Kudos Ridhwan! Ridhawan kama matanzania yeyote anahaki ya kutoa mawazo yake hata kama yatakingana na Mwenyekit wake wa Chama. Tusimhukumu Ridhwan kama mtoto wa Kikwete bali kama Mwanachama wa CCM na ikaotekea kuwa Baba yake ni mwenyekiti wa Chama. Sijasoma yote aliyoyasema lakini hayo machache yaliyowekwa hapo nasifu ukomavu wa huyu kijana. Binafsi, naona Ridhwan ameweka wazi kuwa CCM siyo chama cha familia kwamba akisema basi anauharibiua mradi wa familia. Aliyoyasema Ridhwani ndiyo malalamiko ya Wa-Tanzania wengi kushu hatima ya ya CCM na uongozi wa nchi kwa ujumla. Kwamba CCM inahitaji mabadiliko makubwa ni ukweli usiopingika. Hiki si chama kilichokuwa na muelekeo na mtazamo kuhusu maendeleo ya Tanzania na Wa-Tanzania. Nyerere katika ubinaadamu wake alijitahidi kuishi yale aliyoyafundisha lakini si CCM ya leo. Kikubwa kwa Ridhwani ni kuwasaidia vijana wenzake ndani ya CCM ambao ni uzao wa hii CCM mbovu waweze kuelewa kuwa nchi haijengwi, kuendeshwa kwa majungu, unafiki, uongo, fitna, ufisadi, uswahiba, ufadhilina, uwizi, utapeli na sifa nyingine nyingi ambazo ndiyo zimekuwa sura ya CCM ya sasa.
Kuhusu serikali, alilolisema Ridhwani ni ukweli uliowazi hauhitaji miwani kuona. Serikali imejaa watu wasiotenda kazi ama kwa vile hawana uwezo ama kwa vile hawana wakuwafuatilia, ama uwajibikaji mdogo. Kwamba wengi waliomo serikalini wanadumu kwa uongo, majungu, fitina, ufisadi, na ufadhilina si uowong wala kumtukana Rais ama Baba yake. Huu ni ukweli usiofichika. Tumekua tunawapigia kelele wanasiasa lakini adui mkubwa wa Mtanzania ni mtumishi wa umma ambaye yeye haoni kwanini awajibike kwa umma bali waliomteuwa. Kikwete amerithi watendaji wengi wabovu na yeye akaongeza wabovu wake wengine na hao ndiyo wanaomsumbua na kumuangusha. Lakini Kikwete amewapataje watendaji hao wabovu? na ni kwa vipi watendaji wabovu ndiyo wamepenyeza kwenye utumishi wa umma? Jibu liko kwenye utaratibu wa uteuzi ambao hauna uwazi, umetawaliwa na ukabila/udini; matabaka, uwenzetu, usehemu-kusini, kaskazini etc. Rais huteuwa watu kutokana na ushauri wa watendaji wakuu- hawandiyo wanapendekeza na kwa kadri mambo yalivyo wanapendekeza watu wanaowajua lakini lawama inakwenda kwa Rais. Ndiyo maana Ridhwani akitaka Tanzania ibadilike ili hata yeye asijeakatengwa na watawala wajao kwa ajili ya chuki na baba yake, ashinikize tupate katiba mpya na endelevu. Huu ubovu wote utapungua kawa kiasi kikubwa. Salaam zangu kwa Ridhwani ni kuwa wewe na ndugu zako mtapata shida sana Rais akiondoka bila kubadilisha hii katiba. Utaratibu wa Kutesa kwa zamu Tanzania ndiyo falsafa ya watawala wa sasa. wat wata kuhukumu na marafiki na wapiga debe kukukimbia kipindi tuu Rais Kikwete atakapoondoka. Bahati mbaya wewe na jamaa yako mtapata shida sana kwasababu pamoja na mapungufu yake Rais Kikwete ameachia mabadiliko yaliyotingisha misingi na mamlaka ya matajiri na wababe wa kisiasa wa-Tanzania. Hawa hawatawaachieni. Watu waliopoteza uwaziri, ukatibu mkuu na ulaji uliowazi nk watahakikisha jamii ya Kikwete haiendi popote. Lakini katiba mpya endelevu, itawalinda jamii ya Kikwete sasa na vizazi vijavyo na hata jamii za wale walioathirika na mabadiliko aliyoyaruhusu Rais Kikwete. Ridhwani akitaka kugombea urais atahukumiwa kama mtanzania mwingine yeyote na siyo kwa dhambi ya kufikirika ya Baba yake ama Mama yake. Tuliona huko nyuma jinsi Makamba alivyotaka kumkomoa Nnape Mnauye lakini akaokolewa na Rais Kikwete. Bahati mbaya labda huko tuendako kwa katiba hii Ridhwani hata kuwa na mtu wa kumuokoa. Tudai katika mpya endelevu ili maisha ya Ridhwani yasitegemee kuokolewa na mtu ila sheria na taratibu.
Kuhusu serikali, alilolisema Ridhwani ni ukweli uliowazi hauhitaji miwani kuona. Serikali imejaa watu wasiotenda kazi ama kwa vile hawana uwezo ama kwa vile hawana wakuwafuatilia, ama uwajibikaji mdogo. Kwamba wengi waliomo serikalini wanadumu kwa uongo, majungu, fitina, ufisadi, na ufadhilina si uowong wala kumtukana Rais ama Baba yake. Huu ni ukweli usiofichika. Tumekua tunawapigia kelele wanasiasa lakini adui mkubwa wa Mtanzania ni mtumishi wa umma ambaye yeye haoni kwanini awajibike kwa umma bali waliomteuwa. Kikwete amerithi watendaji wengi wabovu na yeye akaongeza wabovu wake wengine na hao ndiyo wanaomsumbua na kumuangusha. Lakini Kikwete amewapataje watendaji hao wabovu? na ni kwa vipi watendaji wabovu ndiyo wamepenyeza kwenye utumishi wa umma? Jibu liko kwenye utaratibu wa uteuzi ambao hauna uwazi, umetawaliwa na ukabila/udini; matabaka, uwenzetu, usehemu-kusini, kaskazini etc. Rais huteuwa watu kutokana na ushauri wa watendaji wakuu- hawandiyo wanapendekeza na kwa kadri mambo yalivyo wanapendekeza watu wanaowajua lakini lawama inakwenda kwa Rais. Ndiyo maana Ridhwani akitaka Tanzania ibadilike ili hata yeye asijeakatengwa na watawala wajao kwa ajili ya chuki na baba yake, ashinikize tupate katiba mpya na endelevu. Huu ubovu wote utapungua kawa kiasi kikubwa. Salaam zangu kwa Ridhwani ni kuwa wewe na ndugu zako mtapata shida sana Rais akiondoka bila kubadilisha hii katiba. Utaratibu wa Kutesa kwa zamu Tanzania ndiyo falsafa ya watawala wa sasa. wat wata kuhukumu na marafiki na wapiga debe kukukimbia kipindi tuu Rais Kikwete atakapoondoka. Bahati mbaya wewe na jamaa yako mtapata shida sana kwasababu pamoja na mapungufu yake Rais Kikwete ameachia mabadiliko yaliyotingisha misingi na mamlaka ya matajiri na wababe wa kisiasa wa-Tanzania. Hawa hawatawaachieni. Watu waliopoteza uwaziri, ukatibu mkuu na ulaji uliowazi nk watahakikisha jamii ya Kikwete haiendi popote. Lakini katiba mpya endelevu, itawalinda jamii ya Kikwete sasa na vizazi vijavyo na hata jamii za wale walioathirika na mabadiliko aliyoyaruhusu Rais Kikwete. Ridhwani akitaka kugombea urais atahukumiwa kama mtanzania mwingine yeyote na siyo kwa dhambi ya kufikirika ya Baba yake ama Mama yake. Tuliona huko nyuma jinsi Makamba alivyotaka kumkomoa Nnape Mnauye lakini akaokolewa na Rais Kikwete. Bahati mbaya labda huko tuendako kwa katiba hii Ridhwani hata kuwa na mtu wa kumuokoa. Tudai katika mpya endelevu ili maisha ya Ridhwani yasitegemee kuokolewa na mtu ila sheria na taratibu.