Radio Tumaini..... Kulikoni?

Mwendabure

JF-Expert Member
Mar 10, 2011
2,138
1,040
Wakuu Nawasalimu!
Kuna hii Radio Tumaini inayopatikana ktk masafa ya 105.9FM (kwa Dar) ambayo hupiga rekodi za kizamani (zilipendwa) kwa muda mwingi. Binafsi ni mpenzi wa nyimbo za zamani zile za hapa nyumbani na hata nje na nimefarijika kwa kuwepo kwa kituo hiki cha Radio inazopiga nyimbo za enzi hizo. Pia naamini sipo peke yangu ktk hili. Lakini nashangazwa na mtindo wa kurudia nyimbo zilezile kila siku kiasi unaweza kujua wimbo gani utafuata baada ya ule uliopo hewani. Pia huwa inatokea kutoweka hewani kwa muda mwingi hata zaidi ya majuma mawili bila taarifa kwa wasikilizaji. Hali hii imenifanya nijiulize maswali mengi kuhusu lengo na dhumuni hasa la kuanzishwa kwake. Pai naamini kuwa rekodi zipo nyingi mno za kizamani kiasi cha kutolazimika kurudiarudia nyimbo hata zaidi ya mara nne kwa wimbo mmoja kwa siku.
Naomba kuwauliza wadau wa kituo hiki (najua mpo humu) kulikoni? Kama suala ni ukosefu wa nyimbo za kutosha kwanini msitoe ombi kwa wadau ili tujitolee kuwapatia hizo nyimbo?
Ukweli kituo hiki kimekuwa kimbilio la wale wenzangu na mimi ambao tunachoshwa na hivi vituo vingine ambavyo vinapiga nyimbo za kisasa na vimejaa matangazo lukuki tena ya mara kwa mara. Jirekebisheni hima!
Nawasilisha!
 
pole mwendabure, nlishawahi kuitembelea radio tumaini ikiwepo hii studio.Kuanzishwa kwale ilikuwa ni kwaajili ya habari za nche kama RADIO CANADA,VATICAN,DW,VOA nadhani hawa jamaa walikatisha ufadhili wao ndipo wakaona bora iwe kwaajili ya wananchi wote wakabuni kucheza nyimbo za zamani. bado wanadesign ili baadae iweze kuwa nzuri kwa sasa wako bize kuhamishia studio zao RADIO TUMAIN 96.3 NA HIYO TUMAIN TWO PAMOJA NA TV TUMAIN kwenda TABATA KRISTO MFALME,wakisetle mambo yatakuwa mswano.PILI HAWANA DJ wa kazi hiyo kwani wameprogram nyimbo kwenye computer muda mwingi inajiendesha yenyewe, pia garama za kurun radio ni kubwa, TUWE NA SUBIRA wakisetle itakuwa bomba. SIWATETEI ila ndio hivo naelewa baada ya kuwaona.
 
pole mwendabure, nlishawahi kuitembelea radio tumaini ikiwepo hii studio.Kuanzishwa kwale ilikuwa ni kwaajili ya habari za nche kama RADIO CANADA,VATICAN,DW,VOA nadhani hawa jamaa walikatisha ufadhili wao ndipo wakaona bora iwe kwaajili ya wananchi wote wakabuni kucheza nyimbo za zamani. bado wanadesign ili baadae iweze kuwa nzuri kwa sasa wako bize kuhamishia studio zao RADIO TUMAIN 96.3 NA HIYO TUMAIN TWO PAMOJA NA TV TUMAIN kwenda TABATA KRISTO MFALME,wakisetle mambo yatakuwa mswano.PILI HAWANA DJ wa kazi hiyo kwani wameprogram nyimbo kwenye computer muda mwingi inajiendesha yenyewe, pia garama za kurun radio ni kubwa, TUWE NA SUBIRA wakisetle itakuwa bomba. SIWATETEI ila ndio hivo naelewa baada ya kuwaona.
<br />
<br />
Asante kwa majibu yako Mkuu! Kidogo nimepata mwanga.
 
MwendaBure vituo vingine vinavyopiga nyimbo za zamani ni Radio one siku ya ijumaa saa tatu hadi saa sita adhuhuri, RFA saa 4-6 usiku siku ya alhamis.
 
MwendaBure vituo vingine vinavyopiga nyimbo za zamani ni Radio one siku ya ijumaa saa tatu hadi saa sita adhuhuri, RFA saa 4-6 usiku siku ya alhamis.
<br />
<br />
Asante kwa kukumbushia ratiba Mkuu! Ni wazi kuna kundi kubwa la wapenzi wa muziki wa enzi zile ambao tunakosa uhondo au tunaonjeshwa kwa uchache. Binafsi nadhani ipo haja ya kuanzishwa kituo cha radio kitakachokuwa kinapiga muziki wa enzi kwa muda mwingi. Nawashauri wadau kuliona hili na kujaribu kulifanyia kazi jamani..!
 
MwendaBure vituo vingine vinavyopiga nyimbo za zamani ni Radio one siku ya ijumaa saa tatu hadi saa sita adhuhuri, RFA saa 4-6 usiku siku ya alhamis.
<br />
<br />
Pia TBC fm siku ya Jumapili kuanzia saa 10jioni hadi 12jioni.
 
Radio MLIMANI jpili kuanzia saa 9 alasiri mpaka saa kumi na mbili jioni, radio uhuru kuanzia saa nne usiku mpaka saa saba usiku jpili chini ya nguli Mikidadi Mahmoud!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom