lifetimesolutions
Member
- Apr 24, 2017
- 67
- 47
Kwanza niseme hii QNET nshaenda hadi training zao kwa kiasi flani niseme sio utapeli bali wanachembe chembe za uongo mwingi sana tena sana.
Ofisi zao Dar es Salaam Sinza Makaburini,Ubungo Mawasiliano,Kinondoni Studio(Stereo Bar karibu na kwa TID) na mpya ya juzi ipo Mikocheni B.
Mtu wako wa karibu ana kupick anakukaribisha ooh njoo on time sehem flan,ukifika vaap unapigwa kitraining pale ukiona zile hesabu za hela hautamani kuondoka sawa eeh uende mchana asubuhi jioni salamu yao ni good morning(wierd)
Kesho yake wanakuonyesha hayo mapackage yao ya millions and millions Holiday,Education & saa etc.
afu ujiunge uingee training ila wao wanakuaminisha usijali sisi tutakusapoti hao watu wawil wa kuwaweka usijali,ila kwangu ilikuwa ndivyo sivyo mm ni mwajiriwa ambae asilimia kubwa ya kazi yang ni safiri nakosa nafasi za kupeleka watu ilinipa shida kila siku wananipigia simu leta watu leta watu nilikuwa kama chizi.
Shida aliyenipeleka ni ndugu nkashindwa kumwambia umenipeleka choo gani,ila yy bado anashabikia sana kuna faida,kwahiyo nililiwa hela yangu yote na nashindwa hata namna ya kufanya.(88BB,na paradigm shif zao na welcome proffesional zao zote nnazo)
USHAURI:
Kama unataka kujiunga jua haya:
1.Utatakiwa kudedicate all of your free time kwenda hapo ofisini.
2.Kwa wiki hakikisha unapeleka watu tano zikapigwe somo
3.ujifunze kuedify na show products.
Well there is no easy money,
ILA QNET KUWENI WA KWELI UNAJUA MTU MUAJIRIWA NA MSAFIRI SANA UKISHACHUKUA HELA NDO UNAANZA KUMNANGA OOH AJIRA INAKUPA HELA NDOGO SANA NJOO QNET.
KINGINE SAA YA KUCHUKUA HELA HATA UWAAMBIE UPO KIMBIJI WANAKUJA SUMBUANENI SASA NJOO OFISI NJOO KWA UPLINE NJOO KWENYE MEETING NJOO LEADERSHIP CAMP.
KWELI QNET NI YA KUANGALIA KWA JICHO LA TATU.