mfereji maringo
JF-Expert Member
- Nov 19, 2010
- 1,037
- 251
Danniair Tuwaache wachina wapige kazi, maana watanzania ni kama miungu watu, mtu unamtafuta fundi akufanyie kazi, sasa wewe unageuka mtumwa, yaani kama anakufanyia bure, na kazi yenyewe haina viwango, naomba nitoe mfano niliwahi kumpigia simu fundi selemala aje nyumbani nimpe kazi, alikuja baada ya wiki, kazi ilikuwa ni kutengeneza shelf ya kuweka viatu, nikamwambia nahitaji kubwa, akasema nimpe elfu 30, nikampa,
basi kila nikipiga simu kumuuliza kama iko tayari mara anasema ameenda kuzika, mara naimalizia, hiyo ilikuwa mwezi wa pili, tukasumbuana sana mara nyingi nikifika kiwandani kwake na kumpigia simu kwa pesa zangu mara nyingi, aliponambia ipo tayari nikaenda nilivyoiona yaani ni kituko nikaondoka bila kuaga hadi leo sijaichukua, na fundi hata hajajiuliza kwanini niliamua kuiacha sasa ni mwezi wa saba,
nikaamua kuisamehe sababu niliona nitaendelea kuumia kwa kumpigia simu na kuchoma petrol kwa kitu ambacho sitakipenda, nikaamua kwenda dukani kununua shelf za kichina dukani mbili na kila moja inauzwa elfu 12, mbili kwa elfu 24, kumbuka fundi wa kitanzania nilimlipa elfu 30, na akanisumbua sana hatimae akanitengenezea kituko ambacho ningekiweka ndani ungekuwa ni uchafu.
sasa hawa ndio aina ya wajasiliamali wa kitanzania ambao mtoa mada anataka waachwe peke yao bila ushindani wa kibiashara,
hivi ujiulize kwanini wachina wanapata kazi zote hizo? ukweli ni kuwa sisi u-capitalism wetu ni uchwara kama alivyowahi kuandika Ayoub Rioba katika moja ya makala zake
ndugu zangu itachukua muda sana kufanya biashara ktk kiwango kitakachowaridhisha wateja na kukubalika na kila mtu
yangu hayo tu
basi kila nikipiga simu kumuuliza kama iko tayari mara anasema ameenda kuzika, mara naimalizia, hiyo ilikuwa mwezi wa pili, tukasumbuana sana mara nyingi nikifika kiwandani kwake na kumpigia simu kwa pesa zangu mara nyingi, aliponambia ipo tayari nikaenda nilivyoiona yaani ni kituko nikaondoka bila kuaga hadi leo sijaichukua, na fundi hata hajajiuliza kwanini niliamua kuiacha sasa ni mwezi wa saba,
nikaamua kuisamehe sababu niliona nitaendelea kuumia kwa kumpigia simu na kuchoma petrol kwa kitu ambacho sitakipenda, nikaamua kwenda dukani kununua shelf za kichina dukani mbili na kila moja inauzwa elfu 12, mbili kwa elfu 24, kumbuka fundi wa kitanzania nilimlipa elfu 30, na akanisumbua sana hatimae akanitengenezea kituko ambacho ningekiweka ndani ungekuwa ni uchafu.
sasa hawa ndio aina ya wajasiliamali wa kitanzania ambao mtoa mada anataka waachwe peke yao bila ushindani wa kibiashara,
hivi ujiulize kwanini wachina wanapata kazi zote hizo? ukweli ni kuwa sisi u-capitalism wetu ni uchwara kama alivyowahi kuandika Ayoub Rioba katika moja ya makala zake
ndugu zangu itachukua muda sana kufanya biashara ktk kiwango kitakachowaridhisha wateja na kukubalika na kila mtu
yangu hayo tu
Last edited by a moderator: