.
“Kesho kuanzia saambili na nusu mnatakiwa muwe kiwandani kwake ili kuweza kufanya uchunguzi kabla ya vitendo, kwani ukitaka vitendo vipendeze jua nyendo za mtu umtakaye.Mukifika mtahitaji kuongea naye kwa ajili ya kununua radio kwa bei ya jumla ili nanyi mkauze kwa bei ya jumla. Katika maongezi yenu hakikisheni mnatumia ujanja wowote kujua kama juma mosi atakuwa na safari.Kesho ni Alhamisi na kufikia ijumaa tunatakiwa tuwe na mpango kamili wa kazi. Mimi nitaanza kufatilia nyendo zake kuanzia asubuhi akingali nymbani kwake hivyo tutaonana saa saba River Side kwa ajili ya chakula cha mchana. Nafikiri mmeelewa kipi mnachotakiwa kufanya pamoja na kuwa nimeeleza kwa kifupi.”
“Bila shaka” Alijibu Sonno huku akitabasamu.
“Ikibidi kuionana kabla ya hizo saa basi tuonane Mwaza Hotel, nadhani patakuwa mahali pazuri pa kupotezea muda.” Niliongezea.
“Nilitaka kuuliza swali lakini naona jibu lake umeishanipa. “Aliongea Kikakika huku gali likikata kona kuingia mwisho wa safari yetu.Sonno alielekeza gari mpaka maegesho ya Msufini Restaurant ndipo tukashuka.
“Ngoja sisi tuingie kwanza bar tupate bia moja moja wakati wewe unaendelea na shughuli zako.”Alieleza Sonno.
“Sawa nami nitapata moja kabla ya kuchukua chumba” Nilisema huku tukiwa tunaingia mlangoni pa bar.
Tulikaa baada ya kupata viti katika meza moja iliyokuwa pembeni ya bar ikitazamana na dirisha. “Tuletee safari tatu baridi” Aliagiza Sonno baada ya muhudumu kufika. Wakati muhudumu anaondoka kufuata vinywaji nami niliondoka kwenda kupata chumba sehemu ya guest.
“Habari za saa hizi?” Nilimsalimu muhudumu baada ya kumkuta akiandika stakabadhi za nyumba ya kulala wageni”
“Salama kaka, Karibu tupo.” Alijibu.
“Naitaji chumba, je nimepata?” Nliuliza.
“Bila wasiwasi, vipo vyumba vitatu bado” Alijibu.
“Naomba kimoja kizuri” Nilieleza naye alinyanyuka na kuniongoza kwenda kuangalia. Tuliongozana mpaka chumba namba ishirini na na saba, alinifungulia nikaangalia kilikuwa chumba chenye kuridhisha. Nilimlipa pesa yake huku nikiwambia kuwa nitapititia stakabadhi hapo mapokezi.
Nilikikagua vizuri chumba baada ya muhudumu kuondoka,baada ya ukaguzi wangu niliondoka na kupitia stakabadhi yangu mapokezi na kuongoza moja kwa moja bar ambapo niliwakuta Kikakika na Sonno wakiwa wanamalizia bia zao.Nilikunywa bia yangu haraka ili nisiwachelewashe jamaa zangu kwa wasichana wao.
Ilikuwa imetimu saa nne na nusu wakati tulipokuwa tumefika Vijana Social Hall na kuwakuta wasichana wa akina Sonno wakicheza mziki.Tulichagua meza tukakaa na kuagiza vinywaji, baada ya wimbo wa Nakei Nairobi kwisha wale wasichana waliangaza angaza baada ya kutuona walikuja na kuvuta viti vilivyokuwa wazi katika meza yetu na kukaa. Walikuwa wawili.
“Habari za saa hizi kaka” Walinisalimu kwa pamoja.
“Nzuri, je wenzangu mna khali gani?” Nilijibu na kuuliza.
“Salama tu” walijibu.
“Samahani” Alikatisha Sonno. Inabidi niwatambulishe, huyu ni rafiki yetu anaitwa Pheady na ni mfanya biashara vilevile na ndie kiini cha safari yetu kwani yeye ni mwenyeji wa Ukerewe. Aisee Pheady hawa ni Zinduna na rafike Mtuli. Ni wenyeji wa hapahapa Mwanza. Sonno alimaliza kutambuilisha.
“Nafurahi kufahamiana nanyi” Nilisema huku tukipeana mikono. Baada ya hapo Kikakika aliagiza vinywaji tukaendelea na kunywa. Ilipotimia saa sita kasoro robo niliwaaga huku nikiwakumbushia umuhimu wa kazi, nilipita maegesho nikamuaga mlinzi na kuchukua pikipiki yangu na ilipotimu saa sita na nusu nilishamaliza kupanga vitu vyangu chumbani na kuelekea kuoga tayari kwa kulala.
 
Tuendelee **********************************************
Ilikuwa saa kumi na mbili kasoro robo nilipoamka. Kwa kuwa chumba kilikuwa na kilikuwa na uwazi wa kutosha, nilifanya mazoezi ya viungo na baada ya hapo nilielekea bafuni kuoga . Baada ya kuwa nimemaliza kuoga na kubadili nguo niliitupia saa yangu macho na kuonyesha saa moja na robo. Ilinibidi nifanye mambo yangu kwa haraka kwani nilitakiwa saa moja na nusu niwe Isamilo na mwendo wa kutoka hapa mpaka Isamilo ni robo saa ukiwa na pikipiki.
Ilikuwa ni saa mbili kasora dakika ishirini hivi nilipofika Isamilo katika hiyo nyumba ya Bwana Catto, namba 72. Niliweza kuiona vizuri kwani jana baada ya kufika kabla ya kwenda kuonana na akina Sonno nilipita kuikagua lakini kulikuwa na giza hivyo sikuweza kuona vizuri baadhi ya mambo.Niliipita ile nyumba katika mwendo wa polepole na kuona kulikuwa na mtu anasafisha gari. Ilikuwa gari la kifahari haswa bila wasiwasi lilikuwa ni gali linalotumiwa na Bwana Catto.
Baada ya kuwa nimevuka eneo la geti la kwa Bwana Catto na kuhakikisha kuwa sionwi na walinzi nilizima ghafla pikipiki na kuonekana kuwa imeharibika machoni pa wapita njia.Niliisukuma pembeni ya barabara na kutoa spana tayari kwa kuanza kazi yangu ya ufundi wenye lengo.Nilikuwa nimekaa kama hapo kama nusu saa hivi nikiendelea na shughuli zangu. Nilikuwa nimechomoa plug na kuwa naisafisha mara niliona gari aina ya Benz ikitoka katika geti la nyumba ya Bwana Catto, nikaikumbuka kwani ndio ilikuwa ikioshwa. Ilikuja kwa mwendo wa taratibu nami nilirudishia plug haraka huku nikiangalia kwa chati, ilnipita kama hatua kumi hivi lakini hawakuwa na habari na mimi kwa jinsi walivyokuwa wamenogewa na maongezi.
Waliponipita niilwaacha kwa dakika mbili hivi nami nikawasha pikipiki tayari kwa kuwafuata. Nilichukua tahadhari ya hali ya juu kuwafuata ili nisije kuwashtua, kwa hiyo nilipitia njia nyingine nikiwa nimewapigia hesabu ya kuonana nao kwenye mzunguko wa mtaa wa mviringo karibu na shule ya msingi Milongo.Nilichukua kasi ya kutosha kwa tahadhali ya kutokukuta wamepita, pamoja na kwamba walikuwa na mwendo mdogo nilihofia wanaweza kuongeza mwendo wakati wowote nami sikutaka niwakose katika mzunguko huo. Kwani nilitaka kujua nini watafanya mjini kabla ya kuelekea ofisini.
Wakati nafika kwenye mzunguko wa Milongo nilijikuta nikiwa mbele yao, nilitaka kupunguza mwendo ila nikashituka kuwa naweza kuwashtuwa hivyo niliendelea kuwa mbele yao mpaka nilipoona duka pembeni ya barabara na kulielekea huku nikiwaacha wanipite.Baada ya kupoteza lengo kwa kununua Panadol pale dukani niliendelea kuwafuata kwa nyuma huku kukiwa na magari manne katikati yetu. Walipofika usawa wa jengo la CCM niliona gari lao likielekea forodhani na ilipofika usawa wa kituo cha polisi ilisimama. Mimi nilipitiliza mpaka kwenye ofisi za kampuni ya Singer, nilipaki pikipiki na kumuomba mlinzi wa hapo aniangalizie huku nikimwachia shilingi mia tano.
Nilipofika karibu na kituo cha polisi cha kati nilimuona Bwana Catto akiagana na askari mmoja mwenye cheo cha Inspekta. Huku nikitembea kwa mguu,nilikuwa nimefika usawa wa gari la Bwana Catto aalipofungua mlango na kuingia ndani ya gari. Nilisimama ili kumpa nafasi ya kugeuza gari, hapo ndipo nilisikia akiwambia wenzake. “Atakuja saa mbili na mzigo hivyo twende tukachukue samaki tayari kwa maandalizi.” Sikuweza kusikia zaidi kwani gari iliondoka.
Niliendelea mpaka forodhani ambako nilikutana na watu wa ukerewe ambao walikuwa wakisubiri boti, niliongea nao kwa marefu kidogo kwani kazi yangu niliona inaleta matumaini, sikuwa na haja ya kuendelea kumfuata Bwana Catto nilikuwa nimemsikia alivyo sema na kujenga tafsiri akilini mwangu.
Saa sita na nusu niliingia Mwanza Hotel kuona kama akina Sonno walikuwa wamefika, hiyo ni baada ya kufika hotelini kwangu na kutafakari jinsi shughuli nzima itakavyokuwa. Hii shughuri ilijengeka akilini mwangu kama UCHUNGU WA MAISHA kutokana na jinsi itakavyofanyika, maeneo yapi itakapo fanyika na nilipanga iwe shughuri yangu ya mwisho katika tasinia hii. Nilipanga baada ya hii kazi ningebadili kabisa muelekeo wa shughuli zangu.
Nilitafakari nikifanya ambushi nyumbani kwake kwenda kuzichukua mikononi mwao itakuwa vigumu ukizingatia ulinzi wa mbwa wanne ni hatari kwa kuwa mbwa hunusa harufu kwa mbali. Vilevile kupora wakati wakielekea uwanja wa ndege ni vigumu kutokana na ukosefu wa msongamano wa magari katika barabara itakuwa tatizo kupotea kwa urahisi.
Niliwaza kuhusu kumteka yule askari kwani nilihisi kuwa ndie anayekuja na zile dhahabu kutokana na mazungumozo yao niliyoyasikia baina yake na Mr Catto. Ila suala hilo lilikuwa na ugumu kutokana na kutokuwa na uhakika na yale ninayoyahisi, vilevile ugumu wa kufatilia nyendo za yule askari aliyeingia kwenye mchezo ghafla. Ilipofika saa saba na dakika nane niliona gari wanalotumia Sonno na Kikakika likiegesha maegesho ya Mwanza Hotel. Nilifurahi kwani nilitaka tuchange mawazo pamoja kuhusu waliyoyapata huko na niliyonayo ili tupange mpangilio kamili wa kazi. Lakini niliona anashuka Sonno peke yake na kufunga milango ya gari, nilivuta pumzi na kumsubiri alete habari huku nikiwasha sigara.
Sonno alifika na kuvuta kiti na kukaa, nilimwagizia chupa yake ya konyagi, ilipoletwa muhudumu alimimina kwenye bilauri na Sonno aliweka kipande cha ndimu na kumea funda moja kisha akaanza kueleza;
Tuliondoka asubuhi muda wa saa nne na kuelekea ofisini kwa Catto,tulipofika tulikuta hajafika hivyo ilibidi tusubiri mpaka alipofika saa tano na nusu.Alipofika Kikakika alishauri niende nikauone na yeye angebaki kwenye gari kama dereva wangu. Nilielekea ofisini kwa Catto na kukuta wahasibu mukhtasi wawili wa kiume, niliomba kumwona bosi wao mmoja aliyekuwa anajishughulisha na simu aliniambia pita ndani. Niliingia na kujikuta kwenye ofisi moja iliyonadhifishwa kwa umaridadi wa hali ya juu na huku kuta zote zikiwa zimetandwa na vioo.
Nilimsabahi, alinijibu na kunikalibisha kwenye sofa iliyokuwa pembeni mwa meza.
Habari za shughuri? Niliendelea na maongezi.
Nzuri tu ndugu, alijibu.
Mimi ni mfanyabiashara natoka Mbeya nina duka la kuuza bidhaa kwa jumla,hivyo nimefika kukuona kama kuna uwezekano wa kupata redio kutoka hapa kiwandani kwako. Nilimwambia huku nikimkabidhi kadi yangu kibiashara iliyoonyesha namiliki kampuni ya iitwayo BUDINGI.Wakati anasoma kadi yangu simu iliita, alinyanyua simu nyeupe kwani mezani kulikuwa na simu tatu nyeupe, nyeusi na nyekundu.
Hallo, alisikika akiongea kwenye simu. Kwa kuwa nilikuwa nikisikia maongezi ya upande mmoja yalisikika kama hivi:
“Ohoo! Kumbe ni wewe”.
“Je ni mzigo mkubwa ulioongezeka?” Alisahili kwenye simu.
“Ok, kwa hiyo tuonane saa tisa Pamba hostel, uje na mzigo wote nitakuwa nimeandaa usafir”i. Alimaliza na kusikiliza simu.
“Sawa nitaandaa kila kitu kama ulivyosema”, “ok kwa heri”. Alikata simu.
Baada ya hapo aliendelea kuongea na mimi. “Umesema una duka la kuuza bidhaa za jumla?”
“Ndiyo”. Nilijibu.
“Kwa hiyo unataka unataka redio kiasi gani? Na malipo utalipa kwa njia ipi?”
“Naitaji redio ishirini na nne elfu zikiwa bend tatu na nne na kuhusu malipo ningependa kujua utaratibu mnaotumia.” Nilijibu kwa mkato huku nikiwa nimeisha gundua kitu kwenye mazungumzo niliyosikia kwenye simu.
Tunazo taratibu za aina tatu katika malipo ila kwa sasa nina shughuli nyingi kidogo hivyo inabidi nikupeleke kwa karani ili akufafanulie.Alimaliza maelezo na kuanza kuongea na simu nyeusi, baada ya kuongea na simu aliniambia nisubiri kidogo na kuanza kupekua makablasha.
Baada ya dakika tatu hivi aliingia kijana mmoja miongoni mwa wale wawili waliokuwa mapokezi. “Halo mimi natoka hivyo mwelekeze huyu ndugu jinsi ya kuweza kupata bidhaa hapa kiwandani. Ofisi itakuwa chini yako mpaka saa kumi na nusu nitakuja kufunga shughuri nisubiri usiondoke.” Alimueleza yule kijana. Baada ya kutoa maelezo aliingia katika mlango uliokuwa ofisini kwake na karani alianza kunipa maelezo ya namna ya malipo na jinsi ya kupata mzigo. Wakati naendelea kumsikiliza Mr Catto alitoka alikoingia na kuelekea mlango wa kutokea nje.
“Halo ndugu mimi natoka, kama kutatokea kutokuelewa njoo unione kesho nitakuwepo” Mr Catto aliniambia.
“Sawa.” Nilimjibu huku akiondoka.
Baada ya maelezo ya karani tulikubaliana niende kesho nikiwa nimeandaa hundi ya malipo pamoja na ya usafiri.
Ilikuwa ni baada ya dakika kumi na tano nilipotoka na kutomkuta Kikakika na gari ikiwa imepaki na funguo zikiwa ndani. Nilisubiri dakika tano sikuona dalili zake, nikapiga honi lakini hakutokea. Hivyo nikaondoka na kuja hapa.
Sonno alipomaliza maelezo hayo nilikaa kimya nikitafakari, nilianza kuhisi kuwa huenda kuna kidudu mtu tayari ameishanusa kazi yetu.
“Kwa hiyo una mawazo gani?” Nilimuuliza Sonno.
“Inawezekana Kikakika amegundua jambo au limempata jambo wakati mimi nikiwa ndani ya kiwanda.” Alijibu Sonno.
Sasa sikiliza: Itabidi tuachane hapa, mimi nitapiga simu Tabora kueleza hali halisi kwani kuna mambo niliyoyagundua ambayo itabidi niongee na ofisi yetu kwanza alafu nitoe mpangilio wa wa kazi, yawezekana tukachukua mali leo hii. Kwa hiyo wewe piga simu hotelini kwa Kikakika uulize kama kafika hapo au waweza kwenda muulizia hapo. Alafu tuonane saa nane kamili Delux Hotel kwa majadiliano kamili. Nilieleaza.
Tuliongoza kutoka huku tukiwa na fikra za namna ya kumpata Kikakika,, wakati huo ilikuwa ni saa saba na nusu hivyo tulikuwa na nusu saa tu ili tuonane tena kwa mipango mingine huko Delux. Wakati tunafika getini gari aina ya 110 Land Rover ilipaki maegesho akashuka Kikakika akiwa ameshikilia funguo. Alikuwa hajatuona, nilimwambia Sonno waongozane tuonane saa nane kama tulivyopanga. Niliwasha pikipiki Kikakika akashtuka na kuangalia muungulumo ulipotokea nikampungia mkono na kumuonyesha Sonno alipo. Nikaondoka.











4
Ilikuwa ni saa nane kasoro dakika ishirini niippopiga honi katika jumba moja la kifahari liliopo Kirumba mwanza, alitokeza msichana na kuchungulia alafu akafungua geti. Hapo palikuwa ni nyumbani kwa shemeji yangu, niiingiza pikipiki ndani ya geti. Niliingia ndani nikasalimmiana na dada na kuomba simu. Aliniruhusu kutumia simu iliyokuwa kwenye chumba cha vijana wake ambao hawakuwepo kwa wakati huo. Hivyo nilikuwa huru kuongea mambo yangu bila mtu yeyote kusikia, baada ya dada kunufungulia mlango nani kuingia niliufunga kwa ndani.
Nilizungusha namba za Tabora ofisini baada ya sekunde kadhaa simu ilipokelewa upande wa pili
Halow naomba kuongea na mzee Chata. Nilisema bila salaam.
Nani wewe? Niliulizwa na sauti nzito.
Pheady. Nilijibu haraka.
Ohoo! Kumbe ni wewe kijana.Mimi ndie hasa uliyemuhitaji.
Shikamoo, nilisalimu baada ya kusikiliza sauti yake kwa makini na kuitambua.
Marahaba, vipi mipangilio ya kazi. Alijibu na kuuliza.
Sikiliza mzee, nilianza kumueleza; Kutokana na mpangilio mzima ulivyo sasa ni kwamba hiyo mali inaweza kupatikana ila kuna kitu kimoja kinachotatiza, kwani kuna uwezekano wa mmoja au wawili wetu kuwa chini ya ulinzi wa polisi kutokana na ufanikishaji wa hii kazi lakini uwezekano wa mali kupatikana na kuwa imeondoka na mmoja wetu atakayesalimika upo. Suala ni je? Kama itatokea hivyo kuna ufumbuzi gani? Maana uwezekano wa kuondoka na mali bila kugusana na dola ni mdogo mno. Nilimaliza maelezo yangu.

Sikiliza Pheady, kutokana na uzito wahiyo kazi mliyopewa ofisi zote Tanzania zilizo chini ya kivuli chetu zinawaangalieni ninyi na kuhakikisha kuwa mnafanikiwa. Hivyo suala la polisi lisiwape tabu ofisi zetu zilizopo hapo zinaweza kumaliza hayo matatizo bila bughuza yoyote ili mradi msisihikwe na kizibiti. Nawataka mtumie akili sana ili kusiwepo makosa ya wazi yatakayo watia hatiani, natumaini unanielewa ila ikibidi kuua ua bila tatizo kinachotakiwa ni kufanikisha azima yetu. Ofisi iliyopo hapo inashughulikia suala lenu, nimetoka kuongea na mkurugenzi wa hapo kaniambia mnatakiwa kwenda kusaini hati za malipo kwa ajili ya walithi wenu huenda kukatokea maafa kwa upande wetu vilevile. Hiyo sio kai ya lelemama najua ikifanikiwa itatuweka kwenye chati ya juu katika masuala ya kifedha.
Sawa nimekuelewa mkuu hivyo nitawasiiana na ofisi ya hapa Mwanza kwa mambo hayo na yoyote yatakayojitokeza.
Ndivyo ilivyo na si ofisi hiyo tu bali ofisi yoyote wakati wowote na sehemu yoyote ili kufanikisha zoezi hilo. Alisema mzee Chatta
Ok, kwa heri mzee jitahidi usikilize taarifa ya habari ya saa tano usiku. Nilimalia na kukata simu kabla ya kujibu.
Nilitoka na kumuaga dada huku nikimuahidi kuwa ningurudi kula chakula cha usiku. Ilipofika saa nane na dakika tatu niliingia Deluxe Hotel na kuwakuta wakiwa wanakunywa sharubati.
Hali vipi? Niliwauiza huku nikivuta kiti na kukaa.
Safi, walijibu kwa pamoja huku Sonno akimuita muhudumu.
Utakunywa nini? Aliuliza Sonno.
Sharubati ya ndimu, nilijibu.
Lete sharubati ya ndimu, Sonno aliagiza.
Ndio mr Kikakika, naona ushakutana na vibweka vya mitaani maana naona sio kawaida au siyo? Nilianza maongezi.
Kama ulikuwepo vile. Aijibu Kikakika ambaye wakati wote alikuwa kimya. Inaonekana hii shughili si ya kitoto, inatubidi tuwe waangalifu sana kutokana na jinsi ilivyo ni kuwa baada ya Sonno kuingia katika ofisi za pale kiwandani mimi nilibaki nimeegemea gari huku nikivuta sigara. Kikakika alieleza.
Baada ya muda wa dakika tano hivi ilifika land rover 110 ikiwa na dreva ambaye alishuka na kuongea na kijana mmoja hivi niliyemuhisi kuwa muhudumu wa ofisi za hapo kuwandani. Muonekano wa huyo dreva ulinivuia, kwani alikuwa kijana wa miaka kama ishirini na nne hivi alivaa suti ya rangi ya maziwa na miwani ya jua pamoja na kofia ya Mungu usinione. Baada ya kuongea na huyo muhudumu alirudi na kugeuza gari lake kuelekea barabara kuu na kulizima huku akiwa amebaki ndani ya gari.Wakati wote huo nilikuwa namuangalia kwa kutumia kioo cha gari yetu.
Baada ya muda nilisikia muungurumo wa gari nyingine nikageza shingo kuangalia barabarani, kwanza nilimuona dereva wa 110 akifanya haraka kuvua kofia na kuishikilia mkononi huku akitoa mkono wenye kofia nje kupitia dirishani. Muda mfupi baadae ilipita gari aina ya pajero ikiwa katika mwendo wa polepole tofauti na muungurumo ulio sikika, ndani ya pajero kulikuwa na vijana wawili ambao macho yao yalielekea upande wa gali zetu ziliposimama. Niliwea kuwaona vizuri kwani kwani maegesho ya ofisi ya Mr Catto hayapo mbali na barabara kuu. Ilipokuwa imepita hiyo gari niligeua shingo na kuangalia kwenye kioo cha gari letu papo niliwea kumuona dereva yule wa 110 akiangalia saa na kuangaa huku na huko alafu akainama ndani ya gari usawa ambao haonekani dirishani mpaka uwe karibu. Mpaka hapo nikawa nimemuhisi vibaya.
Haukupita muda akashuka kwenye gari na kulekebisha vioo vya gari lake vinavyotumika kuangalia nyuma. Akiwa katika kulekebisha ilitokea gari ya Mr Catto nyuma ya jengo la ofisi, alirudi haraka kwenye mlango wa gari lake akaingiza mkono kwa dirishani na kuutoa. Wakati huo gari la Mr Catto lilikuwa linampita kwa karibu. Nilichukua nafasi hiyo na kutoka kwenye gari na kusogea karibu na gari lake wakati yeye akizunguka kuelekea mlango wa dereza. Nilipofika usawa wa mlango wa mbele niliweza kuona radio call ndogo pembeni ya kiti cha dereva, wakati huo yeye alishakaa kwenye kiti cha dereva na kufunga mlango. Kutokana na kutolidhika kwangu na vitendo vyake nilivyoviona kwake niliamua nimfuate.
Nilikatisha mbele ya gari lake wakati yeye akilitia funguo, niliwahi kumsemesha huku nikiangaza macho kuona kama kuna mtu yeyote karibu anayetuangalia. Kutokana na hali ya maeneo hayo sikuona mtu zaidi ya sisi na magari manne yaliyokuwa yamepaki hapo.
Samahani naomba msaada wako kidogo. Nilimsemesha.
Msaada gani? Aliuliza.
Labda ungeshuka uje uangalie ni kwenye gari ile pale. Niimueleza.
Mpaka nije niangalie?!...Kama huwezi kusema nipishe huko nina haraka zangu. Alinijibu kifedhuli.

Kwa kuwa dirisha la mlango wa nyuma ya dereva ulikuwa wazi na kitasa cha mlango kilionyesha kuwa wazi nilitoa pisto yangu kwa mkono wa kulia huku mkono wangu wa kushoto ukifungua mlango kwa kasi ya ajabu na kumuwekea sikioni mdomo wa pisto.

Tulia kijana usitikisike wala kupepesa, niliunguruma huku nilijisogeza kukaa kiti cha nyuma yake, alikuwa amekauka kama mti mikono juu ya usukani. Aliponiona nasogea kukaa kiti cha nyuma akatelemsha mkono wa kushoto kwa akili na kutaka kugusa ile simu ya upepo niliwahi kumpiga na kitako cha pisto kwenye mishipa ya fahamu ya kwenye sikio akazimia. Nilimsukuma pembeni mwa kiti cha dereva na kuhanmia kwenye kiti cha dereva mimi mwenyewe. Nilionelea nitafute sehemu nzuri ya kumuhoji, kabla ya kuondoka nilifungua tai yangu na yake na kumfunga mikono na miguu kwa nyuma nilihofia anaweza kuzinduka wakati wowote.

Nilishika barabara kuu na kuchoma mafuta kuelekea upande wa magu, baada ya mwendo kama wa dakika kumi hivi niliona njia ya vumbi inayochepuka kutoka njia kuu nikaifuata ilikuwa inaelekea mashambani. Nilipofika umbali ambao mtu anayepita barabarani hawezi kuniona nilizima gari na kumgeukia mateka wangu.

Alionekana akitweta wakati fahamu vilikuwa hazijamrudia, niliangaza huku na huko kwenye hiyo gari nikaona mkebe wa mafuta ya break. Nilichukua mafuta hayo na kummiminia sikioni akashtuka na kutaharuki, hapo nilitoa kuberiti cha gesi na kumwonesha alafu nikaanza kumuhoji maswali ya kijelajela. Wakati wote nilikuwa sijampekua.
Unaitwa nani na pale kiwandani ulienda kufanya nini? Niliuliza
Unaniuliza hivyo ukiwa kama nani? Alijibu kwa swali.
Sikiliza kijana, nilianza kuongea huku nikimpekua na kabla sijamaliza usemi wangu niligusa kitu kigumu upande wa ubavu wake wa kushoto nilipokitoa nilikutana na pisto hapo nikaanza kuhisi huenda akawa askari lakini niliamua kupambana naye mpaka ajieleze maana hakuwa na kitu kingine cha kumtambulisha zaidi ya pesa ambazo nilizichukua na kuzifunda mfukoni.

Niliwasha kiberiti cha gesi na kuweka chini ya sikio lake. Sema wewe ni nani? Nilimuuliza.
Micky. Alijibu huku akinyanyua sikio lake kuepuka joto la moto wa kiberiti.
Unafanya kazi gani? Niliendelea kuuliza
Alikaa kimya nikasogea kiberiti sikioni, akatoa mguno mkali kasha akasema; mfanya biashara.
Usinidanganye. Nilifoka huku nikisogeza zaidi kiberiti sikioni.
Basi acha nitasema. Alipiga kelele. Nilimuongezea na kofi la kushoto alafu nikatoa moto.
Nimeajiriwa na tajiri mmoja kwa shughuri za ulinzi wake wa siri. Alisema huku macho yamemtoka kwa woga. Nafikiri alidhani mimi ni mpelelezi hivyo akawa anagwaya kosa la kutembea na pisto.

Pale kiwandani ulienda kufanya nini?
Nilitumwa.
Ulitumwa nini?
Kuchunguza nyendo za Mr catto.
Nani alikutuma?
Bosi wangu Patrick.
Anafanya kazi gani?
Ni mfanya biashara huwa anasafiri nje ya nchi mara kwa mara.
Umeanza kumfanyia kazi toka lini?
Huu ni mwezi wa sita.
Hebu niambie kabla ya leo huwa unashughilika na nini haswa. Nilimuuliza huku nikitoa kisu nyuma ya mgongo. Baada ya kuona kisu na jinsi nilivyobadilika usoni alitumbua macho na kuanza kubwabwaja.

Tafadhari kaka nisamehe mimi nimejiunga mda mfupi sijawahi kushiriki kwa lolote hii ndio kazi yangu ya kwanza.
Kwa hiyo pale pale ulikuwa unafanya nini?
Nilitakiwa kuchunguza nyendo za Mr catto na kuwasilisha kwa Patrick.
Ulikuwa unawasiliana naye kwa njia ipi?
Kwa kutumia hiyo radio call.
Kwa nini alitaka kujua nyend za Mr Catto?
Sijui.
Baada ya hapo kiwandani ulitakiwa kufanya nini?
Nilitakiwa kurudi nyumbani kwa Mr Catto kuendelea kufatilia mambo ya pale nyumbani.
Ok, mjulishe Patrick kuwa upo njiani kuelekea kwa Mr Catto. Nilisema.
Lakini mpaka unifungulie mikono. Alijibu.
Nilifikiri kidogo kama anaweza kunipa shida nikimfungua, ila nilikata shauri kumfungulia ili aweze kumtoa wasiwasi Patrick name nizidi kumchimba zaidi hiyo nikamfungua zile tai nilizomfunga kama kamba.

Baada ya kumfungua alichukua ile radio call huku nikiwa nimemuwekea mdomo wa pisto sikioni. Alibonyeza kidude kimoja chekundu na cheusi kwa pamoja nikaona sehemu ya juu ya kioo cha radio call kikionyesha rangi nyekundu na kabla sijaweka uzingativu kwenye hilo ghafla nilipigwa mkono ulioshika pisto nayo ikadondoka nje ya gari kupitia dirishani. Wakati nataka kugeuka nikakutana na ngumi mbili za shingo zilionichanganya na kujikuta nikiwa nimepigwa kabari la sheria yake

Akili zilinichemka haraka baada ya kuona mbo yamenigeuka, pamoja na kuigwa kabari nilijivuta na kujikunja alafu nikakanyaga ubavuni mwa gari kwa ndani upande wa dereva na kujisukuma kwa nguvu zangu zote kwa kutumia miguu tukawa tumeanguka chini kutokana na msukumo uliosababisha kufunguka kwa mlango wa upande wa pili.

Tuliponguka aliniachia huku akiwahi kuamka alitaka kuwahi kuchukua pisto iliyokuwa imeanguka upande wa pili wa gali, lakini alikuwa amechelewa kwani mimi nilikuwa mwepesi zaidi. Alipogeuka tu nilijirusha na kumsimia miguu yangu yote mgongoni, alijigonga kwenye gari, alipogeuka kunukabili nikaona alikuwa amepasuka sehemu ya juu ya jicho. Leo utanitambua alisema huku akivua shati kwa kulirarua.

Mkwara mbuzi tu huo nilisema huku nikijiweka sawa kukabiliana naye. Mwili wake ulikuwa umejengeka misuli yenye nguvu, alijirusha katika mruko wa mkuki, nikamuona na kumkwepa akanipita na kusimama pembeni yangu palepale nikaachia kono langu la kushoto lililommpata usawa wa koromeo akayumba na kukohoa. Nikavurumisha guu langu la kulia akaliona na kulipisha alafu akanipiga kichwa kimoja usawa wa kidevu damu zikanivuja.
Kuona vile nikapandisha mzuka na kuahia ngumi tatu mfululizo ambavyo mbili zilimpata kifuani na moja ikampata usawa wa paji la uso na kumfanya aanguke. Alinyanyua kichwa na kukitingisha alafu akarudi chini na kuzimia. Wakati napanga cha kufanya nilisikia muungurumo wa gari ukielekea njia hii. Palepale niliinama haraka na kumuwekea goti mgongoni mateka wangu alafu nikamvunja shingo na kumsukumiza kwenye nyasi ndefu vilizokuwa pembeni mwa barabara. Niliokota pisto na kurukia ndani ya agari kwa haraka na kurigeuza kwa kasi ya ajabu, likakaa usawa wa barabara nikaongoza kurudi mjini.

Kabla sijafika barabara kuu niliona gari nililoliona wakati nikiwa kiwandani kwa Mr Catto nikajiweka sawa, tulipokalibia kupishana kuna mtu alitoa shingo kuchungulia alafu ghafla zikamwagwa risasi. Niliwahi kuinama zikapita na gari nililokuwa naendesha likayumba na kulipiga lile tulilopishana nalo kwa kitako na kusababisha gari hilo liseleleke wakasimama ghafla na wakati huohuo nami nilichungukia dirishani pisto mkononi na kuachia risasi moja iliyotua kwenye tairi moja la nyuma, hapo nikawaacha kwenye mataa.

Baada ya maelezo ya Kikakika ilikuwa wazi kuwa kuna kundi la watu linalofatilia nyendo za Mr Catto vilevile ambalo kiongozi wake alikuwa Patrick

Sikilizeni, nilianza kuongea mimi Pheady; Kutokana na maelezo yako, inabidi tufanye hii kazi haraka na kwa ufanisi zaidi kwani tofauti na polisi bado kuna watu tunaweza kuambana nao. Nimeongea na ofisi yetu inasema kuwa tunaweza kufanya lolote lile ili kwamba tufanikiwe. Kuhusu polisi tusiwe na wasiwasi isipokuwa isitokee tukashikwa katika mazingira yatakayokuwa na ushahidi wa wazi. Hivyo basi kutokana na taarifa tulizokusanya inabidi tuifanye kazi hii mchana huu kabla ya usiku wa leo.

Tulijadiliana kuhusu utendaji wa kazi hii ya wizi tukaafikiana kuwa mimi na Kikakika twende Pamba Hostel kwa nyakati tofauti, mimi nitatangulia alafu yeye atafuata na awe ananilinda na kuangalia maelekezo yangu kwa siri. Hiyo yote ilitokana na hisia kuwa kutakuwa na mabadilishano ya mali pale Pamba Hostel. Siku zote kazi ya wizi inataka uwe na hisia kali na uwe na uwezo wa kushuku jambo kabla hata ya mpelelezi au askari kujua ili uweze kuwa hodari katika shughuri hii na kukwepa kushikwa hatimaye kuozea gerezani. Kutokana na hayo tuliamua tuchukue hizo dhahabu ale Pamba Hostel kabla ya kufika kwa Mr Catto, ikiwezekana tuchukue na fedha zao za kuuziana na hapo tutakuwa tumeua ndege wawili kwa jiwe moja.

Sonno ilibidi aende katika ofisi zetu za hapa Mwanza kuchukua gari na kutusuburi Chinese Hotel karibu na jumba la sinema la Liberty. Iwapo kutatokea kufukuzana na polisi itabidi mimi niwazuge kwa pikipiki na kwenda kuiacha kwa Sonno alafu naondoka na gari ili kusudi waendelee kumfukuza Sonno wakati mimi naondoka na mali. Kikakika angetumia gari ambalo wamekuja nalo wao kutoka Tabora.

Baada ya majadiliano na malekekebisho machache tulitakiana kila la kheri na kumkumbusha Sonno avae mavazi yatakayolandana na yangu vilevile awe na kofia ya kichwani ya kuendeshea pikipiki inayolandana na niliyonayo. Kama kutatokea hitilafu basi tuonane Igoma bynight, atakayewahi kufika achukue chumba cha vitanda viwili na kusuburi. Nilieleza huku nikijiandaa kuondoka. Zilikuwa zimesalia dakika kumi na saba kufikia saa tisa kamili ambayo ndiyo saa ya wakati wenyewe.

5
 
HAYA TUENDELEE HAPO


Patrick Mwisongo ni kijana mwenye umri wa miaka thelathini na minne alibahatika kupata elimu ya juu na hatimaye na hatimaye kwenda ulaya kuendelea na masomo. Baada ya kuhitimu masomo yake alitakiwa arudi nchini, lakini hakufanya hivyo akawa amepotea kwa muda wa miaka minne, na wakati anarudi Tanzania baada ya miaka hiyo minne alikwa tayari ni tajiri wa kutosha.

Wakati anarudi Tanzania alikuwa ni wakala wa siri katika kitengo kimoja kilichozaliwa kutoka katika shirikala la ujasusi la Afrika Kusini wakati wa utawala wa kibaguzi la BOSS, na hicho ndio kiini cha utajiri wake. Katika miaka aliyopotea alikuwa ameambatana na rafiki yake mmoja wa Afrika Kusini katika kambi moja ya mafunzo huko Colombia.

Hivyo basi wakati huu alikuwa Mwanza kama mfanya biashara na huku akifanya kazi a kijasusi kwa siri. Alikuwa amefanikiwa kujenga kikosi cha watu tisa yeye akiwa wa kumi, miongoni mwao wakiwemo sita waliofuzu kwa mapigano ya mikono na matumizi ya siraha kwa kiwango ha juu. Yeye binafsi alikuwa ni gwiji katika fani hiyo.

Ilikuwa ni saa saba alipopata taarifa ya kuuawa kwa kijana wake mmoja, alichukizwa na hali hiyo na kuwaambia wote wakutane kwake kabla ya nusu saa kupita. Sikilizeni ndugu zangu, aliongea Patrick baada ya wote kuwa wamewasili.
Kitendo cha kuuawa Abbas ni cha kutia aibu na doa katika shughuri zetu, ni kitendo cha kusikitisha vilevile kwa kuondokewa na mwenzi wetu katika shughuri zetu. Kitendo hiki kinaweza kusababisha watu wa serikali na jamii kwa ujumla waanze kutuangalia kwa jicho la maswali, kitu ambacho kitatupa wakati mgumu katika utekelezaji wa mambo yetu. Tumejenga kikosi chetu kwa usiri mkubwa na kufanikiwa kwa kiwango cha juu kuaminika katika jamii na serikali kwa muda mrefu hivyo inabidi tujitafakari kwa nini leo tunaanza kutoa mwanya wa maswali juu yetu. Ebu fikirieni mkuu wa kazi ataelewa vipi atakapo pata taarifa ya kifo cha Abbas.

Pamoja na hayo inabidi sasa tuhakikishe kuwa aliyemuua anapatikana na kutueleza kwa nini amemuua wakati huo huo tuchukue dhahabu kwa Mr Catto. Ni vitu viwili vinavoendana kwani nafikiri muuaji atakuwa ni mshirika wa yule mwenye pikipiki au ndie yeye. Ikiwa ni hivyo basi inabidi mimi na mmoja wenu tufatilie hizi habari za huyu mwenye pikipiki kama ni mpelelezi tutajua vilevile. Hapa tulipo hatujui Abas ameongea nini na huyo mtu kabla ya kuuawa, alafu Moddy na mwingine waendelee kumfuata Mr Catto. Alinyamaza kuwaachia wenzie ukumbi wa kuchangia mawazo.
Hallo Mr Patrick, kwanza kabisa ningeomba tupate picha za huyo mtu mwenye pikipiki, aliongea Moddy, kijana mmoja mdogo wa umbo lakini mavitu yake katika uwanja wa mapambano ni hatari. Hufanya matendo anbayo huwezi tarajia kufanywa na binadamu katika ulimwengu halisi labda katika ulimwengu wa uigizaji kama kwenye sinema.
Sawa, hebu Zuberi tupatie hizo picha. Aliongea Patrick huku akimtazama kijana mmoja mrefu mwembamba wa wastani lakini aliye na misuli yenye nguvu. Si mwingine bali ndiye Zuberi aliye kubuhu katika mapigano ya kareti. Zuberi alisimama na kutoa mkanda wa picha ambao haujasafishwa pamoja na kikaratasi kilihoandikwa namba ya pikipiki.

Unajua hizi picha hazionekani vizuri kwenye huu mkanda kutokana na namna nilivyozipiga kwa kutumia darubini ili nisimshitue huyo jamaa. Kama nilivyowaeleza kuwa nimepiga nikiwa kilimani wakati akitengeneza pikipiki jirani na kwa Mr Catto, nilipiga kwa utashi wangu tu lakini kilichonishitua ni wakati Mr Catto alipotoka na gari lake nilimuona huyu jamaa akilekebisha haraka pikipiki yake na kufuata nyuma, kwa kuwa nilikuwa na darubini sikujisumbua kuwafuata kwa karibu kwani niliweza kuwaona kwa mbali. Baadae huyo jamaa alinipotea kwenye upeo wangu nikaja kumuona tena kule forodhani alipopaki pikipiki katika maegesho ya ofisi za Singer sewing machine na kuelekea karibu na gari la Mr Catto ambaye alikuwa kapaki pale kituo cha kati cha polisi. Alipokuwa karibu na gari la Mr Catto gari la Mr Catto likawa linaondoka akapishana nalo na kuelekea katika geti la forodhani.

Hiii ya kwanza niliipiga akiwa kule kwa Catto amevaa kofia ya kuendeshea pikipiki ya pili nimeipiga wakati amepaki pale Singer na amevua kofia ya kendeshea pikipiki, lakini baati mbaya sikuwa sehemu nzuri hivyo ilinibidi nimpige kiubavu na hiaonyeshi sura yake vivuri. Ndipo ilipobidi nitafute sehemu nzuri na kubahatika kupata hii picha ya tatu ikionyesha sura yake. Hii inayoonekana hapa ni gari ya Mr Catto ikigeuza njia na ndio wakati niliopapa sura yake sawa. Alimaliza kuongea Zuberi.
Sasa wewe Zuberi baada ya hapa nenda kasafishe hizo picha ili tuweze kupata picha zenye kuonyesha sura sawasawa. Alieleza Patrick na kuendelea, Moddy, Gilly na Herbert muondoke mkamfatilie huyo Mr Catto kama mukihisi jambo lolote fanyeni kinachotakiwa muhimu ni dhahabu tu ipatikane. Kwenye mawasiliano hapa nyumbani atabaki Gimpe na Sifongo, mimi kwa sasa nitawasiliana na mkuu wa kazi baada ya hapo nitaondoka na Ebby kwenda kuanza kazi ya kumsaka mwenye pikipiki na kutafuta hiyo gari yetu. Wewe Punzu na Magullu mtakaa geti kama walinzi muwe waangalifu inawezekana siri zetu zikawa nje maana haileweki marehemu kamweleza nini mwenye pikipiki. Zuberi baada ya kazi ya picha nenda kashughurikie kuhifadhi mwili wa marehumu tutashughulika na mazishi yake baada ya pilika hizi kupita.

Baada ya maelezo hayo Mr Patrick aliagana na vijana wake na kuingia kwenye chumba cha mawasiliano tayari kuongea na mzee wa kazi huku Afrika Kusini na vijana walitawanyika kulingana na mpangilio wao wa kazi ulivyo.
############################################################################

Ilikuwa ni saa tisa na dakika saba wakati nilipo kanyaga breki Pamba Hostel, niliingia ndani baada ya kuwa nimeegesha pikipiki yangu chini ya mti karibu na barabara. Nilitafuta kiti kulichokuwa mahali panapofaa nikapata sehemu moja chini ya mwanvuli. Palikuwa pananiwezesha kuona nje kwa kupitia matundu ya vitofari vilivyotumika kujenga kuzunguka sehemu ya nje ya Pamba Hostel. Niliwaza kuona pikipiki yangu ilikuwa upande wa kushoto na nilikuwa nimekaa katika kona ambayo hakukuwa na mtu mwingine nyuma yangu.

Niliagiza Konyagi chupa moja pamoja na krest soda ya kuchanganyia, nilianza kukata hayo makali huku nikiunguza sigara kama sitaki vile. Watu waliokuwepo ndani hawakuwa wengi kiasi kuwa haikunichukua muda kubaini kuwa Mr Catto hakuwepo hapo. Ila miongoni mwa watu waliokuwepo niliweza kuona mtu mmoja amekaa na brifcace pembeni huku akinywa bia na amekaa na vijana wawili walioonekaka kama walinzi machoni pangu. Baada ya kumchunguza kwa siri niliona ameisha angalia saa mara tatu kwa muda usiozidi dakika tisa, ni wazi alikuwa akimsubili mtu. Hisia zikanijia huenda likawa kundi la inspekta likimsubili Mr Catto. Nilikuwa nimekaa kama robo saa hivi ndipo nilipomuona Kikakika akiingia alikuwa amezaa full jeans na chini katupia raba matata aina ya Grand Prix na juu kichwani kava kofia hakika alipendeza kama kijana wa mjini. Alipitiliza na kwenda kukaa kaunta ambapo aliongea na muhudumu na baada ya muda niliona anawekewa chupa ya Long John pamoja na bilauri yenye mabonge ya barafu, aliniangalia kwa chati nami nikama ishara ya kumwambia poa.
Alimuita tena muhudumu na kuongea naye na baada ya hapo alinyanyuka na kwenda kukaa karibu na ile meza aliyokaa Yule mtu mwenye briefcase. Nilifurahi kuona Kikakika akifanya kama nilinzofikiri, muhudumu alimpelekea kinywaji chake na kuondoka.
Wakati wote mimi nilikuwwa naangalia kwa siri, kitambo kidogo niliona ikipaki karibu na pikipiki yangu, alishuka Mr Catto pamoja na watu wengine wawili wenye miili yenye nguvu. Mmoja wao alibaki akifunga milango ya gari wakati mmoja aliongozana na Mr Catto kuingia ndani. Walipofika ukumbi wa bar Mr Catto aliangaza ukumbini na kuongea na mwenzie baada ya hapo walikuja kukaa meza iliyokuwa hatua chache toka nilipokaa kwa mbele. Punde kidogo mwenzie akawafuata na kujumuika nao, walimuita muhudumu na kuongea naye alafu mmoja wao akatoa pesa na kumpatia huku akimuonyesha sehemu aliyokaa Kikakika.
Muhudumu aliondoka na kuelekea kaunta ambapo alichukua chano ya bia na kuelekea meza aliyokaa Yule mtu mwenye briefcase, alipofika aliwawekea bia mezani na kuongea nao kidogo alafu akaondoka na kuchukua bia zingine ambazo alizipeleka kwwnye meza ya Mr Catto. Kitambo niliangaza macho na kuona ongezeko la watu kama sita hivi ndani ya bar tofauti na genge la Mr Catto. Nilipotupa macho kumuangalia Kikakika alinionyesha ishala ya kumufuata alafu akainuka na kuelekea chooni name sikufanya ajizi nilisubiri kidogo alafu nikamfuata kwa usiri.
Sikiliza Pheady, alieleza Kikakika baada ya kukutana chooni. Nilimsikia muhudumu akiwambia wale jamaa waliokaa jirani yangu kuwa Mr Catto atawasuburi chumba namba tatu.
Sawa, kwa hiyo wewe rudi hapo bar uangalie kinachoendelea mimi nikatafute hicho chumba ili tuweze kufahamu kilipo kabla hawajaingia huku. Uwe muangalifu sana maana naona kuna ongezeko la watu saa hizi hatuwezi kujua wepi nko pamoja nao, tutawsiliana itakapobidi, tuliachana na Kikakika akatangulia kutoka mimi mimi nikasubiri kidogo.
Nilipotoka nilirudi katika meza yangu kwa kupita karibu na meza ya Mr Catto ambapo niliona chupa zao za vinywaji zimebaki kidogo. Nilikata bilauri moja ya konyagi alafu nikawasha sigara na kunyanyuka na kuelekea sehemu za vyumba. Nilipita kwenye korido iliyokuwa na vyumba upande mmoja huku nikiangalia namba za vyumba kwa usiri huku nikiendelea mbele, baada ya kuvipita vyumba vinne nilikuta ngazi zikipandisha juu, nilizipanda harakaharaka na mara tu nilipozimaliza tu nikakiona chumba namba tatu kikiwa pembeni yangu upande wa kushoto ambapo mwisho wa hicho chumba ndio mwisho wa nyumba.Kulikuwa na ukuta mfupi wa matundu kuunganisha na safu nyingine.
Niliangaza huku na huko sikuona dalili ya mtu nikasogea na kuchungulia chini kwenye ngazi vilevile sikuona mtu,nilitoa funguo zangu ambazo ni maalumu kwa ufunguaji milango yoyote na kuusogelea mlango. Nilichomeka ufunguo na kujaribu kufungua, mlango ukakubali kufunguka, hapo nilichungulia ndani na kuona vitanda viwili pamoja na meza katikati pembeni kulikuwa na kabati ya nguo yenye kioo cha kuweza kujiona mwili mzima. Kutazamana na hiyo kabati kulikuwa na dirisha la vioo lililofunikwa na pazia nusu. Niliingia na kwenda kufungua dirisha ambapo nilijikuta naangalia stesheni ya treni na kikorido chembamba chenye ukuta mfupi wa wenye matundu.
Nilitoka na kuliacha dirisha wazi, baada ya kufunga mlango nilielekea mbele kutafuta njia ya kunufikisha kule kwenye dirisha, tendo la kuingia mle chumbani na kutoka halikunichukua zaidi ya dakika moja. Niliendelea mbele kuvipita vyumba vitano nikaona njia mkono wa kulia huku nyingine ikiendelea, nilikata na kuifuata njia hiyo ambayo ilinifikisha kwenye korido kiliyoiona kule chumbani kupitia dilishani. Mkono wa kulia ndio kulikuwa na kile chumba kwa mwishoni kabisa alafu upande wa kushoto korido iliendelea ili kuwapa njia watu wa vyumba vilivyokua sehemu hiyo kwani milango ilikuwa inatazama hicho kinjia kwa upande huu wa kushoto. Niliusogelea huo ukuta na kuchungulia chini ambapo kulikuwa na nyasi fupi zilizokatwa kwa ufanisi. Niligeuza njia na kuanza kurudi, nilishapata nilivyohitaji kazi ili baki moja tu ya utekelezaji, yaani kuhakikisha kuwa tunaondoka na hizo mali zao.
Nilipita karibu na alipokaa Kikakika na kumpa ishara anifuate alafu mimi nikaongoza nje na kuelekea kwenye kibanda kilichokuwa umbali kidogo na kinauza sigara na magazeti. Kikakika aliniona na kunifuata name nilinunua sigara na kumsubiri pembeni mwa hicho kibanda, alipofika nilimweleza hali halisi kwa haraka na yeye alininieleza kuhusu watu furani ambao walionekana kuiangalia sana pikipiki yangu. Tulijadiliana mambo mawili matatu hivi tukakubaliana Kikakika aende akamuone Sonno na kumuelekeza aegeshe gari kwa nyuma ya Pamba Hostel upande wa kile chumba kwani kulikuwa na barabara pembeni ya bustani ya nyasi na asicheze mbai na gari awe anaangalia kinachoendelea huko juu ili kusudi iwe rahisi yeye kutusaidia. Baada ya mazungumzo hayo tuliachana na Kikakika akaenda kuchukua gari ili akamuone Sonno mimi nikarudi Pamba Hostel.
Ilikuwa saa kumi na mbili kasoro dakika nane wakati Kikakika alipokuwa anaingia ndani ya ukumbi wa Pamba Hostel baada ya kutoka kwa Sonno, wakati huo Mr Catto alishapotea pale alipokuwa lakini Yule wa briefcase alikuwa bado anaendelea na unywaji. Kikakika alipitiliza mpaka kaunta na kuchukua kinywaji huku akiangaza kila upande kwa siri, nafikiri alikuwa akijaribu kunipata kwa macho. Kutokana na ongezeko la watu lilokuwepo kwa wakati huu isingekua rrahisi kuniona. Mimi niliweza kutambua hali hiyo nikaamua kwenda kuchukua pegi tatu za John Walker kaunta ili tuwasiliane, wakati nakalibia kaunta niliona wale watu wawili na mwenye briefcase wakiamka na kuondoka kuelekea sehemu zilizo kuwa na vyumba. Nilibadili mawazo nilipofika kwa Kikakika, nilimsalimia na kumuambia anifuate kwenye meza niliyokuwa naye akafanya hivyo.
WakinaCatto wameishatangulia huko chumbani na washirika wake naona wanaelekea huko sasa hivi kwa hiyo tusubii kidogo alafu mimi nitatangulia wewe unifuate baada ya dakika tano. Uwe muangalifu sana huenda lile kundi la Yule uliyemuua likawa hapa maana na wao wanafatilia nyendo za Mr Catto. Pisto yako ina kiwambo cha kuzuia sauti? Nilimaliza maeleazo na kuuliza swali.
Ndio. Kikakika alijibu. Tuliendelea na mazungumzo ya utekelezaji kwa muda kidogo ndipo Kikakika akaniambia muda tuliokaa unatosha hivyo niondoke. Ilikuwa ni saa kumi na mbili na nusu giza lilishaanza kuingia.
Niliondoka kuelekea hicho chumba namba tatu, nilipomaliza kupanda ngazi nilimkuta jamaa mmoja ameegemea ule ukuta mfupi wenye matundu akiangalia nje ya jengo. Nilimfahamu kuwa ni mwenzao hivyo nikajua yuko kwenye ulinzi, alionekana kutojali kama kuna mtu anakuja.
Nilipitiliza na kuelekea njia ambayo itanipeleka nyuma kwenye dirisha,nilipotokeza sehemu ya korido la nyuma kwenye dirisha niliona mtu mwingine ameegamia ukuta huku akivuta sigara. Nilipitiliza pia na kuendelea kwenye vyumba ambavyo milango inatazama upande huo, kwa kuwa nina ufungua Malaya nilifungua mlango wa chumba kimojawapo na kabla ya kuingia chumbani nikajipapasa na kutoa paketi ya sigara. Wakati wote huo huyo mtu alikuwa akiniangalia, aliponiona namfuata huku nikitoa sigara kwenye paketi aliingiza mkono mfukoni na kutoka na kiberiti cha gesi huku mkono mwingine umeshikilia sigara. Nilipomfikia alinyoosha mkono kunipa kiberiti kabla hata sijamsemesha, kufumba na kufumbua nilimpiga kareti ya shingo na kmvunja shingo palepale maana ni pigo ambalo hakutegemea akafa bila hata kutoa sauti.
 
TUENDELEE


Nilimchukua na kumuegemeza kwenye ukuta mfupi wenye matobo kama mtu anayechunguia chini. Niliangaza huku na huko sikuona mtu nikasogea dirishani kwa kunyata, hapo dirishani nilichungulia kwa tahadhari lakini sikuona ndani vizuri nikajirekebisha ili niweze kuona vizuri, wakati ajaribu kuona ndani kwa ufasaha ghafla nikasikia kishindo pembeni yangu nikageuka haraka na kukutana na Kikakika akitabasamu huku mtu ameanguka katikati yetu akiwa ameshikilia bastola, nikajua alitaka kunimaliza ila Kikakika akamuwahi, nikamuonyesha ishara achukue tahadhari ya ulinzi ili niweze kuona ndani akafanya hivyo.
Nipotupa macho ndani nikawaona kwenye kioo cha kwenye kabati, wawili wakiwa wanahesabu pesa wakati wawili wengine wakiwa wamekaa na kuangalia alafu briefcase nyingine ilikuwa wazi juu ya meza huku ndani yake kukiwa na mifuko mitatu ya khaki na pembeni mwa meza kulikuwa na chupa za mecury na acid ya kuhakikishia ile dhahabu. Nikajua mambo tayari.
Nilisogeza ile maiti gizani pembeni na kumfuata Kikakika aliyekuwa upande wa pili nikamwambia twende tukafunge kazi nitavuta pazia kwa mkono naye awe tayari kwa kushambulia kwa kutumia bastola mbili nilisema huku nikimkabidhi bastola yangu.
Tulifika dirishani nikavuta pazia kwa nguvu ili kutoa mwanya wa kuona vizuri, waliposhituka kuangalia watatu wakakutana na risasi za Kikakika zilizowapata sawasawa wakawa maiti. Mmoja aliruka na kuchomoa sikumchelewesha kwani nilirusha kisu kwa wepesi na kutua kwenye koromeo lake palepale akaanguka chali. Nilirukia ndani haraka Kikakika akabaki dirishani akiangalia usalama hapo nilikusanya pesa na kuweka kwenye briefcase yenye dhahabu na kuifunga. Nilitoka kwa kutumia mlango baada ya kuona ni shwari na Kikakika naye alipita dirishani na kuja kutokea mlangoni, kutoka hapo tulielekea kwenye ukuta mfupi wenye matundu kule pembeni na tulipofika Kikakika alianza kuteremka kwa kushika matundu ya ukutani alipofika mwisho wa matundu alijirusha kama nyani na kutua chini. Hapakuwa mbali kwani tulikuwa ghorofa ya kwanza na giza lilishaingia, baada ya kutua chini nilimrushia ile brifcase na kumuonyesha ishara aende kwa Sonno. Niligeuka na kuanza kutelemka ngazi kwa haraka, nilipomaliza ngazi niliona watu wawili wakija huku wakionyesha kuwa na wasiwasi, tulipishana nao wakaendelea. Nilipokaribia lango la kutoka nje upande wa bar niliona wale watu wawili wakirudi kwa kasi huku wakiangaza nikahisi jambo hivyo nikaongeza mwendo na kuwahi kutoka kwani walikuwa wameniona.
Nilipofika nje tu nilikimbia na kuwahi kuwasha pikipiki yangu, wakati naanza kuondoka wao ndiyo wanatokeza mlangoni, niliposhika barabara kuu kutoka maegesho nikakoswakoswa na risasi ambapo moja ilipita na kutokeza upande wa pili wa kiti. Niliongeza mwendokasi na kuyumbisha pikipiki ili kuwapoteza shabaha, wakati nafika kwenye mzunguko wa maktaba ya hapa Mwanza ili nishike barabara ya Kenyata nikaona kuna gari inakuja nyuma yangu kama mshale vile.
Hapo nikajua wameamua kula na mimi sahani moja, niliishika barabara ya Kenyata na kuongeza mwendo nilikuwa na uhakika wa kuwapoteza kutokana na kuwa mimi nilikuwa na pikipiki hivyo ni rahisi kupita vichocholo visivyopitika na gari. Ajabu walipo maliza mzunguko wa maktaba gari lao lilinisogelea kwa kasi ya ajabu nikahisi gari yao itakuwa aina ya Range, nilipofika kwenye kona inayounga Lumumba na Kenyata nikaiacha barabara ya Kenyata na kuingia Lumumba nao walikata kona kwa kasi ya ajabu na kuendelea kunifukuza. Kabla sijafika Shinyanga hoteli nilikata kulia katika njia nyembamba ambayo inatokea mtaa wa Rwegasole, walipofika nilipokatia kona wakasimamisha gari huku wanashangaa kwani njia niliyopita gari haliwezi kupita.
Kushituka wakagundua watu wanawashangaa kutokana na kuja kwa kasi sana wakaondoa gari na kwenda zao, hawakuwa wengine ila walikuwa ni kikosi cha Patrick Mwisongo lakini walikuwa wamenikosa kwa hali hiyo. Nilipotokeza Rwegasole niliongoza na kwenda kushika barabara ya Nyerere nikafika mbele nikakata na kushika barabara ya Pamba na kurudi barabara ya Kenyata ambapo niliongoza moja kwa moja mpaka Mwanza south katika nyumba ya mkuu wa kazi wa kikundi cha wizi cha COOL BLOOD hapa Mwanza.
Nilipofika getini nilipiga honi mlinzi akatokeza nami nilimuuliza iwapo mzee yupo, alinijibu yupo ila siwezi kumuona mpaka nijitambulishe kwake. Nilimwambia naitwa Pheady kutoka ofisi ya Tabora. Alienda katika kibanda cha ulinzi na kunyanya simu akaongea baadaye akarudi na kuniambia niende nikamuone ndani nilielekea mlangoni na kabla sijagonga mlango ulifunguliwa akatokeza mtu mmoja mwenye umbo la miraba minne. Nilimsabahi alafu nikatoa kitambulisho change maalumu kwa kazi yetu, alipokiona alifurahi na kunishika mkono huku akiniongoza ndani. Tulipofika ndani nilikuta mkewe na watoto watatu pamoja na kijana mmoja wakiangalia runinga sebuleni. Niliwasalimia na baada ya hapo mzee alinitaka nimfuate niliendelea kumfuata mpaka kwenye chumba kimoja maridadi sana na kukaa kwenye seti ya sofa huku tukiangaliana.
Lete habari kijana, maana taarifa zenu nimezipata ila hatujawasiliana nawe ana kwa ana. Vipi mambo yanaendaje? Aliongea na kuuliza.
Mambo si mabaya ila kuna kitu inabidi utusaidie. Nilieleza
Hamna wasiwasi kijana sema tu chochote kile nina hakika ya kusaidia bila hofu. Alisema mzee.
Kwana kuna gari pale Pamba Hostel namba TZE 192 mali ya ofisi ya Tabora naomba uiondoe pale na kuihifadhi mpaka utakapopata mawasiliano toka Tabora.
Pili naomba uitunze hii pikipiki niliyokuja nayo name unipe usafiri mwingine. Nilimaliza kumuambia mzee.
“Hivyo umefanikiwa bila matatizo”, alijibu
Baada ya hapo nilimpa maelezo kwa kifupi kuhusu mlolongo wa kazi mpaka tulipofikia, alifurahi sana na alinipa gari aina ya Mark II kwa ajili ya usafiri na kumuagiza Yule kijana tuliyemkuta sebuleni aingize pikipiki alafu tukaagana mimi mimi nikaondoka yeye akiahidi kwenda kushughurikia habari niliyompa huku tukiwa na ahadi ya kukutana kesho.





6
Ilikuwa ni saa tatu za usiku wakati Patrick alipoonekana mwenye uso wa huzuni, hii haikuwa kawaida yake ila ilitokana na kitendo cha kuzidiwa akili na kikundi kingine cha wizi kinachoitwa COOL BLOOD katika mkakati wa wizi wa dhahabu. Mkakati huo kwa upande wa Cool Blood uliongozwa na Pheady.
Kwa hakika alikuwa ni mtu mweye mawazo wakati huo akisubiri kikosi chake kikamilike ili aweze kutoa aliyonayo. “Sikilizeni vijana” aliongea baada ya kuwa kikosi chake kimekamilika, ilikuwa ni saa tatu na dakika ishirini hivi za usiku. Nimesikitishwa sana na kitendo cha kushindwa kwetu, tangu nianze hizi shughuri hii imekuwa mara yangu ya kwanza kufanya makosa, ila! Kufanya kosa sio kosa isipokuwa kosa ni kurudia kosa. Alinyamaza na kumeza mate, kwa hiyo basi kazi itakuwa imeanza upya kabisa, kulingana na taarifa nilizonazo dhahabu tayari mikononi mwa mwenye pikipiki na ndie aliyefanya mauaji ya hapo Pamba Hostel.
Baada ya kuwa nimefatilia habari za huyo mwenye pikipiki nimebaini kuwa anaitwa Pheady bhubhwa mwenyeji wa Ukerewe na anajulikana kama mfanya biashara pamoja na kuwa biashara zake hazieleweki. Namba za pikipiki anayotumia zimesajiliwa Tabora na ni ya tajiri mmoja mwenye asili ya kiarabu, hivyo inabidi tumsake huyo Pheady atuonyeshe mahali dhahabu ilipo. Ikibidi kumfata ukerewe tumfate kama tutamkosa ndani ya mji huu ndani ya saa ishirini na nne. Nataka haya mambo yafanyike kwa haraka na kwa ufanisi, sitaki kuona makosa yanafanyika na matokeo ya kosa lolote litakalofanyika ni kuwa kama Mr Catto kwani kwa sasa ni marehemu kutokana na ushenzi wa huyo Pheady.
Pheady ni mtu wa kuagalia sana kutokana na mawasiliano yangu na Wanna See ambaye ndie mkuu wa kazi baada ya kumueleza mkasa uliotokea na kuniomba nimtumie jina lake na picha zake anadai huenda akawa jasusi aliyeasi miaka ya nyuma akiwa akiwa ametumwa hapa Tanzania na shirika la Boss. Kwa hiyo naitaji hizo picha kama ziko tayari tuliahidiana tuwasiliane saa nne usiku niweze kumuonyesha hizo picha ili afanye utafiti haraka kabla ya mapambazuko.
Nafikiri nikimpa habari za kuuawa Mr Catto na watu wengine kuchukua hiyo dhahabu atasikitika sana lakini kwa sababu yeye ndie mkuu wa kazi lazima ajuzwe na huenda akawa na la kushauri. Patrick alimaliza maongezi huku akipokea bahasha ya picha kutoka kwa Zuberi aliyeonekana myonge kutokana na kushindwa kumdhibiti Pheady wakati alipowazidi akili pale Pamba Hostel muda mfupi uliopita. Baada ya hapo alinza kutoa maelezo ya mpango kazi kwa ajili ya kesho.
Hatuwezi kufanya kazi yoyote kabla hatujampata huyo hayawani, lazima tuakikishe tunampata kwani mali aliyochukua ina thamani kubwa na vilevlie ameishatuondolea ndugu na mfanyakazi mwenzetu hivyo tuna kisasi naye. Si utani mali aliyochukua itatufanya matajiri mpaka tunakufa kama tutaitia mikononi mwetu, kwa hiyo inabidi tupambane naye mpaka tuakikishe tunaipata au siyo? Aliuliza Patrick baada ya kutoa maneno ya kuhamasisha.
“Ndoyoo” walijibu wote kwa pamoja.
Kwa hiyo mpangilio wa kazi wa kesho ni wa wawili wawili kila gari na watakao mpatia nafasi wamteke hata ikibidi vurumai lazima apatikane, kuhusu habari za polisi msijari sana muhimu ni kupatikana Pheady aje atueleze alikopeleka hizo dhahabu. Mimi na Herbet tutakuwa pamoja na mlengo wetu utakuwa forodhani huenda akawa na mawazo ya kwenda Ukerewe. Ptrick aliendelea na maelezo.
Gilly utakuwa na Ebby na mlengo wenu mkuu utakuwa kituo cha magari huenda vilevile akawa na wazo la kuacha pikipiki na kutumia usafiri wa jumuhia kumpeleka Tabora kwa mwenye pikipiki ambaye pia namuhisi vibaya kuhusiana na shughuli za Pheady au akaamua kutumia usafiri huo kwenda Ukerewe kwa kupitia Bunda. Moddy utakuwa na Gimpe na mlengo wenu utakuwa kituo cha treni. Punzu na Magullu mtaongoka kuanzia sasa kwenda kufanya doria katika barabara kuu iendayo Shinyanga mpaka Tabora yawezekana akaamua kuondoka usiku huu kwa kutumia pikipiki kwenda Tabora. Zuberi na Sifongo mtafanya kama Punzu na Magullu ila nyie njia yenu itakuwa ya uelekeo wa Bunda.
Tutatumia gari zenye mawasiliano ambazo mkitoka hapa mkazipitie gereji, funguo zake zimo ndani na itabidi tuwasiliane kila wakati ili tuwe pamoja katika matendo. Kuweni makini katika matendo yenu msiwashitue polisi kabla hatujafanikiwa. Patrick alimaliza kueleza na kuongezea “kama kuna mtu hajaikalili vizuri sura yake kwenye picha aje achukue picha hapa maana zipo nyingi. Baada ya hapo kila kikundi kilichukua picha mojamoja na kuagana tayari kwa kumsaka Pheady kuanzia usiku huo.
Wakati Patrick na vijana wake wakiendelea na mikakati yao mie Pheady ndio kwanza nilikuwa na furaha isiyokifani kwa kufanikiwa kilahisi vile, tulikuwa tumeishaonana na wenzangu ambapo tulienda Mwanza guest alikofikia Kikakika na kuanza kupambanua pesa tulizopata. Ilikuwa ni baada ya kuwaeleza nilikoiacha pikipiki na jinsi gari litakavyokuwa limeondolewa pale Pamba Hostel. Ilipofika saa nne usiku tulikuwa tumemaliza kuhesabu pesa na kuafikiana tugawane hizo pesa kwani tulitumwa kuchukua dhahabu hivyo pesa ni halali yetu. Tulikuwa na nyuso za furaha wote ukizingatia tutakapofikisha dhahabu nusu yake itakuwa mali yetu vile vile. Kwa kifupi nilijisikia kama niliyezaliwa upya kutokana na kuwa na mamilioni ya pesa.
Baada ya hapo nilianzisha mjadala wa kuifikisha dhahabu Tabora; Sasa inabidi kuisafirisha hii mali mpaka ofisi zetu za Tabora, lakini kutokana na hali ilivyo lazima tusifanye papara maana kwa vyovyote vile polisi watakuwa mbioni kuwasaka watu waliofanya mauaji pale Pamba Hostel ambao ni sisi. Mpaka sasa taarifa za mauaji watakuwa nazo tayari alafu vilevile kuna hawa watu walionifukuzia wakati natoka pale Pamba nao watakuwa kwenye msako wa kunipata na kama wanajua tuko pamoja watakuwa wanatusaka, wale walionifukuzia nahisi watakuwa kundi moja na yule mtu Kikakika aliyepambana naye kule kiwandani kwa Mr Catto.
Kutokana na hali hiyo inabidi tutulie kwa kuendelea kukaa hapa Mwanza angalao kwa kutwa nzima ya kesho ili tuelewe mambo yalivyo. Nilimaliza kueleza na kuwatazama wenzangu kama kuna nyongeza au marekebisho kwenye maelezo yangu.
“Hiyo ni sawa kabisa” aliongea Sonno na kuendelea, ila inatakiwa mali hii ipate hifadhi nzuri tofauti na maeneo yetu tutakayokuwa ili kuepusha upatikanaji wake kirahisi kwa mtu yeyote na kwa kuzingatia usalama kwa ujumla wake. Sonno alimaliza maelezo.
Hilo lisiwape tabu kwani mimi ni mwenyeji hapa, ninazo sehemu ninazoweza kujificha nisionekane, sembuse mzigo kama huu. Niliongea na kuendelea, nitaondoka nao baada ya hapa na utakuwa katika hifadhi nzuri na salama mpaka tutakapouhitaji tayari kwa mambo yetu. Baada ya hapo tuliendelea na mazungumzo ya kawaida mpaka ilipotimia saa tano na nusu nikawaaga huku tukiwa tumekubaliana kesho saa tatu asubuhi Majukano Restaurant.
Nilipotoka hapo niliongoza moja kwa moja mpaka hotelini kwangu, nikaingiza gari maegesho baada ya mlinzi kunifungulia geti. Kilichofuata ni usingizi wa raha mstarehe huku nikiwa na tumaini la utajiri wa maisha nilioutafuta siku nyingi na sasa ninao katika chumba cha nyumba ya kulala wagani.
Ilikuwa saa moja kasoro dakika ishirini wakati nilipotoka kitandani na kuanza kupasha misuli yangu joto kwa mazoezi na ilipofika saa mbili kasorobo nilikuwa nimeisha vaa tayari kuendelea na shughuri za siku hiyo. Niliondoa gari maegesho nikiwa nimechukua briefcase yenye mali ili kwenda kuihifadhi kwa dada yangu mmoja aliyeishi Kilimahewa hapa Mwanza. Ulikuwa ni mwendo wa robo saa kutoka hapa nilipokuwa.
Nilimkuta anashughurika na shughuri za usafi nje ya nyumba na kumsalimia, alinijibu huku akionyesha uso wa furaha kwa kuniona mdogo wake.
“Habari za siku kidogo?” Aliuliza.
“nzuri tu.” Alijibu.
“vipi nilisikia umeenda Tabora au ndio ulienda kununua gari nini?” aliuliza tulipokuwa tumeishaingia ndani na kukaa.
Kwa kifupi huyu dada yangu ni mfanya biashara hapa Mwanza, anamiliki maduka matatu ya nguo ambayo alianzisha baada ya kuhitimu masomo yake ya chuo kikuu.
“ndio nilikuwa Tabora na nimerudi jana usiku na kuhusu gari ni la rafiki yangu” Nilijibu.
“Vipi biashara yako inaendaje?” Nilimuuliza.
Tunashukuru Mungu kwa kuwa tunapata riziki ya kila siku. Alijibu.
“Ok” sasa mimi sina mda mrefu wa kukaa hapa ila naitaji unitunzie huu mzigo mpaka nitakapokuja kwani nategemea kuondoka mda mfupi ujao kwenda Bukoba alafu nitarudi kesho au kesho kutwa kuja kuuchukua. Nilimueleza huku nikimkabidhi ile briefcase
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom