Rais Samia amdhibiti Bashe, mradi wa Kilimo kwa Vijana ni kichaka cha upotevu wa pesa ya Umma

Daima nimemsifu Bashe kwa msimamo wake wa kutokuzuia wakulima kuuza mazao yao mahali popote, iwe ndani ya nchi au nje ya nchi. Kwenye hilo mpaka sasa namwunga mkono.

Lakini taarifa kwamba Serikali imetumia milioni 16 kwa kila ekari 1 kusafisha shamba/kuandaa shamba, ni upotevu wa pesa wa hali ya juu.

Namwomba Rais ateue kamati ndogo ya watu wachache, au amwombe CAG achunguze ili kujua gharama halisia za kuandaa shamba ekari 1, na kisha kuwapata wahusika wote waliohusika kwenye wizi huu wa pesa ya wananchi.

Pamoja na mambo mengine, nnafanya pia shughuli za kilimo. Nina ekari 657. Nazifahamu gharama halisi kwenye kilimo. Japo kuna utofauti mdogo wa gharama unaotegemea mahali shamba lilipo lakini kiuhalisia hakuna utofauti mkubwa katika gharama.

Uandaaji huu wa shamba unahusisha vitu gani hadi kufikia gharama hiyo?

Kwa ujumla wazo la kuiinua na kuiendeleza sekta ya kilimo, hakika ni wazo zuri sana lakini approach ni completely wrong. Na mpango mzima hautafanikiwa. Pesa hii yote inayopelekwa huko itapotea.

Mpango wa kuinua sekta ya kilimo ulistahili kwa kuwasaidia wale ambao tayari wanafanya shughuli za kilimo huko vijijini. Hao tayari kwanza wanakipenda kilimo, wana mipango, wana elimu ya kilimo iliyotokana na wao kufanya kilimo, na hivyo Serikali ilistahili kuwasaidia kwenye maeneo yale ambayo wao wakulima tayari wanayatambua kama kikwazo kwa wao kufanya kilimo kwa ufanisi. Mafanikio ya wakulima hao, yangewavuta wengine wengi kuingia kwenye kilimo.

Huu mpango wa kuwakokota vijana wa mjini kuwapeleka kwenye kilimo kwa ahadi nyingi za kusaidiwa, wengi watajitokeza, lakini baada ya mwaka mmoja, watabakia si zaidi ya 50% tu kwenye kilimo. Baada ya miaka 3, watakaobakia wakifanya kilimo hawatazidi 25%. Na hao watakaobakia kwenye kilimo, watakaofanikiwa kufanya kilimo chenye faida hawatazidi 10%.

Huu mradi, unaweza kuwa sawa na ule wa 'mabilioni ya Kikwete'; ambao uliishia kwenye upotevu wa mabilioni ya pesa.

Kama ule wa kununua na kugawa simu, wa kupelekea watu majiko ya gesi, na mingine mingi. Ifike mahala sasa, serikali ianze kuwahusisha kwa nguvu zaidi walengwa kwa muundo wa kuwa wafanyabiashara.
Ukianzisha kitu ambacho hakina ownership, uzoefu unaonyesha vinakufa hata havijaanza
Tuanzie kwenye yale mamilioni ya JK. Hivi nani alinufaika na nani anaweza kutoa mahesabu yake?
 
hata hao unao waona wakulima walijifunza Kwanza ndio maana hao vijana wa bbt wamepelekwa kusoma Kwanza ndipo waingie shamba
Huwezi kufanya majaribio ya namna hiyo kutoa pesa nyingi kwa watu ambao hawajakiishi kilimo, hata kozi ya mwaka haitoshi kumfanya mtu awe mkulima, kuna zaidi ya hayo ya kusoma, wameshindwa nini kuwapata watu wanaofanya kilimo throughout kufanya majaribio ya BBT..
 
Mr Bams you seem to be smartest Katika kilimo naomba uendelee kuwapa ushauri Serikali kwakuwa ndo mradi/miradi inaenda kutekelezwa. Recently in wrong way.


Mkuu usichoke kutoa njia sahihi za kufikia lengo
 
Then Kuhusu uzoefu I think it doesn't matter

Swala ni commitment mfano Mimi i never did kilimo lakini naamini nikiwezeshwa vizuri siwezi kuharibu Kazi .


Vijana wa Tz wengi tunakwama Katika ujanja ujanja

Pia mtoa Mada upo sahihi.
 
Huwezi kufanya majaribio ya namna hiyo kutoa pesa nyingi kwa watu ambao hawajakiishi kilimo, hata kozi ya mwaka haitoshi kumfanya mtu awe mkulima, kuna zaidi ya hayo ya kusoma, wameshindwa nini kuwapata watu wanaofanya kilimo throughout kufanya majaribio ya BBT..
Washapewa sana hao unao waita wakulima tena wengine mkawaita investors lakin hamna Cha maana walicho fanya ngoja na vijana nao wapewe
 
Daima nimemsifu Bashe kwa msimamo wake wa kutokuzuia wakulima kuuza mazao yao mahali popote, iwe ndani ya nchi au nje ya nchi. Kwenye hilo mpaka sasa namwunga mkono.

Lakini taarifa kwamba Serikali imetumia milioni 16 kwa kila ekari 1 kusafisha shamba/kuandaa shamba, ni upotevu wa pesa wa hali ya juu.

Namwomba Rais ateue kamati ndogo ya watu wachache, au amwombe CAG achunguze ili kujua gharama halisia za kuandaa shamba ekari 1, na kisha kuwapata wahusika wote waliohusika kwenye wizi huu wa pesa ya wananchi.

Pamoja na mambo mengine, nnafanya pia shughuli za kilimo. Nina ekari 657. Nazifahamu gharama halisi kwenye kilimo. Japo kuna utofauti mdogo wa gharama unaotegemea mahali shamba lilipo lakini kiuhalisia hakuna utofauti mkubwa katika gharama.

Uandaaji huu wa shamba unahusisha vitu gani hadi kufikia gharama hiyo?

Kwa ujumla wazo la kuiinua na kuiendeleza sekta ya kilimo, hakika ni wazo zuri sana lakini approach ni completely wrong. Na mpango mzima hautafanikiwa. Pesa hii yote inayopelekwa huko itapotea.

Mpango wa kuinua sekta ya kilimo ulistahili kwa kuwasaidia wale ambao tayari wanafanya shughuli za kilimo huko vijijini. Hao tayari kwanza wanakipenda kilimo, wana mipango, wana elimu ya kilimo iliyotokana na wao kufanya kilimo, na hivyo Serikali ilistahili kuwasaidia kwenye maeneo yale ambayo wao wakulima tayari wanayatambua kama kikwazo kwa wao kufanya kilimo kwa ufanisi. Mafanikio ya wakulima hao, yangewavuta wengine wengi kuingia kwenye kilimo.

Huu mpango wa kuwakokota vijana wa mjini kuwapeleka kwenye kilimo kwa ahadi nyingi za kusaidiwa, wengi watajitokeza, lakini baada ya mwaka mmoja, watabakia si zaidi ya 50% tu kwenye kilimo. Baada ya miaka 3, watakaobakia wakifanya kilimo hawatazidi 25%. Na hao watakaobakia kwenye kilimo, watakaofanikiwa kufanya kilimo chenye faida hawatazidi 10%.

Huu mradi, unaweza kuwa sawa na ule wa 'mabilioni ya Kikwete'; ambao uliishia kwenye upotevu wa mabilioni ya pesa.
Rais Samia mdhibiti Waziri Bashe, mimi nikajua Rais kamdhibiti Bashe, kumbe unaomba adhibitiwe ili mamilioni ya walipa kodi yasitafunwe na wajanja.
 
Kwenye gharama nakubaliana na wewe kwa 100%, ila the rest, Bashe yuko sahihi. Nami ni mkulima mdogo (nna acre 550) hiyo average ya 16m/acre (kama ni hivyo kweli) hapo ni juu sana. Tutajenga Ghorofa nyingi tu makao makuu ya nchi.
Niliona ile doc inasema 17 per hekta yaani 2.5 acres hiyo ni total cost ya barabara, kusafisha, kuchimba mabwawa ya kuhifadhia maji , kujenga canals za umwagiliaji, kupima afya ya udongo, kutandaza barabara, kusambaza umeme, kumpimia na kutoa hati kila plot
 
Washapewa sana hao unao waita wakulima tena wengine mkawaita investors lakin hamna Cha maana walicho fanya ngoja na vijana nao wapewe
Wapi na lini walipewa, toa mifano halisi..serikali haiwezi amua kutupa pesa kwa jambo halina future eti kwa sababu walifanya awali hawakufanikiwa, ni wakulima gani unaowasema walisaidiwa wakashindwa tofauti na hawa wanaolisha taifa siku zote?
 
Wapi na lini walipewa, toa mifano halisi..serikali haiwezi amua kutupa pesa kwa jambo halina future eti kwa sababu walifanya awali hawakufanikiwa, ni wakulima gani unaowasema walisaidiwa wakashindwa tofauti na hawa wanaolisha taifa siku zote?
nenda iringa vijijini kaangalie hao mnao waita wakulima sijui investors walivyo telekeza mashamba na serikali iliwapa kila aina ya infrastructure
 
Hivi utafiti ulifanywa na Nani?
Je,walishirikisha watu sahihi?
Hivi wanakumbuka yaliyotokea VIJIJI vya ujamaa? MADUKA ya Ushirika nk.
 
nenda iringa vijijini kaangalie hao mnao waita wakulima sijui investors walivyo telekeza mashamba na serikali iliwapa kila aina ya infrastructure
Ni zaidi ya ujinga kudhani muuguzi wa watoto atafanya upasuaji wa tezi dume ukapona ilihali dkt. bingwa wa upasuaji alifanya upasuaji na bado hujapona kama unavyodai wewe..wakulima walipewa kila wanachohitaji walime kwa tija wakashindwa..hiki ndio unapaswa kufahamu wala usisumbue akili kufikiri yatakuwepo mafanikio na BBT.
 
fact inapingwa na fact kijana alete evidence ya alicho sema then namimi nimletee evidence kua anadanganya
Kuna evidence zaidi ya figure 16m kwa ekari km alivyosema mleta mada..sawa, unayosema wewe ni fact ni kiasi gani bila hata evidence, taja tu..
 
Mtoa maada una mtindio wa ubongo ni wapi bashe au wizara wamesema wametumia mil 16 kwa heka moja????
Nimekupuuza. Nitaendelea kubadilishana mawazo na watu wenye hekima na uelewa.
 
Asante kwa kunitia moyo. Comments za baadhi ya watu zinakatisha tamaa, maana wanajua tu kukejeli au kutukana, lakini kwa kuwa mpo wenye hekima mnao-appreciate mawazo ya uboreshaji, basi sitakata tamaa.
 
Then Kuhusu uzoefu I think it doesn't matter

Swala ni commitment mfano Mimi i never did kilimo lakini naamini nikiwezeshwa vizuri siwezi kuharibu Kazi .


Vijana wa Tz wengi tunakwama Katika ujanja ujanja

Pia mtoa Mada upo sahihi.
Mimi nimefanya shughuli za kilimo na bado naendelea kufanya shughuli za kilimo. Na kwa ujumla nakipenda kilimo. Nitafanya kazi nyingine zote, lakini pamoja na hizo shughuli nyingine, ni lazima nifanye kilimo.

Lakini ukweli ni kwamba kilimo siyo rahisi kama wengi wanavyofikiria. Kilimo ni science, tena science mchanganyiko. Na bahati mbaya sana hata wanaojiita wataalam au wasomi wa fani ya kilimo, wanafahamu kiasi kidogo sana kuhusu kilimo.

Kilimo kinahitaji utaalam wa udongo, siyo kuchukua tu sample moja na kuipeleka maabara. Unatakiwa kuifahamu vizuri ardhi yako yote. Unahitaji kuwa mtaalam wa hali ya hewa, kuanzia joto, humidity, moisture, n.k,; na kila kimoja kina athari kwa kilimo. Kilimo ni engineering, hiyo ni kuanzia kwenye zana za kulimia, miundombinu ya umwagiliaji mpaka machinery za kusafirishia inputs na mazao yako. Kila kimoja kina nafasi yake kukufanya upate faida au hasara.

Kilimo ni sayansi ya kemia. Unatakiwa ufahamu aina ya mbolea zinazotumika na athari zake baada ya muda mfupi na mrefu.

Hata ukakalishwa darasani kwa mwaka mzima usidhani baada ya hapo utakuwa umekijua kilimo. Utakuwa umepata mwanga. Na utakuwa umeianza safari ya kukifahamu kilimo.

Commitment ni muhimu sana maana ndiyo itakayokupa ari ya kujifunza ili ukifahamu kilimo.
 
Back
Top Bottom