Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,960
- 32,344
Wanabodi.
Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.
Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.
Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.
Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.
Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.
JF Daima
Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.
Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.
Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.
Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.
Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.
JF Daima