Proper recording: Nini kilimbadili Mzee Mwanakijiji?

Ndugu MM,

Hii note ya mpenda TZ imeeleza na kupitiliza... Hata kwenu unapoona jirani adui anaunguliwa na nyumba halafu ukasimama na kuanza kunyooshea vidole badala ya kukimbilia mchanga na maji kuzima moto ni dhahiri tafsiri yake unatamani nyumba iteketee tena bila mtu mwingine kujua asijeuzima moto!.


MMM nimesoma maelezo yako kwa ufasaha yamekaa kinafiki sana! wewe kama mpiganaji kwanini unanyoosha vidole tu cdm??? kwanini usiibuke kama mwanaume ukawapa ushauri na mawazo kama ulivyowapa Tanzania Police force???? ni dhahiri kabisa unataka mabadiliko sikatai lakini kwa kutumia nguvu nyingi hivi kukosoa tuuuu bila kutoa wazo la kuokoa pale panapokwenda mrama inatafsirika kwamba wewe unahamu kuona nyumba ya jirani yako (cdm) ikiteketea!!!

Naona umeweka mpaka biography yako ya namna umefanya makubwa na mengine yamechukuliwa instantly na kuwekwa kwenye operations na labda zikaleta maendeleo, ni hatua kubwa sana hii!!! tena wewe basi uko popular kimantiki na kimaarifa kwahiyo ukiwaambia cdm sasa hivi wafanye nini naamini instantly watayabeba mawazo na michango yako nakuanza kuyapanga kwenye operation zao na nikuhakikishie cdm wanahamu yakusikia mapungufu yao na wanaham zaidi yakusikia na solutions za mapungufu hayo pia!!!

Lakini Mzee ukinyoosha vidole tuuu kama unavyofanya hapa basi wewe ni piper tu ambae nyuma yake kuna the payer anae determine the tune!!!

japo unasema umesoma kwa makini ni wazi hujasoma vizuri. Kwa sababu kama ungekuwa umesoma kwa makini ungeona kuwa tayari nimeshatoa msaada wa kutosha kwa CDM na ninaendelea kutoa zaidi ya mnavyofikiria. Kufanya hivyo hakunikatazi kuwa critical. Yawezekana wengine ambao wanajionesha kuwa wanaipenda sana CDM na kuikubali hawajafanya lolote kuisaidia ishinde zaidi ya kuisifia tu. Hivyo soma taratibu unaweza ukaibuka na vitu viwili au vitatu badala ya kuita watu majina ukifikiria umesema jambo la maana.
 
Pole sana.kwanza unajipendeza,pili unadhani kuwa na historia ndeefu kunamaanisha kuwa mlikuwa sahihi,tatu ktk red kunaonyesha jinsi hani footer yako "A positive thinker!",inavyopingana na kujihami kwako kuliko kama wenzako wanaopenda jibainisha upande mwingine na kumalizia vibay.Siku hizi huwa nasoma hizi posting zenu kuanzia chini kwanza.Kwa vile juu huwa hakuna connection na malengo yako wala habari yako.

mwisho sema ni wapi hawaajipanga?Na nini ni solution zako ambazo unadhani CDM hawajawahi zifikiri.Sitaki blah blah.


  • Hawajajipanga kiuongozi; huwezi kuwa na viongozi wote wa kitaifa wanagombea ubunge halafu mkatarajia kushinda Urais!
  • Hawajajipanga katika kutengeneza taasisi inayotegemea mfumo badala ya watu. Matokeo yake tatizo lile la watu kuhusu watu lililoko CCM (kwa kidogo) linaikuta CDM kwa kiasi kikubwa
  • Hawajajipanga katika kuelezea mabadiliko ya mfumo ambao wao waataka kuujenga; je wanataka kuja kutawala nchi chini ya mfumo huu huu na vyombo hivi hivi vilivyoshindwa? au watafikiria kuvibadilisha wakishashika madaraka?
  • Hawajajipanga katika kubadilisha sheria ambazo zinatusumbua leo hii; ukiondoa wakati ule Zitto ameleta mswada wa mabadiliko ya sheria ya maadili hatujasikia shinikizo lolote la kuleta mswada mbadala; haikuwa kwenye sheria ya katiba, sheria ya takukuru wala sheria nyingine;
  • Hawajajipanga katika kutengeneza chama ambacho kinatoka chini kwenda juu badala ya kutoka juu kwenda chini. Matokeo yake madudu ya Arusha, Mwanza yametokea na tunaendelea kuona jinsi ambavyo bila viongozi wa juu kushuka chini ni vigumu sana kwa CDM chini kuweza kufanya kazi yake vizuri. CDM inategemea mno nguvu ya viongozi wa kitaifa zaidi ..
  • Hawajajipanga katika kutengeneza mfumo mzuri wa kuhamasisha watu kujiletea maendeleo. Wao wamekuwa kama CCM wanatoa zaidi na kufurahia misaada ya kujenga visima! Hatujawaona wakihamasisha wananchi kwenda kuchimba visima wao wenyewe. Leo tunawaona wakihangaika kutoa misaada kwa wananchi wakati wanadai wana 'nguvu ya umma'. Nguvu ya umma si maandamano! ni mjumuisho wa uwezo wao, nguvu kazi, elimu, raslimali na muda. Ni kwa kiasi gani hivi vimeletwa kujiletea maendeleo?
  • Hawajajipanga katika kutoa changamoto dhidi ya vyombo vya usalama. Tangu mauaji ya Arusha hadi haya ya juzi watu wale wale wanashikilia nafasi zao . Mwema, Chagonja, n.k
  • Hawajajipanga katika kukosoa kisomi sera zilizoshindwa za CCM licha ya kuwa CDM inakusanya wasomi wengi na inakubalika sana na wasomi. Leo hii mwaka wa tatu hakuna hotuba hata moja nzito yenye kufanya contrast ya sera za CCM na zile za CDM na kuonesha kwanini za CDM ni bora!
... inaendelea...
 
lakini si umeniambia kuwa umeanza jikita kuisaidia CDM wa vile imeonyesha ina potential ya kuchukua nchi,na kupendwa na watu?Sasa kuna tofauti gani na hili la umaarufu? Sasa mkuu mbona una crash haraka hivi?Au ndio mwendo wa kurukaruka kama kangaroo?Au swala,kwa sababu swala huwa anakimbia huku akirukaruka,mwishowe husikia raha akadhani yupo ktk gemu,halafu huanza mbio zisizo na malengo na kumfanya predator asubiri kikiwa juu,kinaposhuka anakitafuna tuu.Sasa wewe ndicho unachofanya hapa umekimbia maswali yangu yoote,halafu ukaja angukia hapa.Kupendwa na watu wengi kuna proportionality na umaarufu ndugu yangu.

Hembu tazama hapa kukumbushana


Sasa unasema nini mkuu hapa?Ndio maana nachukia sana Masomo ya UDSM.Masomo ya vita baridi no hovyo sana hasa upande wa ujamaa.

unapozungumza kiungwana utajibiwa kiungwana; ukitaka kujenga hoja kwa kuita watu majina na kejeli mara zote ni dalili ya kushindwa hoja na mwanzo wa kuanza kuleta vioja. Tafadhali yaweke maswali yako hapa tena (maana yakiwa yametawanyika sana na muda ukipita ni kibarua kirefu kuanza kutafuta moja moja. NI kusudio langu kukujibu ili uridhike hata kama hautakubaliana na hayo majibu.
 
unapozungumza kiungwana utajibiwa kiungwana; ukitaka kujenga hoja kwa kuita watu majina na kejeli mara zote ni dalili ya kushindwa hoja na mwanzo wa kuanza kuleta vioja. Tafadhali yaweke maswali yako hapa tena (maana yakiwa yametawanyika sana na muda ukipita ni kibarua kirefu kuanza kutafuta moja moja. NI kusudio langu kukujibu ili uridhike hata kama hautakubaliana na hayo majibu.

Naona umeamua chukua excuse ndogongodo mkuu.kwani upo easily distracted hivyo?yaani vimaudhi kidogo tayari mode ya kususa.Sasa hata JK si anakushinda.CDM watataka nini kwako tena kama unaweza susa hovyo hovyo mambo yakiwa sivyo?Sasa nikirudia tena si nitakuwa najaza database bure tuu kwanini usirudi page km 2 au 3 hivi uyakute?Sasa nishindwe kwa lipi na nikate tamaa kwa lipi wakati nasubiri majibu yangu toka kwako tangu muda mrefu sana.NIkadhani na wewe ulikuwa offline kumbe kuna mida ulikuwa ukirudi na umepost vya watu wengine ila majibu yangu na wengine waliotaka jua zaidi kwa mtazamo wa wazi umesusa.Na ulianza susa mapema sana.

Pia usipende sana kuwa appeased,somewhere ktk discussion kutakuwa na sarcasm,kunakuwa na funny, somewhere utajibu kidhaifu sana kiasi cha kushangaza watu kama ni wewe kweli,halafu bado unakuwa unakomaa tuu.lazima waweke kejeli ili ujiulize wapi umeharibu.uwe unajua pia kuwa Im a radical by nature ,appeasing is not anywhere in my businesses.Ila appreciation ninayo sana.
 
  • Hawajajipanga kiuongozi; huwezi kuwa na viongozi wote wa kitaifa wanagombea ubunge halafu mkatarajia kushinda Urais!
  • Hawajajipanga katika kutengeneza taasisi inayotegemea mfumo badala ya watu. Matokeo yake tatizo lile la watu kuhusu watu lililoko CCM (kwa kidogo) linaikuta CDM kwa kiasi kikubwa
  • Hawajajipanga katika kuelezea mabadiliko ya mfumo ambao wao waataka kuujenga; je wanataka kuja kutawala nchi chini ya mfumo huu huu na vyombo hivi hivi vilivyoshindwa? au watafikiria kuvibadilisha wakishashika madaraka?
  • Hawajajipanga katika kubadilisha sheria ambazo zinatusumbua leo hii; ukiondoa wakati ule Zitto ameleta mswada wa mabadiliko ya sheria ya maadili hatujasikia shinikizo lolote la kuleta mswada mbadala; haikuwa kwenye sheria ya katiba, sheria ya takukuru wala sheria nyingine;
  • Hawajajipanga katika kutengeneza chama ambacho kinatoka chini kwenda juu badala ya kutoka juu kwenda chini. Matokeo yake madudu ya Arusha, Mwanza yametokea na tunaendelea kuona jinsi ambavyo bila viongozi wa juu kushuka chini ni vigumu sana kwa CDM chini kuweza kufanya kazi yake vizuri. CDM inategemea mno nguvu ya viongozi wa kitaifa zaidi ..
  • Hawajajipanga katika kutengeneza mfumo mzuri wa kuhamasisha watu kujiletea maendeleo. Wao wamekuwa kama CCM wanatoa zaidi na kufurahia misaada ya kujenga visima! Hatujawaona wakihamasisha wananchi kwenda kuchimba visima wao wenyewe. Leo tunawaona wakihangaika kutoa misaada kwa wananchi wakati wanadai wana 'nguvu ya umma'. Nguvu ya umma si maandamano! ni mjumuisho wa uwezo wao, nguvu kazi, elimu, raslimali na muda. Ni kwa kiasi gani hivi vimeletwa kujiletea maendeleo?
  • Hawajajipanga katika kutoa changamoto dhidi ya vyombo vya usalama. Tangu mauaji ya Arusha hadi haya ya juzi watu wale wale wanashikilia nafasi zao . Mwema, Chagonja, n.k
  • Hawajajipanga katika kukosoa kisomi sera zilizoshindwa za CCM licha ya kuwa CDM inakusanya wasomi wengi na inakubalika sana na wasomi. Leo hii mwaka wa tatu hakuna hotuba hata moja nzito yenye kufanya contrast ya sera za CCM na zile za CDM na kuonesha kwanini za CDM ni bora!
... inaendelea...
Ni kwamba una ID mbili au umeamua mjibia huku ukiacha wengine hewani kwa tuliyoongea mwanzoni?Naomba ukajibu mkuu ili tuyafunge.

Anyway ngoja nipitie nadharia ambazo kwa kiasi kikubwa ni mawazo yako tuu:
-Kwanini unadhani ukiwa kiongozi wa kitaifa ktk chama cha upinzania huwezi kugombea ubunge?

-Wewe ni mshabiki na mshauri wa Zitto km unavyoonekana ktk postings zako.Pengine ndipo kulikokufanya umshauri apandishe kicha ukidhani kuwa ni tegemeo.Basi subiri akianguka ndipo utakuw aproved wrong.Hujamuuliza Sitta kwa nini alikula kona?kwa vile aliona kanuni za chama hazimruhusu kudandia na kuingia ktik list ya kugombea.Nadhani hata wewe somewhere ktk pitapita utakuwa umeonja hiyo shubiri ya CDM.

-Huo mfumo unaoutaka wautangaze kwani una deadline?What is huu mfumo ni safi tuu ila CCM ndio wame abuse kwa uchafu na udhaifu wao?

-Hawajajipanga kubadili sheria?Hujamiskia Tundu Lissu na Mnyika?Umemwona Zitto tuu.Kwani Ziito yupo wapi?Au mmeshaambiana kuwa si mwana CDM?

-hawajipanga kutengeza chama kutoea chini ila kutokea juu?umesoma ulichoandika mwanzoni?Kuwa haupo tayari kuwasaidi kushinda ubunge bila kushika uraisi.Hiyo kauli haijakutoka bure,ni influence ya CDM walipotangaza mika kadhaa nyuma kuwa wanajenga chama kuanzia chini,wakipanda hadi kufika pa kugombea urais.

-Kuhamasisha watu ,unajua mbowe kawambia nini jimboni kwake?Kuna miradi mingi tuu kawaambia wakichnga kiasi wanachoweza yeye atatoa mara mbili yake?Lema kila mara ana harambee.Sijui kama umepima kw amakini ulichoandika hapa.Kule kaskazini watu wanajiletea maendeleo wenyewe,watu wanajenga makanisa,shulem, dispensary, kurekebisha barabara kwa kujituma na kuongozana.Pengine ndio maana hujasikia sana ktk TV.Hiyo mikoa yenu ndio inahiaji pewa kitu kamili bure.CDM wanafanya hiyo kazi sana hadi nashangaa mwanakijiji gani hujaona haya.

-tehe tehe.changamoto za vyombo vya usalama?pamoja na kwamba tanzania hakuna mtu anayeweza jiengua mwenye hata kwa nini na akienguliwa huanza uadui wa kufa mtu.bado CDM wamesema, na wamesema,wamewapa ultimatum,wamewabana mbele ya mataifa.Na serikali imeshuhudia ikipewa Live.Usalama wa Taifa wamepewa live majukwaani na ktk kura.Sasa sijui ulitaka nini?wafanya vurugu za kipuuzi kama za CUF ili muwahukumu kwa hilo?

-jamani wasomi,wanawakilisha fikra makini, na si lazima waende kwa kutumia conventional ways,conventional ways za nini?ili CCM wazijue na kuziaharibu?CDM wamekuwa wakiendelea kwa kuwa unpredictable wa adui CCM(CCm ni adui kwa vile anapambana kuia CDM na raia).Sasa majukwaani kote CDM waliposimama wameyasema yote,sasa sumary ya nini?Majukwaa wanahiataji kuongea localized problems.Hata makampuni makubwa kama Google huwa na localized contents.Nadhani hii ni idea mpay kwako na wengine waliomshangaa Mbowe alipoongela mapato ya mlima Kilimanjaro akiwa Rombo.Sasa ya nini kuelezea kwa kina makosa 4000 ya CCM ktk hotuba moja?Huo muda utakuwa wapi?Kusema tuu kuwa CDM 1 ni sawa na gamba 30,huku wakiweka mifano hai ya magamba hakutoshi tuu?

Duh..nakushauri kurudia ulichoandika kwanza kabla ya kuendelea.Nimekujibu haraka haraka tuu ili uweze tumia umahiri wako kufikiri zaidi.Hivi kulikuwa na haja ya kuuliza haya maswali bado ukasema unaijua CDM?Sijui Jmushi1 yupo wapi achangie hapa.
 
Ni kwamba una ID mbili au umeamua mjibia huku ukiacha wengine hewani kwa tuliyoongea mwanzoni?Naomba ukajibu mkuu ili tuyafunge.

Hapana nimeamua kujibu tu kwa sababu ni mimi niliyeweka assertion ya kutokujipanga.

Anyway ngoja nipitie nadharia ambazo kwa kiasi kikubwa ni mawazo yako tuu:

-Kwanini unadhani ukiwa kiongozi wa kitaifa ktk chama cha upinzania huwezi kugombea ubunge?

Hapana; sikumaanisha kuwa mtu hawezi kugombea. Kama umesoma "KUtoka hapa mpaka kule" nilisema ni mkakati mbovu na nilieleza ubaya wake. CCM walichohitaji kufanya (na niliweka wazi hili miezi mitatu kabla ya uchaguzi mkuu) ni kuweka pressure kwenye majimbo ya viongozi wa upinzani ili kuhakikisha kuwa hawawezi kukutana na kusimamia kura za urais. Matokeo yake ni kuwa siku ya uchaguzi ile viongozi wote wa kitaifa ukiondoa Slaa walikuwa wamebanwa katika majimbo yao wakilinda "kura"! Ulikuwa ni mkakati mbaya na kwa vile kanuni hazijabadilika utakuwa ni mkakati mbaya 2015.

-Wewe ni mshabiki na mshauri wa Zitto km unavyoonekana ktk postings zako.Pengine ndipo kulikokufanya umshauri apandishe kicha ukidhani kuwa ni tegemeo.Basi subiri akianguka ndipo utakuw aproved wrong.Hujamuuliza Sitta kwa nini alikula kona?kwa vile aliona kanuni za chama hazimruhusu kudandia na kuingia ktik list ya kugombea.Nadhani hata wewe somewhere ktk pitapita utakuwa umeonja hiyo shubiri ya CDM.

Si mshabiki wa watu mimi nashabikia anayefuata kanuni ambazo nimezianisha hapo juu. Lakini pia siyo mshauri wa Zitto so ulichosema hapo hakinihusu.

-Huo mfumo unaoutaka wautangaze kwani una deadline?What is huu mfumo ni safi tuu ila CCM ndio wame abuse kwa uchafu na udhaifu wao?

Well, sijui kama unasema unaamini mfumo huu ni mzuri tatizo ni CCM. Kama unaamini hivyo basi tofauti yangu na wewe ni kubwa zaidi. Mimi ninaamini tatizo siyo chama tu bali na mfumo wenyewe. Chama kitakachoingia madarakani itabidi kifanye overhaul ya mfumo mzima!
-Hawajajipanga kubadili sheria?Hujamiskia Tundu Lissu na Mnyika?Umemwona Zitto tuu.Kwani Ziito yupo wapi?Au mmeshaambiana kuwa si mwana CDM?

Sijui kwanini unaniuliza mambo ya Zitto (soma jibu langu hapo juu). Usidhanie halafu ukaamini ni kweli na ukaanza kuzungumza kwa kudhania unazungumza ukiwa na msingi wa ukweli.

-hawajipanga kutengeza chama kutoea chini ila kutokea juu?umesoma ulichoandika mwanzoni?Kuwa haupo tayari kuwasaidi kushinda ubunge bila kushika uraisi.Hiyo kauli haijakutoka bure,ni influence ya CDM walipotangaza mika kadhaa nyuma kuwa wanajenga chama kuanzia chini,wakipanda hadi kufika pa kugombea urais.

Ukinukuu jaribu kunukuu vizuri na kama hakijawa sawa nitaweka ili ieleweke. Mimi nimesema hivi: Hawajajipanga katika kutengeneza chama ambacho kinatoka chini kwenda juu badala ya kutoka juu kwenda chini.

-Kuhamasisha watu ,unajua mbowe kawambia nini jimboni kwake?Kuna miradi mingi tuu kawaambia wakichnga kiasi wanachoweza yeye atatoa mara mbili yake?

Umethibitisha ninachokisema! Kwa hapo hawana tofauti na wabunge wa CCM sivyo? au hujasikia wabunge wa CCM wakifanya hivyo hivyo?

Lema kila mara ana harambee.Sijui kama umepima kw amakini ulichoandika hapa.Kule kaskazini watu wanajiletea maendeleo wenyewe,watu wanajenga makanisa,shulem, dispensary, kurekebisha barabara kwa kujituma na kuongozana.Pengine ndio maana hujasikia sana ktk TV.Hiyo mikoa yenu ndio inahiaji pewa kitu kamili bure.CDM wanafanya hiyo kazi sana hadi nashangaa mwanakijiji gani hujaona haya.

Ouuuch!!! nahofia kuelewa unachokisema. Hili la Ukaskazini limetoka wapi tena? Ni kwamba kuna hisia ya superiority complex ya watu wa Kaskazini? Sitaki hata kudhania umesema ulichosema.
-tehe tehe.changamoto za vyombo vya usalama?pamoja na kwamba tanzania hakuna mtu anayeweza jiengua mwenye hata kwa nini na akienguliwa huanza uadui wa kufa mtu.bado CDM wamesema, na wamesema,wamewapa ultimatum,wamewabana mbele ya mataifa.Na serikali imeshuhudia ikipewa Live.Usalama wa Taifa wamepewa live majukwaani na ktk kura.Sasa sijui ulitaka nini?wafanya vurugu za kipuuzi kama za CUF ili muwahukumu kwa hilo?

Thats exactyl the weakness; wametoa hotuba ngapi? Wamezungumza mara ngapi kwa ukali. Wamehotubia mara ngapi majukwaani wakishika vichwa na kupiga mayowe? NIni kimebadilika?


-jamani wasomi,wanawakilisha fikra makini, na si lazima waende kwa kutumia conventional ways,conventional ways za nini?ili CCM wazijue na kuziaharibu?CDM wamekuwa wakiendelea kwa kuwa unpredictable wa adui CCM(CCm ni adui kwa vile anapambana kuia CDM na raia).

Are you serious? really? Kwamba mbinu zake ni unpredictable? Sasa hivi ukiangalia sana ni CCM imewageuka CDM na inawafanya CDM wafuate. CCM imefanya political triangulation na hadi sasa CDM hawajaweza kujibu.

Sasa majukwaani kote CDM waliposimama wameyasema yote,sasa sumary ya nini?Majukwaa wanahiataji kuongea localized problems.Hata makampuni makubwa kama Google huwa na localized contents.Nadhani hii ni idea mpay kwako na wengine waliomshangaa Mbowe alipoongela mapato ya mlima Kilimanjaro akiwa Rombo.Sasa ya nini kuelezea kwa kina makosa 4000 ya CCM ktk hotuba moja?Huo muda utakuwa wapi?Kusema tuu kuwa CDM 1 ni sawa na gamba 30,huku wakiweka mifano hai ya magamba hakutoshi tuu?

Sawa waendelee kuzungumza na kuhotubia. Kwani si walizungumza na kuhotubia 2005, 2006, 2007, 2008, 2009, 2010, 2011, na sasa ni 2012. Kama ni hotuba tu kwa kweli si utani zinatia moyo na kufurahisha. Zinavutia watu wengi sana na hili si dogo. Na sitoshangaa kikija kikao kijacho cha bunge tutasikia tena hotuba motomoto; na kikao kijacho cha bajeti nacho kitakuwa na hotuba nzuri vile vile.
 
2010 mnasema chadema haikujipanga kiuongozi na hili hamkulisema wakati ule na mpaka mlishiriki kuandika ilani ya chadema ya uchaguzi ..wala hamkushauri ..leo mnasema chadema haijajipanga na bado wanaendelea na makosa yale yale na mnadiriki kusema hawawezi kushinda ...sasa je ni kwamba chadema wanakataa ushauri wenu? .....mnawauma kisha mnawapuliza!!.....

Nitakujibu kwa ufupi; ushauri unaweza kukubaliwa au kukataliwa. Ukiona watu wanakuja hadharani manake ni kuwa huko kwingine imeshindikana. Mabadiliko usidhani ni rahisi sana, siyo rahisi kihivyo.
 
MMK nimeangalia angle zote na kuona kuna makosa.Au kwa vile umeona nimejibu haraka sana?Ni kawaida yangu nikijibu haraka ndio nakuwa accurate.Ingawa mengi ya uandikayo yana literal meening zaidi ya figurative au nyingine.

mfano kuna swali umelikimbia...Kuwa umeichagua CDM kwa vile ina potential kuchukua madaraka ya nchi?Sijui wewe ukienda waambia ndugu zako girlfriend wako anakupenda na angependa muoane kwa vile unaonekana unauwezo wa kuwa tajiri sijui kam akuna haja tena ya kupigana na watakachokuambia.

Ninaamini kama ingekuwa inaweza kujipanga inaweza kweli kuchukua madaraka ya nchi; lakini katika hilo siishi katika kuona potentiality tu nataka iwe katika nafasi ya kuweza kushika madaraka ya nchi. Ukifika mahali na kuona gari linatengenezwa na ukaona linavyoweza kuwa husifii tu na kuanza kuendesha. Unahitaji kuona likiwa limekamilika na kama una uwezo kusaidia kuona linakamilika.
 
Ila kwa sababu hamjaiona mikakati na mipango ya CDM 2015, wewe na Mzee Mwanakijiji, mtatoa Tathimini ya kushinda CCM, naamini ni kwa kuwa mnakula CCM mnalala Chadema, Well done Guys.

mnawaendekeza sana CCM kiasi kwamba yeyote akiwa critical wa CDM basi anakula CCM. Well, ninampenda rafiki yangu anayeniambia ukweli ukaniumiza kuliko adui yangu anayenisifia nikajisikia raha. Yawezekana kuna watu hawataki kweli CDM ijipange kushinda na wanaridhika na hali ilivyo sasa kwani wanajua ilivyo sasa itakuwa ni ngumu sana kushinda uchaguzi mkuu.
 
Kama bado unaamini kuwa CDM wanashngilia umati wa watu,basi bado huja update database yako na hivyo hoja zako si valid.Hata mwana CCM hard core anajua kuwa CDM umati wao unamaanisha kura,ndio maana daftari la wapiga kuwa halikurekebishwa, na mara nyingine walinunua vitambulisho,wengine majina yao hayakubandikwa,wengine yalibadilishwa kidogo ili yasiwe sawa yakitambulisho na haya yalifanyika shemu CCM wanajua hawakuwa na wafuasi wengi.Huu ni ushahidi mkubwa toka kwa CCM kuliko wako_Once again unaonekana kuwa mzuri kujibia watu maswali kuliko hata kujibu yako.

Are you serious? una matumaini sana ndugu yangu. Ingekuwa umati unamaanisha kura tungekuwa mbali sana. Kutoka umati kwenda kura siyo rahisi kihivyo. HIvi unajua hata ni asilimia ngapi ya wanachama wa CDM wamejiandikisha kupiga kura?
 
Nakumbuka na wakati wa uchaguzi mdogo wa Igunga ulisema hivi hivi, huwa nashindwa kukuelewa ama unataka viongozi wa CDM wawe wanakuezeza wewe mikakati yao? ulisema tena kwa mifana kibao ya chaguzi dogo, lakini nadhani mpaka sasa kupitia Igunga umeshapata picha kwa nini chadema wakati mwingine huwa wanashindwa?

of course, ila ukumbuke nasema nini. CCM wanajua jinsi ya kushinda kwa mbinde na kwa upinde. Lile la Igunga mbona lilikuwa wazi sana. Lakini guess what? CDM walienda kwenye uchaguzi ule katika mazingira yale yale. HIvi leo ukirudiwa uchaguzi wa Arusha na CCM wakashinda mtashangaa? Hivi, imekuwaje CCM wameweza kushinda kiti cha umeya wa jiji la Mwanza? Unafikiri imetokea tu hivi hivi? You guys are underestimating CCM's resolve to stay in power. Mnafikiri itakuja kuachia madaraka hivi hivi.
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji kama utaniruhusu nikuulize kiswali cha kitoto tu kwa viwango vyako. Kama ikitokea kwamba CCM bado ikawa inachukiwa hivihivi ifikapo mwaka 2015 na CDM ikawa "inashabikiwa" hivihivi wakati huo na ikawa CDM bado haijajiweka sawa na kujiandaa vya kutosha "kustahili" kupatiwa madaraka. Uhusika wako kwenye siasa hasa za uchaguzi, hapo 2015 utakuaje? Tu-assume mazingira mengine kama vyama vingine kubakia constant(katika hali hii ya leo). Ahsante

Swali zuri. Ni jukumu la kila mpenda mageuzi nchini kuhakikisha kuwa hali haibakii hivi hivi. Kwa sababu kama ikibakia manake ni kuwa CCM itarudi madarakani na kweli kabisa itakuwa ni mwisho wa upinzani nchini. Kwa sababu ninaamini mwaka 2015 kizazi kipya cha vijana kitakuwa kinashika madaraka ya CCM na kuingia kwenye utawala. Tayari tumewaona wakiandaliwa miaka hii mitano na uchaguzi wa CCM unaondelea sasa unathibitisha hili. CDM ikishindwa 2015 itakuwa si kwa sababu ya CCM bali kwa sababu ya CDM. I intend God willing not to let that happen. Badala ya kujihusisha na CDM mwishoni kama 2010 nimeanza mapema zaidi. Na tutawapitisha kwenye tanuru ya moto kwa kweli.
 
kuna sehemu Mkandara enzi hizo alikuwa akijibainisha kama great thinker alikuwa akishauri CDM wamchukue MMK ili akawasaidie.Niliwahi muuliza sehemu mkandara km ana ushahidi kuwa MMK alivyo machachari kwa CDM si huo ushauri ulimuaffect na hakupenda CDM walivyo potezea?Mkandara kama kawa aliplay kamikaze zake mwishowe akaanza susa km Mentor wake.

Naona CDM wapo sahihi na makini sana kwani hali inavyoonekana MMK hakufaa CDM na hadi sasa Hafai kuwa kiongozi wa CDM.Kama amekimbia maswali kibao humu ndani na katishia susa, ni wazi hii ni issue.

Well, what can I say? Sijawahi kukimbia swali la mtu kwani hakuna swali lisilojibika. KUna maswali mengine ambayo siyajibu tu kwa sababu nitakuwa narudia majibu ambayo tayari yapo. Na kama ni uongozi hujui kitu kimoja - I hate politics! Siwezi kuwa kiongozi wa kisiasa; at least sivyo kama ilivyo sasa.
 
Bado naendelea kuzipitia makala zako na kuzitafakari kuona kama una nia gani haswa.

You are doing very good, kwa kweli umenifurahisha sana. Naweza kuona tofauti ya yule na huyu. Keep it up. Ila kwa vile umekaa hapo muda mrefu nina uhakika hutapata shida kufikia hitimisho ambalo litakupa faraja.
 
mwisho sema ni wapi hawaajipanga?Na nini ni solution zako ambazo unadhani CDM hawajawahi zifikiri.Sitaki blah blah.
.Mkuu Nicholas, unataka tuendelee kuisema jinsi ambavyo Chadema haijajipanga kwenye kila thread?, au nikusaidie kukuelekeza thread zipi zimejikita kwenye hilo?. Hii ni mifano michache!, nakuomba kama una hoja, nenda kazijibu huko huko na tutakutana. Hii sio thread ya jinsi ambavyo Chadema hawajipanga!.
  1. CCM Imechokwa; CHADEMA Haijajipanga!
  2. Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM...
  3. Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If ...
  4. CHADEMA: Tujadili Utayari wa Kutawala Nchi 2015

Hakuna ubishi kuwa humu jf wengi wetu ni wanachama, mashabiki na wafuasi wa Chadema. Ukitokea kuwa tofauti, basi unanyooshewa kidole "CCM", "Gamba" etc!. Hawa wafuasi wa Chadema, wengi wao wanakabiliwa na tatizo kubwa sana la kutoukubali ukweli kuwa "Chadema Haijajipanga", na kazi yao ni kukanusha kwa kutumia "negation" kwa kujifariji kuwa kila anae ikosoa CDM basi lazima ni CCM!.

Ukombozi wa pili wa kweli wa Mtanzania, utaweza kupatikana pale tuu tutakapo kubali kwa dhati kusimama kwenye KWELI, na ni KWELI tuu ndio itatuweka HURU toka madhila haya tuliyopo!.

Mimi kila siku napiga kelele humu. kuendelea kuiimbia Chadema nyimbo za sifa na mapambio!, hakuisaidii CDM. Mtakuja kukuta sisi tunaoipitisha Chadema kwenye tanuru la moto kwa kuikosoa, ndio tunao isaidia zaidi kuliko hawa wanao iimbia nyimbo za sifa na mapambio kila uchao!.

Tukubali, tukatae, Chadema bado haijajipanga kisawa sawa, inao muda wa kujipanga vizuri!, ila ikiendelea hivi hivi ilivyo, 2015 ni CCM tena!.

P.
 
Hahahaa..!! Siasa kweli si-hasa! Wenzetu mmejaaliwa kuwa na muda wa kutosha kufanya hii game kwani kwa namna moja au nyingine game lipo intertwined na mkate wa leo na maslahi ya kesho.
Hii aya ni football analogy ya striker anawaambia mabeki wa opposing side jipangeni vizuri kuna mahala mmeacha gap nisije nikawafunga magoli mengi mechi ikakosa ushindani.
Kwetu sie wengine ni ngumu kweli kuwaamini. Too good to be true mzee. Pasco kweli usingependa CDM isambaratike kabla ya 2015 ili iwe rahisi zaidi kwa mgombea wako umpendaye EL?
Mshindo, hata Simba ikimfunga Yanga, huwa inafurahi, lakini ikitokea Yanga ikashushwa daraja au ikafa kabisa kama Pan na Cosmo, Simba itanyong'onyea and reduced to nothing!. Kweli mgombea wangu ni EL, ila nimeshajitabaisha kuwa support yangu kwa EL ni kwa maslahi ya taifa!. Amini nakuambia, kuna wana CCM kibao wanaipenda Chadema kwa dhati!. Mimi sina tatizo na na ndio maana mara kibao ninaikosoa humu!. Kama ni kuumunga kwangu ZZK ndiko kunatafsiriwa kuwa nataka CDM isambaratike, then let it be, ili EL/Membe wapete!.
P.
 
Sijawahi kusoma UDSM; usiamini sana masimulizi yanayonihusu humu.
Mkuu Mzee Mwanakijiji, uwongo ukisemwa sana na kurudiwa rudiwa bila kukanushwa, mwishowe huonekana ni ukweli. Aliyesema wewe umesoma UD ni huyu na hukukanusha popote!.

Kilichoandikwa hapo juu kina ukweli fulani lakini si ukweli wote. Kwa hiyo hili ni kasa mnalishwa na Edson halafu nashangaa kuona MM hajalipinga.

Mimi nimesoma darasa moja na MM hapa Tanzania. Na alikuwa mwanamapinduzi wa dhati nilipokuwa naye. Hakusoma BA pale UDSM, bali alisoma kozi nyingine( kwa sasa naihifadhi). MM amesoma Masters ya Uchumi USA. Lakini sasa MM amebadilika. Tulipokuwa chuo kaka zetu waliotupika kuwa wazalendo ni kina Kitila Mkumbo ambaye wakati huo alikuwa Rais wa DARUSO. Jakaya Kikwete ni sisi tumechangia kwa kiasi kikubwa kumweka madarakani na ndio maana tunatamani tumtoe hata leo kwa jinsi alivyotusaliti. RIDHIWANI ANALIJUA VYEMA HILI. NCHIMBI NDIYO KINARA HASWA(MBA UDSM!!!!)

MMM alikuwa ni kiongozi wa DARUSO Kwenye wizara nyeti ( Naihifadhi kwa sasa). MM alifukuzwa pamoja nami kwenye mgomo wa mwaka ambao kulikuwa na uchaguzi wa Rais, Hivyo MM hakumaliza masomo yake TZ. Alipoenda marekani kwa jitihada za kuuza ng'ombe wa mama yake kijijini ndipo alipobadilisha masomo.

MM hakupitia Mbweni hivyo si mwajiriwa wa TISS hata kidogo! Huwezi kuwa Ofisa wa jeshi kwa kupitia kwa amiri jeshi mkuu bila kupita Monduli kwa JWTZ au Mbweni kwa kupitia TISS. Japo sikatai kuwa anaweza kutumiwa na TISS kama anavyotumiwa mgombea Urais wetu Zitto Zuberi Kabwe.( Sijui kama anakumbuka kiapo chetu pale nyumbani kwa mama yake Magomeni mwembechai- kwa sababu tume ya madini ya Kikwete ilimvuruga kabisa)

Kwa kifupi niseme tu hapa mnalishwa kasa na Edson, na jambo la pili ni kuwa kina MMM wana msemo wao huko wanakotumiwa kuwa 'every head has got a price tag on it'.

Haya aliyoyasema ni kama ifuatavyo

  1. Mimi nimesoma darasa moja na MM hapa Tanzania. Na alikuwa mwanamapinduzi wa dhati nilipokuwa naye. Hakusoma BA pale UDSM, bali alisoma kozi nyingine( kwa sasa naihifadhi).
  2. MM amesoma Masters ya Uchumi USA. Lakini sasa MM amebadilika. Tulipokuwa chuo kaka zetu waliotupika kuwa wazalendo ni kina Kitila Mkumbo ambaye wakati huo alikuwa Rais wa DARUSO.
  3. Jakaya Kikwete ni sisi tumechangia kwa kiasi kikubwa kumweka madarakani na ndio maana tunatamani tumtoe hata leo kwa jinsi alivyotusaliti. RIDHIWANI ANALIJUA VYEMA HILI. NCHIMBI NDIYO KINARA HASWA(MBA UDSM!!!!)
  4. MMM alikuwa ni kiongozi wa DARUSO Kwenye wizara nyeti ( Naihifadhi kwa sasa).
  5. MM alifukuzwa pamoja nami kwenye mgomo wa mwaka ambao kulikuwa na uchaguzi wa Rais,
  6. MM hakumaliza masomo yake TZ. Alipoenda marekani kwa jitihada za kuuza ng'ombe wa mama yake kijijini ndipo alipobadilisha masomo.
  7. MM hakupitia Mbweni hivyo si mwajiriwa wa TISS hata kidogo!. Japo sikatai kuwa anaweza kutumiwa na TISS ( Sijui kama anakumbuka kiapo chetu pale nyumbani kwa mama yake Magomeni mwembechai- kwa sababu tume ya madini ya Kikwete ilimvuruga kabisa)
  8. Kwa kifupi niseme tu kuwa kina MMM wana msemo wao huko wanakotumiwa kuwa 'every head has got a price tag on it'.
Mwanakijiji ulipaswa kukanusha kwa sentensi moja tuu kuwa "its a mistaken identity na sio wewe, then the rest yanakuwa ni redundant!.
P.

 
Hapa Duniani Kuna mambo mengi sana.......lakini lililo kuu ni kujua kuwa jambo unalolikumbatia lina Maslahi Binafsi kwanza then mengine baadaye siyo kushabikia na kushadadia tu kila kitu.....Hakuna Maslahi hakuna Mapenzi.....Asikuambie mtu Bana hii ndiyo DUNIA....
 
Back
Top Bottom