dazu
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 365
- 76
Ukienda mahakamani, unapocite sheria mbele ya Jaji unatakiwa kutumia kutumia chapter no, revised ed 2002 kwa mfano, The criminal procedure Act, Cap 20 RE 2002, Kwa upande mwingine Wabunge wetu ambao ndio watunzi wa sheria zenyewe hawatambui revised edition ya 2002 badala yake hutumia namba ya sheria kama walivyoitunga wenyewe, mfano, The criminal procedure Act, no. 5 of 1985. Sasa hapa sisi wadau wengine tumfuate nani? Bunge lililotunga au mahakama zinazotafsiri? Naomba mwongozo wenu wana jamvi