tity
Member
- Oct 16, 2015
- 44
- 15
Kwa wale wana CCM mtakwazika sana, ila kwa watu wengi wenye uelewa mtaungana na mimi mimi binafsi sio mwanachama wa chama chochote ila ni mfwasi mkubwa wamabadiliko.
Ninasema na nitaendelea kusimamia kauli yangu,tawala huu mpya katika miaka 5 ijayo hautoweza kufikia hata 35% ya matarajio ya walio wengi sabau ni nyingi sana,leo ntatoa chache tu.
1. Rais atahitaji kutumia mda mwingi kuijua serikali kuliko kushugulikia changamoto za wananchi ndugu zangu tusidanganyane, mimi naamini kwa level aliofikia rais kama mtumishi wa serikali kwa ngazi ya uwaziri haiwezi kutumika kama kigezo kwamba anaijua serikali vizuri kwa kuwa kafanya kazi ya uwaziri kwa miaka zaidi ya 15.
Nani alishawahi msikia rais huyu akizungumzia ufisadi, nani alimsikia akizunguzia dawa za kulevya,nani alimsikia akizungumzia mapato ya taifa, nani alimsikia akizungumzia ujangili unajua ni kwanini?
Huwezi kuongelea jambo usilolijua,ni kwanini hakujua? ni kwasababu alijikita zaidi katika mambo yaliyokuwa yana husu wizara yake tu changamoto nyingi alizopuuza kuzifwatilia akiwa waziri leo anaenda kuzikuta ikulu ataanzia wapi kuzishughulikia?
2. Kiongozi bora ni yule anae heshimika na si kuogopwa...kwa nchi kama tanzania inayokabiliwa na changamoto lukuki,inahitaji mshikamano mkubwa wa watendaji na wananchi,je rais anauwezo wa kuwaunganisha watanzania kama baba anavyowaweka pamoja watoto wake?busara na hekima nyingi zinatakiwa kulifanyikisha hio...mpaka sasa kwa kiongozi huyu mimi uwezo huo sijauona..
3. Mfumo uliopo una nguvu sana kumliko...ndugu zangu,nadhani wengi mn?liona hilo,kitendo cha kumteua mwanasheria yule yule,kufanya vikao na makatibu wale wale kutoka katika serikali iliyojaa kasoro nyingi ni kiashirio kikubwa kuwa huyu mzee hakujipanga...mtu aliejipanga lazima ajiandae vya kutosha ikiwa ni pamoja na kujua ni yupi utafanya nae kazi..sintashangaa kuona wakuu wa mikoa na wakuu wilaya wengi wakibaki wale wale...
4. Kukosa nguvu kwenye chama chake...hakuwai kuwa hata kiongozi kwenye chama katika ngazi yoyote...chama kwa sasa kinaendeshwa na kikundi kidogo cha watu tena kwa maslahi binafsi,hilo kila mtu ameliona...kukosa kauli kwenye chama kutamfanya ashindwe kutekeleza yale mengi anayoamini haswa kwenye kuwashugulikia mafisadi ufisadi unaofanyika tanzania sio wa mtu mmoja mmoja,ni wa kimfumo (its a chain).
5. Sakata la Zanzibar.
Ninasema na nitaendelea kusimamia kauli yangu,tawala huu mpya katika miaka 5 ijayo hautoweza kufikia hata 35% ya matarajio ya walio wengi sabau ni nyingi sana,leo ntatoa chache tu.
1. Rais atahitaji kutumia mda mwingi kuijua serikali kuliko kushugulikia changamoto za wananchi ndugu zangu tusidanganyane, mimi naamini kwa level aliofikia rais kama mtumishi wa serikali kwa ngazi ya uwaziri haiwezi kutumika kama kigezo kwamba anaijua serikali vizuri kwa kuwa kafanya kazi ya uwaziri kwa miaka zaidi ya 15.
Nani alishawahi msikia rais huyu akizungumzia ufisadi, nani alimsikia akizunguzia dawa za kulevya,nani alimsikia akizungumzia mapato ya taifa, nani alimsikia akizungumzia ujangili unajua ni kwanini?
Huwezi kuongelea jambo usilolijua,ni kwanini hakujua? ni kwasababu alijikita zaidi katika mambo yaliyokuwa yana husu wizara yake tu changamoto nyingi alizopuuza kuzifwatilia akiwa waziri leo anaenda kuzikuta ikulu ataanzia wapi kuzishughulikia?
2. Kiongozi bora ni yule anae heshimika na si kuogopwa...kwa nchi kama tanzania inayokabiliwa na changamoto lukuki,inahitaji mshikamano mkubwa wa watendaji na wananchi,je rais anauwezo wa kuwaunganisha watanzania kama baba anavyowaweka pamoja watoto wake?busara na hekima nyingi zinatakiwa kulifanyikisha hio...mpaka sasa kwa kiongozi huyu mimi uwezo huo sijauona..
3. Mfumo uliopo una nguvu sana kumliko...ndugu zangu,nadhani wengi mn?liona hilo,kitendo cha kumteua mwanasheria yule yule,kufanya vikao na makatibu wale wale kutoka katika serikali iliyojaa kasoro nyingi ni kiashirio kikubwa kuwa huyu mzee hakujipanga...mtu aliejipanga lazima ajiandae vya kutosha ikiwa ni pamoja na kujua ni yupi utafanya nae kazi..sintashangaa kuona wakuu wa mikoa na wakuu wilaya wengi wakibaki wale wale...
4. Kukosa nguvu kwenye chama chake...hakuwai kuwa hata kiongozi kwenye chama katika ngazi yoyote...chama kwa sasa kinaendeshwa na kikundi kidogo cha watu tena kwa maslahi binafsi,hilo kila mtu ameliona...kukosa kauli kwenye chama kutamfanya ashindwe kutekeleza yale mengi anayoamini haswa kwenye kuwashugulikia mafisadi ufisadi unaofanyika tanzania sio wa mtu mmoja mmoja,ni wa kimfumo (its a chain).
5. Sakata la Zanzibar.
Nitatoa mifano michache,
1.Hali ya uchumi wa Tanzania kwa sasa ni mbovu sana kwa serikali na kwa mwananchi moja ,takwimu hazi akisi uhalisia kama alivyo sema magufuli kwenye hotuba yake. sababu ni moja kuwa mapato mengi yanatokana na makampuni au viwanda au sekta amabazo hazijumulishi idadi kubwa ya watanza ktk ajira,ameachiwa nchi ikiwa kwenye hali mbaya tofauti kikwete alivyo achiwa na Mkapa angalau uchumi ulikuwa vizuri kiasi.sasa hivi serikali ina madeni likuki ndani na Nje nakisi ya budgeti ni kubwa sana means production ni kidogo sana-na kwa hali hiyo inabidi kinachopatikana ktk pato la Taifa kilipe hayo madeni ili interest isiongozeka kwa kufanya hivyo government expenditure kwenye development projects inapungua vilivyo mfano nenda halmashauri yoyote uulize fedha za CDG,CDF,LDF,DIDF,RWSSP,CHF,SEDP,HSBF na ROAD FUND kama zinafika kwa wakati na kiwango kinachotakiwa.kuziba hayo mabonde ( ku stablize) si kazi ya mwaka 1 au 2 kama wengi wavyo fikiri.
2.Mfumo wa kisiasa wa chama chake kumbuka Magufli ni rais lakini kwenye chama hana nguvu yoyote mpaka sasa na teuzi zate zimefanyika kichama si mtu(nraisi ) kama wengi walivyo fikiria sababu yeye yupo pale kwa niaba ya chama na sio chama kwa niaba ya yeye-hii inatokana na mfumo wa kisiasa wa nchi za kiafrika.ninacho manisha ni kuwa performance ya hapo juu inategemeana sana na teuzi za kisisa sote tumisha ona teuzi ambazo zimisha fanyika zime base kichama zaidi.ili aende vizuri inabidi awe na kofia zote 2 ingawa si guarantee maana yeye hakujiweka mwenyewe kuwa rais tofauti na watangulizi wake kama mwinyi, mkapa alikuwa na back up ya Mwl.Nyerere na Kiwete alikuwa na back-up ya wanachama,ni wazi magufuli hana back-up ya wanachama bali ana ya mkapa ambaye hana nguvu kama aliyokuwa nayo nyerere kwenye chama na back-up ya kiwete kama mwenyekiti wa chama ambaye ana nguvu ndani ya CCM kwa 100% hii inaonyesha itakuwa vigumu kwa magufuli kuwa against kikwete kwa miaka hi mpaka 2017.toka 2017-2020 ni miaka 3 uatawezaje kutengeneza base nzuri ya uchumi kwa miaka 3 au 2.5
3.Kuna ule msemo unao sema I am part of them,kutokana na mfumo wa serikali chini ya chama cha CCM kodi zote anazo sema magufuli kuwa ni za hovyo zimepitishwa na wabunge wa CCM na kweli ilibidi wapitishe ili serikali ipate kodi kwa sababu vyanzo vyote vikubwa ambavyo vingetoa kodi kubwa lakini ndo havito kodi vingi vinamilikiwa au wanamiliki % kubwa ya hisa ia wana CCM hao hao na wengine ni viongozi humo humo CCM-rejea utajiri wa Rostam Aziz huyu in moja kati ya 100 waliopo ndani ya CCM.hili lingewezekana kama mfumo wa hapo na 2 ungekuwa tofauti
4.Kodi zinazokwepa kupitia makampuni makubwa ya humu ndani na mult-national company hapa nchini in ubwa mara 200 kuliko hayo matumizi ya kusafiri.na bado hapo kwenye mult national company viongozi wa CCM wanamiliki hisa kubwa sana.
Utawala wa magufuli utakuwa mgumu sana sababu maamuzi yote makubwa yapo mikoni mwa watu-utaweza kudhibiti hivi vidogo kwa ajili ya kupata sympathy ya watu lakini ninaamini hata yeye moyoni mwake anajua wenye power ni watu wengine.
Mh Rais John Pombe Magufuli, salaam zikufikiee...
Kwanza Nikupongeze kwa hotuba nzito uliyoitoa jana wakati wa ufunguzi wa bunge letu la 11.
Mh Rais pamoja na kwamba ulizungumza kero zote zinazoikumba nchi hii bila unafki, na zingine nyingi ambazo ni matatizo ambayo kwa makusudi yalifanywa na mtangulizi wako, nakupongeza kwa ujasiri huo mkubwaa.
Awali ya yote Mh Rais Napenda pia kukukosoa kidogo kwa jambo ulilolipuuza jana, pale ambapo wabunge wa UKAWA walipo paza sauti yao kupinga kitendo cha Shein kuingia bungeni kama Rais wa Zanzibar huku ukitambua kuwa mgogoro wa Zanzibar unahitaji busara zako.
Mh Rais wabunge wa UKAWA hawakuigomea hotuba yako, bali hawakutaka kumtambua Shein kama rais wa Zanzibar.
Unaweza kupuuza kitendo walichokifanya jana, lakini kumbuka kuwa hili linaweza kukufanya ushindwe kutimiza yale ambayo umehaidi kuwatimizia watanzania kipindi hiki cha miaka 5.
Mh Rais tukiachana na hayo ya UKAWA naomba niendelee na mada yangu.
Mh Rais naona unamoyo wa dhati wa kuwatumikia watanzania, naiona dhati hiyo toka sakafu ya moyo wako. Lakini Mh Rais pamoja na dhati hiyo bado naona ukinzani mzito unaopinga dhati yako, hapa ndipo mtihani ulipo.
Mh Rais kwa miaka hii mitano najua itakuwa migumu kwako, hasa katika maeneo haya matatu tena kwa mfuatano.
1. Upinzani toka CCM
2. Upinzani toka mataifa makubwa
3. Sakata la Zanzibar
1. UPINZANI TOKA CCM
Mh Rais unaweza kufikiri kuwa kwa sasa adui zako wakubwa ni UKAWA lakini nataka nikufahamishe kuwa safari hii adui yako atakuwa chama chako.
Mh Rais unajua mfumo unaoiendesha chama chako, unajua watu wa chama chako, hao ndio watakuwa kizingiti kwako.
Mh Rais kuubadili mfumo unaoiongoza CCM ambao sisi tunajua ni mlezi wa serikali kuna hatari kubwa katika hili.
Matatizo yote uliyo yasema jana yanayo wakumba watanzania, yote husababishwa na hao wakubwa zako katika chama na waliokutanguliaa.
Hivyo unapaswa kujua kuwa hao ndio maadui wakubwa kwako.
Mh Rais maadui hao ndio walio kumbatia matajiri wakubwa, wakwepaji kodi na mataifa makubwa ambao ni wanyonyaji wa nchi hii.
Watu hao unahitaji nguvu ya ziada kupambana nao.
2. UPINZANI TOKA MATAIFA MAKUBWA.
Mh Rais nchi hizi ndogo hususani za Afrika ni nchi ambazo kwa muda mrefu tumekuwa wanyonywaji wa muda mrefu wa mataifa Makubwa duniani.
Mataifa haya ndio yanayoiweka CCM madarakani mpaka sasa. Mataifa haya yenye nguvu za kifedha, jeshi na ushawishi duniani ndio yameifikisha nchi yetu ilipo sasa.
Mh Rais unapokwenda kupambana na mikataba mibovu, jua unapambana na mataifa hayo, Unapokwenda kupambana kuinyanyua shillingi yetu, kufufua viwanda jua unapambana na mataifa hayo.
3. SAKATA LA ZANZIBAR
Mh Rais nafikiri unajua vema mgogoro unaoendelea zanzibar.
Mgogoro huu unahitaji busara kubwa kuitatua, lakini kama utatumia ubabe wa chama chako basi hili linaweza kukukwamisha katika safari yako ya miaka 5.
Hapa ndipo maraifa makubwa yanasubiri ufanye nini, kuwa makini katika hili.
NINI KIFANYIKEE.....
Mh Rais mtihani ulio nao wakuitengeneza Tanzania uliyotuhaidi unahitaji kugusa sehemu hizi
1. Ondoa Mamluki ndani ya serikali yako.
Najua mamluki ktk chama chako ambao wengi wamefanikisha ushindi wako.
Hawa watu hupaswi kuwaaangalia usoni hata kidogo, hawa ni kuwaondoa ktk utendaji wa chama na serikali yako.
2. Usalama wa taifa, Jeshi la police na JWTZ
Mh Rais hapo ndipo nchi ilipo. Kwanza inabidi uwatambuee maofisa wa majeshi hayo.
Najua kuna mamluki wengi ambao wamepenyezwa kwa makusudi kukukwamisha katika utendaji wako. Kuwaondoa hao inahitaji ufundi wa hali ya juu.
Unapaswa kuitengeneza team katika majeshi hayo kufanya nao kazi, team ya uaminifu kweli.
3. JENGA USHIRIKIANO NA UKAWA
Mh Rais najua unaweza fikiri Ukawa ndio maadui zako wakubwa.
Najua pia wanaweza kukujengea chuki juu ya watu hawa, ili wafanye yao, kuwa makini katika hili. Ukijenga uadui na kundi hili, mwisho wa siku utajikuta mwenyewe, utashindwa kufanya kazi.
Mh Rais unahitaji timu aminifu ya ushauri juu ya masuala ya uendeshaji wa nchi, timu nzuri itafunga magoli kila siku inapocheza na timu nyingine.
Mh Rais take care.
Asante.
Maisha bora kwa kila mtu ni sera ya CCM, ambayo kiukweli ni nzuri sana na inaleta matumaini kama ikitekelezwa, ila utelezaji wa sera hii unapambana na vikwazo vingi ambavyo sijui rais John Pombe Magufuli ataviweza, maana mtangulizi wake Jakaya Mrisho Kikwete vilimshinda kabisa, vikwazo vikuu vya utekelezaji wa sera hii ya maisha bora kwa kila mtu baadhi ni vifuatavyo:-
- Watumishi wa serikali, hasa wa halmashauri siyo waaminifu (yaani ni one hundred percent corrupt), kwa sababu kutekeleza sera hii serikali kuu inatuma hela nyingi sana kwenye halimashauri za wilaya ambako watu ndiko walipo ili kutekeleleza miradi mbali ya maendeleo. Kule pesa inakutana na watumishi ambao ni corrupt, wanashambulia hela zote za miradi kwa kujenga mabangaloo, wananunua posh cars kwa hiyo miradi ya maendeleo inakwama automatically na sera ya maisha bora kwa kila mtu nayoinakwama.
- Watumishi niliowataja hapo juu kwa mujibu wa utaratibu wanasimamiwa na madiwani waliopo katika halimashauri hizo, sasa madiwani hao uwezo wa kuwasimamia vizuri hawana kwa sababu elimu zao wengine ni duni sana, hasa madiwani wa viti maalumu. Katika halmashauri nyingi madiwani hawa ni mizigo tu, kwa hiyo watumishi ambao sio waaminifu wanautumia vizuri mwanya huu kuikwamisha sera ya maisha bora kwa kila mtu, kwa kuwalambisha hela kidogo madiwani hawa halafu wenyewe wanakwapua nyingi.
- Serikali yenyewe kwa ujumla ni dhaifu, inashindwa kabisa kuwachukulia hatua wabadhirifu hawa inaishia tu kuwahamisha toka halmashauri moja kwenda ingine.
Mh. John Pombe Magufuli akiweza kuyadhibiti hayo hapo juu, basi maisha bora kwa kila mtu inawezekana.
- Idara ya usalama wa taifa(TISS) nayo imezorota sana, kule wanawaona kabisa watumishi ambao siyo waaminifu wanavyofanya wananunua magari mawili mawili na kujenga nyumba kali ndani ya mwaka mmoja tu wa kuajiriwa lakini hawapeleki habari kunakohusika, wanashughulika na mambo yasiyokuwa na tija kama kufuatilia mikutano ya CHADEMA.