Rais Samia sikia kilio cha wananchi hawa wa jijini Mbeya

Mpap Ndabhit

JF-Expert Member
Jan 15, 2014
237
239
Wananchi wa Sae mpya jijini Mbeya wanataka kubomolewa nyumba zao kwa maonevu makubwa. Awali waziri Lukuvi ALIKUJA Kwa Wananchi na kusema umemtuma kurejesha eneo lao ambalo TARI Kwa miaka zaidi ya miaka 40 walilitwaa bila kulipa fidia.

Clip hiyo IPO wakati waziri anakabidhi mbele ya mkuu wa mkoa, mheshimiwa Tulia, spika wa bunge mwenyekiti wa CCM wote, kamishina wa ardhi alikuwepo. Kwa kauli ya waziri Wananchi wakaanza kujenga,na tayari wameanza kuishi katika makazi hayo.

Wakati huu waziri Silaa naye ana maelekezo mapya ya Rais kwamba Hilo eneo ni la kilimo wananchi wabomoe nyumba zao, bila hata kuwasikiliza, wananchi wanaambiwa ni wavamizi kwenye eneo la kilimo.

Mheshimiwa Rais imebaki kauli yako wewe tu. Ikikupendeza Wananchi wanaomba kuachiwa maeneo hayo ambavyo TARi iliyachukulia hati bila kutoa fidia na Wala hawajawahi kuyatumia.
 
Hao wananchi kama wamevamia eneo lisilo lao wabomolewe tu, pia kama TANESCO na Idara ya maji waliwapeleka huduma watumishi wa hizo taasisi washughulikiwe.

Miji lazima ipangwe na iwe na utaratibu.
 
Hao wananchi kama wamevamia eneo lisilo lao wabomolewe tu, pia kama TANESCO na Idara ya maji waliwapeleka huduma watumishi wa hizo taasisi washughulikiwe...
Wananchi siyo wavamizi, ni maeneo Yao asilia. Wamesubiria kulipwa fidia karibu miaka hamsini Hadi waziri Lukuvi alipoamua kurejesha Kwa Wananchi.. waziri Silaa naye anakuja na kauli tofauti na mtangulizi wake!

Kiufupi kauli za mawaziri wa serikali hii zitakuwa haziaminiki Kwa style hii. Tunataka kauli ya mama Kwa sababu alisema pande mbili kukaa mezani kuumaliza mgogoro lakini Silaa yeye amekaa na TARI bila kusikiliza wananchi.
 
Simu janja ya Zuhuru Yunusi inaweweseka huko magogoni. Ujumbe umemfikia. Tatizo ni nani aliye nyuma ya maeneo hayo. na je, wananchi watasikilizwa?

Hizo hoja zingine ni geresha toto tu.
 
Wananchi wa Sae mpya jijini Mbeya wanataka kubomolewa nyumba zao kwa maonevu makubwa. Awali waziri Lukuvi ALIKUJA Kwa Wananchi na kusema ...
Kuna watu wapumbavu sana nchi hii sijui kwa ujinga au kutaka kuonewa huruma! Wengi wa waliovamia eneo hilo walikuwa hawajazaliwa wakati shirika la Uyole linaanzisha shughuli za utafiti wa mazao na sasa wanadai eti eneo lao la asili. Linakuwaje eneo lako la asili wakati ambapo TARI walipoanza kilimo hapo wazazi wako walikuwa hawajaoana?

Tokeni haraka sana hapo TARI waendelee na shughuli zao!
 
Huruma huruma ni mbaya nyie muwe mfano, wavamizi hamtakiwi
 
Kuna watu wapumbavu sana nchi hii sijui kwa ujinga au kutaka kuonewa huruma! Wengi wa waliovamia eneo hilo walikuwa hawajazaliwa wakati shirika la Uyole linaanzisha shughuli za utafiti wa mazao na sasa wanadai eti eneo lao la asili. Linakuwaje eneo lako la asili wakati ambapo TARI walipoanza kilimo hapo wazazi wako walikuwa hawajaoana?

Tokeni haraka sana hapo TARI waendelee na shughuli zao!
Rais ni wa wote ana uwezo wa kufanya chochote.

Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu ameridhia kufutwa kwa hati za umiliki wa ardhi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Katavi (KUA) na kuwaacha Wananchi wa kaya zaidi ya 400 ambayo inaishi maeneo hayo na kupimiwa ardhi hiyo.

Akiongea mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa ametoa maelekezo kwa Kamishna wa Ardhi nchini kuanzia Jumatatu ya wiki ijayo atoe ilani ya kufanya marekebisho ya daftari ya usajili wa hati ndani ya siku 30
 
Rais ni wa wote ana uwezo wa kufanya chochote.

Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu ameridhia kufutwa kwa hati za umiliki wa ardhi wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Katavi (KUA) na kuwaacha Wananchi wa kaya zaidi ya 400 ambayo inaishi maeneo hayo na kupimiwa ardhi hiyo...
Kwa hiyo mmevamia ili mpate huruma za Samia kama Katavi? Hilo shamba la Uyole lipo kabla hujazaliwa usilinganishe na KUA ya juzi hapa!

Ondokeni kabla hamjapata hasara ya kubomolewa makazi yenu!
 
Wananchi wa Sae mpya jijini Mbeya wanataka kubomolewa nyumba zao kwa maonevu makubwa. Awali waziri Lukuvi ALIKUJA Kwa Wananchi na kusema umemtuma kurejesha eneo lao ambalo TARI Kwa miaka zaidi ya miaka 40 walilitwaa bila kulipa fidia.

Clip hiyo IPO wakati waziri anakabidhi mbele ya mkuu wa mkoa, mheshimiwa Tulia, spika wa bunge mwenyekiti wa CCM wote, kamishina wa ardhi alikuwepo. Kwa kauli ya waziri Wananchi wakaanza kujenga,na tayari wameanza kuishi katika makazi hayo.

Wakati huu waziri Silaa naye ana maelekezo mapya ya Rais kwamba Hilo eneo ni la kilimo wananchi wabomoe nyumba zao, bila hata kuwasikiliza, wananchi wanaambiwa ni wavamizi kwenye eneo la kilimo.

Mheshimiwa Rais imebaki kauli yako wewe tu. Ikikupendeza Wananchi wanaomba kuachiwa maeneo hayo ambavyo TARi iliyachukulia hati bila kutoa fidia na Wala hawajawahi kuyatumia.

View: https://youtu.be/07R4TzuZGWE
 
Kuna watu wapumbavu sana nchi hii sijui kwa ujinga au kutaka kuonewa huruma! Wengi wa waliovamia eneo hilo walikuwa hawajazaliwa wakati shirika la Uyole linaanzisha shughuli za utafiti wa mazao na sasa wanadai eti eneo lao la asili. Linakuwaje eneo lako la asili wakati ambapo TARI walipoanza kilimo hapo wazazi wako walikuwa hawajaoana?

Tokeni haraka sana hapo TARI waendelee na shughuli zao!
Mpumbavu ni wewe unatoa hoja bila kuchunguza mwanzo wa mgogoro na nini kilifanyika mpaka watu wakaanza kujenga, nyumba zote zimejengwa baada ya kurudishiwa eneo mwaka 2021,miaka yote palikuwa pori wakisubiri fidia ambayo haikuwahi kutokea.

View: https://youtu.be/07R4TzuZGWE
 
Kuna watu wapumbavu sana nchi hii sijui kwa ujinga au kutaka kuonewa huruma! Wengi wa waliovamia eneo hilo walikuwa hawajazaliwa wakati shirika la Uyole linaanzisha shughuli za utafiti wa mazao na sasa wanadai eti eneo lao la asili. Linakuwaje eneo lako la asili wakati ambapo TARI walipoanza kilimo hapo wazazi wako walikuwa hawajaoana?

Tokeni haraka sana hapo TARI waendelee na shughuli zao!
Hao TARI ndiyo waondoke, Kilimo cha nini mjini,waende uko Mbarali kwa Wakulima wakafanye shughuli zao!
 
Hao wananchi kama wamevamia eneo lisilo lao wabomolewe tu, pia kama TANESCO na Idara ya maji waliwapeleka huduma watumishi wa hizo taasisi washughulikiwe.

Miji lazima ipangwe na iwe na utaratibu.
Wamejenga kwa mpangilio sana issue ni umiliki tu ndiyo unasumbua
 
Hao TARI ndiyo waondoke, Kilimo cha nini mjini,waende uko Mbarali kwa Wakulima wakafanye shughuli zao!
Na mheshimiwa Jerry Silaa hajawahi kukaa na kuwasikiliza wananchi zaidi ya kuwaita wavamizi na Wakati huohuo kuwataka waende kufanyiwa tathmini ya maeneo Yao Ili kulipwa fidia! Sasa Utamlipaje mtu ambaye umemchafua kwamba ni mvamizi?
 
Hao TARI ndiyo waondoke, Kilimo cha nini mjini,waende uko Mbarali kwa Wakulima wakafanye shughuli zao!
Pumbavu! Kwanza nani alikwambia mjini huwezi kufanya kilimo? Halafu hao wajinga wenzako kwani lazima waishi Mbeya mjini?
 
Na mheshimiwa Jerry Silaa hajawahi kukaa na kuwasikiliza wananchi zaidi ya kuwaita wavamizi na Wakati huohuo kuwataka waende kufanyiwa tathmini ya maeneo Yao Ili kulipwa fidia! Sasa Utamlipaje mtu ambaye umemchafua kwamba ni mvamizi?
Wanajitekenya na kujichekesha wenyewe, hiki ni kitendo kisicho na uweledi wa kazi kabisa.
 
Back
Top Bottom