Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

Ritz

JF-Expert Member
Jan 1, 2011
46,960
32,344
Wanabodi.

Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.

Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.

Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.

Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.

Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.

JF Daima
 
Ritz,

Kwa hayo hayo ndio Kikwete hapendeki. Ukitazama wengi wa wanaoleta chuki na kejeli utakuta wengi ni wale wale waliozibiwa mianya ya wizi kwa mara ya kwanza toka hii nchi ipate Uhuru katika kipindi hiki cha Kikwete.

Baada ya muda mfupi, Kikwete anaanza kushughulikia fedha zilizowekwa nje ya nchi na hawa wizi wa mali za umma. Ni kazi ngumu sana, lakini ipo njiani inakuja, tutaona chuki zikizidi. Ukitazama kijuu juu tu hata bila ya uchunguzi wa kina utakuta wote wenye chuki ni wale wale 83%. Hao ndio "wasomi" bila kuelimika, hao ndio walioifikisha nchi ilipofika na hao ndio wezi wakubwa.

Tunamtakia kila la heri Kikwete kwa hii kazi ngumu aifanyayo sasa, na matokeo tunayaona. Na hapo ndiyo eti "dhaifu".

Subiri uone majibu sifuri sasa hivi.
 
Ritz,

Kwa hayo hayo ndio Kikwete hapendeki. Ukitazama wengi wa wanaoleta chuki na kejeli utakuta wengi ni wale wale waliozibiwa mianya ya wizi kwa mara ya kwanza toka hii nchi ipate Uhuru katika kipindi hiki cha Kikwete.

Baada ya muda mfupi, Kikwete anaanza kushughulikia fedha zilizowekwa nje ya nchi na hawa wizi wa mali za umma. Ni kazi ngumu sana, lakini ipo njiani inakuja, tutaona chuki zikizidi. Ukitazama kijuu juu tu hata bila ya uchunguzi wa kina utakuta wote wenye chuki ni wale wale 83%. Hao ndio "wasomi" bila kuelimika, hao ndio walioifikisha nchi ilipofika na hao ndio wezi wakubwa.

Tunamtakia kila la heri Kikwete kwa hii kazi ngumu aifanyayo sasa, na matokeo tunayaona. Na hapo ndiyo eti "dhaifu".

Subiri uone majibu sifuri sasa hivi.

zomba.

Ni kweli kabisa watu wanamchukia Kikwete sababu kaziba mianya ya rushwa na kulindana...hata hoja inayosimamiwa na Chadema ya Ufisadi haina nguvu tena wanaofanya hivyo wameshulikiwa na ushahidi upo katika mahakama mbali mbali nchini.
 
Last edited by a moderator:
zomba.

Ni kweli kabisa watu wanamchukia Kikwete sababu kaziba mianya ya rushwa na kulindana...hata hoja inayosimamiwa na Chadema ya Ufisadi haina nguvu tena wanaofanya hivyo wameshulikiwa na ushahidi upo katika mahakama mbali mbali nchini.

Kuna mwandishi aliandika kitabu ambacho kinaelezea habari kuwa ni 'kinyumbe cha mambo'. Hakika uliyoyaandika hapa ni kinyume cha mambo!
 
Ndugu mtoa mada nadhani hujafanya reseach ya kutisha unachokiongelea.

Kila siku unasikia watu wanashindwa kusafirisha mazao sababu ya ubovu wa miundo mbinu ya barabara, hata hao wabunge wanaliliamikia hili japo wanakosa uzalendo na wanaogopa kwenda kinyume na maelekezo ya wakuu wao.
 
zomba.

Ni kweli kabisa watu wanamchukia Kikwete sababu kaziba mianya ya rushwa na kulindana...hata hoja inayosimamiwa na Chadema ya Ufisadi haina nguvu tena wanaofanya hivyo wameshulikiwa na ushahidi upo katika mahakama mbali mbali nchini.
Hawa wakulima wadogo (peasants) kule Ruvuma , Njombe, Mbeya, Rukwa, Iringa............ambao hawapati pembejeo za kilimo nao wanamchukia kwa kuwa wamezibiwa mianya ya rushwa?
 
Sikutegemea mchabuzi kama wewe una hoja dhaifu za kuwaelzea chekechea umesahau kuwa hapa ni jamii forum. Tunashukuru kutambua upeo finyu wa fikra yako.Ila punguza kujipendekeza na kuwa mchumia tumbo. Watanzania wa sasa ni waelewa na wanazitambua ghiriba na propanganda za akina TAMBWE HIZA.

Nchi hii ina matatizo mengi na hasa kwa wananchi walio wengi, kwasas iefikia kuwa nchi iliyo na upungufu wa chakula , wakati ina ardhi kubwa yenye rutuba, mabonde mengi na nguvu kazi inayotosha na asili ni kuchapa kazi za kilimo.

Sasa kama wananchi hawasaidiwi kwa hili bali bla bla watakuwa na imani naye kivipi? Namna anavyochukua hatua kuhusu kufufua ushurika ni vichekesho tupu. Nakumbuka wakati anatoa mafedha ya kikwete wachambuzi wengi tusihi fedha hizo zitumike kufufua ushirka na kilimo kwa ujumla ndo hapo impact ingeoneka. Leo hii ukiuliza fedha hizo ni blabla tu na nadharia kubwa.

Kumsifia JK ni uendewazimu. Alingia madarakani kukiwa na tatizo la umeme, leo miak takribani miaka ifikayo 8 bado blabla. Kama angekuwa si dhaifu ingechukua miaka miwili tu lazima tungeona mageuzi katika sekta hii. Tuna tatizo la kupanda bei ya mafuta , lakini maelezo yanatoka bado blabla na hakuna hatua za dhati kuonyesha wanachukua hatua gani.

Hata hao EWURA ni blbabla tu wameshikiliwa na matajiri wa mafuta, tabu kabisa. Uje sekta ya usafirishaji kama ATCL, TRL jamani tunamzimu gani wa kijinga? Halafu unakuja na hoja za chekechea!inaonyesha shule ulikuwa unabebwa sana kwa degree za chupi wewe
 
Sikuwai kufikiri kama ritz una uwezo wa kumtete JK.

Kweli nime amini inabidi nichanganyikiwe kwanza ndio nikubali huo utetezi wako!

Hivi lowasa amefikishwa mahakama gani?
 
Mwenye data halisi atoe, JK na serikali yake wanasema wamejenga barabara zenye urefu wa km 11,000.

Ninazozifahamu ni Minjingu Babati km 160 Babati Singida km 163, Manyoni Singida Kamalizia km 60 zilizobaki katika barabara ya Dodoma mpaka kanda ya ziwa, Ndundu Somanga km 60 alizoacha Ben bado hazijaisha, Handeni Mkata km 110, hazijakamilika, Babati Kondoa km 5 tu zina lami, Kondoa Dodoma imeanza kujengwa km 3 (kuna jumla ya km 290 za barabara hii), Dodoma Mtera Iringa km 320 zimekamilika km 35. Hizo nilizozitaja zina jumla ya km 1,163.

Tuwekeeni mambo hadharani hizo barabara zenye urefu wa km 10,000 nyingine ni zipi? Au ndio zile za Tabora - Nzega, Tabora - Manyoni, Sengerema, Nyakanazi - Kibondo, Kigoma - Kasulu - Mpanda, Tunduma - Sumbawanga na kadhalika. Tuwekeeni data tupate km 11,000 as per magufuli data.
 
Mkuu wangu TOWNSEND usihamaki unaona sasa ukihamaki na akili inahama hatimaye unatoa lugha za matusi..

Sio kila shida zetu za maisha kasababisha JK shida zingine ni matokeo ya yale tuliyoyatengeneza kwa mikono yetu wenyewe.
ritz kuna yale ya mtu mmoja moja na yale ya ujumla ambayo waliomchagua na wasiomchaguwa jk anatakiwa ayafanye kama kiongozi mkuu ...kila mtu anakusanya kodi au anachangia kila ukinunua kitu hata kiberiti mafuta ya taa na bia nk lakini msimamizi mkuu ni yeye
hebu fikiria hakuna kinachoenda hakuna maji ya uhakika hata hapo anapoishi yeye dar kila siku bomba linapasuka ninahamaki ka vile yapo mengi ya kipuuzi kuliko mazuri...hatuna takukuru wala police wala mahakama ndio maana nasema wewe labda haupo nchini.hujawahi kuibiwa ili police na mahakama itende kazi yake inabidi wewe mwenye kuibiwa utoe pesa ili usaidiwe ..ili mtoto wako asome lazima umpeleke privata au st fulani ndio apate eelimu...nyumba ikiwaka moto unaomba mungu hakuna gari za zimamoto...taka unavizia usiku unatupa kwenye chaka lolote'
hivi hata wale wanaochota maji kwa ndoo huwaoni wapo pembeni ya ziwa au mito .
kinachouma zaidi michango yetu wanakula watu wachache yaani rafiki zake waajiriwa serikalini hasa viongozi sio walim na dactari

 
Unapojenga barabara kwa kuomba misaada badala ya rasilimali unazoachia ziondoke!
Unaposamehe kodi kiasi kikubwa kuliko misaada ya masharti
Unapokubali bei ya kujenga barabara kwa kilomita iwe inflated na usiwe na system ya ku-verify
Unapotoa amri zisitekelezwe mfano kiushusha bei ya sukari na usichukue hatua
Unapoanzisha mada kama ya kuvua gamba na isitekelezwe na uliruhusu gamba likusute kwenye kikao unachokiongoza wewe
Unapoita madaktari ukawabembeleza warudi kazini wakakuheshimu na siku ya pili ukawasuta mbele ya 'Wazee wa Dar
Unaporuhusu mbunge aliyepokea milioni moja akamatwe lakini waliooiingiza Tz kwenye mikataba ya kipuuzi na ikathibishwa wameweka fedha zaidi ya bilioni ughaibuni wapete
Unapoangalia wasaidizi wako wakipanda na kushabikia udini
Unapotumia Bakwata kama kipaza sauti chako
Unaposhindwa kuwaadabisha mawaziri wako hadi ushinikizwe na Bunge

Nashindwa kuwa na imani na wewe
 
Wanabodi.

Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.

Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.

Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.

Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.

Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.

JF Daima

Hapo kwenye nyekundu.Naona unajaribu kutudanganya bila mafanikio ,Jk ameingia madarakani fedha za barabaza zilishatengwa na awamu ya tatu.Labda utoe takwimu sahihi kwamba ni barabari ipi mpya ambayo haikuwa kwenye mipango na utekelezaji wa serikali ya awamu ya tatu ameinzisha yeye.Alipoingia madarakani miradi mingi imekwama kutokana na kukosekana kwa fedha.Fedha nyingi amezielekeza kwenye miradi mipya hewa ili wafanye ufiiadi mfano RICHMOND na safari za nje nyingi zisizo na tija kwa taifa.

Ukweli ni kwamba miradi mingi mikubwa wamepindisha ukweli kuwa hakuiazisha wala kuwekea mipango Jk ila wanadanganya uma kwa kujitafutia umaarufu.Mfano daraja la Umoja (Mpakani na Msumbiji) na EPZ (Export Processing zone).

Bado nakubaliana na kauli ya J.Mnyika kwamba Jk ni dhaifu.
 
Mwenye data halisi atoe, JK na serikali yake wanasema wamejenga barabara zenye urefu wa km 11,000. Ninazozifahamu ni Minjingu Babati km 160 Babati Singida km 163, Manyoni Singida Kamalizia km 60 zilizobaki katika barabara ya Dodoma mpaka kanda ya ziwa, Ndundu Somanga km 60 alizoacha Ben bado hazijaisha, Handeni Mkata km 110, hazijakamilika, Babati Kondoa km 5 tu zina lami, Kondoa Dodoma imeanza kujengwa km 3 (kuna jumla ya km 290 za barabara hii), Dodoma Mtera Iringa km 320 zimekamilika km 35. Hizo nilizozitaja zina jumla ya km 1,163. Tuwekeeni mambo hadharani hizo barabara zenye urefu wa km 10,000 nyingine ni zipi? Au ndio zile za Tabora - Nzega, Tabora - Manyoni, Sengerema, Nyakanazi - Kibondo, Kigoma - Kasulu - Mpanda, Tunduma - Sumbawanga na kadhalika. Tuwekeeni data tupate km 11,000 as per magufuli data.

Hadi kufika mwaka 2015 barabara ya kutoka Nyakanazi-Uvinza- Mpanda- Sumbawanga hadi Tunduma itakuwa imekamilika kwa kiwango cha lami, huku barabara ya kutoka Mwandiga jimboni kwa Zitto Kabwe hadi Kidahwe-Nguruka-Urambo hadi Tabora itakuwaimishakamilika baada ya kukamilika ujenzi wa daraja la Mto Malagalasi ambalo lilizishinda serikali zilizotangulia kabla ya JK.
 
Back
Top Bottom