Rais Magufuli: Natamani Malaika ashuke na aifungie mitandao ya kijamii

Vijana wa ufipa walikua wanategemea kupiga perdiem kwenye issues za maandamano, operesheni zisizo na kichwa wala miguu, kama sangara, samaki, ukuta na nyinginezo ambazo mpaka sasa zote zimepigwa pini, yaani ni majanga tu upande wa pili, wanapumulia mashine, hela za viroba hakuna.
Umepatwa na stroke nini mbona unachanganya mada? Tunaongelea mitandao!
Au ni mmoja wao?
 
"Mtu anayekwazwa na meseji za Twitter, Facebook au Whatsapp hapaswi kupewa mamlaka ya kuongoza nchi na kuwa Amiri Jeshi Mkuu"....(Bi. Hilary Clinton, Sept. 26, 2016)
Si nimesikia kuna mpango wa kuanzisha Bustani za free Wi-Fi katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar?
Sasa inakuwaje huku tunaambiwa wanatamani internet isiwepo duniani, huku kwengine tunaambiwa wana mpango wa kuanzisha parks za internet ya bure?
 
maendeleo gani ? Huyu ngosha mshamba sana hutwo tudaladala Twa angani tuwili majigambo kibao, hat mchezaji kama christian Ronaldo anazo, yeye alikimbilia kujenga uwanja chato akasahau hakuna ndege ndo maana ameshindwa kununu madawa Hosp. anakimbilia kununa ndege. chato oyeee!!
Mshara mpaka leo haujaongezwa ndio maajabu hayo.Vijana waliomaliza mwaka jana vyuo wanakutana na mwaka huu taabu tupu.Tuna uwezo wa kutoa $mlns kununua Used, na bado wafanya kazi hawana mazingira mazuri ya kutendea kazi.Watu mpaka sasa wanavinyongo baada tu ya haki yao kisheria kuwekwa pending kwa Nukuu ya hewa hewa wafanyakazi.Wafunge tu hiyo mitandao,kama ni madudu yatajulikana,wamesahau kuwa hiyo mitandao ndio imewapa kura.Wamesahau kuwa palikuwa na TEAM MPJ,vijana hawakulala kwa ajili yao,wamesahau hawa hawa vijana wa mtandao ndio walikuwa wakitia zile point na magroup yoote yale."Masikini akipata matako hulia mbwataa"
 
Nimeshangaa alivyosema.

Uraisi ni MATESO,
Anatamani Uraisi uwe wa miaka miwili!

Au kashasahau aliahidi hatotuangusha!
Inashangaza sana. Km kabana ajira mpaka sasa hivi lazima uwe kweny wakati mgumu.
Cheza uchezavyo ila siyo kweny maisha ya watu lazima cheo ulichonacho ukione kigumu
 
Utendaji wake ni wa hovyo na bado anataka watu tuwe mabubu kwa miaka mitano kuhusu mustakabali wa nchi yetu kwa sababu tu mtakatifu wa Ikulu hapendi na hataki kukosolewa na Watanzania.

Naona Twaweza wanasema 1% ya watanzania ndiyo wanaosupport Maandamano hebu mlioko huko mtuambie.Na kwamba demkrasia imepanda sana.SIjui ni kinyume au?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mtale ni kweli kabisa mitandao hii inauzi sana, tena mno kwa kuwa ndio sehemu maalumu ya waovu [wasiopenda vilivyo sahihi/right] utumia kujifichia [escaping goat].

Marais wa mataifa makubwa Dunia kama Marekani na Ufaransa viongozi wao uwa wanakwazika sana na mitandao,na pale raia anapovuka mpaka kwa matumizi yanayo hatarisha usalama wa Nchi basi vyombo vyao vya ulinzi uwajibika kumtafuta na hata ufikia kuwa adui wa umma [Public Enemy].
Kwetu sisi ujio wa matumizi ya vyombo hivi vya mtandao ndani yake pia pamoja na kuwa na mambo mazuri, kumeibukia ushamba na urimbukeni lakini kibaya sana ni Matusi na Uharakati wa kupinga kila jambo hata yale ambayo tayari yameonyesha kuleta mafanikio kwa umma.

Ili la Matusi na uharakati usio na mwelekeo wa kujenga bali ule wenye mwerekeo wa ''BOMOA BOMOA EEEhh BOMOA MAMA TUTAJENGA KESHO'' ...unapaswa kuangaliwa kwa jicho pana mno tena mno.

Ni kwa style hii ya mitandao Arab Spring and Social Media imeacha MAJANGA na yanaendelea kuwa Majanga ya Mataifa ya Tunisia, Syria,Libya,Yemen, Egypt, Bahrain,Algeria, Iraq, Jordan, Kuwait, Morocco, Oman na kwa udhibiti wa Saudia Arabia kwenye mitandao wao wakasalimika.

Kwenye Mitandao kwa Udhibiti mwema Taifa litafaidika sana, lakini kukikosekana Usidhibiti makini tena ule wenye weredi haswa tutakaribisha majanga.Mtale Inakela lakini ndio hivyo Mzee Mwinyi alishema Utandawazi huu ni sawa na kufungua Dirisha la nyumba yako upate hewa Safi lakini kwa fursa hiyo Nzii nao Watatumia mwanya huo kuingia.

Sasa kama Taifa tukizinduka kuwa kuna Nzi wanatumia mwanya huo kuingia basi lazima tuwe na majibu ya kero za Nzii.Na majibu ya kero za utatuzi wa kuzuia Nzii ziko nyingi chache kuzitaja ni kama ifuatavyo.
A: Kuacha Nzi wakaingia Dirishani.
1: Tukatumia Taa Maalumu kuwavuta na kila wakigusa wanakutana na kifo cha mende
2: Kupaka Mafuta ya Taa au Chumvi ndani ili wakose pa kukanyaga na hatimae kujikuta hawana makazi.
3: Kutumia Doom au X -Spray kuwamaliza

B: Kuzuia Nzi Kabla hawajaingia Dirishani
1: Tujenga wavu dirishani wasiingie kabisa ndani.
2: Tuweke Machine ya kukamata hao Nzi pale Dirishani.

Tunaitaji huduma ya Mitandao, lakini iwe mfano wa hewa safi kutokana na kufunguliwa kwa dirisha la nyumba.Hewa hiyo ije na harufu nzuri ya maua na miti yenye mvumo wa sauti za ndege wanaoimba uko nje lakini si Nzi na Wadudu waharibifu.
 
Kusoana ni kuzuri, tatizo ni pale fisadi au mashabiki/wapambe wake wanapo mkosoa mtu ambae sio fisadi. Ni kama vile mwizi anamkosoa mwenye nyumba eti kwa nini usiku anafunga milango ya nyumba yake.
 
''Natamani malaika ashuke azime mitandao ya kijamii, irudi baada ya mwaka 1 ikute hatua kubwa za kimaendeleo tulizopiga''. Ni kauli ya Rais Magufuli.

Ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa ndege mbili aina ya Bombadier Q400, ambazo zimewasili nchini rasmi kutoka nchini Canada.

Amesema kwenye mitandao ya kijamii watu wengi wanaandika bila kuwa na taarifa sahihi. Amesema, "No research no right to speak"
Tanzania: Earthquake survivors face task of rebuilding
 
Malaika KAMWE hawawezi kushuka kwa tamaa ya mtu asiyejali sheria za nchi na uhuru wa Watanzania kuzungumza na kujadili mambo mbali mbali ya mustakabali wa nchi yao hata kama hawajafanya research yoyote ile. Kujua nini kinachoendelea kwenye nchi yetu haikuhitaji kufanya research yoyote ile tunaona hali halisi kila siku iendayo kwa Mungu na kusikia manung'uniko ya Watanzania wenzetu kuhusu hali ya nchi yetu.

Jaji Warioba hakufanya research yoyote ile lakini naye kahitimisha kwamba nchi inaenda mrama.
IF YOU DO NOT KNOW WHERE YOU ARE GOING ANY ROAD WILL TAKE YOU THERE (TUSIPOKUWA NA VIPAUMBELE NI TATIZO) TUKATUMIA BILA KUFUATA BAJETI YA BUNGE HAPO NI TATIZO KUBWA HII MITANDAO INATUSAIDIA SANA KUPASHANA HATA WAO KUMBE WANASOMA MAWAZO YETU JAPO YANA WAKELA TUSIACHE KUSEMA HII INCHI NI YETU SOTE TUSIOGOPE KUSEMA
 
Hawa Twaweza ni wazushi tu wanawekwa MUJINI na ruzuku toka MACCM ili kufanya tafiti zao za kipumba.vu ambazo hazina mantiki yoyote na haziingii akilini.

Naona Twaweza wanasema 1% ya watanzania ndiyo wanaosupport Maandamano hebu mlioko huko mtuambie.Na kwamba demkrasia imepanda sana.SIjui ni kinyume au?
 
Back
Top Bottom