Mnyamahodzo
JF-Expert Member
- May 23, 2008
- 1,932
- 985
Siku ya Jumatatu saa 4-6 mchana (muda wa kipindi cha Meza Busara) na usiku kuanzia saa 2 mpaka saa 3:30 kama si 4:00 wanakuwa na vipindi vya tiba vinavyoendeshwa na kijana (wakati wa mchana) na binti (wakati wa usiku.) Wageni wao ni wale jamaa wa tiba mbadala toka pande za Ukonga na Makumbusho.
Hawa watangazaji wanawaita wateja wao madokta, ... maana ndivyo wanavyotaka kuitwa.
Kwa mtu unayeifahamu biolojia ya mwili wa mwanadamu (just that of form I-IV) unapowasikia hao "madokta" utagundua ni waongo sana. Wanataja mada wanayokuja kuzungumzia siku husika mfano Magonjwa ya Mfumo wa Chakula. Sasa sikiliza wanapoingia kuelezea mada. Wee!! Wanawaingiza wasikilizaji wa radio kwenye "machaka yenye michongoma, miba-bamba na mbigili hali wasikilizaji wako peku."
Kinachokera ni kuwa kwasababu tu hawajamaa wamelipia muda wa hewani, wanaachwa kuendelea kumwaga sumu kwa jamíi.
Siku moja nikabahatika kuipata line wakati wa mchana nikatoa mchango wangu kuonyesha namna huyo Dr feki alivyomwongo na mtupu katika kuelezea mfumo wa mkojo na magonjwa yanayohusiana nayo kisayansi. Na tiba zake zinakuwaje. Nikawa natoa references, cha ajabu nilipomaliza yule dogo Mbise akasema "hayo ni maoni yake"(yaani maoni/mtazamo wangu tu) hakutaka Dr feki ajibu hoja.
Siku nyingine nikakutana ana kwa ana na mtangazaji wa WAPO Radio, akiwa yupo ndani ya gari ya Radio hiyo, nikamwambia "kwa kuwaingiza hao jamaa wamepunguza sana heshima na mvuto wa kipindi cha Meza ya Busara na Radio WAPO ikiwa anamashaka akajifunze kwa wasikilizaji wa 98.0 FM" Sijui alinielewa kwa kiasi gani.
Hawa watangazaji wanawaita wateja wao madokta, ... maana ndivyo wanavyotaka kuitwa.
Kwa mtu unayeifahamu biolojia ya mwili wa mwanadamu (just that of form I-IV) unapowasikia hao "madokta" utagundua ni waongo sana. Wanataja mada wanayokuja kuzungumzia siku husika mfano Magonjwa ya Mfumo wa Chakula. Sasa sikiliza wanapoingia kuelezea mada. Wee!! Wanawaingiza wasikilizaji wa radio kwenye "machaka yenye michongoma, miba-bamba na mbigili hali wasikilizaji wako peku."
Kinachokera ni kuwa kwasababu tu hawajamaa wamelipia muda wa hewani, wanaachwa kuendelea kumwaga sumu kwa jamíi.
Siku moja nikabahatika kuipata line wakati wa mchana nikatoa mchango wangu kuonyesha namna huyo Dr feki alivyomwongo na mtupu katika kuelezea mfumo wa mkojo na magonjwa yanayohusiana nayo kisayansi. Na tiba zake zinakuwaje. Nikawa natoa references, cha ajabu nilipomaliza yule dogo Mbise akasema "hayo ni maoni yake"(yaani maoni/mtazamo wangu tu) hakutaka Dr feki ajibu hoja.
Siku nyingine nikakutana ana kwa ana na mtangazaji wa WAPO Radio, akiwa yupo ndani ya gari ya Radio hiyo, nikamwambia "kwa kuwaingiza hao jamaa wamepunguza sana heshima na mvuto wa kipindi cha Meza ya Busara na Radio WAPO ikiwa anamashaka akajifunze kwa wasikilizaji wa 98.0 FM" Sijui alinielewa kwa kiasi gani.