Psychic Powers: Ni nguvu za kufanya miujiza. Wengi wanazo bila kujitambua. Je, wewe unazo?

Daaaaaah ais
aisee! Mkuu pasco kwa mara ya kwanza nilimuona mume wangu akiwa kijana nikasema huyu kaka ndio nimpeleke nyumbani kumtambulisha!! Aiseee nikapotezea, yeye akaanza kuja kwa kasi kwangu nilimkataa kbs ni nikawaambia rafiki zangu yani Mimi simtaki kabisa!! Tulipitia changamoto nyingi ila tumeoana na tunaishi vizuri.


Mara ya pili ilikuwa destruction Dada aliniuzi sana kwa kunyanyasa mtoto mmoja hivi nikamnenea kuwa atazaa na hatoolewa na mwanae atapitia hayahaya!! Miezi michache baadae akpata mimba jamaa akaingia mitini!

Ya tatu niliwaangalia wanawake wajawazito nikasema mhhh watazaa watoto Ila kuna atakaekufa!!!!! Lahaula
Mtoto mmoja akafia tumboni kwa mamake!!

Siku za karibuni wish zangu nzuri zuri na za maana positive oriented hazitokei yani nashtukia tukio kabla halijatokea! Nifanyeje hivi vitu positive vitokee!
Unaonekana unaringa sana wewe, halafu ni much know na mjuaji mjuaji hivi, pia huna heshima na ni jeuri! Sasa ulimkataa wa nini na wakati ulimnenea kuwa unataka kumtambulisha?
 
Nakubaliana kabisa na wewe Mkuu Pasco, kipindi fulani katika maisha yangu nilitamani sana kujifunza uchawi mwenye tija, nikajikuta nimeangukia kwenye temple moja south Africa iliyokuwa inafundisha Buddhism Yoga meditation na supernatural powers

Yalikuwa ni masomo magumu ya ajabu na yenye kushangaza kwa jinsi yake, kwa ufupi ni kwamba hakuna chenye nguvu duniani kama bongo(mind) ya binadamu, na tunachokitumia katika mind zetu ni theluthi tu ya kile chote kilichopo

Tunafundishwa kuwa kuna 5senses, lakini Zipo 8 ambapo mtu ukiweza kuzifanyia kazi utafanya maajabu mengi , mind ya mwanadamu imejazwa takataka nyingi mno, illusions na dillusions ukiweza kuziondoa kwenye bongo yako ukabaki na pure and stable mind unakuwa mtu mwingine kabisa mwenye maono na nguvu za ajabu mno

Medition ni kitu cha Mwanzo kabisa kuendea kwenye kudevelop supernatural powers, nilifanya meditation zote, chanting, yoga nikiwa vegitarian kwa miaka mitano nikajikuta nabadilika nikaogopa nikaacha , kwakuwa niliona wazimu kuna mafundisho yanapingana waziwazi na imani yangu

Nimeipenda mada yako sana. Nakaribisha maswali na ufafanuzi nimeisoma sana Buddhism, Taiosm, Satanism na Kshna consciousness

Mwenye kupenda hii mambo atafute kitabu kiitwacho Analects: Way and Its Power.
Hiki kitabu kama unacho soft mkuu nakiomba tafadhal
 
1 Timotheo 4:
1 Timothy

1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

1 Now the Spirit expressly says that in latter times some will depart from the faith, giving heed to deceiving spirits and doctrines of demons,


2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

2 speaking lies in hypocrisy, having their own conscience seared with a hot iron,


3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.

3 forbidding to marry, and commanding to abstain from foods which God created to be received with thanksgiving by those who believe and know the truth.


4 Kwa maana kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna cha kukataliwa, kama kikipokewa kwa shukrani;

4 For every creature of God is good, and nothing is to be refused if it is received with thanksgiving;


5 kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.

5 for it is sanctified by the word of God and prayer.
 
Mh hapa sasa ndio penyewe nimekua nikifanya kitu nahisi kama kuna siku nilishakifanya lakin tatizo sikumbuki ni wapi na lini kwa mfano naweza kukutana na mtu popote pale iwe njiani au kwenye gari na tukianza kupiga piga stori nakuwa kama napata picha ya hayo tunayozungumzia yalishapita lakini kiuhalisia haijawahi kutokea, hapa nitakua katika kundi gani mkuu Pasco
Hii kitu ninayo pia. Hapa nipo njiani natoka Mwanza na ndio mara ya kwanza kufika ila nafeel kwa baadhi ya sehemu kuwa nilishawahifika. Absursly enough hata kuna baadhi ya mazungumzo yetu ni kama nilishawahi kuyafanya kabisaaaaa. Nilipohisi hivyo kuna mada moja niliianzisha ila kabla hajarespond nikamalizia na response yake. Alishangaa sana dogo. Sasa leo ndio nikaona nianze kugoogle. Thank God nimeangukia jukwaa la nyumbani (JF)
 
Mimi umenigusa sana kuna nguvu na mimi ninazo hapo,kwa mfano unaweza ukanisimulia story kuhusu watu au mtu fulani siku nyingine kabla haujanitambulisha naweza kukisia majina yao kutokana na story yako na kweli inakua hivyo

Nguvu nyingine ni ile uswahilin inaitwa machale kwa mfano wakati nasoma nilikua naotea sana maswali kabla ya mtihani,vile vile naweza nikaunganisha matukio kwa mfano mtu anapiga misele sister nikimuona tu mtaani nilikua nikimuhis ni kweli au nikikaa karibu na mtu mbaya jiran sehemu kama bar huwa nahis na siku moja nilishawah hama meza kwa kuhis jiran si mtu mzur baadae mwenyej wangu alivyokuja kabla sijamuhadithia akaniambia "unamuona yule dada ukimtongoza ukakaa naye meza moja anakuwekea madawa kwenye bia au anakutengenezea fumaniz fake ili wakupore na masela wake"

Maajabu yule dada ni mzur na amekaa kistaarab na mimi ni mgeni hiyo mitaa hadi mwenyewe nilijiogopa yale machale
Hii ilinitokea wakati nafanya paper ya NECTA form 6 2002. Nilikaa na maswali 3 ya History Paper 2 nikawqfuata wabobezi wa History nikawaambia nina wasiwasi sana hayo maswali yatatoka. Tuliyasovu kwa umakini sana, huweziamini kesho yake tunayakuta maswali in the same order I sorted in my rough paper. Jamaa walihisi nilikuwa nina gaka. Ila it never happened again hadi namaliza chuo.

Ila juu ya hilo nahisi kuna connection na certain powers, maana wakati huo huo wa mtihani, History 1 sikumaliza mtihani nikifanya maswali 3½ badala ya matano and I was so desparate.
Nahisi huwa nina nguvu flani nikiwa in desparate moments maana nina matukio zaidi ya hilo la mtihani.

Mwaka 2012, mradi niliokuwa nausimamia ofisini ulisitishwa. In the meantime vikao vya harusi yangu vinaendelea na sina kazi kabisaaaa. Jioni ni moja nimekaa najiwazia sana juu ya hilo suala, wakati napika kopo la chumvi likaangukia kwenye sufuria la ugali nililoloweka. Nikaamua kwenda dukani kununua chumvi dukani. Nikiwa njiani narudi nakutana jamaa akanipa mchongo wa kazi kuwa nipeleke CV ofisini kwao. Jamaa sikuwa na mazoea nae kivile zaidi ya salamu na kujuliana hali kijuu juu. Nilipopeleka CV, siku hiyo hiyo nikapigwa interview na tulikuwa watu 6, nilifaulu interview na kuanza kazi.

2016 nilichukua mkopo Mkubwa benki nikafanyia ujenzi nikiamini mwezi wa 7 tungepanda vyeo (hapa tayari nimeajiriwa serikalini). Ndio likaja zuio la serikali ya awamu ya 5 kutopandishwa watumishi vyeo. Niliishi maisha magumu sana kwa miezi miwili.
Siku hiyo nimekaa kuna mtu akanipigia simu akanipa mchongo mmoja wa consultancy in part time basis, nikawa napata pesa nzuri tu ikichanganywa na mshahara. Kazi nimedumu nayo hadi COVID inaingia wale wazungu wakasepa, na miezi sita mbele deni langu likaisha.

Sijajua hii kupata solution in desparate moment kama ni power au Qudra za Mwenyezi Mungu.
 
Nakubaliana kabisa na wewe Mkuu Pasco, kipindi fulani katika maisha yangu nilitamani sana kujifunza uchawi mwenye tija, nikajikuta nimeangukia kwenye temple moja south Africa iliyokuwa inafundisha Buddhism Yoga meditation na supernatural powers

Yalikuwa ni masomo magumu ya ajabu na yenye kushangaza kwa jinsi yake, kwa ufupi ni kwamba hakuna chenye nguvu duniani kama bongo(mind) ya binadamu, na tunachokitumia katika mind zetu ni theluthi tu ya kile chote kilichopo

Tunafundishwa kuwa kuna 5senses, lakini Zipo 8 ambapo mtu ukiweza kuzifanyia kazi utafanya maajabu mengi , mind ya mwanadamu imejazwa takataka nyingi mno, illusions na dillusions ukiweza kuziondoa kwenye bongo yako ukabaki na pure and stable mind unakuwa mtu mwingine kabisa mwenye maono na nguvu za ajabu mno

Medition ni kitu cha Mwanzo kabisa kuendea kwenye kudevelop supernatural powers, nilifanya meditation zote, chanting, yoga nikiwa vegitarian kwa miaka mitano nikajikuta nabadilika nikaogopa nikaacha , kwakuwa niliona wazimu kuna mafundisho yanapingana waziwazi na imani yangu

Nimeipenda mada yako sana. Nakaribisha maswali na ufafanuzi nimeisoma sana Buddhism, Taiosm, Satanism na Kshna consciousness

Mwenye kupenda hii mambo atafute kitabu kiitwacho Analects: Way and Its Power.
I was walking 7miles in each Sunday to get good meals at Kshna temple. Maneno ya stive jobs katika hotuba yake 2005 Stanford University.

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Imani ni ukweri unaosababishwa na struggling ya kutafuta tulikotokea ili kupata utulivu wa nafsi japokuwa hata kwa kupapasa papasa. Na wakati mwingine kutokana na matatizo yetu yaliyojuu ya fikra za binadamu majibu yake yanapatikana kwa Imani na dini ipo siku nyingi Sana toka enzi na enzi Matendo ya mitume 17:22-24.
 
Mkuu Slow, Mungu alipomuumba Adam, alimpa uwezo!. Yesu alipokuja alifanya miujiza, na kila muujiza alisema "imani yako ndiyo imekuponya!", kasome Marko 10 : 52 - Yesu akamwambia, \"Nenda, imani yako imekuponya, na Mathayo 9:22 Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu;imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile, au [h=3]Luka 17:19 "[/h]Akamwambia, ``Inuka, uende; imani yako imekuponya..hiyo imani yako ndio "powers from within!". Akasema laiti watu wangekuwa na imani kama punje ya haradali, wangeiambia milima ondoka!, na milima ikahama!", ina maana hizi imani tunazotumia ni ndogo tuu kama mbegu ya mchicha!.

Shetani pia ana powers, ikumbuke hapo mwanzo shetani ndiye aliyekuwa malaika mkuu, alipoasi, alifukuzwa ila hakunyang'anwa zile powers, ndiye aliyemrubuni Eva kule lile "tunda!". Nguvu za shetani hufanya maovu, nazo pia zimo ndani yetu kama hizo nguvu za Mungu!.

Kitendo cha kuamini, ni kufungua tuu milango. Mimi ni Mkristu Mkatoliki, kwa sababu nimezaliwa huku. Wengi hufuata imani fulani kwa kujikuta ndiko walikozaliwa na wanaendelea kujifungia humo humo kwa kuto look beyond!. Nilipokuwa India, nikasoma kidogo imani za Hindu ndipo nikagundua kumbe Christianity ni dini ya juzu juzi tuu, kwa taarifa tuu, dini za kale zaidi ni shamanism na animism, ambazo zilikuwepo miaka 300,000 kabla ya Kristu ila baadae zilifutika!. Kwa sasa dini ya kale zaidi iliyopo ni Hinduism ikifuatiwa na Buddhism zote za India ndipo ikaja Judaism ya Mashariki ya Kati, Israel, ikaja Taoism ya China na Shitoism ya Japan ndipo ikaja Christianity!. Hapo dini zetu za asili, hazitajiwi kabisa kwa sababu hazikuandikwa!.

Uki take time kutoka nje ya box la Ukristu au Uislamu ambamo ndiomo wengi wetu tumejifungia humo, ukachungulia ndani ya Hinduism au Buddhism, ndiko utakutana na real powers za "enlightenment!", kwa sababu dini hizi zinaamini kwenye "higher powers" bila kumtaja Mungu, Ukristu na Uislamu umezifungia milango, ili ukifuatilia uthabiti wa imani, discpline, na nguvu za kusali, utagundua sisi Wakristu na Waislamu tunatania tuu!.

Kiukweli ukizama sana kwenye hizi powers, unaweza kuingia kanisani na kujikuta unashutukia jinsi watu wanavyofungwa kamba, unaweza ukaacha kwenda!. Mimi bado ni Mkatoliki Die hard japo kuna mambo tunafanya ndivyo sivyo, ukishayangundua, unaachana nayo, bali unaendelea kuenenda kanisani kwa kufuata mafundisho ya Biblia na sio lazima yale yote ya kanisa ambayo umeisha yastukia kuwa sio!.

Wengi wakistuka, huamia makanisa ya wakovu, huko pia huwa nina hudhuria Mama yangu ni Esemblies og God, huko nako ndiko sio tuu unakuta kamba nene, bali watu wanapurushwa na kukamuliwa mpaka wanabaki mifupa!. Wale Wachungaji wameishajistukia jinsi ya kutumia hizi powers kucontrol waumini wao!. Wale wanaopataga mwanga hustuka na kujihamia kimya kimya, wengine wenye imani upofu, ni watumwa wa Wachungaji wao na wachungaji hao huwafanya lolote ikiwemo kuwa nani hii wake zao!, wao wakijua ndio baraka zenyewe kumhudumia mtumishi wa Mungu!.

Bwana wetu Yesu Krisu alisema wazi, watakuja watu, watahubiri kwa jina langu, watafanya miujiza ya uponyaji na kutoa mapepo kwa jina langu lakini sio wangu!. Ukifuatilia sana the working of powers, unaweza kuogopa kuendelea ku practice, ila ukiisoma vizuri Bibilia, utagundua mahali mengi pameandikwa "nguvu imo ndani yako"!. Mungu alituumba kwa mfano wake, na katupa nguvu ambazo ndizo hizo powers from "within".
Pasco.
Ukisoma Bibilia kitabu Cha Yushua Sura yote ya 24 hasa Aya ya 2 na 15. Utaona ukweri kwamba Mambo ya Imani ni kitambo Sana Ibrahim aliitwa kuanzisha Imani ya Kristu. Hivyo aliitwa akatoka kwenye Imani na inazihilisha Imani zilikuwapo toka kitambo zaidi. Umenena vyema Kuwa Kuna two power and both work ( power of lightness and darkness). Sasa ishu ni kwamba power of darkness end yake ni mbaya na power of lightness Ina end nzuri. Kumbuka Mambo ya meditation yako hata katika ukritu hata kwa wakatoriki japokuwa wengi wetu hatujari kufatilia zaidi. Sasa dini ya kweri ni ipi ambayo ndiyo ya lightness?. Mimi mkatoriki muumini wa kawaida tu sijapitia hizo Imani zingine hivyo sizijui Sana but mkatoriki nilibahatika kusoma katekisimu bubwa ya wakatoriki Mambo mengi na misingi kidogo ya ukatoriki nikaifahamu.
Kwangu Mimi Safari ya Ibrahim Hadi Wana wa Islaeri Hadi kuzaliwa Yesu na mitume kutimiza kazi ya kuanzisha jumuiya ya ukiristu imegubikwa na swala na struggle ya ipi ni dini ya kweri Yani lightness Kati ya
Hizo nyingi zilizokuwapo toka 300k kabla.
Nawe Sasa nakuuliza ipi ni dini ya kweri baada ya kujifunza dini nyingi???

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom