G.MWAKASEGE
Senior Member
- Jun 29, 2007
- 153
- 15
Keep it up Dr Mwakyembe na kamati yako,mungu awabariki muwe na msimamo dhabiti
Mwakyembe Mungu akubariki!
Nakubalina na wote waliosema ya kuwa kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania serikali imeanikwa wazi wazi . Nimesoma ripoti nadhani Mwakyembe amepiga msumari wa mwisho kwa Lowassa pale aliposema ...
Ibara ya 52 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 inatamka wazi kuwa Waziri Mkuu ndiye mwenye madaraka ya juu ya udhibiti, usimamiaji, utekelezaji wa siku hadi siku wa kazi na shughuli za Serikali ya Jamhuri ya Muungano na ndiye Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni. Kamati Teule haikufurahishwa hata kidogo na taarifa hizo zinazomgusa moja kwa moja Mhe. Waziri Mkuu katika kuipendelea Richmond Development Company LLC. Hata hivyo Kamati Teule imetimiza wajibu wake kwa uwazi na ukweli kama ilivyoagizwa na Bunge letu Tukufu. Kwa kuzingatia umuhimu wa nafasi aliyonayo Mhe. Waziri Mkuu katika uendeshaji wa shughuli za Serikali na uongozi wa nchi kwa ujumla, ni wajibu wake yeye mwenyewe kupima uzito wa matokeo ya uchunguzi huu na wajibu wake kikatiba ndani na nje ya Bunge. Vile vile ni wajibu wa Bunge ambalo linathibitisha uteuzi wake kwa mujibu wa Ibara ya 51 inayothibitisha uteuzi wake. Kuangalia ikiwa matokeo ya uchunguzi huu hayajaathiri hadhi na uzito wake ndani ya Bunge.
Kwa maana nyingine Mwakyembe anasema ya kuwa Lowassa anatakiwa AFUKUZWE !
Jamaa wanasema wao ni wapambanaji watapigana hadi "Risasi" ya mwisho. Hawajiuzulu labda "maiti" yake. KWAHERINI
Mmmhhhh!!!! Kazi ipo kweli. Wakikataa si watakuwa fired? Labda kama wana ubia na JK.
Inabidi bunge lianze na Rostam. Nategemea upinzani wapigilie misumari kweli kweli kwa Lowassa, Msabaha, karamangi na Hosea. Lakini wasisahau kuomba Rostam achukuliwe hatua na bunge.
Good indeed Dr.Mwakyembe!Live long.Ripoti zote ziwe zinaanikwa,Bado tunasubiri BUZWAGI NA BOT nao waanike jamvini
ripoti kali mno.
imoto inaunguza pande zote
mie liloniumiza ni jinsi gani watanzania tunavyokuwa wapenda majungu na wapenda domo nje ila tukiitwa tuthibitshe ukweli tunaanza kuuma uuma vidole.
ni aibu kutojiamini na kutokuwa jasiri wa kusema ukweli.
hii imeanza kunipa wasi wasi mkuu kuwa watanzania ni watu dhaifu na ni watu ambao tutachelewa sana kuendelea.
kumbe yanayosemwa amani yetu ni ya woga ni maneno ya kweli.
nnaamini kuna ukweli mwingi haujawekwa wazi kwa hofu.
nnaamini kuna mengi yatakuja juu mwaka huu.
hongera wenye kuitakia mema nchi yetu bila ya kujali itikadi zao iwe kisiasa au kidini cha msingi upuuzi wa kuinyonya tanzania na kuwakandamiza watanzania ukomeshwe
Jamaa wanasema wao ni wapambanaji watapigana hadi "Risasi" ya mwisho. Hawajiuzulu labda "maiti" yake. KWAHERINI