Wavaaa Kobazi Wanasemaje???
.
IMG_20231231_013530.jpg


Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Afadhali sense tu huko. Akirudi tutarajie Tume huru ya Uchaguzi inaanza mchakato, DP World nao wanapigwa chini.
Huko anakwenda kukalia kuti kavu kwa Boss wa Marais wote Duniani.
 
Agenda kuu : Ndoa za jinsia moja , Agizo la Papa litakuwa " Mama hakikisha ndoa za jinsia moja zinashamiri Kwa Kasi sana " . Lasivyo huna urais 2025 . Utasikia , Sawa Baba , nitajitahidi katika Hilo
 
Si amekwenda kupokea maagizo ya namna ya kuendesha nchi. Lazima aitii mamlaka iliyo kuu ktk ulimwengu huu.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Kufuatia mualiko wa kiongozi mkuu wa kanisa katoliki duniani na nchi ya Vatican Papa Francis, Rais Samia Hassan atafanya ziara ya kitaifa tarehe 11 hadi 12 Februari, 2024.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amesema lengo la ziara hii ni kukuza ushirikiano kati ya Tanzania na Vatican.

Tanzania na Vatican tangu mwaka wa 1960 zimekuwa zikishirikiana katika masuala ya elimu, afya, masuala ya amani na kiroho.

"Kanisa katoliki linakadiriwa kumiliki zaidi ya shule za chekechea 240, shule za msingi 147, shule za sekondari 245, vyuo vya ufundi 110, na vyuo vikuu 5," inaeleza taarifa iliyotolewa na wizara huku takribani taasisi za afya 473 zikiendeshwa na kanisa katoliki.

Tofauti za udini hazijawafanya viongozi hawa kushindwa kukaa pamoja na kujadili maslahi ya wananchi na uendelezaji wa ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.

=====

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Baba Mtakatifu Francis amemualika Rais Samia Suluhu Hassan Mjini Vatican kwa mazungumzo rasmi ya siku mbili baina ya viongozi hao.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amewaambia waandishi wa habari mkoani Dar es Salaam leo kuwa mazungumzo hayo yatafanyika Februari 11 na 12 Vatican nchini Italia.

Makamba amesema kufuatia mwaliko huo, Rais Samia ameamua kuambatana na waumini wa kawaida wa Katoliki ambao pia wataonana na Papa Francis katika ziara hiyo ya kihistoria.

"Hii ni heshima kubwa kwa nchi yetu na Rais wetu, kwani mazungumzo hayo na Baba Mtakatifu ni ya heshima kubwa na watu wachache sana ndio watapata fursa ya kuhudhuria mazungumzo hayo," amesema Makamba

===
Kujua safari nyingine za Rais Samia, Soma: Safari/Ziara za nje ya Nchi za Rais Samia Suluhu tangu awe Rais wa Tanzania 19 Machi, 2021
Wakosa hoja hawakawii kusema anaenda kupewa maelekezo na kanisa. Subirini
 
Si amekwenda kupokea maagizo ya namna ya kuendesha nchi. Lazima aitii mamlaka iliyo kuu ktk ulimwengu huu.
Watu hawajui kwamba uhuru wa Tanzania unasimamiwa na UN na huko Papa ndiye msuluhishi neutral wa mikataba ya kimataifa ambao ulitupa uhuru wetu pia
 
Mama anajua kwenye dpw wakatoliki tulimtoa moyoni pale huko hajaalikwa aliomba muda kakubaliwa ni ushauri kutulegeza wakatoliki.awafukuze dpw tu ndo njia pekee
 
Back
Top Bottom