Rais Dkt. Hussein Mwinyi: Serikali imefanikiwa kuwa karibu na Wananchi

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Sep 6, 2020
738
479
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imefanikiwa sana kuongeza ukaribu na wananchi kwa kusikiliza changamoto na kuzitatua kwa haraka kupitia Mfumo wa Sema na Rais Mwinyi (SNR).

Rais Dk. Mwinyi amesema Mfumo wa SNR ni kiungo muhimu kati ya Serikali na wananchi pia ni kigezo cha utawala bora unaozingatia ushirikishwaji wa wananchi.

Rais Dk. Mwinyi amesema hayo katika hafla ya Maadhimisho ya Miaka 3 ya Mfumo wa Sema na Rais Mwinyi (SNR) tarehe: 16 Machi 2024 katika Viwanja vya Ikulu Mnazi Mmoja.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi ameeleza kuwa kitengo cha SNR kina wajibu kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kutumia njia mbalimbali kwa wananchi ili waweze kutumia vema Mfumo huu kwa madhumuni yaliyokusudiwa.

Kwa upande mwingine Rais Dk. Mwinyi amesema katika kipindi cha Miaka 3 tangu kuanzishwa kwa Mfumo wa SNR jumla la malalamiko 13,517 yamepokelewa kati ya hayo 11,116 yamepatiwa ufumbuzi na 2,351 yanaendelea kufanyiwa kazi katika hatua mbalimbali.

Viongozi mbalimbali wa Serikali, Vyombo vya ulinzi na usalama na Vyama vya Siasa wamehudhuria hafla hiyo.

🗓️16 Machi, 2024.
📍Ikulu, Zanzibar.

IMG-20240316-WA0024.jpg
IMG-20240316-WA0027.jpg
IMG-20240316-WA0021.jpg
IMG-20240316-WA0026.jpg
IMG-20240316-WA0018.jpg
IMG-20240316-WA0029.jpg
IMG-20240316-WA0025.jpg
IMG-20240316-WA0028.jpg
IMG-20240316-WA0023.jpg
IMG-20240316-WA0022.jpg
IMG-20240316-WA0020.jpg
IMG-20240316-WA0019.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom