Ripoti Maalum: Utetezi wa Tundu Lissu (MB) mbele ya kamati ya Haki na Maadili ya bunge

Hii document nimeisoma yoote, mpaka nimetapika ngoja nii-save wasije wakaitoa hapa, kwa madai kwamba masuala ya kimahakama hayatakiwi kuwa mitandaoni
 
kwenye hoja nzito kama hizi huwezi kuwaona bongo lala wachumia tumbo wa nape, Ritz na rejao woote wamekimbilia jukwaa la mapenz

Ongeza na Zomba!! Wako chooni wana mwendo mkali leo!!! waguse hapa waone cha moto kama si ban ya milele.
 
Weremaaa upooo???chukua hiyo na bi kiroboto wako...wataanza ooh kukutwa na siri za serikali ni kosa,tutamshitaki Tundu lisu...du jamaa amewaacha midomo wazi watoka povu wote!tunamsubiri bingwa wa kuropoka aje atoe povu!Nape wapi wewe?twakusubiri
 
Hii document nimeisoma yoote, mpaka nimetapika ngoja nii-save wasije wakaitoa hapa, kwa madai kwamba masuala ya kimahakama hayatakiwi kuwa mitandaoni

Umenena mkuu. Mimi fasta niliikopi nikaitengeneza safi kwa ukumbusho. Nataka nitoe hard copy ni bind niweke study room home ili wajukuu zangu kwa kutumia hii wajifunze uadilifu wasije wakawa hovyohovyo kama hawa.
 
Weremaaa upooo???chukua hiyo na bi kiroboto wako...wataanza ooh kukutwa na siri za serikali ni kosa,tutamshitaki Tundu lisu...du jamaa amewaacha midomo wazi watoka povu wote!tunamsubiri bingwa wa kuropoka aje atoe povu!Nape wapi wewe?twakusubiri

Nape leo mbio za msalani na nyumba kubwa zitaongezeka maana kisukari kitapanda na muscles zitafungulia hovyo. Nataka atoe tamko!!!
 
Jamani hapo ndio mwisho? Mbona imeisha ghafla? Kwa kweli hii ripoti inasisimua sana.
 
Hata hao akina Tundu wenyewe wanajua kuwa muda wa kujadili mambo ya urais bado.Wapo strong people ndani ya CDM kuliko hata Tundu Lissu,haimaanishi Lissu ndo zaidi ya wote wakati kaka yako mzaramo anasema haitaji kura za wafanyakazi.

Alikuwa anajua hakuna mgombea anaeweza kumtingisha hata kidogo,hakuna aliyejua Dr. Slaa angeweza kuwa chaguo la wengi so mpaka kufikia June 201,tarajia yanaweza kutokea mabadiliko kalagabaho
.
Kaka ni wish yangu tu. Na ninaamini CHADEMA yote tuko makini so passion yangu kwa Lissu haizuii mwingine kuwa Rais.

Kiufupi usiichukulie serious wish, it is just my wish kaka. Mwaka 2005 nilimpigia kura Mbowe(CHADEMA wote), ilihali sikushiriki sana kwenye kampeni.

Mwaka 2010(DR. SLAA + CHADEMA yote), nilishiriki kwenye kampeni haswa. Kwa yeyote atakayekuja basi na atuongoze tusogee maana sio kwamba tumesimama, tunarudi nyuma zama za kale za mawe. Peace!

Halafu mzaramo sio kaka yangu.
 
kweli huu ushaidi umetulia sana na ninaimani hawawezi kuukataa CCM, maana ndio zao na si mahakama tu bali kila sector wanapeana ulaji.
 
Majaji wote ambao wameorodheshwa hapa wanatakiwa kujiuzuru ili kutunza heshima na uadilifu wa judiciary system yetu, kwani kesi zote walizoamua hawa kuanzia sasa zitaleta zogo. Na pia kuna umuhimu kesi zao walizotolea maamuzi zipitiwe upya, vinginevyo idara hii muhimu itakosa heshima miongoni mwa jamii.

Huwezi kuwa na jaji ambaye alikuwa anapanga maamuzi ya mishetini tauni, Mh Lisu kalifumua jipu vibaya mnoi sasa usaha unataka kuangukia machoni.
 
Hebu fikirieni. Kama dhaifu ameweza kufanya hivi kwa mahakama, je katika usalama wa taifa, jeshi la polisi amefanya mangapi kudhoofisha utawala wa kisheria?

Jiulize teuzi nyingi tata za Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi, Mabalozi, RCs, DCs,nk! Lakini hili la Majaji ni aibu kubwa. Ni kosa la kiufindi la Viongozi wa Bunge,AG na Serikali,ndilo limewavua nguo hawa majaji! Kwasababu kwamba kuna majaji bogus ilikua inajulikana. Serikali ingeweza mjibu Lissu awasilishe ushahidi wake vyombo husika. Aibu hii ingeepukwa!
 
Haya waliokuwa wanapiga kelele TL kwisha semeni sasa tuwasikie,utafikiri hampo JF.
Chezea MWANASHERIA TL wewe!!!!!!!hiki ni kichwa zaidi ya wanasheria wote wa magamba
waliomo mjengoni akiwaemo anayetukana watu yaani eti ndio mkuu wao wa sheria!!!!!!!
 
Aibu kama hii inawezekana kwa nchi ya Tanzania tu. Inabidi tuingie kwenye Guiness World Records kwa kuwa na jaji ambaye hajamaliza kusoma!

Ama kweli Kila kitu Tanzania kinawezekana....ndio maana watoto wa darasa la saba wanafaulu huku hawajui kusoma wala kuandika!
 
Nilipoanza kuisoma nilitaka kuiacha maana niliona mada yenyewe refu sana, kumbe ni fupi mno.

Imejaa data/vielelezo, mantiki na utulivu wa ajabu. Lissu kumbe ni mwenye hekima, alikaa akatulia akachunguza kupitia utafiti, akanena.Wao wakadhani amekurupuka. Zomba yuko wapi jamani?
 
Back
Top Bottom