Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,757
- 10,215
Ndugu zangu Watanzania,
Rais samia Anaendelea kuchanja mbuga ulimwenguni kote ambako Dunia inaendelea kutambua mchango wake katika maendeleo na mchango wake katika kile Secta Katika kuleta matokeo chanya kwenye maisha ya watu.
Kwa mara nyingine tena ametajwa na Forbes Kama miongoni mwa wanawake mia moja wenye nguvu na ushawishi mkubwa sana Duniani ambako kwa sasa ameshika nafsi ya 93.ambapo katika list hiyo ya wanawake 100 yupo pia makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris pamoja na wanawake wengine.
Jina la Rais samia limeendelea kuitikisa na kuiteka Dunia kutokana na mchango wake chanya katika uchumi na hatua za kisera na kisheria ambazo amezichukua na ambazo zimeleta matokeo chanya kwa watanzania tangia alipochukua madaraka ya urais katika mazingira magumu kwa kila kitu.
Tumeona namna Rais wetu alivyoifungua nchi yetu kiuchumi na kidiplomasia na sasa jina la Tanzania linatajwa na kutangazwa mpaka na shirika la ujasusi la Marekani CIA. hiyo yote ni kazi ya Rais samia na mikono ya Rais samia katika kuifinyanga Tanzania na kuiweka katika Ramani ya ulimwengu .
Dunia imetambua kazi mbalimbali zilizofanywa na Rais samia.kazi ya kumrejeshea mtoto wa kike ndoto na matumaini ya kutimiza ndoto ya kupata elimu mpaka chuo kikuu,kazi ya kuwafanya hata watoto wa masikini wawe na uhakika wa kupata elimu bila kikwazo baada ya Rais samia kufuta ada hadi kidato cha sita,kazi ya kujenga zahanati,vituo vya afya, hospitali za wilaya, mikoa kanda na hadi rufaa.
kazi ya kutoa ajira na fursa za ajira kwa maelfu ya vijana,kazi ya kuimarisha demokrasia na uhuru wa watu kuzungumza na kujieleza na kutoa maoni yao,kazi ya kuimarisha haki katika utendaji wa serikali,kazi ya kuboresha maslahi ya watumishi wa umma,kazi ya kuwafanya watanzania wajivunie kuzaliwa Tanzania nakuwa Watanzania,kazi ya kuwafanya watu wawe huru kwenda watakako ndani ya nchi yao ,kazi ya kuifungua nchi yetu, kuchochea Secta Binafsi na biashara kwa kuweka mazingira mazuri na wezeshi kwa atakaye kufanya biashara au kuwekeza nchini,kazi ya kujenga uchumi jumuishi unaogusa maisha ya watu na kukua katika mifuko ya watu.
kazi ya kuleta Tabasamu na kuinua viwango vya furaha kwa watanzania,kazi ya kuiweka serikali mikononi mwa Watanzania , kazi ya kuliheshimisha Taifa letu kimataifa,kazi ya kurejesha imani ya wawekezaji na wafanyabishara wakubwa.
Hayo yote yamefanikiwa kutokana na ushupavu na umadhubuti wa Rais samia.ni uhodari na akili kubwa na maono makubwa na ujasiri mkubwa na wa kipekee wa Rais Samia ndio umefanikisha hayo yote ambapo sasa Dunia imetambua mchango wake na ushawishi wake hapa Duniani miongoni mwa mamilioni ya wanawake.
Rais samia ni kama maji usipoyanywa utayaoga tu
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
0742-676627.
Rais samia Anaendelea kuchanja mbuga ulimwenguni kote ambako Dunia inaendelea kutambua mchango wake katika maendeleo na mchango wake katika kile Secta Katika kuleta matokeo chanya kwenye maisha ya watu.
Kwa mara nyingine tena ametajwa na Forbes Kama miongoni mwa wanawake mia moja wenye nguvu na ushawishi mkubwa sana Duniani ambako kwa sasa ameshika nafsi ya 93.ambapo katika list hiyo ya wanawake 100 yupo pia makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris pamoja na wanawake wengine.
Jina la Rais samia limeendelea kuitikisa na kuiteka Dunia kutokana na mchango wake chanya katika uchumi na hatua za kisera na kisheria ambazo amezichukua na ambazo zimeleta matokeo chanya kwa watanzania tangia alipochukua madaraka ya urais katika mazingira magumu kwa kila kitu.
Tumeona namna Rais wetu alivyoifungua nchi yetu kiuchumi na kidiplomasia na sasa jina la Tanzania linatajwa na kutangazwa mpaka na shirika la ujasusi la Marekani CIA. hiyo yote ni kazi ya Rais samia na mikono ya Rais samia katika kuifinyanga Tanzania na kuiweka katika Ramani ya ulimwengu .
Dunia imetambua kazi mbalimbali zilizofanywa na Rais samia.kazi ya kumrejeshea mtoto wa kike ndoto na matumaini ya kutimiza ndoto ya kupata elimu mpaka chuo kikuu,kazi ya kuwafanya hata watoto wa masikini wawe na uhakika wa kupata elimu bila kikwazo baada ya Rais samia kufuta ada hadi kidato cha sita,kazi ya kujenga zahanati,vituo vya afya, hospitali za wilaya, mikoa kanda na hadi rufaa.
kazi ya kutoa ajira na fursa za ajira kwa maelfu ya vijana,kazi ya kuimarisha demokrasia na uhuru wa watu kuzungumza na kujieleza na kutoa maoni yao,kazi ya kuimarisha haki katika utendaji wa serikali,kazi ya kuboresha maslahi ya watumishi wa umma,kazi ya kuwafanya watanzania wajivunie kuzaliwa Tanzania nakuwa Watanzania,kazi ya kuwafanya watu wawe huru kwenda watakako ndani ya nchi yao ,kazi ya kuifungua nchi yetu, kuchochea Secta Binafsi na biashara kwa kuweka mazingira mazuri na wezeshi kwa atakaye kufanya biashara au kuwekeza nchini,kazi ya kujenga uchumi jumuishi unaogusa maisha ya watu na kukua katika mifuko ya watu.
kazi ya kuleta Tabasamu na kuinua viwango vya furaha kwa watanzania,kazi ya kuiweka serikali mikononi mwa Watanzania , kazi ya kuliheshimisha Taifa letu kimataifa,kazi ya kurejesha imani ya wawekezaji na wafanyabishara wakubwa.
Hayo yote yamefanikiwa kutokana na ushupavu na umadhubuti wa Rais samia.ni uhodari na akili kubwa na maono makubwa na ujasiri mkubwa na wa kipekee wa Rais Samia ndio umefanikisha hayo yote ambapo sasa Dunia imetambua mchango wake na ushawishi wake hapa Duniani miongoni mwa mamilioni ya wanawake.
Rais samia ni kama maji usipoyanywa utayaoga tu
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
0742-676627.