Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,814
- 11,991
Fuatilia yanayojiri kwenye Mapokezi ya Rais wa Rwanda Paul Kagame akiwasili nchini Tanzania leo Aprili 27, 2023.
Rais wa Rwanda Paul Kagame amewasili nchini leo na kupokelewa na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Stergomena Lawrence Tax kwenye uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu JK. Nyerere.
Msafara huo umeelekea Ikulu ambapo Rais huyo anatarajia kufanya mazungumzo na Mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan.
UPDATES;
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni wake Rais wa Rwanda, Paul Kagame mara baada ya kuwasili katika Ukumbi wa Kikwete, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 27 Aprili, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mgeni wake Rais wa Rwanda, Paul Kagame mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023.
MAZUNGUMZO
Rais wa Rwanda, Paul Kagame ambaye yupo katika ziara ya siku mbili Nchini Tanzania amewasili Ikulu ya Magogoni, Dar es Salaam na baada ya mapokezi amekutana na mwenyeji wake Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya mazungumzo ya faragha kabla ya kuzungumza na vyombo vya habari.
Rais Samia amesema miongoni mwa Mambo waliyojadili ni kuimarisha Biashara hasa kwa Kuboresha Bandari, Kuzindua mradi wa Rusumo pamoja na Kuendeleza ushirikiano wa vyombo vya Ulinzi na Usalama.
Naye Rais Kagame amemshukuru Rais Samia kwa mapokezi mazuri aliyopata yeye pamoja na ujumbe aliokuja nao, amesisitiza kuendeleza ushirikiano baina ya nchi ya Rwanda na ndio maana kafika Tanzania kwa kazi hiyo.
Amemshukuru pia Rais Samia kwa kujitoa kwake kwenye kushughulikia migogoro ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, amesema amani na utulivu ni hitaji muhimu sana kwa ajili ya maendeleo na umoja wa Afrika.
Rais wa Rwanda Paul Kagame amewasili nchini leo na kupokelewa na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Stergomena Lawrence Tax kwenye uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu JK. Nyerere.
Msafara huo umeelekea Ikulu ambapo Rais huyo anatarajia kufanya mazungumzo na Mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan.
UPDATES;
RAIS SAMIA KUZUNGUMZA NA RAIS KAGAME IKULU YA DAR ES SALAAM
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Rwanda, Paul Kagame mara baada ya kuwasili katika Ukumbi wa Kikwete, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 27 Aprili, 2023.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mgeni wake Rais wa Rwanda, Paul Kagame mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023.
MAZUNGUMZO
Rais wa Rwanda, Paul Kagame ambaye yupo katika ziara ya siku mbili Nchini Tanzania amewasili Ikulu ya Magogoni, Dar es Salaam na baada ya mapokezi amekutana na mwenyeji wake Rais Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya mazungumzo ya faragha kabla ya kuzungumza na vyombo vya habari.
Rais Samia amesema miongoni mwa Mambo waliyojadili ni kuimarisha Biashara hasa kwa Kuboresha Bandari, Kuzindua mradi wa Rusumo pamoja na Kuendeleza ushirikiano wa vyombo vya Ulinzi na Usalama.
Naye Rais Kagame amemshukuru Rais Samia kwa mapokezi mazuri aliyopata yeye pamoja na ujumbe aliokuja nao, amesisitiza kuendeleza ushirikiano baina ya nchi ya Rwanda na ndio maana kafika Tanzania kwa kazi hiyo.
Amemshukuru pia Rais Samia kwa kujitoa kwake kwenye kushughulikia migogoro ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, amesema amani na utulivu ni hitaji muhimu sana kwa ajili ya maendeleo na umoja wa Afrika.