You have really good points.
Solution sio kuongeza road capacities in dar but to have a strategic planning mechanism which will mitigate impacts of increase car ownership and increase need to travel. The country lack (effective) strategic traffic management schemes and there is no qualified and experienced people to carry out these type of studies and projects.. Pia Tanzania tunatatizo la kufikiria kwamba if someone has a PHD in certain field then he is the competent to do the work. This is at all means very wrong and thus is why we ( as the country) keep making decision which are more academic rather than pratical..
The really world of urban and regional planning isn't based on academic research but is based on implementing and adapting tactic which are really workable and doable in really life..
I can understand your view but may be hufahamu how tanzania inafanya kazi. Wanakuwapo wasomi wazuri ambao huwa wanajua vitu na pengine wazuri kuliko huko ulaya but the problem katika utekelezaji (refer back to swali langu ambalo kila siku najiuliza sipati jibu). Inapokuwa sasa wapo katika phase ya utekelezaji there is a different ball game inachezwa. Mkandarasi anataka naye chake, mkuu wa kitengo naye anataka chake, Katibu mkuu wa wizara pia anataka chake na Waziri na rais wake pia wanataka vyao. (Tunaweza kumtoa rais maana sio mara zote anafahamu kinachoendelea).
Sasa basi nini impact ya mazingira kama haya unakuta hata ubora wa barabara unakuwa haupo. Mie binafsi nimewahi kuwa project manager dar utacheka vitu vinavyoendelea when it comes tu utendaji. Nikitumia experience yangu ya kibenki kusimamia mradi nilijikuta mapendekezo yangu yote yalipigwa chini yakaletwa mapendekezo mapya yaliyotoka juu mbinguni (yaani wizarani) sasa unadhani hiyo project itakuwa na manufaa kwa jamii??? Ndio unakuta barabara zinajengwa kwa kiwango cha chini kabisa kulinganisha na awali. Hizo zebra crossing yes inawezekana jamaa hawakuliona (which i doubt kwasababu principles ni zile zile za kitaalamu) but wanaweza pia wakaambiwa bwana michoro mengine inagharimu pesa sana hivyo punguzeni matokeo yake wakawa wanaplan upya michoro kuendana na budget waliyopewa.Ingefaa uwaulize hao waliojenga hiyo barabara waliamuaje halafu ndipo uconclude kuhusu competence za hao wakandarasi. Pesa nyengine wajanja wanakula. Ndio bongo hiyo!!!!
In short bwana tunaweza kusema Miafrika ndivyo tulivyo but hamna lolote watu wanatafuta njia za kupata mirija ya kula tu hamna zaidi ndio wanakuja na elephant projects kama hizi za flyovers just kuweka mazingira ya kufisadi tu!!!
Agizo la rais kikwete ni la kisiasa zaidi... he is good at that!!
Mlioko Dar hivi hizi flyovers zilishajengwa?
ni miaka mi 3 na miezi 10 kasoro siku kama 3 tangu maneno yasiyokuwa na kufikiria ndani yake yalipotolewa...hakuna kilichotekelezeka MZALAMO zaid ya barabara za "magari ya mwendo kasi" za strabag..ngoja niulize kwa wajuv wa akisemacho...hivi aliposema flyover alimaanisha nin eti ZeMarcopolo Ritz na dada yangu FaizaFoxy ????
Ewe punguani, pata darsa dogo hapa:
Tanzania, Japan sign Sh52.2bn flyover deal - National - thecitizen.co.tz
na hapa:
The first flyover project in Tanzania ready for construction — Ministry of Works
na hapa:
TANZANIA STARTS CONSTRUCTION OF FLYOVERS - Corporate Digest
Na hapa:
Na hapa:
Na hapa: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/287933-flyover-tazara-imetengewa-bajeti-magufuli-4.html
Ushapata darsa, sasa kashishii ulale.
Date::6/2/2010i
Mwandishi Maalumu
RAIS Jakaya Kikwete, ameagiza hatua za haraka zichukuliwe, kujenga barabara zinazopita juu katika Jiji la Dar es Salaam, ili kupunguza misongamano mikubwa ya magari.
Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ilisema Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM alitoa agizo hilo juzi, baada ya kupewa taarifa ya utendaji ya CCM katika Mkoa wa Dar es Salaam.
Mwenyekiti huyo alikuwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya siku tatu ya kukagua shughuli za CCM mkoani humo.
"Hili la flyovers lipewa kipaumbele ili tupunguze msongamano wa magari katika Dar es salaam. Tusipofanya hili jiji hili litakuwa halipitiki katika muda wa miaka mitano, ama hata katika miaka miwili ama mitatu ijayo," Rais Kikwete.
Rais Kikwetepia aliwaagiza wataalam wa mipango miji katika Jiji la Dar es Salaam, kuanza kupunguza maeneo yasiyopimwa kwa kuzingatia kuwa kwa sasa ni asilimia 30 ya jiji ndiyo iliyopimwa.
Alisema Jiji la Dar es Salaam, haliwezi kuendelea kupanuka bila mpangilio na kwamba wakati sasa umefika wa kuhakikisha kuwa linajengwa kwa kuzingatia mipango miji.
"Hatuwezi kuendelea namna hii na mji unaopanuka namna hii. Hili ni jambo zito, kubwa linalohitaji umakini wa haraka kutatuliwa. Ndio maana kipindupindu hakiishi katika mji huu." alisema Rais Kikwete baada ya kupata taarifa kutoka kwa watalaam wa huduma za maji, ardhi na barabara.
Katika mkutano huo, Rais Kikwete pia alipewa taarifa kuhusu hatua zinazochukuliwa kukabiliana na ukosefu wa maji ya katika jiji hilo.
Rais Kikwete pia aliusifu utendaji wa CCM katika Mkoa wa Dar es Salaam akiwataka viongozi wa chama hicho kutafuta njia za haraka za kutatua matatizo ya wananchi.
"Angalieni na chunguzeni sana matatizo ya wananchi. Haya ndiyo muhimu kwetu kuyashughulikia, tena kwa haraka. Hii ndiyo nguvu ya chama chetu," amesema Mwenyekiti huyo wa CCM
Source: MWANANCHI
My take:
swala la mpangilio wa mji wa DAR linatia hadi hasira, sijui walikuwa wapi mda wote huo. Then, hao maofisa wa mipango miji wanafanya kazi gani sasa?
Unaweza kukuta wengine hata wamepanga manzese,na kwa nini hadi wapate amri kutoja juu? Tukija kwenye swala la flyovers ni kwamba linatekelezeka au ni kampeni tu? Isije ikawa kama ile ya maisha bora.
Naona Mwaka wa nne sasa, Haraka sana hiyo ni ipi?
Naona Mwaka wa nne sasa, Haraka sana hiyo ni ipi?
Leo tarehe 3/02/2014 hata dalili ya msingi hakuna,kweli wajinga ndio waliwao bora sikumpigia kura..Mlioko Dar hivi hizi flyovers zilishajengwa?