Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
Mwanakijiji,
Hata Lowasa ana akili. Mtu akishakuwa anakununua hawezi kukuajiri maana atakuwa anakuona ni kibaraka tu unayejiuza kwa mwenye nazo zaidi!
FairPlayer, ingekua si mwezi mtukufu ningekupa bonge la ofa ya kiti moto!!!! Lakini itabidi nikuandalie futari la nguvu kule Raskazone!!!! Unajua mtu akikununua anajua iko siku atakuja mwenye fedha zaidi atakununua pia. Iliwahi kunitokea mtu mmoja muhimu a mbaye pia ni source mkubwa wa information akaniomba kwa gharama zozote nimpe source ya information fulani iliyomgusa sana nikamgomea, akakasirika sana, lakini baada ya siku tatu akaniita ofisini kwake, nikajua anaenda kunikomesha, sikuogopa. Nilipofika akanipa information nyingine na kuniambia, "sasa nimepata faraja kuona kwambaunazingatia MAADILI ya kazi zako" kwa hiyo hata hao wanaowanunua waandishi kama Ballile, Kulangwa na wengineo wanajua kwamba iko siku nao watapata mwenye dau kubwa watasalitiwa.